Monday, July 27, 2015

RAIS OBAMA AWASILI NCHINI ETHIOPIA


Rais Barack Obama wa Marekani hatimaye amefika nchini Ethiopia katika ziara yake ya pili ya nchi za Afrika.

Ni mara yake ya kwanza tangu aongoze taifa la Marekani akiwa rais kuhutubia wanachama hamsini na mbili wa umoja wa Afrika katika makao makuu yake yaliyoko Addis ababa.

Mazungumzo yao yakiwa yamelenga kutafuta suluhu ya kutokomeza migogoro ya vita za wenyewe kwa wenyewe sudan ya kusini. 

Rais Obama, aliwasili nchini Ethiopia akiwa anatokea mjini Nairobi ambako aliwaambia wakenya kuwa amna kikomo cha kile wanachokihitaji na kusisitiza kwa kutoa angalizo katika athari za ukabila na rushwa. 

Tamaduni mbaya kama unyanyasaji wa kijinsia, ndoa za kulazimishwa, tohara kwa watoto wa kike na kutopeleka watoto shuleni.

MSANII BOBBI KRISTINA AFARIKI DUNIA


Bobbi Kristina afariki Dunia

Bobbi Kristina Brown, mtoto wa marehemu Whitney Houston ambaye alikuwa gwiji wa muziki wa R&B, amefariki dunia baada ya kupoteza fahamu kwa muda wa miezi sita tangu alipokutwa taabani kwenye bafu lake na pindi alipofikishwa hospitalini na kukutwa na matatizo kwenye ubongo.

Bobbi amekufa akiwa na umri wa miaka 22,huku akivutiwa kuwa muigizaji na muimbaji mahiri na mwenye ubora wa aina yake. Msemaji wa familia Kristen Foster amesema Bobbi amefariki akiwa amezungukwa na familia yake, ''hatimaye yuko salama sasa kwenye mikono ya Mwenyezi Mungu,tunawashukuru wote walioungana nasi katika maombi na kuonesha upendo kwa miezi michache iliyopita''.

Bobbi ambaye alikuwa amepoteza fahamu tangu akutwe ameanguka kwenye bafu lake panapo tarehe 31 januari mwaka huu na kuwekwa kwenye matibabu huku akiwa amekosa ufahamu na mpaka kifo chake kumkuta alikuwa hajapata fahamu bado.

Inakumbukwa kuwa miaka mitatu iliyopita mama yake Bobbi,alikutwa pia kwenye bafu lake amepoteza fahamu baada ya kupitliza kiwango cha dawa za kulevya na pombe mwishowe kufa. Bobbi alikuwa mtoto pekee wa Whitney Houston na Bobby Brown,magwiji wa muziki wa miondoko ya R &B.

Sunday, July 26, 2015

MLIPUKO WAUA WATU 10 SOMALIA


Takriban watu 10 wameuawa katika mlipuko huo

Takriban watu 10 wameuawa kufuatia mlipuko mkubwa uliotokea katika hoteli moja katika mji mkuu wa Somalia Mogadishu.

Mwandishi wa BBC katika mji huo anasema kuwa lori moja lilitumiwa kushambulia hoteli ya Jazeera karibu na uwanja wa ndege wa taifa hilo. Wajumbe wa kimataifa wamekuwa wakiishi katika hoteli hiyo ambayo imelengwa katika siku za nyuma.

Ripota wetu anasema kuwa ni moja ya mashambulizi mabaya kuwahi kushuhudiwa mjini Mogadishu. Anasema kuwa magari ya ambulansi yameanza kuokota miili.

14 WAFA KATIKA SHAMBULIO CAMEROON


Watu 14 wameuawa jana usiku katika shambulizi la bomu lililotekelezwa na Boko Haram

Watu 14 wameuawa jana usiku katika shambulizi la bomu lililofanyika kwenye jumba moja la starehe katika mji wa Maroua Kaskazini mwa Cameroon.

Siku chache baada ya kutokea kwa mashambulizi mawili ya bomu katika mji mkuu wa eneo hilo kulingana na habari kutoka kwa maafisa wa usalama. Afisa mmoja wa jeshi lililopelekwa katika eneo hilo kupambana na Boko Haram ndiye aliyetoa habari hiyo kwa siri.

Shambulizi hilo lilifanyika saa mbili kasorobo jana usiku saa za Afrika Mashariki wakati mwanaume mmoja alirusha bomu ndani ya baa katika wilaya ya Ponre kulingana na afisa huyo wa jeshi ambaye hakutaka kutajwa. Wakazi walijaribu kumfuata lakini aliwarushia grunedi kuwafukuza.

Saturday, July 25, 2015

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JULAI 25, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
.
.
Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

WEMA SEPETU ALA ‘NGUMI’ ZA USO UBUNGE SINGIDA

Wema
Msanii maarufu wa filamu nchini, Wema Abraham Sepetu amepigwa chini katika kura za maoni kugombea ubunge wa viti maalum Singida.
 
Aysharose Mattembe ndiye ameibuka kidedea akimtupa kwa mbali Madam Wema aliyeshika nafasi ya nne.
11228022_1051907251486527_8461334309566372025_n 
Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

ZLATAN YUKO TAYARI KUKIPIGA MAN UNITED, ILA ANAHOFIA JAMBO MOJA


2ABD88C600000578-0-image-a-66_1437751952554
Mshambuliaji msumbufu na mwenye majivuno, Zlatan Ibrahimovic maarufu kama ‘Cadabra’ amesema angependa kuichezea Manchester United siku moja lakini anahofia ‘ngumi’ za kila siku na kocha Louis Van Gaal.

Akiwajibu waandishi wa habari kama yuko tayari kujiunga na mashetani hao wekundu, Cadabra alisema angeweza kuchezea United lakini anahofia ugomvi wa kutoisha baina yake na Louis Van Gaal.

Zlatan na Van Gaal hawakuwa na mahusiano mazuri tangu wakiwa Ajax miaka ya 1990’s lakini moto uliwaka zaidi baada ya Zlatan kumtaja Van Gaal kama ‘pampasi’ katika kitabu chake.

Wawili hao hawana urafiki na kwamba hawawezi kuiva chungu kimoja. Hisia zimekuwa ni nyingi miongoni mwa mashabiki mara baada ya kocha Louis Van Gaal kutangaza kwamba atafanya usajili wa kushitukiza wa mshambuliaji siku za usoni.

Hata hivyo Cadabra nahodha wa Sweden anahusishwa na tetesi za kujiunga na AC Milan ya nchini Italia. Habari zinasema Zlatan amechoshwa na quality ya ligi nchini Ufaransa na sasa anafikiria kuihama klabu yake ya Paris St. Germain. Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

HATIMAYE WAYNE ROONEY AMJIBU VAN GAAL

2AD1593000000578-3173794-image-m-25_1437770313268
Wayne Rooney amesema yuko tayari kuwa mfungaji bora wa Manchester Unites kwa mara nyingine na amewapa changamoto wenzake ya kuandika Historia msimu ujao.
 
Nyota huyo wa England alicheza namba nyingi msimu uliopita chini ya Louis van Gaal na ikifika wakati akashushwa mpaka kiungo cha chini.
 
Kwasasa Rooney anataka kucheza namba anayoipenda yaani namba 9 na amesema yuko tayari kufunga magoli.
 
“Niko tayari kubadili akili yangu na kuwa moja ya wafungaji wa magoli,” Amesema nyota huyo wa zamani wa Everton ambaye msimu uliopita aliifungia United magoli 12.
 
“Nataka kucheza nafasi ya mshambuliaji ambapo nadhani ninaweza kufunga, naamini naweza kulitekeleza hilo”
Rooney performed a number of roles for Manchester United last term but is keen to play as a number nine
Msimu wa 2009-10 na 2011-12, Rooney alifunga magoli 34 kwenye mashindano yote akicheza nafasi ya mshambuliaji wa kati na kama atarudishwa nafasi hiyo anaweza kufanya vizuri.
 
Siku za karibuni, kocha wa Man United, Louis van Gaal alisema anatarajia kumtumia Rooney kama mshambuliaji wa kati msimu ujao na maneno haya ya Wayne ni majibu kwa bosi wake. Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

HATIMAYE WAYNE ROONEY AMJIBU VAN GAAL

2AD1593000000578-3173794-image-m-25_1437770313268
Wayne Rooney amesema yuko tayari kuwa mfungaji bora wa Manchester Unites kwa mara nyingine na amewapa changamoto wenzake ya kuandika Historia msimu ujao.
 
Nyota huyo wa England alicheza namba nyingi msimu uliopita chini ya Louis van Gaal na ikifika wakati akashushwa mpaka kiungo cha chini.
 
Kwasasa Rooney anataka kucheza namba anayoipenda yaani namba 9 na amesema yuko tayari kufunga magoli.
 
“Niko tayari kubadili akili yangu na kuwa moja ya wafungaji wa magoli,” Amesema nyota huyo wa zamani wa Everton ambaye msimu uliopita aliifungia United magoli 12.
 
“Nataka kucheza nafasi ya mshambuliaji ambapo nadhani ninaweza kufunga, naamini naweza kulitekeleza hilo”
Rooney performed a number of roles for Manchester United last term but is keen to play as a number nine
Msimu wa 2009-10 na 2011-12, Rooney alifunga magoli 34 kwenye mashindano yote akicheza nafasi ya mshambuliaji wa kati na kama atarudishwa nafasi hiyo anaweza kufanya vizuri.
 
Siku za karibuni, kocha wa Man United, Louis van Gaal alisema anatarajia kumtumia Rooney kama mshambuliaji wa kati msimu ujao na maneno haya ya Wayne ni majibu kwa bosi wake. Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

Friday, July 24, 2015

WAJUMBE WA CCM WAPATA AJALI, MMOJA AFARIKI


Mtu mmoja amefariki Dunia baada ya basi Dogo aina ya toyota HIACE, lililokuwa limewabeba wajumbe wa chama cha mapinduzi wa kata ya Milanzi kwenye manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa, waliokuwa kwenye kampeni za kura za maoni za udiwani kuacha njia na kupinduka, ambapo pia ajali hiyo imeacha majeruhi kumi na moja.

Akiongea na waandishi wa habari kwenye Hospitali ya rufaa ya mkoa wa Rukwa mjini Sumbawanga, mwenyekiti wa CCM wa kata ya milanzi Bw. Edgar Mwanandenje ambaye ni miongoni mwa majeruhi hao, amesema walikuwa wakitokea kwenye mchakato wa kampeni ya kura za maoni katika kata yao, ndipo dereva wa basi hilo dogo alipolazimisha kuipita kwa kasi pikipiki aina ya bajaj iliyokuwa mbele yao, na kupoteza mwelekeo kabla ya kupinduka. 

Katibu wa ccm wilaya ya sumbawanga mjini Bw Gabriel Kiula akiongelea juu ya ajali hiyo,amemtaja aliyepoteza maisha kuwa ni Didas Mwanisenga aliyekuwa mjumbe wa kamati ya siasa ya kata ya milanzi, huku kamanda wa polisi wa mkoa wa Rukwa Bw. Jacob Mwaruanda akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo.

EU YAJADILI KUKATA MISAADA BURUNDI


Bendera ya Burundi

Muungano wa Ulaya EU umeanza kikao maalum kujadili uwezekano wa kukata msaada wake nchini Burundi. Inakisiwa kuwa fedha kutoka muungano huo unafikia zaidi ya nusu ya bajeti nzima ya Burundi ya kila mwaka. 

Mkuu wa masuala ya kigeni wa Muungano wa EU Federica Mogherini, ameelezea wasiwasi wake juu ya ghasia zilizototokea nchini humo kabla ya kufanyika uchaguzi wa rais, na ametilia shaka iwapo serikali itakayoundwa baada ya uchagzui huo itakuwa wakilishi ya taifa nzima. 

Upande wa uchaguzi ulisusia kura hiyo iliyofanywa siku ya Jumanne. Matokeo rasmi yanatarajiwa kutangazwa Ijumaa hii Uamuzi wa Rais Pierre Nkurunzinza kuwania urais kwa muhula wa tatu umetajwa kwenda kinyume na mkataba waliosaini mjini Arusha miaka kumi na tano iliyopita, ambao ulimaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vya miaka mingi.

Ghasia zimezuka nchini humo tangu rais Pierre Nkurunzinza kutangaza kuwania kiti hicho ambapo zaidi ya watu laki moja wamikimbia nchi hiyo huku makumi ya maelfu wengine wakiuawa katika maandamano. Juhudi kadhaa za kuleta upatanishi kati ya makundi hasimu zimeambulia patupu.

BUHARI "MAREKANI INAWASAIDIA BOKO HARAM"


Rais Mahammadu Buhari akiwa na mwenyeji wake Obama alipokua ziarani nchini Marekani wiki hii.

Marekani "inawasaidia na kuchochea " kundi la wanamgambo wa kiislam wa Boko Haram kwa kukataa kutoa silaha kwa Nigeria, ni kauli ya rais wa Nigeria Mahammadu Buhari.

Sheria ya Marekani inazuia serikali kuuza silaha kwa nchi ambazo zinashindwa kushughulikia ipasavyo masuala ya haki za binadamu.

Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari alikutana na rais Barack Obama Jumatatu kuomba msaada zaidi. Boko Haram limewauwa watu 10,000 tangu mwaka 2009 na limewateka mamia ya wasichana na wanawake.

Thursday, July 23, 2015

MATOKEO YA KURA ZA MAONI UBUNGE CHADEMA MBEYA NA MAJIMBO MENGINE

http://jambotz8.blogspot.com/

http://jambotz8.blogspot.com/

YANGA SC YAZINDUKA, YAWAPIGA 3-0 TELECOM, MSUVA NA TAMBWE WAKOSA PENALTI

Yanga imerejea katika michuano ya Kagame baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Telecom ya Djibout katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Jana.

Katika mechi yake ya kwanza ya michuano hiyo, Yanga ilianza kwa kupoteza kwa mabao 2-1 dhidi ya Gor Mahia huku mshambuliaji wake Donald Ngoma akilambwa kadi ya nyekundu.

Malimi Busungu ndiye shujaa baada ya kufunga mabao mawili huku Geofrey Mwashuya, akifunga bao la tatu.

BENTEKE AHAMIA LIVERPOOL RASMI


Christian Benteke

Timu ya Livepool imekamilisha kumsajili rasmi mshambuliaji mwenye asili ya Jamuhuri ya Kidemokrasia wa kongo Christian Benteke kutoka Aston Villa kwa kitita paundi milion 32.5. 

Benteke alikubali mkataba wa muda mrefu na kuwa mchezaji wa pili kununuliwa kwa gharama kubwa huko England.

Mshambuliaji huyo raia wa Ubelgiji ameifunga magoli 49 katika mechi 101 alizocheza kwenye timu yake ya zamani ya Aston Villa.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...