Wednesday, May 14, 2014

HII NDIO ORODHA YA WASANII WA KILI TOUR 2014

Ile orodha ya wasanii watakaoshiriki kwenye Kili Music Tour 2014 imetangazwa leo. Kwa mwaka huu zaidi ya wasanii 30 watashiriki katika ziara hiyo kwenye mikoa zaidi ya 10 nchini na itakayoanza ambao Mei hadi Septemba 2014. Wasanii hao ni pamoja na Diamond, Ommy Dimpoz, Linex, Proffesor Jay, Izzo Biznes, Kala Jeremiah, Fid Q, Snura, Weusi, Ben Pol, Mzee Yusuph, Shilole na Mwasiti.
 
Wengine ni Nay wa Mitego, Mwana FA, Khadija Kopa, Juma Nature, Warriors From the East, Madee, Young Killer, Jambo Squad, AY, Vanessa Mdee, Mashujaa Band, Rich Mavoko na Christian Bella. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

HAWA NDIO WATU 10 TANZANIA WANAOTISHA KWA UTAJIRI


 1. SAID BAKHRESA
Jina lake kamili ni Said Salim Awadh Bakhresa. Jarida la Forbes mwaka jana, lilimuorodhesha miongoni mwa matajiri 40 Afrika kwamba anamiliki utajiri wenye thamani ya dola milioni 620 (karibu shilingi trilioni moja). 
Hata hivyo, inadaiwa kuwa tabia ya usiri wa Bakhresa inafanya mali zake zisijulikane sana, ila ni tajiri zaidi ya kiwango hicho.

Ndiye mmiliki wa makampuni ya Bakhresa yanayotoa bidhaa zenye chapa ya Azam ambazo zinauzwa nchi mbalimbali Afrika. Ana viwanda vya nafaka na vinywaji, vyombo vya usafiri wa majini, uuzaji wa chakula, bidhaa za plastiki na kadhalika. Ndiye mmiliki wa Klabu ya Azam FC.

2. GULAM DEWJI

Huyu ni baba wa mfanyabiashara maarufu nchini, Mohamed Dewji ‘Mo’. Jarida la Forbes mwaka jana lilimtaja kuwa na utajiri wenye thamani ya dola milioni 560 (karibu shilingi bilioni 900). Mafanikio yake kibiashara yalianza mwaka 1970. Kiwanda chake cha 21st Century Textiles, kinatajwa kuwa moja ya viwanda vikubwa vya nguo Afrika. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
3. ROSTAM AZIZ
Inadaiwa anamiliki utajiri wenye thamani ya dola milioni 420 (shilingi bilioni 672). Anamiliki karibu asilimia 40 ya hisa Kampuni ya Vodacom Tanzania. Ni mmiliki wa Kampuni ya Caspian inayohusika na uchimbaji wa madini na ukandarasi nchini Tanzania, nchi kadhaa za Afrika na Asia.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO MEI 14, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

FERDINAND KUONDOKA OLD TRAFFORD

Mlinzi wa Manchester United Rio Ferdinand amesema ataondoka Old trafford msimu ujao baada ya klabu hiyo kukataa kumuongezea muda kwenye kandarasi yake.
Kauli hiyo inamaanisha Ferdinand ambaye amefunga mabao nane Old Trafford katika miaka 12 na kushiriki katika mechi 454 ataingia katika orodha ndefu ya wachezaji wakongwe mabalozi wa klabu hiyo.
Mwandishi wa BBC anasema kuwa mlinzi huyo anapania kuendelea kucheza lakini haijulikani ataichezea klabu ipi.
pics Rio
Ferdinand kuhama Old Trafford.
Ferdinand alisema katika barua ya wazi kwa klabu hiyo kuwa angelipenda kuwaaaga mashabiki wake kwa njia bora zaidi lakini kutokana na ati ati hangeweza .
Hata hivyo amesema kuwa amefikiria sana kuhusu hatima yake na umewadia wakati wake kuwaaga.
Ferdinand aliwasili United Agosti 2002 kutokea klabu ya Leeds timu hiyo ilipokuwaikikabiliana na Hungary Zalaegerszeg katika mechi ya ligi ya mabingwa barani Ulaya.
Ameshinda mataji 6 ya ligi kuu ya premia mbali na mataji mawili ya nyumbani .
Manchester Utd pia ilishinda taji la klabu bingwa duniani mbali na taji la mabingwa barani Uropa. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Chanzo: BBCswahili

WACHIMBA MADINI 200 WAFARIKI UTURUKI

157 wameaga dunia katika mkasa wa moto ndani ya mgodi
Mlipuko katika mgodi wa makaa ya mawe magharibi mwa Uturuki umesababisha vifo vya zaidi ya wachimbaji migodi 200 na kujeruhi wengine wengi kujeruhiwa kwa mujibu wa maafisa nchini humo.
Waziri wa kawi, Taner Yildiz, amesema kuwa zaidi ya wafanyikazi 780 walikuwa katika mgodi huo pale kuliposikika mlipuko katika kitengo cha kusambazia umeme.
Waokoaji wanajaribu kila mbinu kuwafikia mamia ya wachimba migodi.
Inahofiwa kuwa wachimbaji mgodi wengine wengi bado wamefukiwa chini ya mgodi huo.
Inakadiriwa kuwa wakati mlipuko huo ulipotokea wafanyikazi 780 walikuwa ndani ya mgodi huo japo inaaminika wengi waliweza kukimbilia usalama wao .
Bado idadi ya walionaswa ndani ya mgodi huo haijabainika.
Mgodi huo uko katika mji wa Soma, mkoani Manisa , takriban kilomita 250 kusini mwa Istanbul. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
157 wameaga dunia katika mkasa wa moto ndani ya mgodi
Jamaa za wachimbaji migodi hao wamekusanyika katika makundi karibu na mgodi huo ambao unamilikiwa na wawekezaji wa kibinafsi huku wengi wao wakilia hadharani na kububujikwa na machozi.
Waziri wa nishati Taner Yildiz ameimabia televisheni ya Uturuki kuwa huenda wengi wamekufa kutokana na sumu ya gesi aina ya carbon monoxide.
Amesema moto huo umesababishwa na hitilafu ya umeme.
Picha za televisheni zinaonyesha maafisa wa uokoaji wakiokoa wafanyikazi wa mgodi huo, huku nyuso zao zao zikiwa zimejaa vumbi.
Baadhi yao wanaweza kutembea na wengine wanabebwa na kupelekwa ndani ya magari ya kubebea wagonjwa yaliyoegezwa karibu na eneo la tukio. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Tuesday, May 13, 2014

TAZAMA VIDEO YA JAY Z AKIPIGWA NA SHEMEJI YAKE MBELE YA MKEWE BEYONCE

Screen Shot 2014-05-12 at 11.40.31 PM 
Ni video kamili ikionyesha kilichotokea kwenye lifti ambapo rapper Jay Z anaonekana akipigwa na shemeji yake ambae ni Solange kwa muda usiopungua dakika 2 kwa kutumia pochi na mateke na baada ya hapo wakatoka nje ya lift.
Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, haya yalitokea wiki iliyopita kwenye After Party ya Met Gala ndani ya Standard Hotel, NYC na ndani ya video inaonesha Jay Z, Beyonce na Solange wakiingia katika Lifti halafu Solange anaanza kumuwakia Jay z kabla ya kuanza kumvamia wakati huo Beyonce akiwa pembeni tu ametulia na wala haingilii.

Bodyguard aliekuemo katika lifti hiyo alianza kumzuia Solange lakini alifanikiwa kuponyoka kama mara tatu hivi na kuendelea kumpiga Jay Z pia kuna muda Solange alirusha teke na Jay Z akazuia lakini hakurudisha kwa aina yeyote ile, sio kwamba alishindwa kumpiga ili alifanya maamuzi ya kuwa mstaarabu tu. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAREKANI KUTAFUTA MATEKA NIGERIA

Marekani kusaidia kuwasaka wasichana waliotekwa na Boko Haram
Marekani imesema inapeleka vifaa vya uchunguzi nchini Nigeria kusaidia katika juhudi za kuwatafuta wasichana wanaozuiliwa na kundi la Boko Haram.
Wasichana hao walitekwa nyara kutoka shule moja Kusini mwa eneo la Borno mwezi mmoja uliopita.
Msemaji wa Rais Obama Jay Carney amesema kikosi cha maafisa 30 kiko nchini Nigeria tayari kushiriki juhudi hizo.
Amesema msaada huo wa Marekani kutoka wizara za mambo ya nje na ulinzi na pia kutoka idara ya uchunguzi ya FBI. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Hatua hiyo imechukuliwa wakati baadhi ya Jamaa za wasichana waliotekwa nyara wakielezea majonzi baada ya kutazama kanda ya video iliyotolewa na kundi hilo.
Marekani kusaidia kuwasaka wasichana waliotekwa na Boko Haram
Baadhi wameiambia BBC kuwa kanda hiyo imewapa matumaini lakini wameshangaa kuona wasichana hao ambao wengi ni Wakristu wamevalia mavazi ya Kiislam.

Akizungumza kwa uchungu nduguye mmoja wa wasicha waliotekwa ameiambia BBC ni heri kanda hiyo ingeonyesha maiti za wasichana hao kwa kuwa hiyo ingeondoa wasiwasi unaoendelea kukithiri na kuumiza mioyo ya wengi.
Kwenye kanda hiyo ya video kiongozi wa Boko Haram , Abubakar Shekau anasikika akiambia serikali ya Nigeria yuko tayari kubadilishana baadhi ya wasichana hao na wafuasi wake waliofungwa jela.
Hatahivyo wizara ya mambo ya ndani ya Nigeria imetupilia mbali pendekezo hilo.
Seneta Ali Ndume kutoka eneo ambapo wasichana hao walitekwa nyara anaisihi serikali kulegeza msimamo. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Chanzo: BBC

MAGAZETI YA LEO JUMANNE MEI 13, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

mg 2
mg 1
13 
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

TAARIFA YA WIZARA YA AFYA KUHUSU UGONJWA WA HOMA YA DENGUE


mg1
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Seif Rashid na Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,Charles Pallangyo.
Utangulizi
Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii inapenda kutoa taarifa kwa Umma juu ya mwenendo wa ugonjwa wa homa ya dengue yaani “dengue fever” hapa nchini.Ugonjwa huu umethibitishwabaada ya sampuli zilizochukuliwa kutoka kwa watu waliohisiwa kuwa na ugonjwa huu jijini Dar es Salaam kupelekwa kwenye maabara yetu ya Taifa Dar es salaam na kuthibitisha kuwa na virusi vya homa ya dengue mnamo mwishoni mwa mwezi wa Januari 2014. Hadi sasa idadi ya wagonjwa ambao wamethibishwa kuwa na ugonjwa huuni 400 na Vifo 3. Kwa wiki iliyoshia tarehe 9 Mei 2014 ya idadi ya wagonjwa waliogundulika mkoani Dar es salaam ni 60 (42-Kinondoni, 14-Temeke na 4-Ilala) na idadi ya wagonjwa waliopo wodini mpaka sasa ni 13.
Aidha, mlipuko wa ugonjwa huu si mpya hapa nchini kwani uligundulika kwa
mara ya kwanza mnamo Juni 2010 mkoani Dar es Salaam ambapo idadi ya watu 40 walithibitika kuwa na ugonjwa. Pia, kati ya mwezi Mei hadi Julai 2013,wagonjwa 172 walithibitishwa kuugua ugonjwa huu.
Homa ya Dengue
Homa ya dengue ni ugonjwa unaosababishwa na kirusi ambacho kinaenezwa na mbu wa aina ya Aedes.
Dengue in ugonjwa uliosambaa duniani katika nchi za ukanda wa joto. Takribani asilimia 40 ya watu wote duniani wanaishi katika nchi zenye ugonjwa huu. Takwimu za Shirika la Afya Duniani zinathibitisha kuwa takribani matukio milioni 5 ya Dengue yanatolewa taarifa kila mwaka. Watu laki 5 hulazwa hospitali kwa kuathirika na Dengue kali. Homa ya Dengue imeshatokea katika nchi zipatazo 34 barani Afrika.
Hapa Afrika Dengue ni ugonjwa unaojulikana kwa kiwango kidogo sana. Licha ya kwamba milipuko ya kwanza imetokea tangu mwanzoni wa karne ya 19. Matukio ya Ugonjwa huu yameongezeka Afrika tangu miaka ya 1980, matukio mengi yakitokea nchi za ukanda wa Mashariki mwa Afrika ikiwa ni pamoja na Msumbiji, Somalia, Kenya, Komoro, Djibouti na Tanzania. Ikumbukwe kuwa jina “Dengue” linatokana na neno “Dinga” la kiswahili linalolomaanisha ugonjwa unaotakana na pepo yaani Kudinga pepo. Mabaharia wa Kispanish walipokuja kwenye pwani ya Afrika Mashariki walirudi kwao na kuuita “Dengue”.

MCHWA WAVAMIA IKULU...!!!

Mchwa wavamia ikulu ya Paraguay
Mchwa wamevamia makaazi rasmi ya rais wa Paraguay na kutishia udhabiti wa jengo hilo.
Watalamu wa maswala ya ujenzi wameonya kwamba huenda Rais huyo akapoteza makaazi yake iwapo hatua za dharura hazitachukuliwa kuwaangamiza mchwa.
Kwa mujibu wa wanasayasi wa kibiolojia mchwa ni mdudu mwenye bidii sana na kamwe hachoki kutekeleza majukumu yake.
Na ni kutokana na hilo ndipo wahenga katika juhudi za kutoa motisha kwa yeyote yule anayetaka kufanikiwa maishani wakasema ''lazima awe na bidii ya mchwa''.
Msemo huu umedhihirika nchini Paraguay baada ya habari kwamba mchwa wamevamia makaazi rasmi ya Rais Horacio Cartes.
Wataalam wa maswala ya ujenzi wanasema mchwa hao wameharibu sakafu na sehemu zilizojengwa kwa mbao.
Wahandisi hao wameonya kuwa huenda sehemu moja ya jengo hilo likaanguka iwapo hatua za haraka hazitachukuliwa.
Wamependekeza Rais huyo ahamishwe kutoka jengo hilo ili wataalam waweze kupambana na wadudu hao wenye bidii na ukarabati uweze kufanyiwa jengo hilo.
Ni dhahiri kuwa wageni hao waharibifu sasa wanatishia starehe na itifaki ya Rais Horacio Cartes. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Chanzo: BBC

Friday, May 09, 2014

JAQUELINE WOLPER AFUNGUKA KUHUSU KUBADILI DINI, KUCHANA, USAGAJI

Screen Shot 2014-05-09 at 7.02.35 AM 
Ni longtime mwigizaji Mtanzania Jaqueline Wolper amekua kimya na hajasikika akiyatoa ya moyoni kuhusu yote yaliyompata kwenye miezi iliyopita na kumfanya amiliki sana headlines za magazeti, blogs, website pia facebook na twitter huku wengi wakiwa na hamu ya kusikia akiyaongelea.
Kwenye Exclusive interview na mtangazaji Sporah wa The Sporah show, Jaq amekanusha kwamba yeye ni msagaji japo mara kadhaa ameonekana akivaa kiume na kusisitiza ‘sasa hivi nimepunguza sana kuvaa nguo za kiume, wengi walikua wanahisi lakini sijawahi kufanya vitendo vya usagaji na wala sijawahi kushawishiwa na mtu anaejihusisha na vitendo hivyo, boyfriend wangu hana tatizo na mavazi ya kiume ninayovaa… hatujawahi kupangiana mavazi’
Kwenye jibu jingine alilotoa J anasema ‘sijaolewa na wala sijawahi kuolewa, nilishawahi kubadili dini kweli… ni vitu vinatokea na usimuhukumu mtu bila kumuuliza’
Sporah: Ni kweli kwamba ulikutana na mtu ana uwezo wa kifedha na kulikua kuna vitu unataka akununulie akasema hawezi kukufanyia mpaka ubadilishe dini ili upate hizo mali?
J Wolper: ‘Sio hivyo, dini nilikuja kubadilisha wakati nimeshapata mali, nilibadilisha mwishoni kabisa baada ya huyu mwanaume kuja kwetu akitaka kunioa, alinipa mali na vitu vya thamani kabla ya sisi kukutana, unajua unaweza ukawa unachat na mtu mkapendana lakini hamjawahi kukutana… ni mzuri wa kukushawishi, unajua sio rahisi mtu akiwa mbali aweze kukushawishi mkapendana wakati yeye yuko mbali na wewe uko mbali, namsifia kwa uzuri wake… sio wa umbo wala sura bali ana roho nzuri na alinitreat vizuri mpaka nikaona huyu ni sahihi nikabadilisha dini’
Screen Shot 2014-05-09 at 4.43.46 AM 
Sporah:     Ulifikiria kwamba dini yako sio nzuri au?

MAGAZETI YA LEO IJUMAA MEI 09, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

RAY C AFUNGUKA KUHUSU KUNUSURIKA KIFO KWA GONJWA HATARI LA DENGUE...!!!

http://jambotz8.blogspot.com/
Staa wa muziki wa Kizazi Kipya Bongo, Rehema Chalamila ‘Ray C’.
MUNGU mkubwa! Staa wa muziki wa Kizazi Kipya Bongo, Rehema Chalamila ‘Ray C’, amesimulia jinsi alivyochungulia kifo baada ya kutikiswa na ugonjwa hatari na tishio ulioibuka hivi karibuni wa Homa ya DengueAkifunguka mbele ya gazeti hili juzi baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini Mwananyamala, Dar alikokuwa amelazwa, Ray C au Kiuno Bila Mfupa alisema kwamba kwenye maisha yake hajawahi kushikwa na ugonjwa wenye mateso makali, tena ya muda mfupi kama ilivyokuwa juzikati alipopata ugonjwa huo.

http://jambotz8.blogspot.com/Alisema kwamba dakika chache tu baada ya kuamka kitandani alikuwa akijisikia kichwa kikiuma kama kinataka kuchomoka ambapo bila kuremba aliwasha gari lake na kukimbilia Hospitali ya Mwananyamala.Staa huyo wa Ngoma ya Na Wewe Milele alisema alipofika kwa kudra za muumba alilazwa tayari kwa kutundikwa dripu. “Huwezi kuamini baada ya madaktari kunipima na kugundua nina Ugonjwa wa Dengue, walinishangaa sana hata namna nilipofika pale na kwamba sikutumia dawa yoyote ya kutuliza maumivu kwa sababu maumivu yake huwa ni lazima utatafuta tu dawa ya kukufanya upoze maumivu. 
“Madaktari wengine wakatishika zaidi maana walisema kama ukimeza vidonge vya ‘Diclopa’ unaweza kupoteza maisha mara moja. 
“Katika magonjwa ya ajabu na yanayostahili kutafutiwa kinga mara moja basi huu ni ugonjwa wa kwanza ambao serikali inatakiwa iwe macho sana maana haufai hata kidogo.
“Tena unatisha sana na wasipoangalia utapoteza maisha ya Watanzania kibao kama hawatautafutia kinga au kuwapa Watanzania elimu ya kutosha.“Mateso niliyoyapata kwa siku mbili nilizolazwa Mwananyamala ni elimu tosha kabisa na kwamba ningekuwa na uwezo wa kuzunguka au kupata nafasi ya kuongea na wakuu wa nchi basi mara moja ningewaomba wafanye jitihada za haraka kuhakikisha wanapata chanjo kwa ajili ya kuudhibiti mfumko wa gonjwa hilo.
“Dengue unaambukizwa na mbu tena wa mchana na dawa yake ni panadol tu!” alimalizia Ray 
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

MAREKANI 'INAIFUNGIA MLANGO' SYRIA

Viongozi wa upinzani wa serikali ya Syria wapo Washington Marekani kwa mashauriano
Marekani imeiwekea vikwazo benki moja ya Urusi inayofanya biashara na Syria kama sehemu ya jitihada za kuzidisha shinikizo za kiuchumi dhidi ya serikali ya Syria.
Hatua hiyo ilitangazwa wakati viongozi wa upinzani walioitembelea Washington wameanza kukutana na maafisa wakuu wa utawala.

Hii ni mara ya kwanza Marekani imeiwekea vikwazo benki ya Urussi inayofanya biashara na Syria.
Maafisa wa hazina ya Marekani wanasema hatua hii inanuiwa kuifungia milango Syria isiweze kuendelea kupenya mfumo wa kifedha wa dunia.
Vikwazo zaidi pia vimewekewa viwanda kadhaa vya kusafisha mafuta pamoja na maafisa sita wa ngazi ya juu katia serikali ya Syria.
Hayo yalitangazwa mda mfupi tu kabla ya kiongozi wa upinzani wa serikali ya Syria Ahmad Jarba alipokutana na waziri wa mambo ya nje wa wa Marekani John Kerry.
Ahmad Jarba yuko katika ziara ya kwanza rasmi huko Marekani ambako anatarajiwa pia kukutana na rais wa Marekani Barack Obama. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Chanzo BBC

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...