Saturday, July 26, 2014

BASI LA HOOD LAPATA AJALI ASUBUHI YA LEO LIKITOKEA MBEYA


Muda mchache baada ajali kutokea. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
 Askari wa usalama wa barabarani wakiwa wamefika eneo la tukio  na baadhi ya Mashuhuda wakishuhudia ajali hiyo

SUDAN KUSINI YAKABILIWA NA BAA LA NJAA

Baa la njaa nchini Sudan Kusini

Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limeelezea uhaba wa chakula nchini Sudan Kusini kama mbaya zaidi kuwahi kuonekana duniani na kuyataka mataifa ambayo yaliahidi kutoa msaada wa zaidi ya dola millioni mia sita kutoa fedha hizo.
Limeonya kuwa vita vinavyoendelea kati ya vikosi vya serikali na waasi huenda vikasababisha baa la njaa nchini humo.
Shirika la chakula duniani WFP limesema kuwa iwapo hatua za haraka hazitachukuliwa watoto elfu hamsini huenda wakapoteza maisha yao kutokana na utapia mlo mwaka huu huku thuluthi moja ya raia wakikabiliwa na na viwango hatari vya njaa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

REINA ATHIBITISHA KUPENDA KUENDELEA KUICHEZEA LIVERPOOL

438662_heroa
MLINDA mlango wa Liverpool, Pepe Reina amejitia kitanzi mwenyewe katika klabu hiyo, licha ya kudai anapenda kustaafu soka la kimataifa nchini Hispania.
 Akicheza kwa mkopo Seria A katika klabu ya Napoli msimu uliopita-Reina alianza kuhusishwa kujiunga na bosi wake  wa zamani wa Anfield Rafael Benitez-na kuzua maswali juu ya hatima yake Liverpool.
 Reina amesisitiza kuwa anaheshimu mkataba wake Anfield-ambao utamalizka mwaka 2016 kabla ya kwenda nchini Hispania.
 “Nina mkataba ambao nahitaji kuuheshimu Liverpool,” Reina aliiambia radio ya Hispania ya Cadena Ser. “Ninafanya mazoezi vizuri na nipo sawa na wachezaji wenzangu”.
 “Nipo hapa kwa ajili ya kukaa”.
 “Sijazungumza na Brendan Rodgers, ni siku nne tu tangu nifike hapa, naangalia kufanya mazoezi vizuri ili kurudi katika kiwango changu”.
 Reina mwenye miaka 31 alianza maisha yake ya soka katika klabu ya Barcelona, kabla ya kwenda Villarreal na kuelekea ligi kuu nchini England, na sasa amekiri kuwa kurudi La Liga itakuwa nafasi nzuri kwake. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
 “Nimekuwa nikiwaza hili kwa muda mrefu kuwa ni vizuri kurudi ulipotoka,” Reina aliongeza.
 “Wakati Rafa Benitez ananisajili Liverpool mwaka 2005, nilikubali na nilisema nitarudi Hispania baadaye”.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JULAI 26, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC01150
DSC01151
DSC01152
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KATIBA MPYA NJIA PANDA, UKAWA WAAPA KUENDELEA KUSUSIA VIKAO

Mwenyekiti wa Bunge la Katiba, Samuel Sitta akisisitiza jambo juzi, baada ya mkutano wa Kamati ya Maridhiano uliofanyika jijini Dar es Salaam. 

Wakati Bunge Maalumu la Katiba likiazimia kuzifanyia marekebisho kanuni zake ili kuwabana wajumbe wa Bunge hilo ambao ni wanachama wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), viongozi wa kundi hilo wamesema hawatishwi na uamuzi huo na kwamba wataendelea kususia vikao hivyo.
Kikao kilichokuwa kiwe cha mashauriano kilichoitishwa juzi na Mwenyekiti wa Bunge Maalumu, Samuel Sitta kiliazimia kuzifanya marekebisho baadhi kanuni za uendeshaji kwa lengo la kusimamia nidhamu wajumbe wake, hatua inayotafsiriwa kwamba inawalenga Ukawa.
Jana Sitta akizungumza na Mwananchi Jumamosi alisema mabadiliko yanayokusudiwa kufanywa yatahusisha masuala ya nidhamu, yakiwamo fujo na utoro, mambo ambayo hivi sasa hayawezi kudhibitiwa moja kwa moja na mwenyekiti wa Bunge hilo.
Sitta alikuwa akitoa ufafanuzi wa taarifa iliyotolewa na ofisi yake jana na kusomwa mbele ya waandishi wa habari na Katibu wa Bunge Maalumu, Yahya Khamis Hamad, ikieleza maazimio ya kikao ya usuluhishi alichokuwa amekiitisha kwa ajili ya kutanzua mzozo unaotishia kukwama kwa mchakato wa Katiba Mpya.
Hata hivyo, Ukawa unaoundwa na wajumbe wa Bunge Maalumu kutoka Vyama vya Chadema, NCCR Mageuzi, CUF na baadhi ya wajumbe kutoka Kundi la 201 walioteuliwa na Rais, walisusia kikao hicho na kusababisha uamuzi uliofikiwa kuwa wa upande mmoja. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

OKWI, KIIZA WAMPASUA KICHWA MAXIMO

 Kocha wa Yanga, Marcio Maximo amesema mchezaji yeyote mwenye ubinafsi hana nafasi kwenye kikosi chake, huku akishindwa kujua yupi wa kumuacha kati ya wachezaji wawili wa kimataifa.
Akizungumza jana mara baada ya mazoezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Loyola, Maximo alisema hadi sasa hajaamua wa kumuacha kati ya Emmanuel Okwi na Hamis Kiiza.
“Kwa sasa siwezi kusema ninayemuacha hadi Septemba 17, nitatangaza nitakayemuacha, ila wachezaji wabinafsi hawatakuwa na nafasi katika kikosi changu.
“Nataka mchezaji anayejituma kwa moyo, anayepigania maslahi ya timu kwanza na si kukimbilia maslahi yake peke yake, tukiwa na umoja tunashinda pamoja, na kama tunapoteza tunaumia pamoja,” alisema Maximo. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Friday, July 25, 2014

MAGAZETI YA LEO IJUMAA JULAI 25, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


1_ba461.jpg
2_a3788.jpg
3_25f32.jpg 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TIBA, KINGA YA UKIMWI VYANUKIA

Watafiti wakitoa sampuli za damu kutoka kwa sokwe mtu katika utafiti wa Ukimwi huko Gabon. Picha ya Mtandao 

Watafiti katika Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba cha Temple, Marekani wamegundua dawa ya kuangamiza Virusi Vya Ukimwi (VVU) ambayo ni ya uhakika zaidi ukilinganisha na zilizowahi kupatikana katika tafiti za awali duniani.
Dawa yao inaweza kutumika kwa tiba ya wanaoishi na VVU na kinga kwa wale ambao bado hawajaambukizwa.
Mmoja wa watafiti hao, Dk Kamel Khalili aliwaambia waandishi wa habari juzi mjini Philadelphia, Marekani kuwa tofauti na utafiti mwingine, wao wamegundua namna ya kukiondoa kirusi kilichoingia kwenye kinasaba (DNA) ndani ya CD4 na kukitoa nje na hatimaye kukiua.
Alisema dawa hiyo inafanya kazi hiyo bila kuathiri seli za mwili wa binadamu.
Dk Khalili alisema ugunduzi wao ni wa hali ya juu zaidi kwa sababu teknolojia ya kutengeneza dawa hiyo ni tofauti na nyingine zilizokwisha kugunduliwa ambazo hazina uwezo wa kupenya ndani ya seli za binadamu, bali kuathiri tu VVU vilivyopo nje yake, ndani ya mfumo wa damu.
“Dawa yetu inakivuta kirusi nje ya seli (CD4) bila kuiathiri seli yenyewe na kukiua. Hivyo dawa hii itatumika kwa muda fulani na kuua virusi vyote mwilini na hakuna haja ya kuitumia wakati wote kama ilivyo dawa ya kufubaza VVU (ARV).” Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MABAKI YA NDEGE ALGERIA YAONEKANA

Mabaki ya ndege iliyopotea ikiwa na watu 116 njiani kutoka Burkanafaso kwenda Algers yamepatikana nchini Mali. Maafisa wa Jeshi wa Burkina faso wamesema ndege hiyo iliyokuwa chini ya shirika la ndege la Algeria imeanguka karibia kilomita 50 kutoka mpaka wa Burkanafaso.
Waongoza ndege walipoteza mawasilino na ndege hiyo muda mfupi baada ya kupata taarifa kutoka kwa Rubani kuwa alikuwa kwenye eneo lenye hali mbaya ya hewa. Utafutaji wa ndege hiyo umeanzia katika eneo la Gao mpaka Tessalit. 
Kumekuwepo na hali mbaya ya hewa kwa zaidi ya saa 24. Waziri wa mambo ya nje wa ufaransa, Laurent Fabius amesema inaonekana ndege ilihamishwa mwelekeo kwa sababu ya hali mbaya ya hewa.
 "Walikuwa wameelekezwa kubadili njia ya kawaida kutoka na mabadiliko ya hali ya hewa. Ndege ilikuwa ikipaa juu ya eneo la Malian. Pamoja na juhudi kubwa , mapaka sasa hakuna dalili za kupatika na kwa ndege hiyo. Pengine ndege imeangua" Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Sunday, June 29, 2014

HOTUBU YA WAZIRI MKUU MHESHIMIWA MIZENGO P. PINDA YA KUAHIRISHA BUNGE

PG4A9702
UTANGULIZI

a)    Masuala ya Jumla

Mheshimiwa Spika,
1.    Naomba nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu mwenye wingi wa Rehema kwa kutupatia uzima na afya hadi kufikia siku ya leo. Tumekuwepo hapa kwa takriban miezi miwili ambapo tumeweza kupokea na kujadili Taarifa za Mapitio ya Utekelezaji wa Kazi za Serikali kwa mwaka 2013/2014 na Mwelekeo kwa mwaka 2014/2015 kwa Wizara mbalimbali na hatimaye kupitisha Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2014/2015.


2.    Napenda kutumia nafasi hii ya awali kuwapongeza Waheshimiwa Wabunge wote kwa kazi nzuri ya kutukuka ambayo wameifanya kwa nidhamu na ufanisi mkubwa, hususan wakati wa Mjadala wa Bajeti ya Serikali na Mafungu ya Wizara za Kisekta. Kipekee niwashukuru Wajumbe wa Kamati ya Bajeti chini ya Uongozi mahiri wa Mheshimiwa Mtemi Andrew John Chenge, Mbunge wa Jimbo la Bariadi Magharibi kwa kazi yao nzuri ya kuchambua Bajeti ya Serikali na Sheria zinazoambatana na masuala ya Bajeti. Changamoto zilikuwa nyingi,   lakini   kwa   pamoja   tumekubaliana   na   kuafikiana. Kazi kubwa iliyoko mbele yetu ni kwenda kushirikiana na Wananchi katika utekelezaji wa Bajeti hii ili kuwaletea maendeleo.

Mheshimiwa Spika,
3.    Katika kipindi hiki tukiwa hapa Bungeni, yapo matukio ya kusikitisha yaliyotokea ambapo baadhi ya Waheshimiwa Wabunge walipoteza Wapendwa wao. Aidha, yapo matukio ya Kitaifa yaliyosababisha kupoteza maisha ya Ndugu, Jamaa na Marafiki. Napenda kutumia nafasi hii kuwapa pole Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote waliofikwa na misiba na majanga mbalimbali, ikiwa ni pamoja na wote waliopotelewa na Ndugu, Jamaa na Marafiki. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

JAMBO TZ BLOG INAWATAKIA WATU WOTE KHERI YA MFUNGO WA RAMADHANI

http://jambotz8.blogspot.com/

 Jambo Tz Blog inawatakia Watanzania wote kheri ya mfungo mtukufu wa Ramadan.
http://jambotz8.blogspot.com/
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JUNI 29, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ANGALIA PICHA ZA KIATU CHA MALKIA ELIZABETH WA UINGEREZA ALICHOVAA KWA MIAKA 50...!!!

kiatu

Hizi ndiz0 Picha za kiatu cha aina moja alichovaa malkia Elizabeth wa Uingereza kwa miaka 50. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

kiatu1
kiatu2
kiatu4
kiatu5 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ADA YA VYUO VYA UALIMU YAPANDA MARADUFU...!!!


Baadhi ya wahitimu wa chuo cha Ualimu.PICHA|MAKTABA
Serikali imepandisha maradufu ada kwa wanafunzi wanaosomea ualimu kwenye vyuo vya ualimu nchini kuanzia muhula ujao wa masomo. Ada hizo kwa wale wa ngazi za cheti na stashahada ambazo zimeongezwa kwa karibu mara mbili au zaidi ya zile zilizokuwa zikilipwa awali. Uamuzi huo ambao huenda ukawaathiri zaidi wanafunzi ambao waliona ualimu kama kimbilio, unaelezwa na baadhi ya wadau wakiwamo walimu, wanafunzi na hata wakufunzi wa baadhi ya vyuo nchini kuwa ni wa ghafla.
Kwa mujibu wa baadhi ya wakufunzi, uamuzi huo umetolewa kupitia waraka wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na unatarajiwa kuanza kutekelezwa muhula wa pili wa masomo utakaoanza Julai 2, mwaka huu.
Kabla ya kupandishwa kwa ada hizo, wanafunzi wanaosomea ualimu kwa ngazi ya cheti walikuwa wakilipa Sh200,000, lakini sasa watalazimika kulipa Sh300,000, ikiwa ni ongezeko la asilimia 50. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

CHINA HAITATUMIA MABAVU DHIDI YA MATAIFA MENGINE

Rais Xi Jinping amesema nchi yake haitawahi kutumia nguvu dhidi ya mataifa mengine Rais Xi Jinping wa Uchina amesema nchi yake daima haitojaribu kulazimisha nchi nyengine kufuata matakwa ya Uchina, hata Uchina itapokuwa na nguvu kubwa zaidi.

Alisema hayo mjini Beijing ambapo aliwapokea viongozi wa India na Myanmar (Burma). Rais Xi alisema tabia ya uonevu na kutumia nguvu za kijeshi haimo katika damu ya watu wa Uchina, na kwamba enzi za mabavu ya mataifa makuu zimekwisha.
Mwandishi wa BBC mjini Beijing anasema hotuba ya Rais Xi ilikusudiwa kuwatuliza majirani wa Uchina pamoja na Marekani, ambao wana wasi-wasi kwa vile bajeti ya jeshi la Uchina inazidi kuongezeka, na kile kinachoonekana kama sera ya Uchina ya kudai ardhi katika mizozo kadha na majirani zake.
Mkutano unaofanywa Beijing unaadhimisha miaka 60 ya makubaliano ya ushirikiano wa salama uliotiwa saini na Uchina, India na Burma - ambayo piya inajulikana kama Myanmar. Na nchini Taiwan shughuli mbili zimefutwa wakati wa ziara ya afisa mwandamizi wa Uchina, baada ya waandamanaji kuurushia rangi msafara wa magari yaliyokuwa yakimsindikiza afisa huyo.
Zhang Zhijun, ambaye amemaliza ziara ya siku nne Jumamosi, hakuumia katika mvurugano huo. Watu wengi wa Taiwan hawapendi Uchina kuonesha madaraka yake juu ya kisiwa hicho kinachojitawala, na ambacho Uchina inakiona kama ni chake. Katika miaka ya karibuni kiongozi wa Taiwan amekuwa akijaribu kuzidisha fungamanisho za kibiashara baina ya nchi mbili hizo.
Siku ya Ijumaa, Bwana Zhang alisema Beijing inaheshimu uamuzi wa watu wa Taiwan kuhusu aina ya maisha yao na mfumo wao wa jamii. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC Swahili

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...