Waziri Mkuu, Mizengo
Pinda amesema kama Serikali ingejua, ingeanza kwa kura za maoni ya
wananchi kuamua aina ya muungano wanaoutaka, kabla ya kuendelea na
mchakato wa Katiba.
“Tungejua kama hali ya aina hii itajitokeza, basi
tungeanza na kura ya maoni, tungewauliza wananchi kama wanautaka
muungano na kama ndiyo, basi uwe wa aina gani au serikali ngapi, mtu
angesema moja, mbili, tatu na kadhalika,” alisema Pinda jana kwenye
Viwanja vya Bunge mjini hapa.
Pinda alikuwa akijibu swali kuhusu hatima ya Bunge
Maalumu kutokana na wajumbe wa Bunge hilo ambao ni wanachama wa Umoja
wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kususia vikao hivyo wakishinikiza kile
walichokiita kujadiliwa kwa rasimu iliyowasilishwa na Tume ya Mabadiliko
ya Katiba na siyo vinginevyo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz