Tuesday, August 05, 2014

MJUMBE WA UKAWA ATINGA BUNGENI...!!!

Bunge  

Wakati wajumbe wa Bunge la Katiba wanaounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wakiendelea na msimamo wa kususia vikao vinavyotarajiwa kuanza leo mjini Dodoma, mmoja wa wajumbe wake jana aliripoti bungeni na kujiandikisha.
Mjumbe huyo, Clara Mwatuka ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu (CUF), alionekana katika Viwanja vya Bunge saa 6:30 mchana akiwa ameongozana na wabunge kadhaa wa CCM wakiwamo Livingstone Lusinde (Mtera) na Jerome Bwanausi (Lulindi).
CUF ni moja ya vyama vinavyounda Ukawa, pamoja na Chadema na NCCR Mageuzi na tayari viongozi wakuu wa vyama hivyo, Profesa Ibrahim Lipumba, Freeman Mbowe na James Mbatia wametangaza kwamba wajumbe wote wanaotokana na umoja wao hawatashiriki vikao vya Bunge hilo.
Mwatuka baada ya kujaza fomu maalumu za kujiandikisha, alielekea lango la Magharibi na kuingia kwenye gari la Bwanausi.
Awali, alipoulizwa kwenye Viwanja vya Bunge kuhusu kuwapo kwake Dodoma, alikataa kuzungumza lakini alikiri kujiandikisha bungeni.
Baadaye alipoulizwa imekuwaje akajiandikisha ilhali uongozi wa chama chake umesema hawatashiriki, Mwatuka alijibu: “Kwa hapo ni mapema sana kuzungumzia suala hilo, nitazungumza kesho (leo) kule bungeni ukinitafuta.” Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMANNE AGOSTI 05, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ISRAEL NA HAMAS KUSIMAMISHA MAPIGANO?

Mwanajeshi wa Israel
Israel na Hamas yamekubaliana kufuata maombi ya Misri ya kusimamisha mapigano kwa siku tatu huko Gaza, kuanzia leo jumanne asubuhi.
Israel inasema kuwa itakubaliana na mpango huo bila ya masharti yoyote.
Nayo Misri inasema kuwa muafaka huo unafaa kufuatiwa na mazungumzo ya amani yenye nia ya kuboresha kabisa usalama.
Majeshi ya Israeli awali yalirejelea operesheni kali zaidi huko Gaza, baada ya kumalizika kwa makataa ya saa saba ya kukomesha mapigano. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BENKI YA DUNIA YASAIDIA EBOLA

Wahudumu wa afya katika tahadhari ya kukabiliana na Ebola
Benki ya Dunia imetangaza kutoa msaada wa hadi dola milioni mia mbili, kutoka mfuko wa dharura wa msaada, ili kuzisaidia mataifa matatu ya Afrika magharibi kukabiliana na ugonjwa hatari wa ebola.
Pesa hizo zitasaidia Liberia, Sierra Leone na Guinea, ili kuboresha vifaa vya afya ya umma na kushughulikia matatizo ya uchumi yaliyosababishwa na ugonjwa huo.
Rais wa Bank ya Dunia Jim Yong Kim amesema amehuzunishwa sana kwa jinsi Ebola unavyoendelea kuvuruga mfumo wa afya kwa nchi tatu.
Kwa mwaka huu pekee karibu watu mia nane na tisini wamekufa kutokanana Ebola katika nchi za Afrika Magharibi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

RAGE APATA AJARI DODOMA...!!!

adenrage
RAIS Mstaafu wa klabu ya Simba Sc  Mbunge wa Jimbo la Tabora Mjini, Ismail Aden Rage (CCM), ambaye pia ni Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, amenusurika kifo na kuumia bega la Kushoto akiwa na watu wengine watatu baada ya gari alilokuwa akitumia kusafiria aina ya Toyota Land Cruser T 845 BQS (gari binafsi) kuacha njia na kuanguka katika eneo la Chigongwe wakati akiwa njiani kuelekea mjini Dodoma kuanza vikao vya Bunge la Katiba leo.
 Kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma, David Misime, amesema ajali hiyo imetokea jana Agost 4, 2014 na kuwa imetokea katika eneo la Njia panda ya Kigwe katika barabara ya Singida Dodoma, wakati mbunge huyo akielekea mkoani Dodoma kwa ajili ya kuanza vikao vya Bunge Maalum la katiba.
 Amesema Rage, ameumia katika bega la kushoto na mgongoni huku Mbunge wa viti maalumu mkoa wa Tabora, Munde Abdalla Tambwe, akiumia sehemu za kichwani na kuwa majeruhi hao wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Dodoma. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
 Amesema watu wengine waliokuwepo katika gari hilo ni pamoja na Mwanahamis Athumani, John Hoya ambao wote kwa pamoja wanaendelea na matibabu katika hospitali hiyo. Hata hivyo amesema chanzo cha ajali hiyo bado hakijafahamika, na kuwa polisi wanaendelea na uchunguzi ili kujua chanzo cha ajali hiyo.

LIGU KUU KUTANGAZA MASHINDANO MAPYA YA ULAYA KWA VIJANA CHINI YA MIAKA 21

1407189839139_wps_2_Football_Chelsea_lift_the
Mabingwa: Chelsea wakishangilia kombe la vijana chini ya miaka 21 kutoka timu za ligi kuu msimu wa 2013/14 
MSIMU huu uongozi wa ligi kuu unatarajia kuzindua mashindano mapya ya kombe la ulaya kwa timu za ligi kuu nchini England chini ya miaka 21 na timu kutoka nje ya England.
Vikosi vya vijana chini ya miaka 21 kutoka timu nane (8) za juu katika msimamo wa ligi kuu Engalnd  zikiwemo klabu za Manchester City, Manchester United  na Chelsea vitashiriki pamoja na timu nane (8) kutoka nje ya England ambapo jumla ya timu itakuwa ni 16.
Hii hatua ni kutekeleza mkakati maalumu wa soka la vijana ulioanzishwa mwaka 2011 ili kuwaimarisha vijana wanaozalishwa na klabu za juu za England.
TIMU 16 ZITAKAZOSHIRIKI 
Timu za England: Chelsea, Fulham, Leicester City, Man City, Man Utd, Southampton, Sunderland, West Ham.
 
Timu za Ulaya: Celtic, Athletic Bilbao, Benfica, Borussia Monchengladbach, Schalke, FC Porto, PSV Eindhoven, Villarreal
Liverpool, walioshiriki ligi ya vijana chini ya miaka 21 msimu uliopita hawatashiriki mashindano hayo na badala yake nafasi hiyo imeenda kwa West Ham waliomaliza nafasi ya tisa katika msimamo msimu uliopita.
Mashindano hayo yataenda sambamba na ligi ya vijana chini ya miaka 21. 
Kwa sasa yatawavutia watu wengi zaidi kwasababu Sky Sports na BT Sports watarusha ‘Laivu’ mechi 10.
Waandaaji wana matumaini kuwa michuano hii itawavutia watu wengi na timu zitapata wachezaji wao wazuri ili kuwaingia katika timu za wakubwa.
Mkurugenzi wa akademi ya Schalke ,Oliver Ruhnert  alisaidia kuzalisha wachezaji wanne walioisadia Ujerumani kutwaa kombe la dunia mwaka huu na timu yake itashiriki michuano hiyo ya vijana chini ya miaka 21. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

YANGA SC HAWATASHIRIKI KOMBE LA KAGAME 2014, WAGOMA KUBADILI KIKOSI...!!!

126
TAARIFA Mpya usiku huu! Yanga hawatashiriki michuano ya klabu bingwa kwa ukanda wa Afrika mashariki na kati, maarufu kwa jina la Kombe la Kagame inayotarajia kuanza kutimua vumbi Agosi 8 mwaka huu,, mjini Kigali, Rwanda.
Hii imetokana na Yanga kugoma kubadili kikosi chao kama walivyotakiwa na CECAFA leo hii.
Taarifa zinaeleza kuwa Yanga wamekomaa na kikosi B kama walivyopanga wakati CECAFA wamewataka kwenda na kikosi B.
Awali ilielezwa kuwa Yanga wanatakiwa kubadilisha kikosi hicho kufikia alfajiri ya kesho na kama haitafanya hivyo, basi timu itatolewa kwenye mashindo.
Kwa mana hiyo, mabingwa wa ligi kuu soka Tanzania bara, Azam fc wanaweza kupewa nafasi hiyo kama ilivyoelezwa awali. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Monday, August 04, 2014

SUMAYE ATAJA SIFA 10 ZA RAIS AJAYE...!!!

Waziri Mkuu Mstaafu, Fredrick Sumaye 

Dar es Salaam. Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye ametaja sifa 10 za mtu anayefaa kuwania urais katika Uchaguzi Mkuu mwaka 2015 akiwataka wananchi kuzizingatia na kutokubali kudanganyika.
Alisema mbali na sifa hizo, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) inatakiwa kusimamia uchaguzi huo kwa haki na kuhakikisha kuwa daftari la kudumu la wapiga kura linafanyiwa maboresho ili kila Mtanzania apige kura kwa mujibu wa Katiba.
Sumaye alisema hayo jana wakati wa uzinduzi wa albamu Rose Muhando iitwayo ‘Kamata Pindo la Yesu’ katika Ukumbi wa Diamond Jubilee.
Sifa 10
Alisema sifa ya kwanza ni kuwa na kiongozi anayetambua, kuulinda na kuthamini umoja... “Kiongozi tunayemtaka lazima atambue hilo na awe tayari kuchukua hatua za kutuimarisha kuwa na nguvu zaidi za kiuchumi na kuimarisha muungano wetu na baadaye muungano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na hatimaye Afrika.” Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ASKOFU KAKOBE AWAUNGA MKONO UKAWA KWA KITENDO CHA KUSUSIA BUNGE

Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Zachary Kakobe (asiye vaa suti) akiongoza maandamano ya kuadhimisha miaka 25 ya kuanzishwa kwa kanisa hilo  yalianzia Viwanja vya Chuo Kikuu hadi Kanisani hapo eneo la Mwenge jirani na Mlimani City jijini Dar es Salaam jana. 

Askofu Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship (FGBF), Zachary Kakobe ameongeza chumvi katika Mchakato wa Katiba kwa kueleza kuwa anaunga mkono msimamo wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kutorejea kwenye awamu ya pili ya vikao vya Bunge Maalumu la Katiba.
Kakobe pia alimtupia lawama Rais Jakaya Kikwete akisema  hotuba yake ya kufungua Bunge hilo ndiyo chanzo cha kuvuruga mchakato mzima wa kupata Katiba Mpya.
Kakobe ametoa kauli hiyo zikiwa zimepita takriban siku tatu tangu Rais Kikwete alipotoa  hotuba yake ya kila mwezi na kujivua lawama hizo alizokuwa akitupiwa na watu wa kada mbalimbali.
“Naunga mkono Ukawa si kwa asilimia 100 bali asilimia 150 kwa msimamo wao wa kususia vikao. Tena sitegemei kusikia wamerejea bungeni, wakirejea watakuwa wamelogwa. Lazima wahakikishe upungufu huo unafanyiwa kazi kabla ya kurejea kwenye awamu ya pili ya vikao hivyo vilivyopangwa kuanza Agosti 5,” alisema. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KUHUSU TAARIFA ZA KUACHANA NA JAY Z, BEYONCE ATUMIA 'KUCHA' KUWAJIBU WATU...!!!

Picha: Beyonce atumia
Jay Z na Beyonce wanaendelea na ‘On The Run Tour’ ambayo imefanikiwa kwa kiasi kikubwa sana.
Taarifa za maandilizi ya talaka kati ya wanandoa Jay Z na Beyonce zimendelea kuandikwa na vyombo vikubwa vya habari ambavyo huaminika sana nchini Marekani na Uingereza.
Taarifa hizo zinazotolewa na vyanzo vya karibu zinaeleza kuwa wanandoa hao wameshatengana hata vyumba vya kulala wakati wakiwa wanaendelea na tour yao.
Hata hivyo, Beyonce amekuwa kimya huku akitumia lugha ya picha mara kadhaa kueleza kinachoendelea, na hivi sasa ameamua kutumia kucha zake kuonesha jinsi yeye na mumewe walivyoshibana tofauti na taarifa zilizoripotiwa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATATU AGOSTI 04, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAHASIMU WA SUDANI KUSINI WAKUTANA TENA

Kuna hofu na tisho la njaa Sudan Kusini
Mazungumzo ya amani kati ya serikali ya Sudan Kusini na waasi yameanza tena katika nchi jirani ya Ethiopia. Mazungumzo hayo, yalikuwa yameahirishwa kwa wiki kadhaa. Vita vimeendelea nchini Sudan Kusini licha ya makubaliano ya kusitisha vita kufikiwa kati ya pande husika.

Zaidi ya watu milioni moja unusu, wameachwa bila makazi kutokana na vita hivyo. Umoja wa Mataifa na mataifa mengine ya Magharibi yameonya kua Sudan Kusini inakabiliwa na tisho la kukumbwa na njaa.
Maafisa wa baraza la usalama la Umoja huo, wanatarajiwa kuzuru nchi hio wiki ijayo.

Katika mazungumzo hayo, serikali na waasi wanatarajiwa kuzungumzia swala la kubuni serikali ya mpito pamoja na muundo wake. Makataa ya makubaliano hayo ni chini ya wiki moja na huenda muda huo usifikiwe. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KESI YA WANABLOG YAAHIRISHWA

Kesi ya wanablogu kumi waliokuwa wanakabiliwa na mashitaka ya ugaidi imeahairishwa hadi Agosti 20.
Kesi hiyo ilianza leo miezi mitatu baada ya tisa kati yao kukamatwa na polisi.
Mmoja wa wanablogu hao alishtakiwa bila kuwepo mahakamani.
Wanakabiliwa na mashitaka ya ugaidi chini ya sheria iliyoshutumiwa ya kupinga ugaidi.
Kesi hii imevutia hisia kubwa nje na ndani ya Ethiopia, hiyo basi hakukuwa na tofauti kubwa ilipoanza hivi leo.
Mahakama hiyo ilijazwa na raia wa Ethiopia, wanahabari hali kadhalika maafisa wa kidiplomasia. Wote walioshitakiwa walifika mahakamani. Mawakili walikuwa wamepinga kwa mapema mashitaka hayo wakisema kuwa hayakuwa na msingi.
Hata hivyo mahakama ilikataa kuwaachilia kwa dhamana wanablogu hao jinsi walivyokuwa wakitaka mawakili wao. Wote kumi wameshitakiwa kwa kubuni kikundi haramu vile vile kushirikiana na makundi ya upinzani yaliyopigwa marufuku ng’ambo na nchini.
Waendesha mashtaka walisema kuwa washtakiwa hao walipokea ufadhili na mafunzo ya kutengeneza vilipuzi.
Kitendo hicho cha kuwakamata wanablogu kimesababisha serikali ya Ethiopia kushutumiwa kimataifa na kutaja kuwa inatumia sheria dhidi ya ugaidi kukandamiza upinzani na uhuru wa vyombo vya habari nchini humo.
Katika mahojiano ya hivi majuzi na BBC waziri mkuu wa Ethiopia alikanusha madai ya kuwakandamiza wanahabari lakini akasema kuwa serikali haitawavumilia wanablogu na wanaharakati wanaonekana kushirikiana na makundi ya kigaidi nchini humo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Tuesday, July 29, 2014

KAMA ULIKUWA HUJUI, HUYU NDIE ASKOFU BILLIONEA TANZANIA ... ANALINDWA KAMA RAIS.....!!!

ASKOFU na Nabii George David ‘Geordavie’ wa Kanisa la Geordavie Ministry ‘Ngurumo ya Upako’ lililoko jijini Arusha na Kawe, Dar hivi karibuni alifanya mkutano mkubwa na kutikisa nchini  kwa kuwa na magari ya kifahari na ndege aina ya helikopta ‘chopa’ iliyokuwa ikirandaranda juu ya anga kulinda usalama wake.

Katika mkutano huo uliofanyika Karatu mkoani Manyara, mwandishi wetu alishuhudia msafara wa Geordavie ambaye hutoa huduma ya uponyaji kwa njia za miujiza, ukiwavutia watu wengi kwa kuwa ulikuwa na ulinzi mkali ambao haujawahi kutokea. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SAKATA LA KUTUPWA KWA VIUNGO VYA BINADAMU, IMTU WAPANDA KIZIMBANI


Wafanyakazi  wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Tiba na Teknolojia (IMTU) cha Dar es Salaam wakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kinondoni jana.

Sakata la kutupwa kwa viungo vya binadamu bila kufuata utaratibu jana liligeuka sinema wakati maofisa wanne wa Chuo Kikuu cha Tiba na Teknolojia (IMTU), walipofikishwa mahakamani Dar es Salaam.
Maofisa hao ambao ni maprofesa na wahadhiri wa chuo hicho walifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni wakikabiliwa na mashtaka mawili likiwamo la kushindwa kufukia viroba 83 vya miili ya binadamu.
Baada ya mashtaka hayo kusomwa na taratibu za dhamana kukamilika huku mmoja wao akishindwa kutimiza masharti, watuhumiwa hao walirejeshwa kizimbani na kufutiwa mashtaka hayo kwa amri ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DDP) aliyewasilisha hati ya kutokuwa na nia ya kuendelea na mashtaka hayo.
Hata hivyo, furaha waliyoipata washtakiwa hao, Venkat Subbaiah (57), Appm Shankar Rao (64), Prabhakar  Rai (69) na Dinesh Kumar (27) ilikuwa ya muda tu, kwani polisi waliokuwapo mahakamani hapo waliwakamata tena na kuondoka nao.
Hati ya mashtaka
Akiwasomea mashtaka, Mwendesha Mashtaka Mwandamizi wa Polisi, Magoma Mtani alidai kuwa washtakiwa hao Julai 2014 katika eneo la Mpigi Majohe, walishindwa kufukia viroba 83 vya miili ya binadamu waliyoitumia kufundishia wanafunzi wa udaktari kinyume na Kifungu cha 128 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16 ya mwaka 2002. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...