Tuesday, May 28, 2013

SOMA ALICHOKISEMA BUSHOKE AKIWA SOUTH AFRIKA KUHUSU KIFO CHA NGWAIR

Kuna taarifa kuwa chanzo cha kifo cha ghafla cha rapper Mangweir ni kuzidisha madawa ya kulevya aliyotumia usiku wa kuamkia leo. Inadaiwa kuwa Mangwea alikuwa pamoja na mtu aitwaye M TO THE P ambaye naye yupo mahututi kwa sasa.


Hata hivyo mwenyeji wa rapper Albert Mangwea aliyefariki leo jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini, amesema hit maker huyo wa Mikasi amefariki akiwa usingizini.



Akiongea na Clouds FM muda mfupi uliopita, mwenyeji huyo aitwaye Jonathan amesema usiku wa kuamkia leo Mangwair alirudi nyumbani alikofikia akiwa mzima wa afya lakini mpaka kunakucha hakuonesha dalili za kuamka.

“Sijui hata huko alitumia nini,” amesema.

Ameongeza kuwa asubuhi kulipokucha aliondoka kuendela na mishemishe yake na alipokuwa huko wenzake walimpigia simu kumtaarifu kuwa wamempeleka hospitali ya St. Helen ya jijini humo kwakuwa alikuwa bado hajaamka na ndipo walipogundua kuwa ameshafariki.

Hata hivyo amesema hakuweza kujua sababu za kifo cha Ngwair kwakuwa maelezo ya daktari yalikuwa kitaalam kiasi cha kushindwa kuelewa. Ngwair alikuwa amepanga kurudi leo nchini.

HII NDIO SABABU INAYODAIWA KUSABABISHA KIFO CHA NGWAIR. SOMA HAPA


ripoti kamili
Taarifa Nilizo Pata Kutoka South
Africa Kutoka Kwa Hussein
Original Ambaye Yupo Pretoria
Amesema Ngwear Amefariki Leo

Asubuhi. Alikuwa Ghetto Moja Na
Msanii M To The P.
Walivyokwenda Kuwagongea
Asubuhi Walikuta Ngwear
Amefariki Na M To The P
Amepoteza Fahamu Kabisa. Pia
Daktari Ameshatoa Taarifa Kwa
Watu Wa Karibu Wa Ngwear
Huko South Africa. Ngwea akiwa na msanii M to the P jana south africa.mtu wa karibu anasema walitakiwa kurudi dar leo lakini waliwakuta wamezima kwenye room wote wawili baada ya kuji overdose madawa ya kulevya na M to the P yupo hoi hospitali.

BREAKING NEWZZZZZZZZZZ....!!! MSANII ALBERT MANGWAIR AFARIKI DUNIA LEO HUKO AFRIKA KUSINI


Mwanamuziki wa Hip-Hop ALBERT MANGWAIR amefariki dunia LEO huko Afrika Kusini katika hospitali ya Hellena Joseph.

DR CHENI ALISHWA CHAKULA CHENYE SUMU NA KUKIMBIZWA HOSPITALI, LULU AHAHA HOSPITALINI.



Katika hali ya kushangaza na isiyo eleweka mwigizaji Mahsein Awadhi maarufu kama Dr. Cheni amekumbwa na balaa la kulishwa chakula chenye sumu weekend iliyopita alipokuwa kwenye sherehe moja ya harusi jijini Dar es Salaam alipohudhuria kama MC au mshereheshaji wa harusi hiyo.

Akiongea na bongo movies leo asubuhi, Dr. cheni alisema kuwa baada ya kumaliza kula chakula ambacho alipakuliwa na mmoja wa wahudumu wa sherehe hiyo alianza kujisikia vibaya na kuishiwa nguvu na aliamua kutoka nje kujaribu kupata hewa akidhani ladba ni joto la ukumbini ila hali ilizidi kuwa mbaya na aliamua kutafuta maziwa akihisi labda inaweza kuwa vidonda vya tumbo ndipo alipoanza kutapika na baadae kukumbizwa hospitalini na ndipo alipogungulika kuwa amelishwa chakula chenye sumu.

Tulipomuuliza labda sababu gani anahisi zinaweza kuwa zimepelekea watu hao kutaka kumdhuru alisema kuwa, mpaka sasa hajaweza kupata jibu kamili ila anaamini watu waliofanya hivyo wanamfahamu na wana nia mbaya sana kwake na sio watu wema. Dr. Cheni alisema kuwa kwa sasa hali yake inaendelea vizuri na moja ya watu walikuwa wa kwanza kufika hospitalini baada ya yeye kupatwa na majanga hayo ni mwigizaji Elizabeth Michael (LULU) ambaye kwa sasa yupo karibu sana na Dr. Cheni aliyekuwa mstari wa mbele katika kushughulikia mpaka kufanikisha suala la dhamana ya kesi iliyokuwa inamkabili mwanadada huyo. Pole sana Dr. Cheni.

KIJANA AKUTWA NA SEHEMU ZA SIRI ZA MWANAUME AKIZIUZA

Foster Mangani
Jeshi la polisi nchini malawi wanamshikilia kijana mmoja baada ya kumkuta akiuza sehemu ya siri ya mwanaume.kijana huyo mwenye miaka 24 alikamatwa baada ya wananchi kutoa ripoti kituo cha polisi kuwa kunamzee kalala relini huku akiwa anatokwa damu nyingi ndipo polisi walipofika eneo la tukio na kumkuta mzee huyo akiwa hio na kuamua kumkimbiza hosipitali.
Mtuhumiwa Samuel Banda
 
Baada ya kufikishwa hosipitali ndipo madaktari walipo gundua kuwa mzee huyo alikuwa amejeruhiwa kwa kukatwa sehemu zake za siri,mara moja madaktari walilipoti wa maofisa hao wa polisi na ndipo msako mkali ulipo pita katika wilaya ya Lakeshore huko mjini Salima na polisi hao kufanikiwa kumtia mbaroni kijana huyo baada ya kumkuta kijana huyo akiwa ktk gesti bubu akijaribu kuuza uume huo kwa dola za kimarekani 360.

Polisi walisema mtuhumiwa Samuel Banda alikamatwa na kiungo hicho ambacho alikuwa amekifunga ktk karatasi nyeupe na mtuhumiwa alikiri kuwa huwa anauza viungo mbalimbali vya binadamu kwa wafanya biashara maarufu nchini humo ambao wanaamini wakivipata viungo hivyo huwasaidia katika biashara zao na huwaongezea utajiri.
Mtuhumiwa Samuel Banda

MAGAZETI YA LEO JUMANNE MEI 28, 2013

7 5c323

1 bfd68

HUYU NDIO MSANII MAARUFU KUTOKA NIGERIA ALIYEFANYA MAPENZI NA MBWA

 


Suprise i’m bring this up again?

Well it’s about time i unleash thehidden secret, I randomly stumbled upon the video but i’ll not publish it, though so many people were not opportuned to watch it so i’ve took some snapshots from the video… Another photo when you continue;  To Cossy Orjiakor is involve in LOTS of Soft Porn scenes as she plays the Role of A Nigerian prostitute in Italy. And theres actually a Scene in which cossy had fun with some guys and a DOG

BRAZIL KUIFUTIA MADENI AFRIKA

Rais wa Brazil Dilma Rousseffalitoa matamshi yake katika mkutano wa AU nchini Ethiopia
Brazil imetangaza kuwa itafutilia mbali au kuwa na makubaliano mapya kuhusu madeni inayozidai nchi za Afrika ambayo yanakisiwa kuwa dola milioni 900.

Miongoni mwa nchi 12 zilizo kwenye orodha ya mataifa yanayodaiwa ni pamoja na Congo-Brazzaville yenye uitajiri mkubwa wa mafuta na gesi, Tanzania ambayo hivi karibuni itaanza kuchimba gesi pamoja na Zambia
Wadadisi wanahisi kuwa hii ni njia mojawapo ya Brazil kutaka kukuza uhusiano wa kiuchumi kati yake ambayo ni ya saba kwa ukubwa kiuchumi na Bara la Afrika.

Taarifa rasmi zinaonyesha kuwa uhusiano wa Brazil na bara la Afrika umeongezeka mara tano katika mwongo mmoja uliopita.

Tangazo hili, lilitolewa wakati wa ziara ya tatu kwa miezi mitatu ya rais wa Brazil Dilma Rousseff,aliyehudhuria mkutano wa Muungano wa Afrika nchini Ethiopia.
"takriban madeni yote huenda yakafutwa , '' alisema msemaji wa Rais Rousseff Thomas Traumann.
"ili kukuza uhusiano kati ya Afrika ni muhimu kwa sera ya kigeni ya Brazil."
Aliongeza kuwa nyingi ya madeni hayo yaliongezeka miaka ya sabini na kuwa kulikuwa na mazungumzo kuyahusu wakati huo.

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Brazil, alisema kuwa baadhi ya nchi huenda zikafaidika na makubaliano mazuri kuhusu namna ya kulipa madeni hayo huku muda wa kuyalipa ukiongezeka.
Congo-Brazzaville, inadaiwa dola milioni 352 ikifuatiwa na Tanzania inayodaiwa dola milioni 237 Zambia nayo ikidaiwa dola milioni 113.4.

Nchi zingine zitakazofaidika ni pamoja na Ivory Coast, Gabon, Guinea, Guinea Bissau, Mauritania, DRC, Sao Tome and Principe, Senegal na Sudan.

Brazil imekuwa ikiimarisha uhusiano wake wa kibiashara na Afrika, kitovu cha madini kama sehemu ya kile kinachojulikana kama ushirikiano wa kanda ya Afrika Kusini.
Kampuni nyingi za Brazil huekeza sana katika sekta ya mafuta na madini na zimekuwa zikifanya miradi mikubwa ya miundo mbinu barani humo.

Monday, May 27, 2013

NAY WA MITEGO AFUNGUKIA ISHU YA KUPIGWA KIBUTI NA WEMA SEPETU...!!

WIKI iliyopita tulimleta kwenu msanii wa Bongo Fleva anayetamba na ngoma aliyomshirikisha Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ya Muziki Gani, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ ili umchambue ambapo mlituma maswali, hapa anajibu na kufafanua moja baada ya lingine. SHUKA NAYO…

PONGEZI
Nakukubali sana kaka na ngoma zako unavyochana ukweli, kaza buti utafi ka mbali. Roja, Dar, 0657888221
NAY WA MITEGO: Asante.

VIPI KUHUSU NISHA?
Nay wa Mitego uliwahi kuwadisi Bongo Movies na kusema kwamba wanawake wote wanaojiuza wanatoka kwenye tasnia hiyo, je, ilikuwaje ukatoka na Salma Jabu ‘Nisha’ kwani yeye si mmoja wa Bongo Movies? Rocky, Moshi, 0715289337
NAY WA MITEGO: Sijawahi kutoka na Nisha ni mshkaji wangu tu.

YEYE NA DIAMOND
Kwanza hongera kwa kazi zako nzuri kaka, naomba kufahamu kuhusu ule wimbo uliokuwa ukimrekebisha tabia dogo (Diamond), hivi aliyetunga ni wewe au yeye au mlikaa chini na kutunga pamoja? Siyo siri umetulia hongereni sana. Julianitha Jamushi, Dar, 0712089824
NAY WA MITEGO: Asante, Muziki Gani tumeandika pamoja.

"USHAURI

MIDUME YAPIGANA VIKUMBO KUGOMBANIA PENZI LA WASTARA...!!

TAKRIBAN  wiki moja baada ya kumaliza eda tangu alipofariki mumewe Juma Kilowoko ‘Sajuki’ Januari 2, mwaka huu, staa mkubwa wa filamu za Kibongo, Wastara Juma anagombewa na midume ikitaka kumuoa.
 
Akizungumza na mwandishi wetu  akiwa nchini Oman, Wastara alifunguka kuwa tangu amalize eda yake hiyo amekuwa akipata usumbufu mkubwa kutoka kwa wanaume mitandaoni na wanaomtamkia mwenyewe.
“Jamani mpaka nahisi kuchanganyikiwa kabisa, wanaume zaidi ya mia tano hata sijui walipotokea wanataka kunioa, hadi nahisi majanga,” alisema Wastara.

Wastara alisema kuwa wanaume hao wamekuwa wakihangaika bure kwa sababu kwa sasa hafikirii kabisa kuolewa kwani anapotembea bado anasikia harufu ya mumewe Sajuki.
 
“Bado harufu ya Sajuki ipo mwilini mwangu, wanaume wanaonitolea macho mtoto wa mwenzao wanakosea sana, sifikirii kabisa suala hilo kwa sasa,” alisema Wastara mwenye mtoto mdogo aliyezaa na Sajuki.

MAMA AMUUNGUZA MOTO MWANAE WA KUMZAA.....!!!

 Mkono wa Fikiri Haus 13 uliounguzwa unavyo onekana kwa karibu huo ni ukatiri ulio kithiri
Mtoto Fikili Hausi Mwanafunzi wa Darasa la Tatu Shule ya Msingi ya Majengo Mansipaa ya Songea akiwa amelazwa Hospitali ya Mkoa baada ya Kunguzwa Moto na Mama yake.
Jeshi la Police lina endelea kumtafuta mama yake Fikili Hausi
  Msomaji hebu angalia Jamii ya watanzania kila siku inafanya makongamano ya kuzuia vitendo vya ukatili dhidi ya watoto na mama, je kitendo kama hiki watanzania tunaenda wapi?
(Picha na Songea Habari)

MKE AMNASA MUMEWE AKIMLAWITI SHOGA WAKIWA GESTI, MKE AANGUA KILIO....HII NI ZAIDI YA LAANA...!!!

OPARESHENI Fichua Maovu 'OFM' inayoendeshwa namtandao huu, hivi karibuni mwanaume mmoja aliyefahamika kwa jina la Ezekiel Malika 'Baba Kulwa' amenaswa gesti na mkewe akiserebuka na shoga aitwaye Aunt Steve na kuibua mtiti mzito, 


 

Tukio hilo lililovuta umati lilijiri Mei 20, mwaka huu kwenye gesti moja (jina tunalo) iliyopo Mwananyamala, Dar ambapo mke wa Ezekiel alivamia na kutembeza mkong’oto wa hasira kwa mumewe.
ILIKUWAJE?
Mei 19, mwaka huu, saa 3:15 asubuhi, mwanamke mmoja ambaye aliomba hifadhi ya jina lake kwa ajili ya heshima yake mtaani alilipigia simu gazeti hili na kutoa malalamiko kwamba mumewe amekuwa na tabia ya kulala na wanaume wenzake ambao ni mashoga.
“Jamani, mimi naitwa… (akataja jina), naomba jina langu lisiandikwe gezetini. Malalamiko yangu ni kwamba, mume wangu amekuwa na tabia ya kulala na mashoga, hivi ninavyoongea ana ahadi ya kukutana na mmoja wao gesti kama si kesho basi keshokutwa, niliona meseji kwenye simu ya mume wangu.



“Nawaomba chondechonde, mnisaidie ili hii tabia ikome. Nipo tayari kusikia maelekezo yenu kwa sababu nimesoma kwenye gazeti lenu kwamba mnafichua maovu na huu nao ni uovu,” alisema kwa masikitiko mwanamke huyo.
MKE APEWA MAELEKEZO
Mratibu wa Oparesheni Fichua Maovu alimpa maelekezo mwanamke huyo akimtaka kufuatilia kwenye simu ya mumewe ili kubaini siku ya wawili hao kukutana gesti.
“Nawaahidi kwamba leo hiihii kabla giza halijaingia nitakuwa nimejua siku yao ya kukutana, naomba msiache kupokea simu yangu jamani.”
OFM: Sawa mama, pole sana.


Mwanamke: Asante sana.

ANGALIA PICHA ZA LADY J DEE AKIWA MAHAKAMANI LEO

Mwanamuziki wa kizazi kipya Judith Wambura 'Jay Dee' akiwa na mumewe Gadner Habash kabla ya wakisuburi kesi kutajwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kindondoni leo asubuhi saa 3, angalia picha zaidi

KESI YA LADY JAYDEE NA LWAKATARE KUNGURUMA LEO



WAKATI kesi ya Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatare ikitarajiwa kusikilizwa leo Mei 27 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Kesi ya msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Judith Wambura (Lady JayDee) pia inatarajia kusikilizwa tarehemu hiyo katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Kesi hizo zinatarajia kuvuta hisia za watanzania kutokana na mvuto na aina ya kesi hizo,Lwakatale atapanda kizimbani kwa mara nyingine huku akitarajia kupata dhamana ya kesi yake baada ya Mahakama Kuu kumfutia mashtaka ya Ugaidi yaliyokuwa yakimkabili awali na kubaki na shitaka la kula njama ya kumdhuru Denis Msacky ambayo inadhaminika.
 Kwa upande wa Lady JayDee anatarajia kupanda kizimbani kwa mara ya kwanza baada ya kukabidhiwa hati ya mashtaka na kutakiwa kurudi mahakamani hapo kesho mei 27 .

Waandishi wa habari walishuhudia barua kutoka mahakamani hapo pamoja na nyakara zilizochapishwa na vyombo mbalimbali vya habari zikiwamo blogu zilizoelezea ugomvi wake kati ya Mkurugenzi Mtendaji wa Clouds Media Group, Joseph Kusaga na Mkurugenzi wa Utafiti na Matukio Ruge Mutahaba.

WALIOFELI KIDATO CHA NNE WAULA, UFAULU SASA WAONGEZEKA....!!!



Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk. Joyce Ndalichako  

Dar es Salaam. Idadi ya watahiniwa waliofaulu mtihani wa kidato cha nne mwaka jana imeongezeka kwa kati ya asilimia 20 na 23 baada ya Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), kufanya marekebisho alama za viwango vya ufaulu, Mwananchi limebaini.
Habari ambazo gazeti hili imezipata zinasema matokeo hayo ambayo yamewezesha kiwango cha ufaulu kupanda na kufikia asilimia kati ya 54 na 57, huenda yakatangazwa wiki hii pamoja na yale ya kidato cha sita ambayo pia yamechelewa kutangazwa.
Chanzo cha habari kutoka Necta kimesema matokeo hayo mapya yanaonyesha kuwa, ufaulu wa kuanzia daraja la kwanza hadi la nne umeongezeka kutoka asilimia 34.5 kwa matokeo yaliyotangazwa awali na huenda yakafikia asilimia 57. Hii inamaanisha kwamba watahiniwa wapatao 82,000 ambao awali walikuwa wamepata sifuri katika matokeo ya awali sasa wamepanda na kupata madaraja ya ufaulu katika matokeo mapya.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU MEI 27, 2013

7 bc143
3 47ad9

FEZA KESSY NA AMMY NANDO NDIO WAWAKILISHI WA TANZANIA KWENYE BBA ‘THE CHASE’



ANGALIA PICHA ZA LULU ANAVYOZIDI KUWA NA MVUTO


Muigizaji wa kike aliyekulia kwenye tasnia ya bongo movie, kwa kuwa alianza tangu akiwa mdogo na hadi sasa kipaji chake kinazidi kung’aa. Haishii kung’arisha kipaji chake tu bali anazidi kuwa na muonekano wenye mvuto pia.

Lulu anaonekana hana stress tena kama ilivyokuwa siku kadhaa zilizopita alipokuwa chini ya ulinzi mkali akituhumiwa kusababisha kifo cha muigizaji mwenzake Steven Kanumba.

Huu ndio muonekano wa Lulu sasa hivi:

 
 

Sunday, May 26, 2013

MULUGO NA WANAFUNZI WANAOMILIKI SIMU


NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo, amesema atafanya ziara katika shule zote za msingi na sekondari ili kuwabaini wanafunzi wanaotumia simu za mkononi shuleni.
Mulugo alitoa kauli hiyo mjini hapa juzi alipokuwa akizindua mpango mkakati wa elimu ya haki za binadamu na kuongeza ataanzia Mkoa wa Dodoma na atakaowabaini atawanyang’anya na kuzichoma moto.
Alisema suala la utandawazi limechangia kwa kiasi kikubwa wanafunzi kuharibika na kuwa na nidhamu mbovu, ikiwa ni pamoja na kuwadharau walimu na wazazi.


Mulugo alisema kitendo cha wanafunzi kwenda na simu shuleni kimesababisha mmomonyoko mkubwa wa maadili, ambapo pia kimechangiwa na baadhi ya wazazi kujifanya wanawapenda watoto wao: “Hivi sasa limekuwa ni jambo la kawaida kuwakuta wanafunzi wa ngazi zote wakiwa na simu shuleni. Mimi sikubaliani nalo, nimeamua nitafanya 
ziara shule moja baada ya nyingine nikimkagua mwanafunzi mmoja baada ya mwingine nikianzia na Mkoa wa Dodoma katika kipindi hiki cha Bunge. Ole wake mwanafunzi nitakayemkuta na simu nitamnyang’anya na kuichoma moto maana walimu wanawalea sana… halafu na mimi mniimbie ‘tunataka haki zetu’,” alisema Mulugo.

RAIS NKURUNZIZA WA BURUNDI AJA KUHUBIRI INJILI TANZANIA

Rais Pierre Nkurunziza.
Rais wa Burundi, Pierre Nkurunziza, anatarajiwa kuja nchini Agosti, kuhubiri Injili katika mkutano mkubwa wa Injili unaoandaliwa na Baraza la Makanisa ya Kipentekoste nchini (PCT), imefahamika.
Kwa mujibu wa Askofu Samson Mlawi aliyezungumza na mwandishi wa habari hizi mwishoni mwa wiki, tayari  Kamati ya  Maandalizi imefanya vikao kadhaa ambavyo pamoja na mambo mengine, kamati ndogo zimeundwa ili kurahisisha ujio wa Rais huyo.
Alisema, kwa kutambua umuhimu na uzito wa ujio huo katika shughuli hiyo ya kiroho, kamati imeweka mtandao wa mawasiliano kuhakikisha waumini wa madhehebu hayo kutoka mikoa mbalimbali wanahudhuria mkutano huo ambao bado unatafutiwa uwanja.
Askofu huyo alisema Rais Nkurunziza pamoja na mambo mengine, anatarajiwa kuleta ujumbe wa amani na uvumilivu wa kidini hususan katika kipindi hiki cha mpito baina ya madhehebu ya Kikristo na Waislamu nchini.
“Mimi na wanakamati wenzangu, tunaamini Mungu atafanya kazi yake kupitia Rais kuhubiri Habari Njema kwa Watanzania kama ambavyo angehubiri mtu mwingine yeyote, lakini kutokana na nafasi yake ni matumaini yetu kwamba ujumbe huo utachukuliwa kwa uzito wa kipekee,” alisema.

Hata hivyo, kwa mujibu wa Askofu, mwezi huo huo wa Agosti, Mwinjilisti wa Kimataifa wa Huduma ya Christ For All Nations (CFaN), Reinhard Bonkke anatarajiwa kuwasili nchini kwa ujumbe maalumu kwa waumini wa madhehebu ya Kikristo na  Taifa kwa ujumla.
 
Alisema, ujio wa wageni hao mashuhuri nchini, utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza shaka na wasiwasi kwa baadhi ya Wakristo ambao wako njia panda kuhusu masuala muhimu ya kiimani, ikiwa ni pamoja na suala la kuchinja.

WANASHERIA WAAPA KUWASHITAKI WASANII WA KUNDI LA ZE KOMEDY KWA KUPIGA PICHA ZA UTUPU...!!


Zile picha za kundi la Ze Komedy la linalorusha kipindi chake kupitia televisheni ya East Africa TV zinazowaonesha wasanii hao wakiwa na mabint ufukweni zimechukua sura mpya baada ya wanasheria  kuahidi kuzisaidia familia za wazaza wa mabint hao.

Wakitoa maoni yao kwa nyakati tofauti, wananchi hao wamesema" Nimeziona picha hizo kupitia mtandao wenu kweli imeniuma kama mzazi kwani huo ni unyanyasaji ambao haukubariki hata kidogo naziomba familia za mabint hao kuchukuwa hatua kali ikiwa ni pamoja na kushtaki ili iwe fundisho kwa wasanii wengine wanaopenda kudhalilisha watu wengine kwa masrahi yao binafsi" Alisema Fortunatus Kasomfi ambae ni mtanzania anaeishi nchini Afrika Kusini

Aidha nae Hawamu Juma ambae ni mkazi wa Arusha maeneo ya Unga Limited ambae ni Mwanasheria maarufu Mkoani humo alioneshwa kusikitishwa sana na tukio na kuwashauri wazazi wa wasichana hao kumtafuta kwa ajili ya kuwafungulia mashtaka wasanii hao
 
" Napenda kuwashauri wazazi wa wabinti hao kama wanahitaji msaada wa kisheria wanitafute kupitia  simu namba 0713-146416 nitawapa mawazo ya kitaalam ya kisheria ili wasanii hao wafikishwe mahakamani" Alisema Mwanasheria huyo.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MEI 26, 2013

1 a2e01
8 67be7
4 30be2

MAPACHA WATANO WALIOZALIWA WAKATI MMOJA WAFARIKI DUNIA

 Mwalimu Sofia Mgaya akiwa amelala na watoto wake wote watano  kitandani baada ya kujifungua
...............................................................................
Na Nathan Mtega,Songea

 WATOTO watano waliozaliwa kwa njia ya upasuaji katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Ruvuma kwa wakati mmoja kwa mwanamke aliyejulikana kwa jina la Sophia Mgaya(28) mkazi wa Ruhuwiko mjini Songea mkoani Ruvuma wamefariki dunia baada ya kuishi hai kwa muda wa masaa kumi.
 Akizungumza kwa njia  ya simu mganga mkuu mfawidhi wa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Ruvuma Dkt Benedict Ngaiza alisema kuwa watoto hao watano ambao walizaliwa kwa njia ya upasuaji wakiwa na umri wa miezi nane tofauti na inavyotakiwa  umri wa mtoto kuzaliwa kuwa ni miezi tisa.

DIAMOND ATOA SIRI YA MUZIKI WAKE....!!!


Mengi yamekuwa yakisemwa juu ya msanii ambae inaaminika ndiye mfalme wa muziki wa bongo fleva Wapo wanaosema anatumia nguvu za giza ikiwemo ushirikina na wapo wanaosema yuko powered na Imani ya Free mason ingawa TEENTZ tunaamini juhudi na kujituma ndiyo njia pekee ya mafanikio kwa chochote TEENTZ ilipiga story na Diamond na kueleza moja ya sababu kubwa why yuko juu na  na kila siku ananendelea kuwa juu tofauti na baadhi ya wanamzki wengine


1-"Mungu ndio kila kitu kwa maisha ya binadamu,so napenda kumtanguliza Mungu kwa kila nikifanyacho"
2-"Sipendi starehe,kutumia pesa vibaya,naiheshimu sana pesa yangu,matumizi yake makubwa ni chakula,pengine mafuta kwa ajili ya gari matumizi mengine ya mhimu kwa binadamu na zaidi naitumia pesa yangu kufanya kitu kitakachoendelea kumantain muziki wangu"

3"-Sibani pesa kwenye swala la kujijenga kimziki,niko tayali nitumie milioni kadhaa kufanya kitu kitakachojenga status yangu vizuri,mfano kugharamikia mavazi ya shows n.k"

VIKONGWE WATATU WACHINJWA KAMA KUKU NA KUCHOMWA MOTO

Matukio kama haya ya watu kujichukulia sheria mikononi na kuwauwa wenzao kwa kuwachoma moto yamekithiri katika jamii na ndiyo yaliyosababisha ajuza watatu kuuwawa kikatili usiku wa kuamkia leo huko Bunda, Mara

MAUAJI ya kikatili yametokea usiku wa kuamkia leo wilayani Bunda, mkoani Mara baada ya watu wenye hasira wa kijiji cha Kasaula kuwauwa kwa kuwachinja kama Kuku kisha kuwachoma moto ajuza watatu kwa kuwatuhumu wanajihusisha na vitendo vya kishirikina.
Pia watu hao mbali na kuwaua kikatili vibibi hivyo kwa tuhuma kwamba walimuua kijana mmoja aitwaye Sale Ligolo, walichoma moto na kuteketeza nyumba walizokuwa wakiishi wazee hao pamoja na kupora kuku waliokuwa wakiwafuga na kuatafuna kumaliza hasira zao.
Kwa mujibu wa wa taarifa ya mwandishi Masau Bwire aliyepo Bunda kwa sasa, tukio hilo limetokea usiku wa kumakia leo baada ya watu hao wenye hasira kuwasaka ajuza hao baada ya kuwepo tuhuma kwamba walishirikiana kumuua kijana huyo hivi karibuni.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...