Saturday, July 25, 2015

ZLATAN YUKO TAYARI KUKIPIGA MAN UNITED, ILA ANAHOFIA JAMBO MOJA


2ABD88C600000578-0-image-a-66_1437751952554
Mshambuliaji msumbufu na mwenye majivuno, Zlatan Ibrahimovic maarufu kama ‘Cadabra’ amesema angependa kuichezea Manchester United siku moja lakini anahofia ‘ngumi’ za kila siku na kocha Louis Van Gaal.

Akiwajibu waandishi wa habari kama yuko tayari kujiunga na mashetani hao wekundu, Cadabra alisema angeweza kuchezea United lakini anahofia ugomvi wa kutoisha baina yake na Louis Van Gaal.

Zlatan na Van Gaal hawakuwa na mahusiano mazuri tangu wakiwa Ajax miaka ya 1990’s lakini moto uliwaka zaidi baada ya Zlatan kumtaja Van Gaal kama ‘pampasi’ katika kitabu chake.

Wawili hao hawana urafiki na kwamba hawawezi kuiva chungu kimoja. Hisia zimekuwa ni nyingi miongoni mwa mashabiki mara baada ya kocha Louis Van Gaal kutangaza kwamba atafanya usajili wa kushitukiza wa mshambuliaji siku za usoni.

Hata hivyo Cadabra nahodha wa Sweden anahusishwa na tetesi za kujiunga na AC Milan ya nchini Italia. Habari zinasema Zlatan amechoshwa na quality ya ligi nchini Ufaransa na sasa anafikiria kuihama klabu yake ya Paris St. Germain. Je unahitaji kununua gari kwa bei nafuu, bofya hapa au tuambie unataka gari gani na ya bei gani tukutafutie haraka.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...