Friday, May 09, 2014

JAQUELINE WOLPER AFUNGUKA KUHUSU KUBADILI DINI, KUCHANA, USAGAJI

Screen Shot 2014-05-09 at 7.02.35 AM 
Ni longtime mwigizaji Mtanzania Jaqueline Wolper amekua kimya na hajasikika akiyatoa ya moyoni kuhusu yote yaliyompata kwenye miezi iliyopita na kumfanya amiliki sana headlines za magazeti, blogs, website pia facebook na twitter huku wengi wakiwa na hamu ya kusikia akiyaongelea.
Kwenye Exclusive interview na mtangazaji Sporah wa The Sporah show, Jaq amekanusha kwamba yeye ni msagaji japo mara kadhaa ameonekana akivaa kiume na kusisitiza ‘sasa hivi nimepunguza sana kuvaa nguo za kiume, wengi walikua wanahisi lakini sijawahi kufanya vitendo vya usagaji na wala sijawahi kushawishiwa na mtu anaejihusisha na vitendo hivyo, boyfriend wangu hana tatizo na mavazi ya kiume ninayovaa… hatujawahi kupangiana mavazi’
Kwenye jibu jingine alilotoa J anasema ‘sijaolewa na wala sijawahi kuolewa, nilishawahi kubadili dini kweli… ni vitu vinatokea na usimuhukumu mtu bila kumuuliza’
Sporah: Ni kweli kwamba ulikutana na mtu ana uwezo wa kifedha na kulikua kuna vitu unataka akununulie akasema hawezi kukufanyia mpaka ubadilishe dini ili upate hizo mali?
J Wolper: ‘Sio hivyo, dini nilikuja kubadilisha wakati nimeshapata mali, nilibadilisha mwishoni kabisa baada ya huyu mwanaume kuja kwetu akitaka kunioa, alinipa mali na vitu vya thamani kabla ya sisi kukutana, unajua unaweza ukawa unachat na mtu mkapendana lakini hamjawahi kukutana… ni mzuri wa kukushawishi, unajua sio rahisi mtu akiwa mbali aweze kukushawishi mkapendana wakati yeye yuko mbali na wewe uko mbali, namsifia kwa uzuri wake… sio wa umbo wala sura bali ana roho nzuri na alinitreat vizuri mpaka nikaona huyu ni sahihi nikabadilisha dini’
Screen Shot 2014-05-09 at 4.43.46 AM 
Sporah:     Ulifikiria kwamba dini yako sio nzuri au?

J Wolper: ‘Kwa utamaduni wetu sisi Afrika, Tanzania ninavyojua hata kwa mama yangu imetokea, Mwanamke lazima ufate dini ya Mwanaume wako’
Sporah: Lakini alikua bado hajakuoa?
J Wolper: Nilikua tayari nimeshajiona kama mke wake, ni mtu ambae alinipenda sana…
Sporah: Ulijichora na tatoo ya jina lake?
J Wolper: Kwa nini nichore jina la mtu kwenye mwili wangu, kwanza yeye ni Muislamu hapendi tatoo… nilibadili dini kwa mapenzi yangu mwenyewe kutokana na mtu niliekua nae na hawajui alivyonishawishi mpaka mimi nikabadili, sio kwa kulazimishwa….
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
‘Ninachojua mimi heshima ni kufata dini ya Mwanaume ukishachumbiwa, haikua kama girlfriend na boyfriend… alikua ananifanya kama mke wake japo hatukua tumekutana’ – J Wolper
Sporah: Ulijisikiaje pale vitu havikwenda vizuri?
J Wolper: ‘Mi naona ni sawa tu kwa sababu Mungu pia anapanga ila sikuumia sana, ningeumia kama mimi ndio ningekua nimetaka kuolewa ila yeye ndio alitaka ndoa, mimi bado mdogo… watu wa mitandao kwao ni big deal ila kwangu sio kitu’
Screen Shot 2014-05-09 at 7.02.19 AM
‘Haukuwa uamuzi mgumu, napenda sana kufata moyo wangu… siwezi kufata moyo wa mtu, wengi waliniambia sijui ukibadili dini tena sijui mashabiki wako sijui nini nini… NOOOO! sio kuhusu mashabiki, mimi ni mimi kama mimi sikupenda kilichotokea na bado niko chini ya wazazi wangu, vp ikitokea nimekufa nitazikwaje sijaolewa??! mi siwezi kumchezea Mungu ndio maana ukiangalia instagram yangu mimi kila Jumapili lazima niende kanisani’ – Wolper
J Wolper: ‘Nilikaa miezi miwili bila kwenda Msikitini wala Kanisani, nilikonda kwa sababu siwezi kukaa bila kusali na wazazi wangu nakua nawakosea, kuna neno mama yangu mdogo aliniambia baada ya kukaa na mama na kuongea nikasema ngoja nirudi kanisani, siwezi kufaidisha watu na kuacha wazazi wangu wakasononeka… nilibadili dini kwa heshima ya mchumba wangu lakini sasa hivi nimerudi kwa heshima ya wazazi wangu’
J Wolper: ‘Bado Dallas ni rafiki yangu mkubwa sana kwangu na ni mtu poa, haongei mapenzi maskini… ni rafiki yangu ni kaka yangu, hatuwezi tena kuwa wapenzi… nampenda bado’
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz
Interview nyingine ya Jackline iliyobaki unaweza kuitazama hapa chini…

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...