Tuesday, August 23, 2016

POLISI WAMZUIA LOWASSA KUINGIA RUKWA

Msafara wa aliyekuwa mgombea wa Urais kupitia Chadema, Edward Lowassa umekwama kwenda Mikoa ya Rukwa na Katavi baada ya polisi kuuzuia kwa hofu kwamba unaweza kuingilia ziara ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa anayetembelea mikoa hiyo.
Lowassa ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema alianzia ziara yake mkoani hapa tangu Agosti 21 na juzi alifanya vikao vya ndani katika majimbo yanayoshikiliwa na wabunge wa chama chake mkoani Songwe wakati leo asubuhi alitarajiwa kwenda Katavi na Rukwa.
Katika Mikoa ya Rukwa na Katavi alitarajiwa kufanya mikutano ya ndani Majimbo ya Nkasi Kaskazini na Kusini na Sumbawanga. Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

Katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini wanayoiita ‘Kanda ya Nyasa’, Frank Mwaisumbe alisema kwamba polisi walimpigia simu Lowassa juzi saa 1.00 jioni akiwa Tunduma wakimtaka aahirishe ziara yake Mkoa wa Rukwa.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Rukwa, Gorge Kyando alipoulizwa kwa njia ya simu alisema waliwashauri viongozi wa Chadema wapange siku nyingine ya ziara kwa sababu mkoa ulikuwa na ugeni mkubwa.

MAZEMBE YAICHAPA YANGA 3-1 NA KUONGOZA KUNDI A

MZ 6
Mchezo wa mwisho wa Kundi A michuano ya kombe la Shirikisho Afrika kati ya TP Mazembe dhidi ya Yanga umemalizika kwa Yanga kukubali kichapo cha magoli 3-1 ikiwa ugenini na kuendeleza rekodi yake ya kutoshinda michezo yake mitatu ya hatua ya nane bora msimu huu.
Bolingi alianza kuifungia Mazembe bao la kwanza dakika ya 28 kipindi cha kwanza.
Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

MZ 4
Yanga ilipata pigo dakika mbili baada ya kuruhusu goli, Andrew Vicent ‘Dante’ alioneshwa kadi nyekundu na kuiacha Yanga ikicheza pungufu kwa dakika zote zilizobaki.
MZ 2
Dakika 11 baada ya kipindi cha pili kuanza, Rainford Kalaba aliifungia Mazembe bao la pili kabla kuongeza bao lake la pili likiwa ni bao la tatu kwa Mazembe mnamo dakika ya 64.
Amis Tambe aliifungia Yanga bao pekee akiunganisha mpira uliogonga ‘mtambaa panya’ baada ya Haruna Niyonzima kupiga mpira wa adhabu ndogo.
MZ 5
Matokeo hayo yanaipa Mazembe fursa ya kuongoza Kundi A kwa pointi 13 bila kujali matokeo ya wapinzani wake Medeama na MO Bejaia.
Yanga  imemaliza ikiwa nafasi ya nne (yamwisho) kwenye Kundi A ikiwa na pointi nne baada ya kupata ushindi katika mechi moja (Yanga 1-0 MO Bejaia) sare moja (Yanga 1-1 Medeama) huku mechi nyingine nne ikiwa imepoteza. (MO Bejaia 1-0 Yanga, Yanga 0-1 TP Mazembe, Medeama 3-1 Yanga, Mazembe 3-1 Yanga).
Yanga imefunga jumla ya magoli 9 huku yenyewe ikiwa imefunga magoli manne.
Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU AUGUST 23, 2016 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

IMG_20160823_045122 IMG_20160823_045138 IMG_20160823_045153


Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

Saturday, August 13, 2016

KAMA UNATAKA KUMUOA JOHARI SOMA HII

Blandina Chagula ‘Johari’

  STAA wa kitambo kwenye filamu za Kibongo, Blandina Chagula ‘Johari’ amesema baada ya kukaa singo kwa muda mrefu, sasa yupo tayari kuingia kwenye ndoa wakati wowote.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii, Johari amesema anatamani sasa naye aingie kwenye ndoa kwa kuwa umri wake unamruhusu kufanya hivyo.

“Mimi ni mwanamke kamili, ni mtu mzima. Nimeshakuwa sasa, kwahiyo kiukweli nina kiu ya mume. Mungu akinipa mume bora, nitaolewa. Sitaki kuzungumzia sana mambo yaliyopita, lakini muhimu kwa sasa ni mume,” anasema Johari.
Blandina Chagula ‘Johari’
Kuhusu sifa za mwanaume anayependa awe mumewe, Johari alisema: “Napenda mwanaume mwenye upendo wa dhati   kwangu na awe mtafutaji, pia aheshimu kazi yangu.

“Historia yangu ya mapenzi imenifundisha mengi, najielewa na kujitambua vizuri. Kuna tofauti kubwa sana kati ya Johari wa zamani na wa sasa. Kwanza nimekomaa kiakili, nimekutana na vitu vingi na nimejua maisha ni nini. Nipo tayari kufanya maisha na mwanaume serious.”

MAALIM SEIF AMTEMBELEA MH. NDUGAI

Ujumbe wa Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad umemtembelea Spika wa Bunge, Job Ndugai nyumbani kwake Salasala Dar es Salaam kumjulia hali baada ya kutoka India alikokwenda kuchunguzwa afya yake.

Maalim Seif ambaye pia ni Makamu wa Kwanza Rais Mstaafu wa Serikali ya Zanzibar, ameambatana na Kaimu Mwenyekiti wa CUF, Severina Mwijage, Naibu Katibu Mkuu CUF Tanzania Bara, Magdalena Sakaya na Naibu Katibu Mkuu mstaafu, Julius Mtatiro.
 
Ndugai amemhakikishia Maalim Seif kuwa hali yake kiafya imeimarika sana.

Sunday, July 10, 2016

JE, WAMJUA MNYAMA MWENYE WIVU KUPITA KIASI....??!

Nyegere ni moja kati ya wanyama wenye wivu sana hapa duniani. Chakula chake kikubwa ni asali, yeye hupanda juu ya mzinga wa asali na kuujambia, baada ya mashuzi yake nyuki wote hulewa na yeye kupakua asali na masega yake na kula. Mwili wake una ngozi ngumu sana kiasi hata nyuki akimuuma hakuna chochote kinatokea.

Nyegere ni mnyama mwenye wivu na mapenzi makubwa sana kwa jike lake, hutembea nyuma ya jike huku akiwa ameziba sehemu za siri za jike, hata jani tu likiigusa sehemu ya siri ya jike litararuliwa na kupokea kichapo cha hatari, maana wivu wake ni kuwa jani laitakuwa "limefaidi utamu" wa jike.
Nyegere anaweza kununua ugomvi mpaka kijiji cha sita, walina asali ndio waathirika wakubwa wa hasira za Nyegere, anaweza kuujambia mzinga akala kidogo asali na kupeleka kwa mke, mlina asali akifika na kupakua, nyegere ana uwezo ya kufuatilia harufu ya aliyeiba asali yake mpaka nyumbani, na akifika anavunja mlango na kuingia ndani na kumvamia mwizi wa asali yake (ukizingatia milango ya vijijini si imara). Watu wengi vijini wameuwawa kwa namna hii. Like page yetu ya facebook ya Jambo Tz. Pia tu-follow instagram @jambotz.

Friday, June 24, 2016

MAOMBI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU 2016/2017

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu inapenda kutoa taarifa kwa Umma na wadau wake wote kuwa inatarajia kuanza kupokea maombi ya Mikopo kwa mwaka wa masomo 2016 /2017 kuanzia tarehe 27 Juni 2016 hadi tarehe 31 2016.

Katika kipindi hicho waombaji wa mikopo watarajiwa wanapaswa kusoma mwongozo wa utoaji mikopo na ruzuku (GUIDELINES AND CRITERIA FOR ISSUANCE OF STUDENTS’ LOANS AND GRANTS FOR THE 2016/2017 ACADEMIC YEAR) uliopo kwenye tovuti hii ya Bodi ili kufahamu sifa za mwombaji na taratibu kufuata kabla ya kuomba mikopo kwa njia ya mtandao.

Utoaji wa Mikopo unaongozwa na Sheria ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya juu Na. 9 ya 2004 (kama ilivyorekebishwa) hususani vifungu vyake vya 16 na 17.
Kwa taarifa hii, waombaji wote wa mikopo wanatakiwa kusoma mwongozo huo kabla ya kujaza maombi ya mikopo na wazingatie kuwa tarehe ya mwisho ya kuomba mikopo ni Julai 31, 2016.

Wednesday, June 22, 2016

MMILIKI WA TP MAZEMBE AHUKUMIWA MIAKA MITATU JELA

Mmiliki wa klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Moise Katumbi amehukumiwa kwenda jela, Katumbi ambaye ni boss wa TP Mazembe amehukumiwa kwenda jela miaka mitatu.
Katumbi amehukumiwa miaka mitatu sambamba na kutozwa faini ya dola milioni 6 kwa kosa la kujimilikisha eneo, Katumbi pia alikuwa anatajwa kugombea nafasi ya Urais wa Kongo mwishoni mwa mwaka 2016 kupitia chama cha upinzania kushinda na Rais anayemaliza muda wake Joseph Kabila.
rts7qug-e1462504316478
Hata hivyo wakati wa kutolewa hukumu hiyo Moise Katumbi hakuwepo Kongo, siku moja kabla ya hukumu alikuwa kasafiri kwenda Afrika Kusini kupata matibabu, makosa mengina anayotuhumiwa nayo Katumbi ni pamoja na kutajwa kuajiri wa geni kutoka nje ya Kongo kwa ajili ya kuandaa njama za kumuondoa Rais Kabila.
Moise Katumbi ndio Rais wa klabu ya TP Mazembe aliyoingoza kucheza hadi hatua ya fainali ya klabu Bingwa ya dunia dhidi ya Inter Milan December 18 2016, rekodi ambayo hakuna klabu ya Afrika imewahi kuifikia, TP Mazembe ndio ya kwanza, TP Mazembe wanakuja Tanzania June 28 kucheza mchezo wao wa pili wa nane bora dhidi ya Yanga.

Monday, June 20, 2016

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JUNI 20, 2016 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

IMG_20160620_060923 IMG_20160620_060948 IMG_20160620_061043 
Tangaza biashara yako hapa. Pia like page yetu ya facebook Jambo Tz. tu-follow instagram @jambotz.

YANGA YASHINDWA KUTAMBA KWA WAARABU YAPIGWA 1-0

 Mabingwa wa soka la Tanzania bara Yanga SC wameanza vibaya kampeni zao za kuwania kombe la Shirikisho Afrika baada ya kupoteza mchezo wao wa kwanza kwa bao 1-0 dhidi ya MO Bejaia ukiwa ni chezo wa Kundi A.

Yassin Sahli alifunga bao pekee kwenye mchezo huo na kuipa pointi tatu MO Bejaia iliyokuwa ikicheza kwenye uwanja wake wa nyumbani Stade de I’Unite Maghrebine mjini Bejaia, Algeria.
Matokeo hayo yanaiacha Yanga katika nafasi ya tatu huku TP Mazembe wakiwa ndiyo vinara wa Kundi baada ya kushinda mchezo wao kwa magoli 3-0 dhidi ya Medeama ambayo inaburuza mkia.

Mazembe na MO Bejaia zinapointi sawa (pointi tatu) lakini TP Mazembe anaongoza kundi kwa tofauti ya magoli wakati Yanga na Medeama zikiwa hazina pointi lakini Yanga inakaa nafasi ya tatu kwa tofauti ya magoli. Medeama imefungwa magoli matatu wakati Yanga wameruhusu bao moja pekee.
Mchezo ujao wa Yanga utakuwa nyumbani (Dar es Salaam) June 28 itakapowaalika TP Mazembe kwenye uwanja wa taifa.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...