Friday, March 21, 2014

SAUDI ARABIA YAPIGA MARUFKU KUWAPA WATOTO MAJINA HAYA......!!!

Screen Shot 2014-03-21 at 5.23.39 AM
Wizara ya mambo ya ndani ya Saudi Arabia imepiga marufuku majina hamsini ambayo yapo kinyume na tamaduni pamoja na dini ambapo kuanzia sasa, wazazi kutoka falme hiyo hawataruhusiwa tena kuwapa watoto wao.
Majina hayo ni kama Linda, Alice, Elaine au Binyamin (jina lenye maana Benjamin) ambapo jina la Benjamin (Binyamin) kwa dini ya kiislamu linaaminika kuwa jina la mtoto wa mtume Jacob, yaani Yacoub kwa dini. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 
Mengine katika orodha hiyo ambayo hayatoruhusiwa ni kwa sababu yanaaminika kuwa yenye kufuru, yasiyo ya kiarabu na yasio ya kiislamu au yenye kupingana na tamaduni na dini ya falme hiyo.
Sababu nyingine ni ya kigeni ama ya ughaibuni yakiwemo yenye maana ya ufalme au ukubwa, cheo flani kama Sumuw (mtukufu), Malek (mfalme) na Malika (Malkia).
Screen Shot 2014-03-21 at 5.23.23 AM
Majina mengine hayapo katika jamii hizi hivyo hakuna sababu zilizotolewa juu yake, hii ni sehemu nyingine ya orodha yenyewe ambapo ni Malaak (angel), Abdul Aati, Abdul Naser, Abdul Musleh, Binyamin (Arabic for Benjamin) Naris, Yara, Sitav.
Mengine ni Loland, Tilaj, Barrah, Abdul Nabi, Abdul Rasool, Sumuw (highness), Al Mamlaka (the kingdom), Malika (queen), Mamlaka (kingdom), Tabarak (blessed), Nardeen, Sandy, Rama (Hindu god), Maline, Elaine, Inar, Maliktina
Maya. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 

Wednesday, March 19, 2014

CCM YAZINDUA KAMPENI KWA KISHINDO CHALINZE

 Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana akimnadi mgombea wa Ubunge katika uchaguzi mdogo jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete, katika mkutano wa uzinduzi wa kampeni za CCM uliofanyika leo kwenye Uwanja wa  Miembesaba, Chalinze mkoa wa Pwani. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 
Mgombvea ubunge katika uchaguzi mdogo jimbo la Chalinze, kwa tiketi ya CCM, Ridhiwani Kikwete akiomba kura katika mkutano wa uzinduzi wa kampeni za CCM za uchaguzi huo leo kwenye Uwanja wa Miembe saba, Chalienze.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 

MAGAZETI YA LEO JUMATANO MARCH 19, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


..



RAIS KIKWETE KUHUTUBIA BUNGE IJUMAA WIKI HII

D92A0027_3d92f.jpg
Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kuhutubia Bunge Maalum Machi 21 mwaka huu mjini DodomaKauli hiyo imetolewa leo na Katibu wa bunge hilo, Yahya Khamis Hamad wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa waandishi wa habari wa ofisi za Bunge mjini Dodoma.
"Kwa mujibu wa kanuni ya 75 (1), Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atalihutubia Bunge Maalum siku ya Ijumaa Machi 21 ,mwaka 2014 saa 10:jioni, ambapo wageni waalikwa wote watatakiwa kuwa wameingia na kuketi katika maeneo watakayoelekezwa saa 9:00 alasiri," alisema Katibu huyo.
Aidha Katibu huyo alisema ratiba ya shughuli hiyo itaanza na kikao cha Bunge saa 9:10 na baadae kikao hicho kitaanza saa 9:20 kwa ajili ya kumpokea Rais.
Aliongeza kuwa mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Bunge, Rais Kikwete atapokewa na Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu, Naibu Katibu wa Bunge Maalum, ambapo baadae ataelekea katika jukwaa maalum kwa ajili ya kupokea salamu za heshima na kukagua Gwaride Maalum ambalo limeandaliwa na jeshi la polisi.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 

MCHINA AFUNGWA JELA MIAKA 20 KWA KUKUTWA NA MENO YA TEMBO

Suleiman-Kova-March19-2014_a498c.png
Kamanda Kanda Maalum, Seleman Kova akiwa ameshika meno ya tembo.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imemhukumu raia wa China, Yu Bo (45), kulipa faini ya Shilingi bilioni tisa au kwenda jela miaka 20 baada ya kukiri kukutwa na nyara za serikali.
Yu, alikamatwa akiwa na kilo 303 za nyara hizo ikiwamo ngozi za vinyonga wawili vyote vikiwa na thamani ya Sh. milioni 975 mali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi, Devota Kisoka, baada ya upande wa Jamhuri kumsomea mshtakiwa mashitaka na kukiri.
Alisema baada ya mshtakiwa kukiri makosa yake, mahakama imemtia hatiani na kumhukumu kulipa faini ya Shilingi bilioni tisa na akishindwa aende jela miaka 20.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 

Tuesday, March 18, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMANNE MARCHI 18, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


WAPINZANI WAHUKUMIWA MAISHA JELA BURUNDI

Kiongozi wa chama cha MSD Alexis Sinduhije
Wanachama kadhaa kati ya sitini wa chama cha upinzani nchini Burundi MSD waliofikishwa mahakamani leo , wamehukumiwa kifungo cha maisha jela.
Hii ni baada ya serikali kuwatuhumu kwa kosa la kusababisha vurugu na kupanga njama ya mapinduzi dhidi yake.

Wengine bado wanasubiri hukumu huku kesi zao zikiendelea.
Walikamatwa baada ya kuhusishwa na purukushani iliyotokea tarehe nane mwezi Machi baina ya wafuasi wa chama hicho na polisi.
Kesi hiyo imeanza kusikilizwa leo katika mahakama ya jiji la Bujumbura.
Mawakili wao wamekosoa uamuzi huo wakisema kuwa umekiuka sheria kwa kile wamesema kwamba kuna maombi mengi waliomba kabla ya kesi hii kusikilizwa ingawa hayakuzingatiwa na mahakama.
Serikali ya Rais Pierre Nkurunziza imesema wapinzani walihusika na vurugu pamoja na kupanga njama ya mapinduzi
Mnamo siku ya Jumatatu, Umoja wa mataifa na Muungano wa Ulaya zilielezea wasiwasi kuhusu mvutano wa kisiasa unaozidi kutokota kati ya serikali na vyama vya upinzani nchini Burundi.
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, alilaani hali ya kisiasa nchini humo,akisema kuwa serikali inakandamiza uhuru wa kisiasa, uhuru wa kuongea na watu kukutana.
Bwana Ban alisema kuwa sio jambo zuri kwa polisi kuingilia maandamano ya upinzani.
Agizo hili lilitokana na ghasia za kisiasa kati ya wanaharakati wa upinzani na polisi mapema mwezi huu.
Wiki jana mahakama nchini humo ilimchukulia hatua kiongozi wa chama cha upinzani (Movement for Solidarity and Development party) ambaye pia ni mwandishi habari wa zamani, Alexis Sinduhije na wanaharakati wengine 71 kwa madai ya njama ya mapinduzi.
Serikali pia ilisitisha shughuli zote za chama cha upinzani cha MSD kwa kipindi cha miezi minne baada ya kukishutumu kwa kuzua vurugu.
Chama hicho kimekanusha kusababisha vurugu zozote.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

AL-SHABAB WALIPIZA KISASI AU

Al Shabaab
Wanamgambo wa kiislam nchini Somalia wameshambulia hoteli moja muhimu katika eneo la Kati mwa Somalia ambalo wanamgambo hao walipoteza udhibiti wake wiki iliyopita.
Walioshuhudia shambulio hilo wameiambia BBC kuwa gari lililipuka nje ya hoteli katika mji wa Bulo-burde wanakoishi askari wa muungano wa Afrika na makamanda katika jeshi la Somalia .
Mlipuko huo ulifuatiwa na makabiliano ya risasi yaliyodumu kwa muda wa saa tano .
Walioshuhudia wanasema takriban watu kumi na wanne wameuawa katika shambulio hilo , ambalo wapiganaji wa al-Shabab wamesema walilitekeleza.
Mji wa Bulo-burde ulitwaliwa tena katika moja ya harakati za kijeshi zinazoendeshwa na vikosi vya Amison na vile vya serikali dhidi ya wanamgambo hao.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Saturday, March 15, 2014

HELKOPTA YA CHADEMA YAPIGWA MARUFUKU KUONEKANA ANGA LA KALENGA

JESHI la Polisi, limepiga marufuku chama chochote kurusha helkopta kwenye anga la jimbo la Kalenga, na limeahidi kushughulikia kikamilifu kundi au yeyote atakayejaribu kusababisha au kufanya vujo wakati wa uchaguzi na matokeo ya uchaguzi huo.
Onyo hilo limetolewa asubuhi hii na Kamanda wa Polisi mkoa wa Iringa, Ramadhani Mungi, wakati akieleza Polisi ilivyojiandaa kuhakikisha uchaguzi mdogo jimbo la Kalenga, Iringa Vijijini, unafanyika kwa amani na utulivu, Jumapili hii, ya Marchi 16, 2014.
Kamanda Mungi amesema, Intelijensia ya jeshi hilo, imeshawabaini watu ambao wameletwa na baadhi ya vyama vinavyoshiriki kwenye uchaguzi huo, wakitokea mikoa mbalimbali kwa lengo la kufanya vurugu au kutisha wananchi wakati wa kupiga kura na kwamba ikiwa watathubutu kufanya vurugu watakiona cha moto.

“Tunafahamu na tunawajua watu walioletwa na baadhi ya vyama kwa lengo la kufanya vujo hapa Kalenga. Nawatahadharisha watu hao wajue kwamba wakijaribu kufanya vurugu, waliowaleta wataondoka halafu sisi tutabaki nao hapa Iringa kuhakikisha wanakiona cha moto”, alisema kamanda wa Polisi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

ALIYEKUWA RAIS WA SIERRA LEONE AFARIKI DUNIA

Marehemu AL Hajj Kabbah
Amefariki nyumbani kwake akiwa na miaka 82.Alhaji Ahmad Tejan Kabbah alizaliwa February 16, 1932. Aliongoza Sierra Leone kati ya mwaka wa 1996 hadi 1997 na kisha tena mwaka wa 98 hadi mwaka wa 2007.
Katika miaka mingi ya utu uzima wake, alihudumu kama mtaalamu wa uchumi na sheria. Alifanya kazi kwa miaka mingi na shirika la maendeleo la Umoja wa mataifa UNDP. Baada ya kujiuzulu kutoka umoja huo mwaka wa 92, alirudi zake nchini Sierra Leone na kujiingiza katika siasa za nchi hiyo
Maisha yake ya siasaMnamo mwaka wa tisini na sita, bwana Kabbah alichaguliwa kuwa kiongozi wa chama Sierra Leone's People's Party (SLPP) na kuwania urais kwa tikiti ya chama hicho mwaka wa 96.
Katika kinyanganyiro hicho, alishinda na kuwa rais kwa 59% ya kura na kumpiku mpinzani wake mkuu John Karefa-Smart wa chama cha United National People's Party (UNPP) aliyepata 40% tu ya kura.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 

DUNIA IMEISHA... BABU ADAIWA KUMBAKA MJUKUU WAKE...!!!


BABU mwenye umri wa miaka (80), Benedict mkazi wa Tandika Kilimahewa, jijini Dar ametiwa mbaroni kwa madai ya kumbaka mjukuu wake wa kike (jina linahifadhiwa) mwenye umri wa miaka (6). 
Tukio hilo la kuhuzunisha linadaiwa kutokea Machi 8, mwaka huu usiku wakati babu na mjukuu wake huyo wakiwa wamelala pamoja chumbani kwake.
Akizungumza na mwandishi wetu, jirani wa babu huyo ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini alidai kwamba aliyegundua mtoto huyo kabakwa ni mjumbe wa nyumba kumi wa eneo analoishi mtuhumiwa anayefahamika kwa jina la Bibi China.
“Sisi hatukuwa na habari ila mjumbe wetu aliposikia watoto wakisema nguo ya ndani ya mwenzao (mtoto aliyebakwa) ilikuwa na damu alimwita na kumkagua, alipomuuliza alipatwa na nini akamwambia babu yake alimfanyia mchezo mbaya,” alidai jirani huyo. 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

DANIEL STURRIDGE MCHEZAJI BORA WA MWEZI ENGLAND, SAM ALLARDYCE KOCHA BORA

Daniel Sturridge akiwa na tuzo ya Mchezaji Bora wa Februari
MSHAMBULIAJI wa Liverpool, Daniel Sturridge ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya England kwa mwezi Februari, baada ya kufunga mabao matano katika mechi nne.
Nyota huyo ameisaidia Liverpool kushinda dhidi ya Swansea na Fulham pamoja na kuitandika mabao 5-1 Arsenal timu hiyo ya Anfield ikiweka hai matumaini ya kutwaa ubingwa.
Winning: Sam Allardyce led West Ham into the top 10 with four wins from four last month
Sam Allardyce ameiongoza West Ham kuingia kwenye 10 Bora kwa kushinda mechi nne mwezi uliopita
Kocha wa West Ham, Sam Allardyce, ameshinda tuzo ya Kocha Bora wa Mwezi baada ya kuiongoza timu yake kushinda mechi nne. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

WAJUMBE WA BUNGE MAALUM LA KATIBA WAAPISHWAMJINI DODOMA

Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Bw. Samwel Sitta akila kiapo mbele ya  Katibu wa Bunge hilo Bw. Yahya Khamis Hamad, wakati wa hafla ya kuwaapisha wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba Mjini Dodoma.Kulia ni Naibu Katibu wa Bunge Hilo Thomas Kashilila.
>Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Samia Suluhu Hassan akila kiapo mbele ya Naibu Katibu wa Bunge Hilo Thomas Kashilila, wakati wa hafla ya kuwaapisha wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba leo Mjini Dodoma.Kulia ni Katibu wa Bunge Hilo Yahya Khamis Hamad.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI MARCHI 15, 20014, YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

ULI HOUNESS AJIUZULU NAFASI YA URAISI WA FC BAYERN MUNICH

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...