Wednesday, July 05, 2017

MSHINDI WA KUCHORA NEMBO YA EAC KUNYAKUA KITITA CHA DOLA 25,000

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Kikanda na Kimataifa, imewataka vijana wenye uwezo wa kubuni na kuchora kujitokeza kushiriki shindano la kubuni nembo mpya ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Msemaji wa wizara hiyo,  Mindi Kasiga amesema shindano hilo ni fursa kwa vijana kuonyesha uwezo wao, pia kujipatia kipato iwapo watashinda. 

Shindano hilo limeanza Juni Mosi na mwisho ni Agosti 31.



“Shindano hili limezinduliwa mwezi uliopita pale Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kigezo ni vijana wenye umri kati ya miaka 18 na 35 wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wote wanaruhusiwa kushiriki,” amesema Kasiga leo (Julai 5).

Amesema kuzindulia shindano hilo chuo kikuu haimaanishi kuwa shindano hilo linalenga wanafunzi pekee, bali vijana wote wenye uwezo wa kubuni kwa njia yoyote si lazima iwe ya kompyuta.

“Tunahitaji wajitokeze kwa wingi, hili ndilo linatoa nafasi nzuri ya kushinda, sisi katika jumuiya tunafanya mambo mengi na tuna umuhimu, tuna eneo kubwa kuliko nchi zingine wanachama, makao makuu yapo huku, vijana wajitokeze ili waweze kupata fedha za ushindi zilizoandaliwa,” amesema Kasiga.

Amesema mshindi wa kwanza atazawadiwa Dola 25,000 za Marekani (Sh55 milioni) wa pili atapewa Dola 5,000 (Sh11 milioni) na wa tatu Dola 2,500 (Sh5.5 milioni).

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...