Monday, August 11, 2014

BUNGE LAKODI VIPAZA SAUTI KWA SH. 8.9 MILLION KILA SIKU....!!!


Kwa maana hiyo Bunge, hilo linatumia Dola 5,400 sawa na Sh8.91 milioni kwa siku kugharimia vipaza sauti katika vyumba 12 vinavyotumiwa na kamati hizo na kwa siku 16  ambazo kamati zitakutana, gharama hizo zitafikia Sh142.56


Wakati kukiwa na malalamiko kwamba Bunge la Maalumu la Katiba linagharimu fedha nyingi za walipakodi, uongozi wa taasisi hiyo umetumia Sh142.56 milioni kukodi vipaza sauti kutoka Kituo cha Mikutano cha Kimataifa Arusha (AICC).

Katibu wa Bunge Maalumu, Yahya Khamis Hamad alithibitisha kukodiwa kwa vipaza sauti hivyo kwa ajili kamati zote 12 na kwamba kila gharama ya chumba kimoja kwa siku ni Dola 450 za Marekani (Dola moja ni wastani wa Sh1,650).

Kwa maana hiyo Bunge, hilo linatumia Dola 5,400 sawa na Sh8.91 milioni kwa siku kugharimia vipaza sauti katika vyumba 12 vinavyotumiwa na kamati hizo na kwa siku 16  ambazo kamati zitakutana, gharama hizo zitafikia Sh142.56. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MREMA AWATAMBIA UKAWA, AMUONYA MBATIA

Mbunge wa Vunjo, Augustine Mrema (TLP)

Mbunge wa Vunjo, Augustine Mrema (TLP) amedai kitendo cha yeye kubaki kwenye Bunge Maalumu la Katiba kumetumiwa vibaya na wahasimu wake wa kisiasa jimboni kwake.

“Ukawa na ubunge wa Vunjo vimegeuka propaganda chafu dhidi yangu. Wamediriki kuwaambia wananchi wangu kuwa nimeahidi kuwaachia jimbo langu,” alisema.
Mrema ambaye pia ni mwenyekiti wa taifa wa TLP, alitoa kauli hiyo jana jimboni kwake katika mkutano na waandishi wa habari aliouitisha kuelezea kwa nini hakuwaunga mkono Ukawa.
Mrema alisema malengo ya Ukawa siyo katiba bali Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 na ndiyo maana tangu waliposusia Bunge agenda yao imebadilika na kuwa muungano wa kuelekea uchaguzi 2015.
“Mimi nimeamua kubaki bungeni kwa ajili ya masilahi mapana ya wananchi wa jimbo langu la Vunjo na Watanzania kwa jumla. Sitishwi na Ukawa na nitatetea kiti changu 2015,” alisisitiza.
Mrema alitumia mkutano huo kumshambulia mbunge wa kuteuliwa na Rais, ambaye ni James Mbatia kutokana na uamuzi wake wa kutangaza nia ya kuwania ubunge wa Jimbo hilo mwakani. Kwa mujibu wa Mrema, ndiye Mtanzania pekee mwenye sifa na aliweza kugombea ubunge katika majimbo matatu tofauti na kushinda.
“Mimi ni Mtanzania pekee ambaye nimewahi kuwa mbunge wa majimbo matatu tofauti ya Moshi Vijijini, Temeke na Vunjo. Sifa hizo hazipo kwa wengine,” alisema. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ZESCO YATIBUA SHEREHE YA SIMBA DAY...!!!

Mabao matatu yaliyofungwa na Jackson Mwanza, Clatons Chama na Winston Kalenga, yamesababisha siku ya Simba ‘Simba Day’ kuwa chungu baada ya Zesco kuizamisha miamba hiyo kwa mabao 3-0.
Safu ya ulinzi ya Simba iliyoshindwa kuelewana iliizawadia Zesco ya Zambia mabao matatu, wakati wa mchezo huo wa kuadhimisha siku muhimu ya klabu hiyo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ikiwa inatumia mchezo huo kwa ajili ya kutambulisha wachezaji wake wapya iliyowasajili, Simba iliendeleza rekodi yao ya kutoshinda katika mchezo wa Simba Day tangu kuanza kuiadhimisha siku hiyo.
Ukihudhuriwa na mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Fedha, Adam Malima, ambaye aliwataka Simba kucheza kimataifa zaidi, kikosi hicho cha kocha Zdravko Logarusic kilijikuta katika siku mbaya msimu huu.
Simba ilianza kuruhusu bao la kwanza dakika ya 14, wakati Mwanza akiunganisha kwa kichwa krosi safi kutoka wingi ya kushoto. Mabeki wa kati wa Simba, Donaldi Mosoti na Joseph Owino walionekana kushindwa kujua nani wa kumkaba na kumuacha Mwanza akiruka peke yake.
Mshambuliaji mpya wa Simba, Paul Kiongera alishirikiana vizuri na Amissi Tambwe, lakini hawakuwa makini kwani Tambwe alikosa nafasi kadhaa za wazi.
Nafasi ya kwanza kwa Tambwe ilikuwa dakika ya saba, wakati shuti la Kiongera lilipopanguliwa na kipa wa Zesco, lakini Tambwe alishindwa kuumalizia mpira huo vizuri.
Simba ilikuwa na kipindi cha pili kibaya zaidi, kwani mabeki wake wa kati walisababisha penalti kwa kumwangusha Chama aliyekuwa anakwenda kufunga na mshambuliaji huyo kuukwamisha mkwaju huo wavuni.
Dakika tano za nyongeza zilikuwa mbaya zaidi kwa Simba, ambapo shambulizi la kushtukiza lilizaa bao baada ya mabeki wa Simba kwa mara nyingine wakishindwa kuondoa krosi ndogo ambayo ilimaliziwa kiufundi na Kalenga. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATATU AGOSTI 11, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MADAKTARI WATOA TAHADHARI YA EBOLA

madaktari wakitoa huduma dhidi ya Ebola
Shirika la Madaktari wasio na mipaka Medecins Sans Frontiers wametahadharisha kuhusu wizara ya afya nchini Liberia kuzidiwa nguvu na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola katika eneo la Afrika Magharibi.
Mratibu wa mambo ya dharura wa shirika hilo nchini humo amesema serikali haikutilia maanani vya kutosha madhara ambgayo yangesababishwa na ugonjwa huo na kwamba mfumo wa afya kwa sasa upo katika hali ya kushindwa.
Nchini Siera Lione, majeshi yameweka vizuizi katika maeneo yaliyoathirika na ugonjwa huo.
Raia wa Uingereza ambaye ni mfanya biashara katika eneo la Kanema kaskazini mwa nchini hiyo anaeleza madhara wanayopata kutokana vizuizi vya zilivyowekwa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAREKANI KUENDELEA KUISHAMBULIA IRAQ

Wapiganaji wa Kurdi
Marekani imeendeleza mashambulizi ya anga kaskazini mwa Iraq kwa lengo la kuwasaidia Wakrud katika mji wa Erbil dhidi ya wapiganaji wa kiislam wa kundi la Jihad.
Wapiganaji wa kundi hilo la Kiislam hivi karibuni wameendelea kuimarisha ngome yao katika eneo hilo ikiwa ni pamoja na kuiteka ngome kubwa ya Iraq katika mji wa Mosul. Jeshi la Marekani limesema limefanya mashambulizi dhidi ya wapiganaji wa Sunni waliokuwa wamejificha katika milima iliyo eneo la wakimbizi la Yazid.
Hata hivyo Uingereza imesema inaendelea kutoa misaada ya kibinadamu kwa Wakurdi ambapo Ofisa wa zamani wa mambo ya kigeni wa Uingereza Alistair Burt anasema nchi hiyo inaweza kusaidia eshi la Wakurdi.
Wakati huo huo vikosi vya majeshi ya Iraq na vyombo vya usalama vimesambaa katika katika maeneo mbalimbali ya mji wa Baghdad huku kukiwa na hali ya wasiwasi kufuatia kauli iliyotolewa na waziri mkuu wa nchi hiyo ya Iraq Nouri al-Maliki inayodaiwa kuwa ni ya utovu wa nidhamu kwa Rais wa nchi hiyo Fuad Masum.
Amesema kuwa Rais wa Jamhuri hiyo amevunja katiba mara mbili,mara ya kwanza ni pale alipojiongezea muda wa kukaa madarakani,wakati alistahili kutangaza kuvunja bunge. Hata hivyo kipindi chake kiliisha august saba alhamisi iliyopopita.
Hata hivyo papa Francis ameelezea gogoro wa Ira kwamba msingi wake mkubwa ni masuala ya tofauti za kidini. Melfu ya watu nchini Iraq wamekuwa wakilazimishwa na wapiganaji wa kiislam ambao wameimarisha ngome ao kaskazini mwa nchi hiyo.Katika ujumbe wake wa jumapili ,papa Francis ametoa wito kwa dunia kukomesha uhalifu huo unaoendelea nchini Iraq. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Saturday, August 09, 2014

WASALITI UKAWA: WAJIANDAE KUWA 'WABUNGE WA MAHAKAMA'

Mjumbe wa Bunge la Katiba (Chadema) Said Arfi  akisaini karatasi ya mahudhurio bungeni jana, kabla ya kwenda  kushiriki mjadala wa kamati  yake.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema kuwa wabunge wote walio wanachama wake, lakini wanakiuka msimamo wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kwa kuingia katika Bunge la Katiba, wajiandae kuongeza idadi ya ‘wabunge wa mahakama’.
Kauli hiyo ya tahadhari imetolewa na Mwanasheria Mkuu wa Chadema, Tundu Lissu alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu hatua ya baadhi ya wabunge wa chama hicho kuonekana mjini Dodoma, kunakofanyika vikao vya Bunge Maalumu la Katiba (BMK) ambalo Ukawawamesusia kuhudhuria.
“Ni bora wawe wabunge wa mahakama kama mwenzao (akimlenga Zitto Kabwe), kuliko kuendeleza usaliti ndani ya chama. Tunatarajia kukaa na wenzetu kushauriana nini cha kufanya dhidi ya wote wanaoenda kinyume na  msimamo wa Ukawa,” alisema Tundu Lissu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI AGOSTI 09, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

LIPUA LIPUA YA KAMATI ZA BUNGE MAALUMU LA KATIBA

Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba wakitoka kwenye ukumbi wa Bunge mjini Dodoma wakati wa mapumziko ya mchana. Picha na Emmanuel Herman.

Kamati za Bunge Maalumu la Katiba zilizoanza vikao vyake juzi mjini Dodoma, zimejikuta zikifanya kazi kwa kulipua kutokana na uchache wa muda uliotengwa, ikilinganishwa na ukubwa wa kazi ya uchambuzi wa ibara za rasimu ya Katiba hiyo.
Kamati hizo zimetengewa siku 14 kwa ajili ya kujadili na kuchambua sura 15 za rasimu hiyo na siku mbili za kuandaa taarifa ambazo zitaanza kuwasilishwa kwenye Bunge Maalumu, Septemba 2, mwaka huu.
 Hata hivyo, baadhi ya wajumbe wamekuwa wakilalamikia ufinyu wa muda uliotengwa na kwamba kazi imekuwa ikifanyika kwa kulipua, ili kuhakikisha kwamba wanamaliza katika muda uliopangwa.
 Malalamiko hayo yanatokana na ukweli kwamba baadhi ya sura za rasimu zina ibara nyingi ambazo ni vigumu kuzijadili kwa kina, kuzifanyia marekebisho kisha kuzipigia kura kwa lengo la kuzipitisha.
 Waraka wa mgawanyo wa sura kwa siku za mjadala katika Kamati za Bunge Maalumu unaonyesha kuwa kamati zilipaswa kujadili sura ya pili na ya tatu za rasimu hiyo siku ya kwanza zilipoanza kuketi, sura hizo zina jumla ya ibara 13, kazi ambayo baadhi ya wajumbe walisema ilikuwa ni vigumu kuikamilisha kwa siku moja.
 Mwenyekiti wa Kamati namba tano, Hamad Rashid Mohamed juzi alikiri kuwapo kwa changamoto ya muda lakini akasema: “Hiyo ndiyo hali halisi, lazima tutumie muda huo ambao tumepewa na tufanye kazi kwa ufanisi”. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WABUNGE WA CCM WAMEGUKA KATIBA MPYA...!!!




Kwa nini tukae siku 87 au 90 wakati tunajua upande wa pili haujakamilika? Kwa mujibu wa sheria inatakiwa ridhaa ya theluthi mbili. Mwigulu Nchemba 

Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimeanza kumeguka baada ya baadhi ya wabunge wake ambao ni Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, kuunga mkono kauli ya Naibu Katibu Mkuu wake, Mwigulu Nchemba.

Nchemba ambaye pia ni Naibu Waziri wa Fedha, Jumanne iliyopita akichangia wakati wa mjadala wa mabadiliko ya kanuni, alilitaka Bunge Maalumu la Katiba lijitathmini kama lina ulazima wa kuendelea wakati hakuna uhakika wa kupatikana kwa theluthi mbili.


Alisema kitendo cha Bunge hilo kukaa kwa siku 84 bila uhakika wa kupatikana kwa theluthi mbili kwa pande zote mbili inayohitajika kupitisha Rasimu ya Katiba Mpya, hakiwezi kueleweka kwa Watanzania.

Nchemba alisema ni vyema kujua idadi ya wanaoshiriki awamu ya pili ya Bunge hilo ili kutoa uthibitisho  kimahesabu kama uamuzi wa kuendelea kwa Bunge unaweza kuwa na maana.

Jana Mwigulu Nchemba alizidi kusisitiza kauli aliyoitoa akisema ni msimamo wake binafsi kama mtoto wa maskini. Alisema anatambua jinsi walipa kodi watakavyoumia, rasimu hiyo itakapokwama kupita kutokana na kukosekana kwa theluthi mbili ya pande zote.


Hata hivyo, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye  juzi alijibu akisema kauli ya Nchemba ni mtazamo wake binafsi na hakuongea kama kiongozi wa chama hicho.

Lakini jana wabunge mbalimbali wa CCM walijitokeza hadharani wakisema wanaunga mkono kauli ya Nchemba ili hesabu ijulikane badala ya kuendelea kutafuna fedha za wananchi bila tija.

Ali Keissy

Mbunge wa Nkasi Kaskazini, Ali Keissy, alisema msimamo wa Nchemba ndiyo msimamo sahihi ambao unapaswa kufuatwa kuliko kuendelea na Bunge wakati wakijua kuwa theluthi mbili haitapatikana.

“Kama kuna wabunge wa CCM wanaounga mkono kauli ya Mwigulu kwa asilimia 100 basi mimi naunga mkono kwa asilimia 500 na wako wabunge wengi tu wa CCM wanaunga mkono,” alisema. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WATU 6 WAUAWA KATIKA GHASIA SOMALIA

Wapiganaji wa Al-shabaab
Takriban watu sita wameuawa katika ghasia katikati mwa Somali.
Ijumaa usiku, wanamgambo kutoka kundi la Alshabaab walishambulia kambi moja ya wanajeshi wa Umoja wa Afrika katika mji wa Buloburde ,yapata kilomita 200 kazkazini mwa mji mkuu wa Mogadishu.
Vikosi vya Amisom viliuteka mji wa Buloburde kutoka kwa Alshabaab mapema mwaka huu,lakini wanamgambo hao bado wanadhibiti eneo kubwa la viungani mwa mji huo.
Wameendelea kutekeleza mashambulizi mjini Mogadishu ili kujaribu kuiondoa serikali inayoungwa mkono na jamii ya kimataifa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Thursday, August 07, 2014

MBUNGE CHADEMA ATINGA BUNGENI...!!!

Mbunge wa Viti Maalumu, Chadema  Leticia Nyerere akiwa kwenye viwanja vya bunge jana mjini Dodoma. 

Mjumbe mwingine wa Bunge la Katiba kutoka Kundi la Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) jana alionekana kwenye Viwanja vya Bunge na alisaini za mahudhurio.
Mjumbe aliyeonekana jana, Leticia Nyerere wa viti maalumu, Chadema, anafanya idadi ya wajumbe waliotinga kwenye viwanja hivyo hadi sasa kufikia watatu baada ya Chiku Abwao (viti maalumu Chadema) kuonekana juzi na Clara Mwatuka (viti maalumu CUF) kuonekana Jumapili.
Nyerere hakuwa akihudhuria vikao baada ya Ukawa kutangaza kususia Bunge mwezi Aprili na jana hakupatika kuzungumzia suala hilo.
Kuonekana kwa mjumbe hao kunaweza kutafsiriwa kuwa ni kubomoka kwa ngome za Vyama vya Chadema, NCCR na CUF vinavyounda umoja huo kwani tangu awali walikubaliana kutoshiriki shughuli za Bunge hadi pale watakapofikia makubaliano ya hoja zao. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

POLEPOLE: 'ANAYEZUIA MIJAALA YA KATIBA AMEPOTEZA SIFA YA KUWA RAIS'

Aliyekuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Hamphrey Polepole akizungumza kwenye mjadala wa wazi kuhusu Katiba mpya, uliofanyika jijini Dar es Salaam jana.

Aliyekuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Humphrey Polepole amesema makongamano na mijadala inayohusu Katiba mpya yataendelea kwa sababu ni ya lazima pia ni haki ya kikatiba.
Akizungumza kwenye Kongamano la Katiba lilioandaliwa na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) jana, Polepole alisema mtu anayezuia wananchi kuendelea kuzungumzia Katiba amepoteza sifa za kuwa kiongozi wa nchi.
Huku akishangiliwa na washiriki wa kongamano hilo, Polepole alisema Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi ya kidemokrasia, inayoheshimu haki za binadamu na utawala wa kiraia. Hivyo inashangaza kusikia kuna kiongozi anajaribu kuwafunga mdomo wananchi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAPENZI YA KWELI: WAAGA DUNIA PAMOJA BAADA YA MIAKA 62...!!!

Don na Maxine Simpson wakiwa hospitalini
Amini Usiamini mapenzi ya kweli bado yapo humu duniani!
Kisa kimoja ambacho kimedhibitishia wengi baada ya wapenzi wawili waliooana na kuishi pamoja kwa takriban miaka 62 walipoaga dunia pamoja.
Don na Maxine Simpson walikuwa wakazi wa mji wa Bakersfield, ulioko jimbo la California, Marekani waliaga dunia saa nne baada ya kushikana mikono hospitalini na kuahidiana penzi lao halitafifia kamwe hata mauti iwapate.
Walikuwa wamelazwa hospitalini kufuatia hali duni ya afya inayotokana na umri wao mkubwa.
Don na Maxine Simpson wakiwa bukheri wa afya
Lakini punde alipoaga Maxine na mwili wake ukaondolewa chumbani walikokuwa wamelazwa pamoja na mumewe Don, zilipata saa nne tu uchungu ulipomzidi Don na akakata roho iliwaendelee kupendana na mkewe ahera.
Mjukuu wao Melissa Sloan aliiambia runinga ya KERO-TV Kuwa Don alimhusudu sana nyanya yake yaani Maxine tangu alipomtupia jicho mnamo mwaka wa 1952 walipokutana katika mashindano ya Bowling.
Wapenzi hao wawili waliooana mwak huohuo na hawajawahi kuachana tangu hata katika mauti.
''Babu yangu alikuwa anatamani kuishi na nyanya yangu na hata baada ya wawili hao kuanza kuugua kutokana na umri wao mkubwa waliwaomba wasimamizi wa hospitali walimolazwa wasiwatenge.''
Don alikuwa na miaka 90 huku mke wake akiwa na miaka 87.
Don na Maxine Simpson walipokutana
''Babu yangu alihudumu kama mwanajeshi katika jeshi la Marekani naye bibi alikuwa ni muuguzi haswa walipokuwa huko Ujerumani ambapo waliwahi kuishi kwa muda mrefu.''alisema mjukuu wao Melissa.
Wamemuacha nyuma mtoto mmoja wa kiume na wajukuu watano.
Je unaamini kuna penzi la kweli ?
Tuwachie jibu lako katika mtandao wetu wa facebook BBCSwahili.com na pia kwenye tweeter @bbcswahili. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

BOKO HARAM WASHAMBULIA CAMEROON

Wapiganaji wa Boko haram
Watu wanaodaiwa kuwa ni kundi la Boko Haramu wameshambulia raia na wanajeshi kaskazini mwa Cameroon ambapo watu kumi wanasadikiwa kufariki dunia.
Shambulio hilo linakuja baada ya shambulio jingine la hivi karibu ambapo wapiganaji wa kundi hilo walivuka mpaka kutoka Nigeria na kufanya mashambulizi kadhaa kwa wiki za hivi karibuni nchini Cameroon.
Tayari majeshi kutoka katika ukanda huo yameahidi kupambana na wapiganaji hao wa Boko Haramu walioua watu 4000 wasio na hatia kwa mwaka huu pekee.

Ni shambulizi la mchana la kusikitisha. Waendesha piki piki wanadaiwa kuwa ni wapiganaji wa Boko Haram waliolenga kukishambulia kijiji caha Zigague kaskazini mwa Cameron.
Walimshambulia kiongozi wa jadi wa baadae kurushiana risasi na kundi la wanajeshi wa Jeshi la Cameroon. Mwanajeshi mmoja aliuawa pamona na raia nane.
Kundi hilo pia lilishambulia kituo cha polis.
Katika siku za hivi karibu wapiganaji wa Boko Haramu wamekuwa wakifanya mashambulizi katika nchi ya Cameroon. Kumekuwa na matukio kadhaa ya utekaji nyara jambo lilosukuma jeshi kuanza mapambano ya angani.
Mashambulizi mengi yanayofanywa Boko Haramu yamekuwa yakielekezwa nchini Nigeria ambapo mashirika ya kutetea haki za binadamu yanasema zaidi ya watu 4000 wameuawa kwa mwaka huu pekee.
Karika siku za hivi karibuni, Camerooni, Nigeria, Chad na Niger zilikubalina kuunda jeshi la pamoja la kanda hiyo ili kupambana na wapiganaji hao wa Boko Haramu. Hata hivyo Cameoroon wakati inatafuta namna ya kupambana Boko haram kunaongeza hali isiyo tabirika ya kuongezeka kwa mashambulizi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...