Wednesday, August 06, 2014

PINDA: TUNGEJUA TUNGEAMUA AINA YA MUUNGANO KWANZA

Waziri Mkuu Mizengo Pinda PICHA|MAKTABA

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amesema kama Serikali ingejua, ingeanza kwa kura za maoni ya wananchi kuamua aina ya muungano wanaoutaka, kabla ya kuendelea na mchakato wa Katiba.
“Tungejua kama hali ya aina hii itajitokeza, basi tungeanza na kura ya maoni, tungewauliza wananchi kama wanautaka muungano na kama ndiyo, basi uwe wa aina gani au serikali ngapi, mtu angesema moja, mbili, tatu na kadhalika,” alisema Pinda jana kwenye Viwanja vya Bunge mjini hapa.
Pinda alikuwa akijibu swali kuhusu hatima ya Bunge Maalumu kutokana na wajumbe wa Bunge hilo ambao ni wanachama wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kususia vikao hivyo wakishinikiza kile walichokiita kujadiliwa kwa rasimu iliyowasilishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba na siyo vinginevyo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

YANGA SC WAIBUKA NA KUIPA MAKAVU ‘LAIVU’ CECAFA, WASEMA INALICHIMBIA SOKA KABURI


benomarcio

Katibu Mkuu wa Young Africans Bw Beno Njovu akiongea na waandishi wa habari leo makao makuu ya klabu ya Yanga, kushoto kwake ni Kocha Mkuu Marcio Maximo na afisa habari Baraka Kizuguto
Uongozi wa klabu ya Young Africans leo umefanya mkutano na waandishi wa habari juu na kusema kilichofanywa na waandaji wa michuano ya Kombe la Vilabu Bingwa ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) kuiondoa timu isishiriki ni cha kushangaza sana na kinadidimiza soka kwa ujumla.
Katibu Mkuu wa Young Africans Bw Beno Njovu amesema walipata barua ya mwaliko wa kushiriki mashindano tarehe 25/7/2014 na kudhibitisha kushiriki michuano hiyo kwa kuandika barua iliyokwenda TFF na kisha wao kuiwasilisha kwa CECAFA.
“Baada ya kudhibitisha kushiriki michuano hiyo tuliambiwa na CECAFA tutume orodha ya wachezaji na viongozi ambao watasafiri kuelekea nchini Rwanda kwenye michuano hiyo ili waweze kuandaa tiketi za ndege na sehemu ya malazi kitu ambacho tulitimiza” alisema Beno. 
Lakini katika hali ya kushangaza jana tulipokea barua kutoka TFF ikisema CECAFA imetuondoa kwenye mashindano hayo kwa kushindwa kukidhi vigezo na kuiteua timu ya Azam kuchukua nafasi yetu “aliongeza Beno.”

FRANK LAMPARD ANAWEZA KUFIKIA REKODI YA KUCHEZA MECHI 1,000 AKIWA MANCHESTER CITY

_76387466_frank_lampard_chelsea_getty
FRANK James Lampard, mwenye miaka 36, mpaka sasa amecheza mechi 973 kwa klabu na nchi yake katika maisha ya soka.
Anahitaji mechi 27 tu kufika digiti nne na kitu hicho anaweza kufanya kupitia michuano ya ligi kuu soka nchini England baada ya kujiunga na Manchester City kwa mkopo kutoka klabu ya New York City mwezi huu.
Kiungo huyo mkongwe ataitumikia Man City mpaka mwezi Januari mwakani ambapo ataende NYCFC kujiandaa na michuano ya ligi kuu nchini Marekani.
Atakuwepo kwa michezo 23 ya ligi kuu, mechi sita za ligi ya mabingwa, ataanza kombe la Capital One na FA na mechi ya Ngao ya Hisani itakayopigwa siku ya jumapili.
Lampard ambaye bado hajastaafu soka la kimataifa, ana nafasi kubwa ya kuongeza mechi zake 106 alizocheza kwa timu ya taifa baada ya kurudi ligi kuu.
Lampard ndiye mchezaji aliyecheza mechi nyingi zaidi kwa taifa lake. Pia alicheza England B na alicheza mara 19 katika timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 19.
Kiungo huyo alicheza mechi 187 akiwa na Westaham, klabu yake ya kwanza na alicheza mechi 11 akiwa kwa mkopo Swansea kabla ya kwenda kucheza mechi 649 katika miaka 13 aliyocheza Chelsea, na kujiweka katika nafasi ya tatu ya kucheza mechi nyingi klabuni hapo nyuma ya Peter Bonetti na mchezaji anayeshikilia rekodi Ron Harris.
Mchezaji wa mwisho wa England kufikisha mechi 1,000 katika timu ya wakubwa alikuwa kocha msaidizi wa Manchester United, Ryan Giggs ambapo alifikisha idadi hiyo mwaka 2013 kwenye mechi za ligi ya mabingwa dhidi ya Real Madrid.
Kocha wa sasa wa Fleetwood, Graham Alexander, ambaye aliichezea Scunthorpe United, Luton Town, Preston North End na Burnley alifikisha mechi 1,00 mwezi aprili 2011.

Tuesday, August 05, 2014

MJUMBE WA UKAWA ATINGA BUNGENI...!!!

Bunge  

Wakati wajumbe wa Bunge la Katiba wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wakiendelea na msimamo wa kususia vikao vinavyotarajiwa kuanza leo mjini Dodoma, mmoja wa wajumbe wake jana aliripoti bungeni na kujiandikisha.
Mjumbe huyo, Clara Mwatuka ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu (CUF), alionekana katika Viwanja vya Bunge saa 6:30 mchana akiwa ameongozana na wabunge kadhaa wa CCM wakiwamo Livingstone Lusinde (Mtera) na Jerome Bwanausi (Lulindi).
CUF ni moja ya vyama vinavyounda Ukawa, pamoja na Chadema na NCCR Mageuzi na tayari viongozi wakuu wa vyama hivyo, Profesa Ibrahim Lipumba, Freeman Mbowe na James Mbatia wametangaza kwamba wajumbe wote wanaotokana na umoja wao hawatashiriki vikao vya Bunge hilo.
Mwatuka baada ya kujaza fomu maalumu za kujiandikisha, alielekea lango la Magharibi na kuingia kwenye gari la Bwanausi.
Awali, alipoulizwa kwenye Viwanja vya Bunge kuhusu kuwapo kwake Dodoma, alikataa kuzungumza lakini alikiri kujiandikisha bungeni.
Baadaye alipoulizwa imekuwaje akajiandikisha ilhali uongozi wa chama chake umesema hawatashiriki, Mwatuka alijibu: “Kwa hapo ni mapema sana kuzungumzia suala hilo, nitazungumza kesho (leo) kule bungeni ukinitafuta.” Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMANNE AGOSTI 05, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ISRAEL NA HAMAS KUSIMAMISHA MAPIGANO?

Mwanajeshi wa Israel
Israel na Hamas yamekubaliana kufuata maombi ya Misri ya kusimamisha mapigano kwa siku tatu huko Gaza, kuanzia leo jumanne asubuhi.
Israel inasema kuwa itakubaliana na mpango huo bila ya masharti yoyote.
Nayo Misri inasema kuwa muafaka huo unafaa kufuatiwa na mazungumzo ya amani yenye nia ya kuboresha kabisa usalama.
Majeshi ya Israeli awali yalirejelea operesheni kali zaidi huko Gaza, baada ya kumalizika kwa makataa ya saa saba ya kukomesha mapigano. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BENKI YA DUNIA YASAIDIA EBOLA

Wahudumu wa afya katika tahadhari ya kukabiliana na Ebola
Benki ya Dunia imetangaza kutoa msaada wa hadi dola milioni mia mbili, kutoka mfuko wa dharura wa msaada, ili kuzisaidia mataifa matatu ya Afrika magharibi kukabiliana na ugonjwa hatari wa ebola.
Pesa hizo zitasaidia Liberia, Sierra Leone na Guinea, ili kuboresha vifaa vya afya ya umma na kushughulikia matatizo ya uchumi yaliyosababishwa na ugonjwa huo.
Rais wa Bank ya Dunia Jim Yong Kim amesema amehuzunishwa sana kwa jinsi Ebola unavyoendelea kuvuruga mfumo wa afya kwa nchi tatu.
Kwa mwaka huu pekee karibu watu mia nane na tisini wamekufa kutokanana Ebola katika nchi za Afrika Magharibi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

RAGE APATA AJARI DODOMA...!!!

adenrage
RAIS Mstaafu wa klabu ya Simba Sc  Mbunge wa Jimbo la Tabora Mjini, Ismail Aden Rage (CCM), ambaye pia ni Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, amenusurika kifo na kuumia bega la Kushoto akiwa na watu wengine watatu baada ya gari alilokuwa akitumia kusafiria aina ya Toyota Land Cruser T 845 BQS (gari binafsi) kuacha njia na kuanguka katika eneo la Chigongwe wakati akiwa njiani kuelekea mjini Dodoma kuanza vikao vya Bunge la Katiba leo.
 Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma, David Misime, amesema ajali hiyo imetokea jana Agost 4, 2014 na kuwa imetokea katika eneo la Njia panda ya Kigwe katika barabara ya Singida Dodoma, wakati mbunge huyo akielekea mkoani Dodoma kwa ajili ya kuanza vikao vya Bunge Maalum la katiba.
 Amesema Rage, ameumia katika bega la kushoto na mgongoni huku Mbunge wa viti maalumu mkoa wa Tabora, Munde Abdalla Tambwe, akiumia sehemu za kichwani na kuwa majeruhi hao wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Dodoma. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
 Amesema watu wengine waliokuwepo katika gari hilo ni pamoja na Mwanahamis Athumani, John Hoya ambao wote kwa pamoja wanaendelea na matibabu katika hospitali hiyo. Hata hivyo amesema chanzo cha ajali hiyo bado hakijafahamika, na kuwa polisi wanaendelea na uchunguzi ili kujua chanzo cha ajali hiyo.

LIGU KUU KUTANGAZA MASHINDANO MAPYA YA ULAYA KWA VIJANA CHINI YA MIAKA 21

1407189839139_wps_2_Football_Chelsea_lift_the
Mabingwa: Chelsea wakishangilia kombe la vijana chini ya miaka 21 kutoka timu za ligi kuu msimu wa 2013/14 
MSIMU huu uongozi wa ligi kuu unatarajia kuzindua mashindano mapya ya kombe la ulaya kwa timu za ligi kuu nchini England chini ya miaka 21 na timu kutoka nje ya England.
Vikosi vya vijana chini ya miaka 21 kutoka timu nane (8) za juu katika msimamo wa ligi kuu Engalnd  zikiwemo klabu za Manchester City, Manchester United  na Chelsea vitashiriki pamoja na timu nane (8) kutoka nje ya England ambapo jumla ya timu itakuwa ni 16.
Hii hatua ni kutekeleza mkakati maalumu wa soka la vijana ulioanzishwa mwaka 2011 ili kuwaimarisha vijana wanaozalishwa na klabu za juu za England.
TIMU 16 ZITAKAZOSHIRIKI 
Timu za England: Chelsea, Fulham, Leicester City, Man City, Man Utd, Southampton, Sunderland, West Ham.
 
Timu za Ulaya: Celtic, Athletic Bilbao, Benfica, Borussia Monchengladbach, Schalke, FC Porto, PSV Eindhoven, Villarreal
Liverpool, walioshiriki ligi ya vijana chini ya miaka 21 msimu uliopita hawatashiriki mashindano hayo na badala yake nafasi hiyo imeenda kwa West Ham waliomaliza nafasi ya tisa katika msimamo msimu uliopita.
Mashindano hayo yataenda sambamba na ligi ya vijana chini ya miaka 21. 
Kwa sasa yatawavutia watu wengi zaidi kwasababu Sky Sports na BT Sports watarusha ‘Laivu’ mechi 10.
Waandaaji wana matumaini kuwa michuano hii itawavutia watu wengi na timu zitapata wachezaji wao wazuri ili kuwaingia katika timu za wakubwa.
Mkurugenzi wa akademi ya Schalke ,Oliver Ruhnert  alisaidia kuzalisha wachezaji wanne walioisadia Ujerumani kutwaa kombe la dunia mwaka huu na timu yake itashiriki michuano hiyo ya vijana chini ya miaka 21. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

YANGA SC HAWATASHIRIKI KOMBE LA KAGAME 2014, WAGOMA KUBADILI KIKOSI...!!!

126
TAARIFA Mpya usiku huu! Yanga hawatashiriki michuano ya klabu bingwa kwa ukanda wa Afrika mashariki na kati, maarufu kwa jina la Kombe la Kagame inayotarajia kuanza kutimua vumbi Agosi 8 mwaka huu,, mjini Kigali, Rwanda.
Hii imetokana na Yanga kugoma kubadili kikosi chao kama walivyotakiwa na CECAFA leo hii.
Taarifa zinaeleza kuwa Yanga wamekomaa na kikosi B kama walivyopanga wakati CECAFA wamewataka kwenda na kikosi B.
Awali ilielezwa kuwa Yanga wanatakiwa kubadilisha kikosi hicho kufikia alfajiri ya kesho na kama haitafanya hivyo, basi timu itatolewa kwenye mashindo.
Kwa mana hiyo, mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara, Azam fc wanaweza kupewa nafasi hiyo kama ilivyoelezwa awali. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...