Saturday, July 25, 2015

HATIMAYE WAYNE ROONEY AMJIBU VAN GAAL

2AD1593000000578-3173794-image-m-25_1437770313268
Wayne Rooney amesema yuko tayari kuwa mfungaji bora wa Manchester Unites kwa mara nyingine na amewapa changamoto wenzake ya kuandika Historia msimu ujao.
 
Nyota huyo wa England alicheza namba nyingi msimu uliopita chini ya Louis van Gaal na ikifika wakati akashushwa mpaka kiungo cha chini.
 
Kwasasa Rooney anataka kucheza namba anayoipenda yaani namba 9 na amesema yuko tayari kufunga magoli.
 
“Niko tayari kubadili akili yangu na kuwa moja ya wafungaji wa magoli,” Amesema nyota huyo wa zamani wa Everton ambaye msimu uliopita aliifungia United magoli 12.
 
“Nataka kucheza nafasi ya mshambuliaji ambapo nadhani ninaweza kufunga, naamini naweza kulitekeleza hilo”
Rooney performed a number of roles for Manchester United last term but is keen to play as a number nine
Msimu wa 2009-10 na 2011-12, Rooney alifunga magoli 34 kwenye mashindano yote akicheza nafasi ya mshambuliaji wa kati na kama atarudishwa nafasi hiyo anaweza kufanya vizuri.
 
Siku za karibuni, kocha wa Man United, Louis van Gaal alisema anatarajia kumtumia Rooney kama mshambuliaji wa kati msimu ujao na maneno haya ya Wayne ni majibu kwa bosi wake. Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...