Tuesday, June 13, 2017

LISSU AMGEUKIA KIKWETE ATAKA NAE AJUMUISHWE KWENYE ORODHA YA WASHTAKIWA WA MAKINIKIA.

Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu ameipa changamoto Serikali kwa kuitaka kumuingiza Jakaya Kikwete katika orodha ya watuhumiwa wa sakata la makinikia.

Akichangia bungeni leo Jumanne, katika hotuba ya bajeti ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2017/18, Lissu amesema kuwa wakati wa kusaini mikataba ya madini Kikwete alikuwa ni Waziri wa Maji, Nishati na Madini.

“Katika taarifa hii ya jana wamependekeza watu fulani fulani washtakiwe makamishna, mwanasheria mkuu, Andrew Chenge (Mbunge wa Bariadi), Wiliam Ngeleja (Sengerema) jamani naombeni niwaambie kitu ili  wabunge muwe na maarifa,” amesema na kuongeza:

“Mtu wa kwanza kusaini mikataba na leseni za madini alikuwa ni Meja Jakaya Mrisho Kikwete, Agosti 5 mwaka 1994 alisaini leseni ya Bulyankulu inayopingwa leo hii wakati akiwa Waziri wa Maji, Nishati na Madini wakati huo hakuwa na kinga ya urais.”

Amesema wakati aliposaini leseni na mikataba hiyo alikuwa hana kinga kwa masuala ambayo aliyafanya.

“Rais (Kikwete) alisaini si ya Bulyankulu pekee ya Nzega, ya Geita hizo leseni zina saini ya Kikwete anaponaje kwa mapendekezo haya? Anaponaje kama kweli mnataka kuwashughulikia watu walioshiriki kwenye mambo haya?” amehoji.

“Mbona mnachagua chagua hizi? Leseni na hizi sheria tangu mwaka 1999 tumesema tatizo kubwa ni sheria.”

Amemtaka Spika wa Bunge, Job Ndugai kama anataka kukumbukwa wakati wa uongozi wake basi asikubali kupitisha miswada ya sheria kwa hati ya dharura.

Akijibu swali hilo, Ndugai amesema atairuhusu miswada hiyo ya madini na gesi iingie bungeni kwa hati ya dharura.

“Kwanza wanaoamua siyo mimi tu ni kamati ya uongozi ya Bunge, lakini kama itakuja kwa hati ya dharura hii (madini) itaruhusiwa kwasababu moja tu tunaibiwa sana.” amesema.

Wednesday, June 07, 2017

SHILOLE: WATOTO WANGU HAWATAIGA MAISHA YANGU


MSANII wa muziki wa Bongo Fleva, Zuwena Mohamed ‘Shilole’, amesema kwamba watoto wake hawataiga maisha wala mavazi anayovaa kwenye shoo zake wala maisha ya sanaa anayoishi kwa kuwa wanatambua yupo kazini kwa ajili yao.

Shilole akiongea na mwandishi wa habari hii alisema kwamba, malezi anayowalea watoto wake ni tofauti na maisha anayoishi yeye na watoto hao wanatambua kwamba mama yao ni msanii hivyo hawataiga anachofanya.

 “Watoto wangu nawalea katika maadili kama mama, siwezi kuwalea maisha ya kistaa kama ninavyoishi mimi na wanatambua kwamba mama yao nipo kazini kwa ajili yao na pia hawana ndoto za kuishi maisha yangu ya kisanii,” alieleza Shilole.

Shilole aliongeza kwamba licha ya kulea watoto wake kwa maadili ya dini, lakini hataacha kuendelea kuwapa elimu, mafunzo ya maisha na biashara.

HUDDAH: SITAKI KUOLEWA

MWANAMITINDO maarufu nchini Kenya, Huddah Monroe, amefunguka na kusema kwamba hana mpango wa kuolewa katika maisha yake.

Mrembo huyo ambaye hakauki mitandaoni, amekuwa akihusishwa kutoka na nyota wa soka wa timu ya Taifa ya Kenya na klabu ya Tottenham ya nchini England, Victor Wanyama, lakini amekuwa akikana taarifa hizo na sasa ametangaza kwamba hana mpango wa kuolewa kwenye maisha yake.

“Kila mtu ana mipango yake, hivyo kwa upande wangu sina mpango wowote wa kuolewa. Hata hivyo, kama itakuja kutokea nikaolewa hatakuwa mwanamume wa Nigeria.

“Maana kuna taarifa kwamba natoka na Wizkid, sikushangaa sana kwa kuwa niliwahi kuposti picha nikiwa na msanii huyo nilipokutana naye nchini Marekani, picha hizo zikaleta maneno mengi nina uhusiano naye wa kimapenzi hakuna ukweli na sitaolewa na mwanamume wa Nigeria,” alisema Huddah.

ACT WAZARENDO WAMVUA CHEO MAMA MGHWIRA

Chama cha ACT Wazalendo kimmevua uongozi aliyekuwa mwenyekiti wake, Anna Mgwhira ambaye ameteuliwa na Rais John Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.

Chama hicho kimefikia hatua hiyo kwa kuzingatia ibara ya 17 ya katiba yake ambayo inatamka kuwa kiongozi wa chama atakoma kuendelea na madaraka yake iwapo atashindwa kutekeleza majukumu yake.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatano, Kaimu Kiongozi wa ACT, Samson Mwingamba alisema kamati ya uongozi wa ACT ulikutana leo lengo kuu ni kutafakari lililotokea kuona namna gani Mgwhira anaweza kutimiza majukumu yake kama Mwenyekiti na Mkuu wa Mkoa.

“Kama chama baada ya kutafakari kwa kina na baada ya mashauriano baina yake na viongozi kutumia katiba ya chama anakoma kuwa kiongozi kwa kuwa kutakuwa na mgongano wa majukumu, maslahi hivyo anakoma kuwa mwenyekiti,” alisema Mwigamba.

Mwigamba alisema kamati ya chama imemchagua Yeremia Maganja kuwa  Kaimu Mwenyekiti na kamati ilimpongeza Rais Magufuli kwa kumteua Mgwhira.

Hata hivyo, Mwigamba alisema Mghwira bado ataendelea kuwa mwanachama halali wa chama hicho.

Saturday, June 03, 2017

WEMA SEPETU ABADILISHIWA HATI YA MASHTAKA

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeanza kusikiliza kesi inayomkabili msanii wa filamu, Wema Sepetu na wafanyakazi wake wawili, huku upande wa mashtaka ukiiomba mahakama hiyo kubadili hati ya mashtaka.

Akiwasilisha hoja hiyo juzi mbele ya Hakimu Thomas Simba, Mawakili upande wa jamhuri, Constantine Kakula na Paulina Fungameza, walianza kuwasomea  upya mashtaka washtakiwa hao ambao ni Wema Sepetu na wafanyakazi wake wawili, Angelina Msigwa na Matrida Abas.

Alidai shtaka la kwanza linalowakabili watuhumiwa hao ni pamoja na kukutwa na kiwango kidogo cha dawa za kulevya ambapo mnamo Februari 4, mwaka huu katika maeneo ya Kunduchi Ununio, washtakiwa hao kwa pamoja wanadaiwa kukutwa na msokoto mmoja na vipisi vya dawa za kulevya aina ya bangi yenye gramu 1.08.

MNYIKA ATOLEWA NJE YA BUNGE KWA AMRI YA SPIKA

Mbunge wa Kibamba, John Mnyika ametolewa nje ya Bunge jana Ijumaa kwa agizo la Spika wa Bunge, Job Ndugai.

Licha ya adhabu hiyo, amemzuia kutohudhuria vikao vya Bunge kwa siku saba kuanzia hiyo jana.

Mnyika ametolewa baada ya mmoja wa wabunge kusema 'Mnyika mwizi' akimhusisha na wizi wa madini, hoja inayochangiwa na wengi kwenye mjadala wa Wizara ya Nishati na Madini unaoendelea.

Kutokana na hali hiyo Mnyika alimtaka Spika kuchukua hatua kwa mbunge aliyesema kuwa yeye ni mwizi lakini Spika akasema hajui hilo na haijaingia kwenye hansadi. Hata hivyo Mnyika alisisitiza kuwa mambo hayaweze kwenda hivyo.

Baada ya majibizano kati yake na Spika, Spika akaamuru walinzi wamtoe Mnyika nje ya Bunge na asihudhurie vikao saba vinavyofuata.

Mnyika alikuwa akitoa maelezo baada ya Mbunge wa Mtera, Livingston Lusinde kusema upinzani wa Tanzania ni wa ajabu kwani unatetea wezi wa madini.

Saturday, May 27, 2017

JAMBO TZ INAWATAKIA KHERI NA SWAUM NJEMA WAISLAMU WOTE DUNIANI


MAMBO YANAYOPENDEZA KATIKA MWEZI WA RAMADHANI


Allah (Subhaanahu wa Ta’ala)  alipanga kuwa mwaka uwe na miezi kumi na mbili, na katika hiyo akaichagua baadhi akaitukuza na kuifadhilisha zaidi ya mengine.

Mwenyezi Mungu anasema;

“Hakika idadi ya miezi mbele ya Allah ni miezi kumi na mbili kati ya hiyo mna mine iliyo mitukufu."

Nayo ni (Dhulqaada, Dhulhijja, Muharram, na Rajab).

Baada Allah (Subhaanahu wa Ta’ala) kuifadhilisha miezi hii minne akaufadhilisha vile vile zaidi kuliko hata miezi hii minne mwezi tuliyo ndani yake nao ni mwezi wa Ramadhani, usiku wa cheo (Laylatul Qadr), katika mwezi huu, tokeo kubwa ni kuteremshwa kwa Qurani.

Kwa ilivyokuwa mwezi huu ndio bora wa miezi yote, hivyo basi mema yafanywayo ndani yake yanakuwa ni bora na yanalipwa ziada kuliko miezi mengine. Hivyo basi inatakiwa kwa muislam kujibidiisha katika kufanya mema na kuepuka  mabaya hasa awapo katika mwezi huu mtukufu. Baadhi ya mambo tutakiwayo kuyatekeleza:

1. Kusoma Qurani

 Amesema Allah (Subhaanahu wa Ta’ala);

“Mwezi wa Ramadhani ambayo imeteremshwa ndani yake Qur-an hali ya kuwa ni uongofu kwa watu …………"

Friday, May 26, 2017

MAJERUHI WAWILI WA LUCKY VICENT WARUHUSIWA KUTOKA HOSPITALI

Watoto wawili majeruhi wa ajali ya gari la Shule ya Lucky Vincent wameruhusiwa kutoka hopitalini.

Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu ameandika katika ukurasa wake wa Facebook kuwa watoto hao, Sadia Ismael na Wilson Tarimo waliokuwa wamelazwa katika hospitali ya Mercy ya Marekani wameruhusiwa na sasa wapo katika makazi mapya.

“Watoto Sadia na Wilson waruhusiwa rasmi kutoka hospitali ya Mercy  na wanaelekea kwenye makazi yao mapya mjini Sioux City IA. Mungu azidi kuwaangazia nuru ya uso wake. Amani iwe nawe na Nesi wetu mpendwa kwa huduma kubwa mmefanya kwa watoto hawa na Tanzania,”ameandika Nyalandu.

Jana Nyalandu aliandika kuwa mtoto Doreen ataendelea kuwepo hospitali katika wodi ya watoto akiendelea kupata huduma za karibu hadi itakapoamuliwa vinginevyo.

MTOTO ALIYEISHI KWA KULA MAFUTA ATAMANI KUWA DAKTARI BINGWA

MTOTO Shukuru Kisonga (16) ambaye ameishi muda mrefu kwa kula sukari robo tatu, mafuta ya kula lita moja na maziwa lita tatu, amesema ndoto yake ni kuwa daktari bingwa wa magonjwa ya damu.

Shukuru alisema hayo jana alipozungumza na mwandishi wa habari hii kuhusu maendeleo ya afya yake na kuongeza kuwa ataongeza juhudi katika masomo yake afikie ndoto yake hiyo.

"Niliteseka muda mrefu, namshukuru Mungu sasa sijambo naendelea na matibabu wodini, nikiruhusiwa kurejea nyumbani nitaongeza juhudi katika masomo yangu nitimize ndoto yangu ya kuwa daktari bingwa wa magonjwa ya damu, " alisema.

Shukuru alisema anataka kuwa daktari bingwa wa magonjwa ya damu   awasaidie watu wengi hasa wanaoteseka na ugonjwa kama unaomsumbua yeye.

" Namshukuru daktari wangu hapa Hospitali ya Taifa Muhimbili, amenisaidia mno ndiyo maana na mimi ninataka kuwa kama yeye   niweze kuwasaidia wengine wanaougua Mungu akinijalia, " alisema.

Daktari Bingwa wa magonjwa ya damu, Stella Rwezaula, juzi alisema mtoto huyo anaugua selimundu, ugonjwa ambao amezaliwa nao baada ya kurithi vinasaba kutoka kwa wazazi wake.

Thursday, May 25, 2017

RIPOTI YA MCHANGA YAONESHA NCHI ILIVYOLIWA

 Kamati maalumu iliyoundwa na Rais John Magufuli kuchunguza mchanga wa madini, imebaini kwamba makontena 277 yaliyozuiliwa katika Bandari ya Dar es Salaam yana tani 7.8 za dhahabu yenye thamani ya kati ya Sh676 bilioni na Sh1.147 trilioni.

Rais John Magufuli akizungumza awali alisema kiwango cha juu kinaweza kufika tani 15.5.

Kiwango hicho ni tofauti na kile ambacho kamati hiyo ilielezwa na Wakala wa Ukaguzi wa Madini (TMAA), kwamba makontena hayo yalikuwa na tani 1.1 za dhahabu yenye thamani ya Sh97.5 bilioni.

Kutokana na tofauti iliyopo kati ya taarifa ya TMAA na hali halisi, kamati hiyo iliyokuwa na wajumbe wanane imebaini kwamba Taifa limekuwa likiibiwa kupitia usafirishaji wa mchanga wa madini (makinikia).

Akitoa muhtasari wa kamati hiyo Ikulu jijini Dar es Salaam jana, kabla ya kumkabidhi Rais Magufuli ripoti ya uchunguzi, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Profesa Abdulkarim Mruma alisema kamati yake ilipewa hadidu za rejea ambazo ziliwaongoza katika uchunguzi wao ambazo alizitaja kuwa ni kuchunguza makinikia yaliyopo kwenye Bandari ya Dar es Salaam, bandari kavu na migodini kwa kupekua na kubaini vilivyo ndani. Pia, kufanya uchunguzi wa kimaabara kujua aina, kiasi na viwango vya madini vinavyoonekana kwenye makinikia.

ZARI WA DIAMOND ATHIBITISHA KIFO CHA MUMEWE WA ZAMANI

Zarinah Hassan ‘ZariTheBossLady’ amethibitisha taarifa za kifo cha aliyekuwa mpenzi na baba wa watoto wake watatu, Ivan Semwanga.

Zari ametoa taarifa hzo kupitia akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Instagram kwa kuandika,” God loves those that are special and that’s exactly who you were & I guess that’s why he wanted you to himself. You have touched and helped thousands, you did wonders and I remember you telling me “life is too short let me live it to the fullest”, this very dark hour it makes sense why you always said those words to me. To your sons, you were a hero-some kind of superman. Anyone who has ever been in your presence knows what a charming person you were. You will be missed and remembered in so many ways. You were IVAN THE GREAT! Rest in peace DON”

Kwa Kiswahili, “Mungu anawapenda wale walio muhimu na hakika ndivyo ilivyokuwa kwako, nadhani hiyo ndiyo sababu ya yeye kukuhitaji kwake. Umewagusa na kuwasaidia maelfu, ulifanya maajabu na ninakumbuka ulinambia ”maisha ni mafupi sana acha niishi kwa ukamilifu”, muda huu wenye giza ndiyo inaleta maana kwanini ulisema maneno hayo kwangu. Kwa watoto wako ulikuwa shujaa. Kila mtu aliyekuwepo sehemu ulipokuwa alijua kwa kiasi gani wewe ni mcheshi. Nitakukumbuka kwa namna nyingi. Ulikuwa IVAN THE GREAT. Pumzika kwa amani DON”

Kabla ya taarifa hiyo kulikuwa na taarifa nyingi zikisema kuwa Iavn amefariki lakini Zari alikuwa akikanusha, na taarifa za uhakika akizitoa Zari mwenyewe ambaye wamezaa watoto watatu wote wakiwa wa kiume alfajiri ya alhamisi ya Mei, 25.

RAIS WA FIFA AIPONGEZA YANGA KWA KUSHINDA UBINGWA WA VPL 2016/2017

Rais wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), Gianni Infantino ametuma salamu za pongezi kwa uongozi, wachezaji na mashabiki klabu ya Yanga kwa kuibuka washindi wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) msimu wa 2016/2017.

Salamu za Infantino zimetumwa kwa Yanga kupitia Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi na kuwa pamoja na kuwapongeza kwa ushindi walioupata pia anaitakia kila la kheri Yanga katika michuano iliyopo mbele yake.

Wednesday, May 24, 2017

MBUNGE MSUKUMA AOMBA BUNGE KUCHANGIA RAMBIRAMBI KWA WANAFUNZI WALIOFARIKI GEITA, WABUNGE WENGINE WAZOMEA....!!!

Mbunge wa Geita Vijijini (CCM), Joseph Musukuma, ameomba mwongozo akiliomba Bunge liangalie namna ya kuchangia rambirambi kwa wanafunzi watatu waliofariki kwa kuzama Ziwa Victoria.

Kwa mujibu wa Mbunge huyo, Bunge hilo limekuwa na utamaduni wa kuchangia maafa na majanga mbalimbali na kutolea mfano wa ajali iliyoua ya shule ya msingi ya Lucky Vicent Jijini Arusha.

Katika ajali hiyo, wanafunzi 32 walifariki dunia pamoja na watu wengine watatu ambapo wabunge walichanga rambirambi inayofikia Sh86 milioni ambapo ofisi ya Bunge ilichanga Sh14 milioni.

Hata hivyo, wakati Mbunge huyo akiwasilisha mwongozo huo, baadhi ya wabunge wa upinzani walionekana kupaza sauti yao, hadi mwenyekiti Zungu alipolazimika kukemea hali hiyo.

Zungu akitoa mwongozo wake, alisema ni utamaduni wa chombo hicho kuchangia maafa na majanga mbalimbali kama njia za kuonyesha mshikamano na kwamba hilo analichukua atalitolea majibu baadae.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...