Sunday, November 05, 2017

MAAJABU: MCHUNGAJI ATUMIA POMBE KUBATIZA WAUMINI

Mchungaji mmoja huko Afrika Kusini amekuwa akikosolewa vikali baada ya kuanza kubatiza washirika kwa kutumia vilevi ambavyo wanavipenda kitendo ambacho ni kinyume na utaratibu.

Askofu Tsietsi Makiti, (52) ambaye pia  ni Mwanzilishi wa kanisa hilo linalojulikana kama 'Gabola', amesema kuwa ameongozwa na maandiko katika Biblia ambapo Yesu alibadilisha maji kuwa divai.
"Watu wanao kunywa na kubatizwa na bia wana furaha na amani. Hii inamaanisha kuwa wanaishi katika kivuli cha Mungu, "alisema Makiti.

Kanisa hilo lenye jina 'Gabola' jina likimaanisha 'Kunywa' limesema linakubali kuwapokea waumini waliotoka makanisa mengine huku likiweka wazi kwamba idadi ya watu wameongezeka kufikia 500 ndani ya miezi miwili tangu kuanzishwa kwa kanisa hilo.

Waumini pia wanaruhusiwa kunywa wakati huduma za kanisa zikiendelea. Aidha Askofu huyo ameweka wazi kwamba ana mipango ya kuanzisha matawi ya kanisa lake hilo katika miji mbali mbali.

Saturday, October 28, 2017

TAZAMA PICHA ZA MAFURIKO YALIYOATHIRI MAKAZI YA WATU DAR ES SALAAM

Mvua kubwa ambayo imekuwa ikinyesha maeneo mengi pwani ya Tanzania imesababisha mafuriko na uharibifu mkubwa.

Katika eneo la Mji Mpya, Kawe, nyumba zimebomoka na baadhi ya maeneo hayapitiki. Nyumba zaidi ya 20 zimeharibiwa vibaya na mafuriko.

Hizi hapa ni baadhi ya picha za hali ilivyo mtaani humo.

WALIOMUINGIZA MTU MWEUSI KWENYE JENEZA AKIWA HAI WAFUNGWA

Wakulima wawili wa Afrika Kusini waliomlazimisha mtu mweusi kuingia katika jeneza akiwa hai wamehukumiwa kifungo cha miaka 10 jela.

Theo Martins na Willem Oosthuizen walihukumiwa mnamo mwezi Agosti kwa jaribio la mauaji na utekaji nyara.

Walimtuhumu Victor Mlotshwa kwa kupita katika ardhi, wakamshambulia na kumlazimisha kuingia katika jeneza na kutishia kumchoma akiwa hai.


Kesi hiyo ilizua hisia nchini Afrika Kusini na kuangazia wasiwasi wa ubaguzi wa rangi katika jamii kadhaa za wakulima.

Friday, October 27, 2017

IDADI YA WALIOPIGA KURA KATIKA UCHAGUZI WA MARUDIO NCHINI KENYA UTATA MTUPU

Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Kenya Wafula Chebukati amesema wanakadiria kwamba idadi ya waliojitokeza kupiga kura jana kufikia wakati wa kufungwa kwa vituo saa kumi na moja jioni ni asilimia 48.

Akihutubia wanahabari, mwenyekiti huyo amesema vituo 87 kati ya vituo vyote vya kupigia kura vilifunguliwa, ambavyo ni vituo 35,564.

Kati ya vituo hivyo, fomu za matokeo kutoka kwa fomu za matokeo kutoka kwa fomu 27,124 zimepokelewa.

"Vituo 5,389 ambavyo vimetapakaa kote nchini havikufunguliwa. Baadhi vimo katika kaunti nne ambazo nilitangaza awali kwamba uchaguzi umeahirishwa," amesema.

VIDEO: RAIS MAGUFULI AFANYA UTEUZI MBALIMBALI

Rais John Magufuli amemteua aliyekuwa Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilillah kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, huku aliyekuwa Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP), Ernest Mangu akiteuliwa kuwa balozi.

Dk. Kashilillah ameteuliwa ikiwa ni takriban wiki tatu kupita tangu alipoondolewa katika wadhifa wa Katibu wa Bunge, nafasi iliyochukuliwa na Stephen Kigaigai.
Rais Magufuli Mei 28,2017 alitengua uteuzi wa IGP Mangu na kumteua Simon Sirro kushika wadhifa huo. Mangu anasubiri kupangiwa kituo cha kazi pamoja na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Dk Aziz Mlima.

Monday, October 23, 2017

USHAHIDI ALIOUTOA LULU MAHAKAMANI KUHUSU KIFO CHA KANUMBA

Msanii wa filamu, Elizabeth Michael (22) amejitetea katika kesi ya kuuwa bila kukusudia katika Mahakama Kuu ya Tanzania.

Katika utetezi wake, Lulu amesema anakumbuka siku ya tukio ilikuwa Ijumaa ya April 6, 2012 ambapo aliahidiana na rafiki zake kwamba wangetoka usiku.

Amesema kuwa asubuhi ya siku hiyo alienda kuonana na rafiki zake maeneo ya Mikocheni, ambapo pia alikuwa akiwasiliana na Kanumba.

"Marehemu alikuwa ni msanii mwenzangu lakini pia nilikuwa naye na mahusiano naye ya kimapenzi,".

Lulu alisema kuwa marehemu Kanumba alikuwa hapendi kumuona akitoka, hivyo hadi siku ya tukio hakutaka kumwambia kwamba atatoka na rafiki zake.

Sunday, October 08, 2017

KIM JONG-UN AMPANDISHA CHEO DADA YAKE

Kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong-un, amempandisha cheo dada yake mdogo, na kumpa madaraka zaidi katika chama tawala cha wafanyakazi.

Kim Yo-jong, anayeaminika kuwa na umri wa zaidi ya miaka 26 amekuwa mjumbe katika kamati kuu ya chama, ambalo ni baraza kuu la uamuzi linalojulikana kama politburo.

Bi Kim Yo-jong alipewa kwanza wadhifa wa kuwa afisa wa wa cheo cha juu wa chama, miaka mitatu iliyopita.

Familia ya Kim, imeongoza Korea Kaskazini, tangu nchi hiyo ilipoundwa, mwaka wa 1948.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI OKTOBA 08, 2017 YA MICHEZO, DINI NA HARDNEWS





POLISI YADAI PANYA NDIO WALIOKULA MADAWA YA KULEVYA YALIYOKAMATWA

Police katika mji wa Mumbai nchini India wanawalaumu panya kwa kutoweka kwa kilo 34 za dawa za kulevya kwa jina Ketamine.

Wanasema wanawatuhumu panya hao kwamba ndio wa kulaumiwa baada ya kupata mabagi hayo yalitobolewa kwa chini.

Uchunguzi wa miaka mitatu umekamilika kwamba iwapo ingekuwa binadamu wangechukua mabagi yote.

Dawa hizo zilizohifadhiwa katika ghala moja la serikali zilikuwa miongoni mwa kilo 200 za mihadarati zilizopatikana na walanguzi wa mihadarati 2011.

Hii sio mara ya kwanza kwa maafisa wa polisi nchini India kuwalaumu panya kwa kutoweka kwa mihadarati iliokamatwa.

Saturday, October 07, 2017

RAIS MAGUFULI AFANYA MABADILIKO YA BARAZA LA MAWAZIRI





'KUNA UWEZEKANO WA KUFANYIKA MAPINDUZI NCHINI ZIMBABWE' GRACE MUGABE

Mke wa rais Robert Mugabe, Grace Mugabe ameonya kwamba kuna uwezekano wa kufanyika kwa mapinduzi huku kukiwa kuna wasiwasi mkubwa nchini humo kuhusu harakati za kumrithi rais Mugabe.

Anasema kuwa washirika wa makamu wa rais Emmerson Mnangangwa wanatishia maisha ya wale ambao hawamuungi mkono kumrithi rais Robert Mugabe mwenye umri wa miaka 93.

Bi Mugabe yeye binafsi na bwana Mnangagwa wako kifua mbele na uadui wao umekigawanya chama tawala cha Zanu PF .

Mgogoro huo unajiri baada ya bwana Mgangagwa kudai kwamba aliwekewa sumu katika chakula chake mwezi Agosti.

Wafuasi wake wamesema kuwa wapinzani wake ndani ya Zanu PF ndio wakulaumiwa, ijapokuwa bwana Mnangagwa amejitenga na madai kama hayo.

Alikiambia chombo cha habari cha taifa hilo anasalia kuwa mtiifu kwa rais Mugabe.

Bi Grace Mugabe aliyekasirika alimshutumu bwana Mnangagwa katika hafla moja mjini Harare.

''Tunatishiwa usiku na mchana kwamba iwapo mtu fulani hatokuwa rais , tutauawa'', alisema.

MAREKANI YAIONDOLEA VIKWAZO SUDAN

Marekani imeiondolea vikwazo Sudan ikisema taifa hilo la Afrika lilikuwa limeanza kuangazia maswala kuhusu kukabiliana na ugaidi pamoja na ukiukeaji wa haki za kibinaadamu dhidi ya raia wanaoishi katika jimbo la Darfur.

Uamuzi wa kuiondolea vikwazo na kusitisha vikwazo vya kiuchumi wa taifa hilo unajiri baada ya utawala wa Trump mwezi uliopita kuliondoa taifa hilo katika mataifa ambayo raia wake wamewekwa vikwazo vya kusafiri.

Sudan ndio taifa la pekee ambalo liliondolewa katika orodha hiyo. Lakini uamuzi huo unaviacha vikwazo vingine kuendelea kwa sasa ikiwemo vile dhidi ya watu binafsi walio na agizo la kukamtwa kufuatia unyanyasaji uliofanyika katika eneo la Darfur.

Friday, September 29, 2017

OFISI YA BUNGE YAKANUSHA MBOWE KUNYANG'ANYWA GARI

Ofisi ya Bunge imekanusha kumnyang’anya gari mbunge Freeman Mbowe na kuwa linatafutiwa kibali kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi ili Mbowe akalitumie Nairobi.

GAZETI LA MWANANCHI LATAKIWA KUOMBA RADHI

Serikali ya mapinduzi Zanzibar imewaagiza Wahariri wa Gazeti la Mwananchi kuomba radhi Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati (ZURA) ndani ya saa 24 kuanzia saa 9:00 Alasiri ya jana Septemba 28, 2017.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyotolewa naNaibu Mkurugenzi Idara ya Habari (MAELEZO) Zanzibar, Dk. Juma Mohammed Salum ambapo amesema iwapo wahusika hawatafanya hivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya gazeti hilo la Mwananchi.

Hatua hiyo imekuja baada ya Serikali kudai gazeti hilo la Mwananchi linalochapishwa na kampuni ya Mwananchi Communications Limited Septemba 27, 2017 kuchapisha makala katika Ukurasa wake wa 16 yenye kichwa cha habari kisemacho “Siri ya nini Zabuni ya Mafuta Zanzibar”?

Salum amefafanua kuwa makala hiyo licha ya kujenga picha kwamba hakuna uwazi katika Zabuni ya uletaji Mafuta Zanzibar,msingi na maudhuhi ya Makala yenyewe kwa ujumla ni upotoshaji wa makusudi kwa nia ya kuipaka matope Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Taarifa hiyo pia licha ya kuwataka wahariri wa gazeti hilo kuomba radhi pia imefafanua ukweli wa mambo yalivyo kwa sasa ambapo Serikali, kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar (ZURA) tayari imeanzisha mfumo mpya wa uletaji Mafuta Zanzibar tangu Septemba Mosi, 2017.

Saturday, September 09, 2017

WATOTO WALIOPO TUMBONI WAKUTWA NA MATATIZO YA MOYO

Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Naiz Majani.
 
JUMLA ya wajawazito 35 wamefamyiwa  uchunguzi wa kipimo cha magonjwa ya moyo kwa watoto wachanga waliopo tumboni mwa mama zao (FETAL ECHOCARDIOGRAPHY) ili kujuwa kama wanamatatizo ya moyo au la.

Majibu ya kipimo hicho yalionyesha kuwa kati ya hao watoto watano walikutwa na matatizo ya moyo jambo ambalo litawawezesha   kupata matibabu mapema pindi watakapozaliwa.

Hayo yamesemwa na Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Naiz Majani wakati akiongea na waandishi wa habari hivi karibuni.

Dkt. Naiz alisema kipimo hicho hakina madhara yoyote kwa mama na mtoto na kina  uwezo wa kugundua endapo mtoto ameathirika na ugonjwa wa moyo na hivyo kumuandaa mama mjamzito kwaajili ya uzazi salama.

“Mojawapo ya dalili za mama mjamzito ambazo zinaweza pelekea kupata mtoto mwenye  tatizo la ugonjwa wa moyo ni pamoja na ugonjwa wa kisukari,shinikizo la damu,matumizi ya dawa za muda mrefu,mimba ya mapacha, kuwepo na mtu mwenye tatizo la moyo katika familia na mimba pandikizi”.

“Ninawaomba kina mama wajawazito wenye moja ya dalili nilizozitaja waje tuwafanyie kipimo hiki  kipindi  ambacho mimba zao zitakuwa na umri wa kati ya miezi minne hadi saba hii itawasaidia  kugundua afya za watoto wao na kuepuka na  vifo vya mara  baada ya kuzaliwa vinavyotokea kipindi cha mwezi mmoja hadi  mwaka”, alisema Dkt. Naiz.

Alizitaja changamoto wanazokabiliana nazo kuwa ni pamoja na uelewa mdogo wa kinamama wajawazito juu ya kipimo hicho kwa kufikiria kuwa kinamadhara  jambo ambalo siyo kweli kwani kipimo hicho hakina  madhara yoyote kiafya.

Taasisi ya Moyo  Jakaya Kikwete (JKCI) ilianza kutoa huduma hiyo tangu mwezi wa tatu mwaka huu ili kupunguza  vifo vya watoto vinavyotokana na  magonjwa ya moyo mara baada ya mtoto kuzaliwa.
Na Sweetbert Hudson.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...