Thursday, October 02, 2014

TAARIFA KWA UMMA KUTOKA CHAMA CHA ACT-TANZANIA KUHUSU ZITTO KABWE

 Zitto Kabwe
--
ALLIANCE FOR CHANGE AND TRANSPERANCY. 
--
Ndugu wanahabari kumekuwa na utaratibu wa habari zinazoupotosha umma wa watanzania kuhusu chama chetu cha ACT-Tanzania.

Katika gazeti la mwanahabari toleo na 117 la tarehe 29/09/2014 katika ukurasa wake wa mbele iliandikwa "MKAKATI WA KUKIPA NGUVU CHAMA CHA KIPYA CHA ZITTO KABWE WAVUJA".

Act-Tanzania tunaeleza kuwa ni chama cha watanzania wote kisichokuwa na mmilki wake na tunaunganishwa na misingi kumi ya chama pamoja na Itikadi yetu ya Demokrasia jamii.

Act-Tanzania tunatambua uwezo na mchango wa kisiasa na ujenzi wa demokrasia ya vyama vyingi nchini uliotolewa na Mheshimiwa Zitto Kabwe mbunge wa Kigoma Kaskazini.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KAJALA AMSHTAKI MAMA WEMA...!!!

KIMENUKA! Habari ya mjini kwa sasa ni bethidei ya Miss Tanzania 2006, Wema Sepetu kutimiza miaka 26 tangu kuzaliwa, lakini ndani ya tukio hilo, mengine yameibuka!

Staa katika tasnia ya filamu Bongo, Kajala Masanja.
Miongoni mwa yaliyoibuka kwenye sherehe hiyo iliyofanyika Jumapili iliyopita nyumbani kwa Wema, Mtaa wa Bwawani, Kijitonyama jijini Dar es Salaam ni madai ya mama Wema, Mariam Sepetu kudaiwa kupewa nafasi ya kutoa ‘neno la hekima’ lakini akaitumia kumvurumishia mitusi aliyekuwa shosti wa Wema, Kajala Masanja.
KUNASWA KWA SAUTI NA PICHA
Baada ya sherehe hiyo, Jumatatu na Jumanne, mitandao mingi ya kijamii ilitumbukiza video yenye sauti ikimuonesha mama Wema akimrushia matusi Kajala kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kutokana na kukorofishana kwa mwanaye na Kajala aliyewahi kumfadhili mahakamani kwa kumlipia faini ya shilingi milioni 13 asiende jela kwa kesi ya kuuza nyumba iliyokuwa na zuio la kisheria.
 
Wema Sepetu akiwa na mama yake.
KAJALA AAMUA ZITO
Katika kufuatilia sakata hilo, Amani lilinyetishiwa kwamba Kajala baada ya kushindwa kuvumilia, ameamua kumshitaki mahakamani mama Wema. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

GARDNER ATAKA JIDE AELEZE UKWELI JUU YA NDOA YAO


Habari ya mjini katika ulimwengu wa mastaa Bongo ni kitendo cha mtangazaji mwenye jina kubwa wa Kipindi cha Maskani cha Redio Times FM, Gardner G Habash ‘Kepteini’ kutaka mwanamuziki Judith Wambura Mbibo ‘Jide’ ndiye aeleze ukweli juu ya ndoa yao.
 
Mtangazaji wa Redio Times FM, Gardner G Habash ‘Kepteini’
Akizungumza kwenye Kipindi cha Mkasi kinachorushwa hewani kupitia Televisheni ya EATV chini ya ‘hosti’ wake, Salama Jabir, Jumanne iliyopita, Gardner alikataa kuzungumzia ndoa yake inayodaiwa kuvunjika.
Pamoja na mambo mengine ambayo aliyajibu kwa ufasaha, Gardner alipoulizwa juu ya habari zinazozungumzwa mtaani kuhusu kuvunjika uhusiano wake na Jide au Lady Jaydee, aligoma kulizungumzia kwa kigezo kwamba kipindi hicho kilimhusu yeye tu.
 
Mwanamuziki wa Bongo fleva kitambo, Judith Wambura Mbibo ‘Jide’
Mtangazaji huyo alikwenda mbele zaidi kwa kumwambia Salama kwamba amwite Jaydee kwenye kipindi hicho ili alielezee jambo hilo kwa undani.Gardner na Jaydee ambao walifunga ndoa mwaka 2005, wamekuwa wakidaiwa kuwa hawapo pamoja tena huku majukumu ya mtangazaji huyo ambaye alikuwa meneja wa mwanamuziki huyo yakielea.
Kupitia kipindi chake cha Diary of Lady Jaydee kilichokuwa kikisimamiwa na Gardner ambacho sasa kinaongozwa na ndugu wa msanii huyo aitwaye Wakazi, Jumapili iliyopita Jide alionekana kwenye harusi ya ndugu yake aitwaye Lameck Mbibo ‘Dabo’ ambaye pia ni msanii wa Dance Hall akiwa mpweke bila mumewe kama ilivyozoeleka. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na GPL

RAILA ODINGA ATANDIKWA BAKORA HADHARANI...!!!

Mzee Mdzombo anasemekana kutokuwa timamu kiakili
Kiongozi wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga amemsamehe mzee aliyempiga bakora katika mkutano wa hadhara wa kisiasa katika jimbo la Kwale Pwani ya Kenya,
Mwanamume huyo, Lengo Mdzombo, anayefanya kibarua katika shamba moja Kwale, alikamatwa Jumanne na kufikishwa mahakamani.
Alishitakiwa kwa kosa la kumshambulia kiongozi huyo pamoja na gavana wa Kwale.
Hali ya taharuki ilitanda katika mkutano wa hadhara Jumatatu wiki hii baada ya Mdzombo kwenda ukumbini na kuanza kumtandika bakora kiongozi wa upinzani Raila Odinga pamoja na wanasiasa wengine.
Raila alikuwa amejiunga na kikundi cha wanawake waliokuwa wanacheza densi ya kitamaduni kuwatumbuiza wageni, pamoja na gavana wa jimbo la Kwale Pwani ya Kenya Salim Mvuruya katika mkutanmo wa kisiasa.
Raila alikuwa ameambatana na viongozi wengine, wakiwemo, Seneta Juma Boy, Hassan Omar, Agnes Zani, James Orengo, Johnstone Muthama na wengineo.
Kiongozi wa upinzani Raila Odinga
Mzee huyo alimpiga bakora Odinga ambaye ni waziri mkuu wa zamani kabla ya kumgeukia gavana wa jimbo hilo na kumchapa mara mbili. Hata hivyo mwanamume huyo alishindwa nguvu na walinzi wa Raila Odinga.
Polisi walithibitisha kuwa walimkamata mwanamume huyo na kumwachilia baada ya kugundua kuwa alikuwa na matatizo ya kiakili.
Haijulikani kwa nini mwanamume huyo alimshambulia Raila ila baadhi wanasema ni kwa sababu alighadhabishwa pale waziri mkuu alipocheza densi na mwanamke aliyesemekana kuwa mke wake ambaye alikuwa katika kikundi cha wanawake waliokuwa wanawatumbuiza wageni waheshimiwa.
Viongozi waliofika walilazimika kusitisha densi hiyo kabla ya mwanamume huyo kushindwa nguvu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

ARSENAL YAUA 4-1, WELBECK APIGA HAT-TRICK


Mshambuliaji Danny Welbeck akishangilia baada ya kupiga 'hat-trick'.

Alexis Sanchez akiifungia Arsenal bao la tatu dhidi ya Galatasaray.

Welbeck akitupia bao la nne. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger ametimiza miaka 18 akiwa meneja wa klabu hiyo leo.
KLABU ya Arsenal imetoa kichapo cha mabao 4-1 dhidi ya Galatasaray kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya iliyopigwa Uwanja wa Emirates jijini London usiku huu.
Mshambuliaji Danny Welbeck ametupia kambani mabao matatu 'hat-trick' huku bao la nne likiwekwa kimianai na Alexis Sanchez. Katika mtanange huo, kipa wa Arsenal, Wojciech Szczesny alizawadiwa kadi nyekundu baada ya kumfanyia madhambi mshambuliaji wa Galatasaray, Burak Yilmaz.
Ushindi wa leo wa Arsenal umeongeza furaha kwa Meneja wa timu hiyo, Arsene Wenger aliyetimiza miaka 18 akiwa kocha wa klabu hiyo leo.
VIKOSI: 
Arsenal: Szczesny, Chambers, Mertesacker, Koscielny, Gibbs, Flamini, Cazorla, Ozil (Wilshere 77), Sanchez (Ospina 62), Oxlade-Chamberlain (Rosicky 68), Welbeck.
Waliokuwa benchi: Coquelin, Bellerin, Campbell, Podolski.
Galatasaray: Muslera, Chedjou, Felipe Melo, Semih Kaya, Veysel (Bulut 68), Yekta (Altintop 46), Dzemaili, Telles, Sneijder, Pandev (Bruma 68), Burak Yılmaz.
Waliokuwa benchi: Bolat, Balta, Adin, Camdal. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS OKTOBA 02, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MKUU WA USALAMA MAREKANI JIUZULU

Julia Pierson mkurugenzi wa Usalama wa Taifa, Marekani
Mkuu wa Idara ya Usalama nchini Marekani, aliyekuwa na jukumu la kumlinda Rais Barack Obama, amejiuzulu kufuatia matukio yenye kuhatarisha usalama wa taifa yaliyotokea.
Mkuu huyo wa usalama Julia Pierson alikabidhi barua ya kujiuzulu kwa Waziri wa Usalama wa Ndani, Jumatano.
Siku moja kabla, alikabiliana na maswali ya wajumbe wenye hasira kutoka Baraza la Congress juu ya udhaifu mkubwa wa usalama wa Ikulu ya Marekani
Habari za tukio lingine likimhusisha mtu mwenye silaha kuruhusiwa kuingia katika lifti moja na Bwana Obama kulizidisha kutolewa wito wa kumtaka mkuu wa usalama kujiuzulu.
"Leo, Julia Pierson, mkurugenzi wa usalama wa taifa wa Marekani, amenikabidhi barua ya kujiuzulu, na nimeikubali," Waziri wa Usalama wa Taifa Jeh Johnson aliandika katika taarifa.
"Nampongeza kwa utumishi wake wa miaka 30 katika idara ya usalama na taifa." Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

CHINA YAONYA MGOGORO WA HONG KONG

 Waandamanaji Hong Kong
Waziri wa mambo ya nje wa China Wang Yi ametoa onyo kali dhidi ya maandamano "yasiyo halali" Hong Kong.
Akiwa katika ziara nchini Marekani, Bwana Wang pia alionya kuwa suala la Hong Kong linahusu "mambo ya ndani" ya China
Waziri mwenzake wa mambo ya nje wa Marekani, John Kerry, ameitaka Hong Kong kujizuia na matumizi ya nguvu wakati wa kushughulikia maandamano hayo.
Mapema, waandamanaji wanafunzi waliokasirishwa na China kuwateua wagombea wa uchaguzi wa mwaka 2017 waliapa kuendelea na maandamano iwapo kiongozi wa Hong kong, CY Leung hatajiuzulu.
Wamesema waandamanaji wataanza kukalia majengo ya serikali kama Bwana Leung hatajiuzulu ifikapo Alhamisi.
Waziri wa mambo ya nje wa China Wang Yi na John Kerry wa Marekani
Waandamanaji walikusanyika usiku kucha nje ya ofisi ya Bwana Leung, huku polisi 200 wakiwa katika eneo hilo.
Bwana Wang, afisa mwandamizi wa China wa ngazi ya juu akizungumzia waziwazi suala hili, alisema: "Masuala ya Hong Kong ni masuala ya ndani ya China. Nchi zote lazima ziheshimu uhuru wa China kujiamulia mambo yake yenyewe. Kwa nchi yoyote, kwa jamii yoyote, hakuna atakayeruhusu vitendo vilivyo kinyume cha sheria vinavyokuika utulivu wa umma."
Hata hivyo, alisema: "Tunaamini kuwa Utawala maalum wa serikali ya jimbo la Hong Kong ina uwezo wa kushughulikia hali hii kwa mujibu wa sheria."
Bwana Kerry amesema Marekani inaunga mkono madhila ya jumla huko Hong Kong, akisema: "Tuna matumaini makubwa kwamba mamlaka ya Hong Kong itajizuia kutumia nguvu na kuheshimu haki ya waandamanaji kueleza mawazo yao kwa amani." Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

Wednesday, October 01, 2014

BUNGE LA KATIBA: WALIOPIGA KURA YA HAPANA WATISHIWA MAISHA


Wahudumu  wa Bunge Maalumu la Katiba wakiwa wamebeba masanduku ya kura za wajumbe waliopiga kura za siri kwa Sura ya 11 hadi 19 ya Rasimu ya Katiba inayopendekezwa, mjini Dodoma jana.

Baadhi ya wajumbe wa Bunge la Katiba waliopiga kura za hapana wamelazimika kuondoka Dodoma na kurudi Zanzibar kwa madai ya vitisho walivyopata kutoka kwa wenzao.

Mmoja wa wajumbe hao, Salma Said alisema jana jioni kuwa yeye na wajumbe wenzake wamekataa kuitikia wito wa Mwenyekiti wa Bunge, Samuel Sitta kwenye Kamati ya Mashauriano ili kuhojiwa kuhusu kura hiyo na kutokana na vitisho wanavyopata kutoka kwa wajumbe wenzao wameamua kuondoka Dodoma.

Vitisho hivyo vimeripotiwa muda mfupi baada ya Sitta kuunda Kamati ya Mashauriano ya watu tisa inayoongozwa na Makamu Mwenyekiti, Samia Suluhu Hassan kushughulikia kura hizo zilizopigwa na wajumbe saba zinazoweka njiapanda uwezekano wa kupatikana akidi ya kupitisha Katiba inayopendekezwa.

Wajumbe waliopiga kura za wazi za hapana kwa ibara zote ni Adil Mohamed Adil, Dk Alley Soud Nassor, Fatma Mohamed Hassan, Jamila Ameir Saleh, Salma Hamoud Said, Mwanaidi Othman Twahir na Ali Omary Juma. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WALIODHURIKA KWA TOGWA SONGEA WAFIKIA 340...!!!


 

Idadi ya watu waliolazwa hospitalini kwa kunywa togwa inayosadikiwa kuwa na sumu katika Kijiji cha Litapwasi, Kata ya Mpitimbi mkoani Ruvuma imeongezeka kutoka 270 hadi 340.

Tukio hilo lilitokea Jumapili baada ya watu kushiriki sherehe ya Kipaimara ambako walikula, kunywa pombe na togwa na baadaye wale waliokunywa togwa walianza kuumwa matumbo, kuhara na kutapika.

Hadi jana, watu 102 walikuwa bado wamelazwa katika Zahanati ya Lyangweni, Hospitali ya St. Joseph Peramiho na Hospitali ya Mkoa wa Ruvuma.

Tayari watu watano wanashikiliwa na Polisi kwa upelelezi kuhusiana na tukio hilo, akiwamo Baba Mzazi wa mtoto Dickson aliyepata kipaimara, Enes Nungu (47). Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATANO OKTOBA 01, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MKE WA MUGABE KUSHITAKIWA...!!!

Grace Mugabe kulia
Muungano wa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini Zimbabwe al maarufu Zinasu, umesema kwamba unawasilisha kesi mahakamani hii leo kutafuta ufafanuzi zaidi wa namna mkewe rais Grace Mugabe alivyopata shahada ya udaktari wa falsafa.
Mwanafunzi mmoja mwanaharakati amesema kuwa ni muhimu kwa taifa hilo kuhifadhi hadhi yake ya elimu.
Baadhi ya watu wamehoji kasi aliyosomea shahada hiyo huku wengine wakidai ni njama za kumuandaa kwa urithi wa kiti cha rais baada ya rais Mugabe.
Gazeti moja linalomilikiwa na serikali , the Herald limechapisha kuwa Bi Grace Mugabe alipata shahada hiyo kwa utafiti wake juu ya mabadiliko ya mfumo wa kijamii na miundo ya familia. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

DRC: WAPIGANAJI WA ZAMANI WAFA NJAA

Wapiganaji hao wa zamani wamekuwa wakila chakula kutoka kwa mashamba ya wakulima
Shirika moja la kimataifa la kutetea haki za binadamu linasema kuwa zaidi ya watu mia moja wamefariki kutokana na njaa pamoja na maradhi katika kambi moja ya kijeshi katika Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.
Shirika hilo Human Rights Watch, limesema kuwa watu hao ambao walikuwa wapiganaji wa zamani na wake zao pamoja na watoto walihamishwa katika kambi nyingine iliyotengwa Kaskazini mwa DRC.
Ilikuwa baada ya wao kujisalimisha kutoka kwa kundi la wapiganaji Mashariki ya nchi.
Walipokea chakula kidogo na huduma ya afya baadhi wakiponea kifo kwa kuiba chakula kutoka kwa mashamba ya wakulima.
Serikali ya DRC inasema kuwa inachunguza ripoti hiyo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

UCL: MATOKEO YA CHELSEA VS SPORTING LISBON

IMG_7653.PNG
Usiku wa jana watu wawili waliowahi kuwa vipenzi vya nchi ya Ureno – Jose Mourinho na Nemanja Matic walirejea nchini humo katika jiji la Lisbon lakini safari hii wakiwa kama wapinzani.
Huku Mourinho akionekana kuchukua ‘attention’ yote ya vyombo vya habari ndani ya jiji Lisbon, Nemanja Matic alikuwa kasahaulika.
Lakini katika dakika ya 34, mchezaji huyo wa zamani wa Benfica aliifungia goli pekee Chelsea katika mchezo huo.
Matic alifunga goli hilo kwa kichwa baada ya kuachwa bila kukabwa vizuri na mabeki wa Sporting Lisbon.
Mchezaji wa zamani wa Manchester United Luis Nani alikuwa akiitumikia Sporting jana na hakuwa kwenye kiwango kizuri katika kipindi cha kwanza – kipindi cha pili alijitahidi lakini akashindwa kubadili matokeo ya mwisho dhidi ya vijana wa Jose Mourinho.
Takwimu na timu zilizopangwa
Sporting (4-3-3): Patricio 7; Cedric 6, Mauricio 5.5 (Oliveira 63, 6), Sarr 5, J.Silva 5; Mario 6, Carvalho 6, A.Silva 6 (Montero 81); Carrillo 6.5 (Capel 81), Slimani 6, Nani 6.
Subs not used: Marcelo, Jefferson, Martins, Rosell.
Bookings: Carvalho, Mario, Cedric, Mauricio
Manager: Marco Silva
Chelsea (4-2-3-1): Courtois 6; Ivanovic 6, Cahill 6, Terry 6, Luis 6.5; Matic 8, Fabregas 7; Schurrle 5 (Willian 57, 6), Oscar 7.5 (Mikel 71, 6), Hazard 7 (Salah 84); Costa 6.
Subs not used: Cech, Zouma, Azpilicueta, Remy.
Bookings: Ivanovic, Hazard, Luis Filipe, Fabregas
Manager: Jose Mourinho.

UCL: MATOKEO YA MAN CITY VS AS ROMA

IMG_7652.PNG
Mabingwa wa ligi kuu ya Uingereza klabu ya Manchester City imeendelea kutopata matokeo chanya katika michuano ya ligi ya mabingwa wa ulaya kwa mara ya pili mfululizo msimu huu.
Wakicheza kwenye uwanja wao wa Etihad dhidi ya AS Roma ya Serie A, Sergio Aguero aliipatia timu yake goli katika dakika ya 4 kupitia mkwaju wa penati.
Lakini dakika 19 baadae Francisco Totti ‘Mfalme wa Roma’ akaifungia goli la kusawazisha Roma na kuandika historia ya mchezaji mwenye umri mkubwa zaidi kufunga goli kwenye michuano ya ulaya.
Man City sasa inakuwa imeshindwa kupata matokeo chanya katika mechi 2 za kwanza cha UCL – wiki mbili zilizopita walifungwa na Bayern Munich.
Timu zilipangwa hivi
Manchester City: Hart 7; Zabaleta 6.5, Kompany 6, Demichelis 5.5, Clichy 6; Navas 5 (Milner 46, 6), Toure 5.5, Fernandinho 6, Silva 7; Aguero 6.5 (Jovetic 84), Dzeko 6 (Lampard 57)
Subs (not used): Caballero, Sagna, Kolarov, Mangala
Goals: Aguero (Pen, 4)
Booked: Zabaleta
Roma: Skorupski 6; Maicon 6 (Torosidis, 89), Manolas 6, Yanga-Mbiwa 6.5, Cole 6; Pjanic 7.5, Nainggolan 6.5, Keita 6.5; Florenzi 5.5 (Holebas 83), Totti 7 (Iturbe 72, 6), Gervinho 7.
Subs (not used): Curci, Ljajic, Destro, Paredes
Goals: Totti (23)
Booked: Maicon, Nainggolan
Referee: Bjorn Kuipers (Holland) 7
Star man: Miralem Pjanic
Attendance: 37,509

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...