Wednesday, July 12, 2017

DIWANI MWINGINE WA CHADEMA ARUSHA, AJIUZULU LEO







Hali si shwari tena ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Kaskazini, baada ya diwani mwingine wa chama hicho, Japhet Jackson kuandika barua ya kujiuzulu udiwani na kujiunga na CCM.

Diwani huyo ni wa saba kujiuzulu ndani ya mwezi mmoja, katika Jimbo la Arumeru Mashariki na Jimbo la Arusha mjini, majimbo ambayo wabunge wake ni Joshua Nassari na Godbless Lema.

Jackson amewasilisha barua leo mchana ya kuhama Chadema kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Meru, Christopher Kazeri na kueleza anamuunga mkono Rais John Magufuli.

KLABU YA EVERTON YAWASILI NCHINI, WAYNE ROONEY YUMO.

Klabu ya Everton tayari imewasili Jijini Dar es Salam asubuhi ya leo ikitokea nchini Uingereza nakupokelewa na Waziri wa Habari Dr. Harrison Mwakyembe, huku ikiwakosa wachezaji wake watatu muhimu katika kikosi hicho kutokana na majeruhi waliyokuwa nayo.

Pamoja na hayo, timu ya Everton imeongozwa na mchezaji nyota Wayne Rooney pamoja na Davy Klaassen na Michael Keane ambao pia wamejiunga na klabu hivi karibuni.

 Like page yetu ya facebook/jambotz pia tu-follow Instagram @jambotz.

Tuesday, July 11, 2017

DIWANI WA CHADEMA ARUSHA AJIUZULU NA KUMUUNGA MKONO MAGUFULI

Diwani wa Ngabobo (Chadema), Solomon Laizer ameandika barua ya kujiuzulu udiwani na kujiunga na CCM kwa maelezo anamuunga mkono Rais John Magufuli.

Laizer ni diwani wa tano katika Halmashauri ya Meru kujiuzulu kwa kutoa sababu kuwa anamuunga mkono Rais Magufuli.

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, Christopher Kazeri amethibitisha leo (Julai 11) kupata taarifa za kujiuzulu kwa Ngabobo.

Mbunge wa Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Nassari amesema kujiuzulu kwa diwani huyo ni mchezo mchafu akidai  amenunuliwa.

Wednesday, July 05, 2017

MSHINDI WA KUCHORA NEMBO YA EAC KUNYAKUA KITITA CHA DOLA 25,000

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Kikanda na Kimataifa, imewataka vijana wenye uwezo wa kubuni na kuchora kujitokeza kushiriki shindano la kubuni nembo mpya ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Msemaji wa wizara hiyo,  Mindi Kasiga amesema shindano hilo ni fursa kwa vijana kuonyesha uwezo wao, pia kujipatia kipato iwapo watashinda. 

Shindano hilo limeanza Juni Mosi na mwisho ni Agosti 31.

Tuesday, July 04, 2017

MAGUFULI AZITAKA NGO'S ZINAZOTETEA WANAFUNZI WENYE MIMBA WAFUNGUE SHULE ZAO

Rais John Magufuli amezitaka Asasi za Kiraia (NGO’s) kufungua shule kwa wanafunzi wanaopata mimba shuleni kama kweli zinawapenda wanafunzi hao.

Rais ameyasema hayo leo (Jumanne, Julai 4) alipokuwa akihutubia wakati wa uzinduzi wa mradi wa maji Sengerema.

“Si kwamba nawachukia wenye mimba, hata kwa bahati mbaya akapata mimba, kama hizo NGO zinawatetea sana, zifungue shule za wenye mimba, kwa sababu zinawapenda wenye mimba, wafungue shule zao,”amesema Rais leo.

Amesema hata hao wanaofanya makongamano ya kuhamasisha watu wapate mimba wafungue shule zao kwa ajili ya wanafunzi hao.

“ Haiwezekani fedha za walipa kodi, Sh 17 bilioni kila mwaka za kusomesha watoto wetu, kwenda kusomesha wakinamama, wazunguke, waimbe, waseme nini mimi ndiyo Rais, huo ndio ukweli,” amesema.

Amesema tatizo si wanaopata mimba, kwani wapo waliopata matatizo, kama kuugua kwa muda mrefu wakashindwa kwenda shule lakini ulianzishwa mpango maalum wa kuwasomesha katika mfumo usio rasmi.

KINGA YA UKIMWI YAANZA KUONESHA MAFANIKIO

Utafiti wa kinga ya kuzuia maambukizi ya virusi vya  Ukimwi, ulioanza kufanywa nchini miaka kadhaa iliyopita umeana kuonyesha mafanikio.

Lakini watafiti wamesema Watanzania watahitaji kuwa uvumilivu wa miaka michache ijayo kusubiri hatua za mwisho za ukamilishaji utafiti wa kinga hiyo kabla haijaanza kutimika rasmi.

Taarifa hizo zinakuja ikiwa wiki moja baada ya Kenya kuwa nchi ya kwanza barani Afrika kuanza kutumia dawa ya ugonjwa wa Ukimwi ambayo inaweza kuboresha afya na kurefusha maisha ya maelfu ya watu ambao wanasumbuliwa na magonjwa nyemelezi na ambayo hayakubali tiba nyingine.

Kwa miaka kadhaa  Chuo Kikuu cha Afya na Tiba Muhimbili (MUHAS) imekuwa ikiendesha utafiti kuhusiana na chanjo ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi na katika hatua ya awali utafiti huo uliwahusisha baadhi ya watu wanaishi na virusi hivyo.

TIMU YA SINGIDA UNITED YAONESHA JEURI YA PESA, YANUNUA BASI LA MILLION 350/-

Baada ya kupata udhamini mnono kutoka katika kampuni ya michezo ya kubashiri ya SportPesa hatimaye klabu ya Singida United inazidi kutanua misuli yake katika ligi kuu ya Tanzania Bara kwa kutambulisha usafiri wao utakao tumika katika kusafirishia wachezaji.
 Akizungumza na waandishi wa habari jana katibu Mwenezi wa klabu hiyo Festo Sanga amethibitisha Singida United kununua Basi jipya lenye gharama ya shilling milioni 350.

Sunday, July 02, 2017

MTANGAZAJI WA AZAM TV ALIEPOTEA APATIKANA

Mtangazaji wa Kituo cha Televisheni cha Azam, Fatna Ramole amepatikana ikiwa ni saa 48 baada ya kudaiwa kutoweka.

Ndugu yake, Lulu Ramole amezungumza na mwandishi wa habari hii jana (Julai mosi) na kueleza kuwa kwa sasa yeye na Fatna wapo kituo cha Polisi, Kinondoni.

Lulu aliandika katika ukurasa wake wa twitter leo saa nane mchana akiwashukuru Watanzania kwa ushirikiano waliompa hadi dada yake kupatikana.

“Msamaria alitupigia simu amepatikana Makongo, nipo naye lakini siwezi kueleza kwa undani alivyopatikana, uchunguzi unaendelea,” amejibu kwa kifupi Lulu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Suzan Kaganda amethibitisha kupatikana kwa Fatna, lakini kwa maelezo na ufafanuzi zaidi alishauri familia ya mwanahabari huyo iulizwe.

“Lakini tutawaita hapa kwa mahojiano zaidi,” amesema

WABUNGE UJERUMANI WAIDHINISHA NDOA YA JINSIA MOJA

Wabunge nchini Ujerumani wameidhinishwa, kwa wingi wa kura, sheria ya kuhalalisha ndoa za wapenzi wa jinsia moja.

Wamefanya hivyos iku chache baada ya Kansela Angela Merkel kuondoa upinzani wake dhidi ya mpango huo.

Chini ya mabadiliko hayo sasa, wapenzi wanaotaka kuoana ambao awali walikubaliwa tu kuwa na ushirika, hadhi ya ndoa kamili na wana haki ya kuasili watoto.

TRUMP: TUMECHOKA KUIVUMILIA KOREA KASKAZINI

Rais wa Marekani, Donald Trump amesisitiza kwamba muda wa kimkakati wa uvumilivu kwa Korea Kaskazini umekwisha.

Katika hotuba ya pamoja juzi, akiwa na mwenzake wa Korea Kusini, Moon Jae katika bustani ya Rose kwenye Ikulu ya White house, Trump aliahidi ‘kuchukua hatua madhubuti’ dhidi ya programu ya nyuklia na makombora ya Korea Kusini akisema vitisho vyake vinafaa kupatiwa majibu ya kijasiri.

“Hizi si zama za kuvuta subira juu ya Serikali ya Korea Kusini ambayo imeshindwa kutekeleza wajibu wake,” alisema Trump.

Tuesday, June 27, 2017

'MARUFUKU CHAKULA KUSAFIRISHWA NJE YA NCHI' MAJALIWA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amepiga marufuku usafirishaji wa chakula nje ya nchi bila kibali na kuwataka wafanyabiashara kuuza chakula kwenye maeneo yenye uhaba nchini.

Majaliwa ametoa agizo hilo jana, Jumatatu wakati akihutubia Baraza la Eid katika Msikiti wa Masjid Riadha mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.

Waziri Mkuu huyo amesema kuwa kuna maeneo ambayo wananchi hawakupata chakula vizuri kutokana na uhaba wa mvua hivyo wafanyabiashara wapeleke chakula kwenye maeneo hayo.

“Serikali bado haijatoa kibali cha kutoa chakula nje ya nchi, kama unaona kuna umuhimu kaombe kibali, lakini utapewa kibali cha kusaga upeleke unga na siyo mahindi,”amesisitiza  Majaliwa.

Majaliwa ameonya kuwa kwa wale watakao kamatwa wakisafirisha mahindi nje ya nchi kinyume na utaratibu, mahindi hayo yatataifishwa na kupelekwa kwenye ghala la Taifa na magari yatapelekwa polisi.

Amesema kuwa Serikali imepokea barua za maombi ya kupeleka chakula nchi jirani, lakini bado haijatoa ruhusa.

Monday, June 26, 2017

JAMBO TZ INAWATAKIA EID MUBARAK WAISLAMU WOTE DUNIANI

Uongozi na wafanyakazi wote wa Jambo Tz Blog wanawatakia watanzania wote kwa ujumla Eid Mubarak na mapumziko mema katika sikukuu ya Eid El Fitr.

Sunday, June 18, 2017

OLE SENDEKA AWAKUBALI WAPINZANI MSIBANI KWA MAMA YAKE

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Christopher Ole Sendeka amesema tofauti za itikadi za kisiasa zisitumike kuwagawa Watanzania, bali ziwe chachu ya kufanikisha maendeleo.

Ole Sendeka aliyasema hayo jana, wakati wa kuaga mwili wa mama yake Raheli Sendeka kwenye ibada iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Engarenarok jijini Arusha.

Alisema baada ya kutokea kwa msiba huo, viongozi wa kwanza kufika nyumbani kwake kumpa pole walikuwa mbunge na diwani wa Chadema, hivyo amepata somo kuwa tofauti za kisiasa hazipaswi kuondoa umoja na upendo wa Watanzania. Alisema mbunge wa kwanza kufika nyumbani kwake Ngarenaro jijini hapa ni wa Siha mkoani Kilimanjaro (Chadema), Dk Godson Mollel na diwani wa Ngarenaro (Chadema), Issaya Doita.

MAJERUHI WA LUCKY VINCENT KUREJEA NCHINI MWEZI WA NANE

Watoto watatu walionusurika katika ajali iliyoua wanafunzi 32, walimu wawili na dereva wa Shule ya Lucky Vincent ya mjini Arusha, huenda wakaruhusiwa kurejea nchini baada ya miezi miwili.

Taarifa hiyo imetolewa na Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu katika mtandao wake wa kijamii wa Facebook.

Pia, Nyalandu ameandika katika mtandao huo kuwa watoto hao; Doreen Mshanga, Saidia Ismael na Wilson Tarimo wanategemewa kutembea tena.

Hata hivyo, kwa sasa Doreen, atahamishiwa katika kituo maalumu kwa ajili ya matibabu ya uti wa mgongo cha Madonna katika mji wa Lincoln, Nebraska.

“Katika watoto wote hao watatu, Doreen ni muujiza mkubwa zaidi,” amesema Nyalandu.

UTHAMINI MOYO WAKO, KAA MBALI NA MAUMIVU

HAKUNA ubishi kuwa mapenzi yanachukua nafasi kubwa sana katika maisha ya binadamu, ipo dhahiri kwamba mapenzi yanaweza kuleta furaha maishani mwako lakini wakati huohuo  maumivu, mateso na karaha.

Watu wengi bado wanalizwa na mapenzi na hii ni kwa sababu hawafuati kanuni sahihi za mapenzi. Ndiyo… mapenzi yana kanuni zake.

Kwa bahati mbaya kabisa, kwa sasa mapenzi yamegeuzwa na kuwa kama kitu cha kujaribu au kufanyia biashara ndiyo maana yanawatesa wengi.

Lakini ni kwa nini mapenzi yaendelee kututesa?  Au ni kwa sababu hatujui maana halisi ya mapenzi? Hebu tuyaangalie mapenzi kwa jicho la tatu, kisha tuchukue hatua.

MAPENZI NI NINI?
Katika hali ya kawaida, mapenzi hayaelezeki kuwa ni nini. Ni vigumu sana mtu kukueleza maana ya mapenzi ndiyo maana kila mtu ana uelewa tofauti juu ya suala hilo.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...