Friday, April 25, 2014

MAGAZETI YA LEO IJUMAA APRIL 25, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
.

SIKU 67 ZA MIPASHO, MATUSI, BUNGE MAALUM LA KATIBA

bunge 4c2f3
Na Hudugu Ng'amilo.
Bunge Maalumu la Katiba linaahirishwa leo baada ya kukutana kwa siku 67 bila kupitisha hata ibara moja kati ya 240 zilizomo katika Rasimu ya Katiba.
Badala yake Bunge hilo likiongozwa na Samuel Sitta "Mzee wa Kasi na Viwango" linaahirishwa hadi Agosti, mwaka huu likiendelea kujadili Sura ya Kwanza na ya Sita zenye jumla ya Ibara 19, zinazohusu masuala yanayojenga msingi wa aina ya Muungano unaopendekezwa.
Tume ya Mabadiliko ya Katiba katika rasimu iliyowasilishwa bungeni na aliyekuwa Mwenyekiti wake, Jaji Joseph Warioba ilipendekeza muundo wa shirikisho lenye serikali tatu, pendekezo ambalo limeligawa Bunge hilo vipande viwili.
Kutokana na mgawanyiko huo, kauli zenye utata, kejeli, matusi, dhihaka na ubaguzi ni mambo yaliyoshika hatamu katika mjadala wa sura hizo mbili, huku viongozi wa Bunge; Sitta na Makamu wake, Samia Suluhu Hassan wakilaumiwa kwa kushindwa kudhibiti hali hiyo.
Mwanzoni mwa wiki hii, Mjumbe wa Bunge hilo, Ezekiah Oluoch alimshutumu Sitta kwamba ameshindwa kudhibiti nidhamu katika Bunge na kwamba ndiye chanzo cha kuondoka kwa wajumbe wapatao 200 ambao ni wanachama wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa). Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

OBAMA AWASILI KOREA KUSINI

Rais Obama akifanya mashauriano na Rais wa Korea Kusini, Park Geun-hye (kushoto) na Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe.
Rais Obama amewasili Korea Kusini huku hofu ikizagaa kwamba Korea Kaskazini huenda inajiandaa kufanya jaribio la nne ya zana zake za nukyla.
Inatarajiwa kwamba shughuli mpya katika kinu cha nuklya mjini Pyongyang zitatawala mazungumzo kati ya bwana Obama na rais wa Korea Kusini Park Geun-hye.
Viongozi hao wawili wanarajiwa kuangazia zaidi jukumu la Uchina katika kuithibiti Korea Kaskazini, jambo ambalo Bwana Obama ametaja kuwa lenye umuhimu mkubwa.
Rais wa Marekani Barack Obama amewasili Korea Kusini katika sehemu yake ya pili ya ziara katika Bara la Asia. Anatarajiwa kukutana na Rais Park baadaye leo na kuwatembelea wanajeshi wa Marekani walioko nchini humo.
Ziara yake inafanywa wakati ambapo kuna hofu kuwa Korea Kaskazini huenda ikafanya jaribio la nne la Kinukilia.
Korea Kaskazini inatarajiwa kujadiliwa na viongozi hao wawili na tayari kuna ripoti kuwa maandalizi ya kufanya jaribio la Kinukilia yanayoendelea kufanywa Korea Kaskazini yatahakikisha kuwa taifa hilo jirani linapewa kipao mbele katika mashauriano.
Picha zilizochukuliwa na mitambo ya Sattelite zinaonyesha kuwa kuna masanduku mengi yanayohamishwa hapa na pale katika eneo linalotarajiwa kufanyiwa zoezi hilo Korea Kaskazini. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

KERRY ASHUTUMU URUSI KWA GHASIA UKRAINE

Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani John Kerry akizungumza na mwenzake wa Urusi Sergei Lavrov.
Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani amelaumu Urusi kwa kuchochea mapigano Mashariki mwa Ukraine.
John Kerry alisema ujasusi wa Marekani una hakika kuwa Urusi imetoa silaha na wapiganaji na pia inaendelea kugharamia na kusimamia wapiganaji wa nchini Ukraine kushiriki ghasia hizo.
Katika lugha ya hasira, Bwana Kerry, alishambulia Urusi akisema kuwa taifa hilo limeshindwa kuchukua hatua madhubuti za kujaribu kutuliza uhasama ulioko nchini Ukraine kama ilivyokubaliwa mjini Geneva juma lililopita.
Bwana Kerry alisema kuwa Urusi inasimamia ghasia zinazoendeshwa na watu wanaotaka kujitenga kutoka kwa Ukraine Mashariki mwa taifa hilo na kujaribu kusababisha ghasia ili kuhujumu uchaguzi unaotazamiwa kufanywa mwezi ujao.
Kwa hasira, Bwana Kerry alilaumu Urusi kwa ghasia zote zinazoendelea Ukraine wakati huu. Ingawa hakutangaza vikwazo inavyoweza kuongezewa Urusi Bwana Kerry alisema mwanya wa kuimarisha amani katika Ukraine unaendelea kuziba. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Thursday, April 24, 2014

KOCHA MPYA WA TAIFA STARS KUWASILI JUMAMOSI APRIL 26.

KOCHA

Kocha Mkuu mpya wa Taifa Stars, Martinus Ignatius Maria maarufu kama Mart Nooij anatarajiwa kuwasili nchini Jumamosi alfajiri (Aprili 26 mwaka huu) tayari kwa ajili ya kuanza kazi ya kuinoa timu hiyo.
Nooij (59) atawasili saa 7.20 usiku kwa ndege ya Ethiopia Airlines ambapo anatarajia kukutana na waandishi wa habari Jumamosi mchana, saa chache kabla ya kuanza mechi ya kirafiki kati ya Taifa Stars na Burundi itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mart Nooij ni raia wa Uholanzi, na ameshawahi kufanya kazi katika nchi ya Mozambique kama kocha mkuu wa timu ya taifa, Burkina Faso U20, na pia ameifundisha timu ya Santos ya Afrika ya Kusini. Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

RAIS KIKWETE AZINDUA UJENZI WA HOSPITALI KUBWA NA YA KISASA YA CHUO KIKUU CHA AFYA NA SAYANSI SHIRIKISHI

 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akipeana mikono na Balozi wa Korea nchini Mhe Chung IL wakiwa mbele ya mchoro wa mfano wa Hospitali ya Chuo Kikuuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili kijijini Mloganzila maeneo ya Kwembe, Kilometa 25 kutoka jijini Dar es salaam, baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa hospitali hiyo itakayokuwa kubwa kuliko zote nchini leo.
 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akifurahi na msanii Mrisho Mpoto baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa  Hospitali kubwa na ya kisasa ya Chuo Kikuuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili kijijini Mloganzila maeneo ya Kwembe, Kilometa 25 kutoka jijini Dar es salaam, baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa hospitali hiyo itakayokuwa kubwa kuliko zote nchini leo.
Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete na Balozi wa Korea nchini Mhe. Chung IL na viongozi wengine  wakikata utepe kuashiria uwekaji wa  jiwe la msingi la ujenzi wa  Hospitali kubwa na ya kisasa ya Chuo Kikuuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili kijijini Mloganzila maeneo ya Kwembe Kilometa 25 kutoka jijini Dar es salaam, April 24, 2014. (PICHA NA IKULU)
Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Sunday, April 20, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI YA PASAKA APRIL 20, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS

.




.Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

HII KALI.. WAUMINI WASAFISHA BARABARA YA LAMI KWA SABUNI...!!!

Screen Shot 2014-04-20 at 1.08.01 AM
Wakazi wa jiji la Eldoret wamemfanya kila alieiona hii kuvutiwa na pengine kujua imekuaje wakafanya hivi kwa mara ya kwanza baada ya kujitosa na kupiga deki barabara ya lami ya Oginga Odinga jijini Eldoret kaunti ya Uasin Gishu nchini Kenya.
Unaambiwa wameamua kufanya hivi ikiwa ni maandalizi ya kumlaki nabii Daktari Awuor kwa ajili ya maombi ya jana na siku ya Jumatatu kuadhimisha Pasaka na kumshukuru Jehova kwa kuwasaidia jiji la Eldoret kufanyika uchaguzi wa amani mwaka 2013.
Hata hivyo kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii maoni yalikotolewa na Wakenya kuhusu ishu hii, maoni mengi yameonekana kupinga kitendo cha waumini hao wa kanisa la Jesus is Lord kwa kumpa Daktari Awuor heshima kupita kiasi.
Mkurugenzi mkuu wa Kass media inayo miliki Radio ya Kass Fm inayotangaza kwa lugha ya Kikalenjin inayozungumzwa na wakazi wa jiji la Eldoret Julius Lamaon, amesema ‘watu wetu waache kupotoka, jiji letu limebadilishwa na kuwa jiji la vituko…… Gavana hatakiwi kuhudhuria mkutano huu’ Tafadhari Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz

Na Millard Ayo

Thursday, April 17, 2014

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS APRIL 17, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.



.


.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz  

ANGALIA UKAWA WALIVYOLISUSA BUNGE MAALUM LA KATIBA JANA

Wajumbe wa Bunge  Maalum la Katiba ambao wanaunga mkono mfumo wa  Serikali za tatu wakitoa katika Ukumbi wa Bunge leo mjini Dodoma baada ya kususia kikao


Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz  

Wednesday, April 02, 2014

POMBE ZA VIROBA KUTOKA NJE YA NCHI ZILIZOPIGWA MARUFUKU ZAINGIZWA NCHINI KWA NJIA ZA PANYA

http://jambotz8.blogspot.com/
 Pichani ni baadhi ya pombe kutoka nje ya nchi zilizopigwa marufuku kuingizwa nchini.
http://jambotz8.blogspot.com/
Meneja wa Mamlaka ya chakula na dawa (TFDA) Mkoa wa Mbeya Rodney Alananga (picha na maktaba)

Na Mwandishi Wetu Wa Jambo Tz, Mbeya

LICHA ya Serikali kukataza uingizaji wa pombe haramu kutoka nchi
jirani za Malawi na Zambia maarufu kama viroba hatimaye wananchi wamezidi kuziingiza pombe hizo na kutapakaa jijini Mbeya.

Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hii Mkoani Mbeya umebaini kuwa pombe
hizo zimekuwa  zikiingizwa kwa njia za panya kupitia vivuko visivyohalali Wilayani Kyela na kusafirisha hadi jijini Mbeya ambako imeonekana kuwa ndiko kuna watumiaji wengi wa pombe hizo.

Katika wilaya ya Kyela wafanyabiashara wa pombe hizo wamekuwa
wakisafirisha mithiri ya gunia la Mchele, juu yake wakiwa wamejaza maharage na wengine huweka dagaa za Nyasa ili vyombo husika visiweze kubaini kilichomo ndani yake.
 

 Imebainika pia kuwa wafanyabiashara hao wamekuwa wakipitisha pombe hizo katika Wilaya ya Ileje kwa kutumia Baiskeli na kuziingiza nchi kupitia eneo la Mbebe, Msia, Mapogolo, Ikumbilo, Bupigu, Ilondo na Ilulu.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz  

Wednesday, March 26, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMATANO MARCH 26, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 

OBAMA AIONYA URUSI KWA VIKWAZO ZAIDI

Rais Obama yuko mjini Brussels ambapo atakutana na viongozi wa muungano wa Ulaya na shirika la kujihami la NATO, kuzungumzia mzozo wa Ukraine.
Rais Obama anatarajiwa kusisitiza umuhimu wa usalama Marekani na Ulaya
Kwenye hotuba muhimu kuhusu sera Rais Obama anatarajiwa kusisitiza umuhimu wa usalama wa Marekani na nchi za Ulaya na pia kuonya Urusi dhidi ya kukiuka sheria za kimataifa.
Akizungumza mjini the Hague kabla ya kuelekea Brussel Rais Obama ameitaja hatua ya Urusi kutwaa eneo la Crimea kutoka kwa Ukraine kama ishara ya udhaifu.
Hatahivyo amesema bado kuna nafasi ya Urusi kusuluhisha mzozo huo kwa njia ya amani la sivyo ikabiliwe na vikwazo zaidi vya kiuchumi. Amesema japo huenda vikwazo hivyo vikaathiri uchumi wa dunia,Urusi ndio itakayoathirika zaidi.
Mkutano huo pia unatarajiwa kuzingatia maswala ya kibiashara na pia wasiwasi kwamba Marekani imekuwa ikichunguza kisiri shuguli za washirika wake kutoka nchi za Ulaya.Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 

UN YALAANI MISRI KWA HUKUMU YA KIFO

Mahakama kuu Misri
Umoja wa Mataifa umelaani kitendo cha Misri kuwahukumu kifo zaidi ya watu miatano ikisema kuwa ni ukiukwaji wa sheria za kimataifa za haki za binadamu.
Umoja huo umesema kuwa idadi ya watu waliohukumiwa Jumatatu, ndio idadi kubwa ya watu kuwahi kuhukumiwa kifo kwa wakati mmoja katika miaka ya hivi karibuni.
Mawakili wa utetezi wamesusia kesi ya pili ya watu wengine karibu miasaba wafuasi wa Morsi wanaokabiliwa na tuhuma sawa na zile zilizowakabili watuhumiwa wa kwanza.
Wamlalamikia kile wanachosema ni mahakama kukosa kufuata utaratibu unaofaa.
Kesi ya wafuasi wengine 682 waliosalia ilianza kusikilizwa mapema leo lakini ikaahirishwa baada ya muda mfupi huku jaji akisema kuwa hukumu itatolewa mwezi ujao.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...