Tuesday, March 18, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMANNE MARCHI 18, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


WAPINZANI WAHUKUMIWA MAISHA JELA BURUNDI

Kiongozi wa chama cha MSD Alexis Sinduhije
Wanachama kadhaa kati ya sitini wa chama cha upinzani nchini Burundi MSD waliofikishwa mahakamani leo , wamehukumiwa kifungo cha maisha jela.
Hii ni baada ya serikali kuwatuhumu kwa kosa la kusababisha vurugu na kupanga njama ya mapinduzi dhidi yake.

Wengine bado wanasubiri hukumu huku kesi zao zikiendelea.
Walikamatwa baada ya kuhusishwa na purukushani iliyotokea tarehe nane mwezi Machi baina ya wafuasi wa chama hicho na polisi.
Kesi hiyo imeanza kusikilizwa leo katika mahakama ya jiji la Bujumbura.
Mawakili wao wamekosoa uamuzi huo wakisema kuwa umekiuka sheria kwa kile wamesema kwamba kuna maombi mengi waliomba kabla ya kesi hii kusikilizwa ingawa hayakuzingatiwa na mahakama.
Serikali ya Rais Pierre Nkurunziza imesema wapinzani walihusika na vurugu pamoja na kupanga njama ya mapinduzi
Mnamo siku ya Jumatatu, Umoja wa mataifa na Muungano wa Ulaya zilielezea wasiwasi kuhusu mvutano wa kisiasa unaozidi kutokota kati ya serikali na vyama vya upinzani nchini Burundi.
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon, alilaani hali ya kisiasa nchini humo,akisema kuwa serikali inakandamiza uhuru wa kisiasa, uhuru wa kuongea na watu kukutana.
Bwana Ban alisema kuwa sio jambo zuri kwa polisi kuingilia maandamano ya upinzani.
Agizo hili lilitokana na ghasia za kisiasa kati ya wanaharakati wa upinzani na polisi mapema mwezi huu.
Wiki jana mahakama nchini humo ilimchukulia hatua kiongozi wa chama cha upinzani (Movement for Solidarity and Development party) ambaye pia ni mwandishi habari wa zamani, Alexis Sinduhije na wanaharakati wengine 71 kwa madai ya njama ya mapinduzi.
Serikali pia ilisitisha shughuli zote za chama cha upinzani cha MSD kwa kipindi cha miezi minne baada ya kukishutumu kwa kuzua vurugu.
Chama hicho kimekanusha kusababisha vurugu zozote.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

AL-SHABAB WALIPIZA KISASI AU

Al Shabaab
Wanamgambo wa kiislam nchini Somalia wameshambulia hoteli moja muhimu katika eneo la Kati mwa Somalia ambalo wanamgambo hao walipoteza udhibiti wake wiki iliyopita.
Walioshuhudia shambulio hilo wameiambia BBC kuwa gari lililipuka nje ya hoteli katika mji wa Bulo-burde wanakoishi askari wa muungano wa Afrika na makamanda katika jeshi la Somalia .
Mlipuko huo ulifuatiwa na makabiliano ya risasi yaliyodumu kwa muda wa saa tano .
Walioshuhudia wanasema takriban watu kumi na wanne wameuawa katika shambulio hilo , ambalo wapiganaji wa al-Shabab wamesema walilitekeleza.
Mji wa Bulo-burde ulitwaliwa tena katika moja ya harakati za kijeshi zinazoendeshwa na vikosi vya Amison na vile vya serikali dhidi ya wanamgambo hao.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Saturday, March 15, 2014

HELKOPTA YA CHADEMA YAPIGWA MARUFUKU KUONEKANA ANGA LA KALENGA

JESHI la Polisi, limepiga marufuku chama chochote kurusha helkopta kwenye anga la jimbo la Kalenga, na limeahidi kushughulikia kikamilifu kundi au yeyote atakayejaribu kusababisha au kufanya vujo wakati wa uchaguzi na matokeo ya uchaguzi huo.
Onyo hilo limetolewa asubuhi hii na Kamanda wa Polisi mkoa wa Iringa, Ramadhani Mungi, wakati akieleza Polisi ilivyojiandaa kuhakikisha uchaguzi mdogo jimbo la Kalenga, Iringa Vijijini, unafanyika kwa amani na utulivu, Jumapili hii, ya Marchi 16, 2014.
Kamanda Mungi amesema, Intelijensia ya jeshi hilo, imeshawabaini watu ambao wameletwa na baadhi ya vyama vinavyoshiriki kwenye uchaguzi huo, wakitokea mikoa mbalimbali kwa lengo la kufanya vurugu au kutisha wananchi wakati wa kupiga kura na kwamba ikiwa watathubutu kufanya vurugu watakiona cha moto.

“Tunafahamu na tunawajua watu walioletwa na baadhi ya vyama kwa lengo la kufanya vujo hapa Kalenga. Nawatahadharisha watu hao wajue kwamba wakijaribu kufanya vurugu, waliowaleta wataondoka halafu sisi tutabaki nao hapa Iringa kuhakikisha wanakiona cha moto”, alisema kamanda wa Polisi. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

ALIYEKUWA RAIS WA SIERRA LEONE AFARIKI DUNIA

Marehemu AL Hajj Kabbah
Amefariki nyumbani kwake akiwa na miaka 82.Alhaji Ahmad Tejan Kabbah alizaliwa February 16, 1932. Aliongoza Sierra Leone kati ya mwaka wa 1996 hadi 1997 na kisha tena mwaka wa 98 hadi mwaka wa 2007.
Katika miaka mingi ya utu uzima wake, alihudumu kama mtaalamu wa uchumi na sheria. Alifanya kazi kwa miaka mingi na shirika la maendeleo la Umoja wa mataifa UNDP. Baada ya kujiuzulu kutoka umoja huo mwaka wa 92, alirudi zake nchini Sierra Leone na kujiingiza katika siasa za nchi hiyo
Maisha yake ya siasaMnamo mwaka wa tisini na sita, bwana Kabbah alichaguliwa kuwa kiongozi wa chama Sierra Leone's People's Party (SLPP) na kuwania urais kwa tikiti ya chama hicho mwaka wa 96.
Katika kinyanganyiro hicho, alishinda na kuwa rais kwa 59% ya kura na kumpiku mpinzani wake mkuu John Karefa-Smart wa chama cha United National People's Party (UNPP) aliyepata 40% tu ya kura.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 

DUNIA IMEISHA... BABU ADAIWA KUMBAKA MJUKUU WAKE...!!!


BABU mwenye umri wa miaka (80), Benedict mkazi wa Tandika Kilimahewa, jijini Dar ametiwa mbaroni kwa madai ya kumbaka mjukuu wake wa kike (jina linahifadhiwa) mwenye umri wa miaka (6). 
Tukio hilo la kuhuzunisha linadaiwa kutokea Machi 8, mwaka huu usiku wakati babu na mjukuu wake huyo wakiwa wamelala pamoja chumbani kwake.
Akizungumza na mwandishi wetu, jirani wa babu huyo ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini alidai kwamba aliyegundua mtoto huyo kabakwa ni mjumbe wa nyumba kumi wa eneo analoishi mtuhumiwa anayefahamika kwa jina la Bibi China.
“Sisi hatukuwa na habari ila mjumbe wetu aliposikia watoto wakisema nguo ya ndani ya mwenzao (mtoto aliyebakwa) ilikuwa na damu alimwita na kumkagua, alipomuuliza alipatwa na nini akamwambia babu yake alimfanyia mchezo mbaya,” alidai jirani huyo. 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

DANIEL STURRIDGE MCHEZAJI BORA WA MWEZI ENGLAND, SAM ALLARDYCE KOCHA BORA

Daniel Sturridge akiwa na tuzo ya Mchezaji Bora wa Februari
MSHAMBULIAJI wa Liverpool, Daniel Sturridge ameshinda tuzo ya Mchezaji Bora wa Ligi Kuu ya England kwa mwezi Februari, baada ya kufunga mabao matano katika mechi nne.
Nyota huyo ameisaidia Liverpool kushinda dhidi ya Swansea na Fulham pamoja na kuitandika mabao 5-1 Arsenal timu hiyo ya Anfield ikiweka hai matumaini ya kutwaa ubingwa.
Winning: Sam Allardyce led West Ham into the top 10 with four wins from four last month
Sam Allardyce ameiongoza West Ham kuingia kwenye 10 Bora kwa kushinda mechi nne mwezi uliopita
Kocha wa West Ham, Sam Allardyce, ameshinda tuzo ya Kocha Bora wa Mwezi baada ya kuiongoza timu yake kushinda mechi nne. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

WAJUMBE WA BUNGE MAALUM LA KATIBA WAAPISHWAMJINI DODOMA

Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Bw. Samwel Sitta akila kiapo mbele ya  Katibu wa Bunge hilo Bw. Yahya Khamis Hamad, wakati wa hafla ya kuwaapisha wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba Mjini Dodoma.Kulia ni Naibu Katibu wa Bunge Hilo Thomas Kashilila.
>Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Samia Suluhu Hassan akila kiapo mbele ya Naibu Katibu wa Bunge Hilo Thomas Kashilila, wakati wa hafla ya kuwaapisha wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba leo Mjini Dodoma.Kulia ni Katibu wa Bunge Hilo Yahya Khamis Hamad.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI MARCHI 15, 20014, YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

ULI HOUNESS AJIUZULU NAFASI YA URAISI WA FC BAYERN MUNICH

Wednesday, March 12, 2014

JK ATANGAZA KIAMA CHA MAJANGILI

Wawakilishi wa Chama cha Uhifadhi wa Wanyama cha Frankfurt (FZS), wakikabidhi magari zaidi ya 11 kwa Rais Jakaya Kikwete Ikulu Dar es Salaam jana, kwa ajili ya kusaidia vita dhidi ya ujangili wa wanyamapori katika hifadhi na mbuga za taifa.Picha na Ikulu
Rais Jakaya Kikwete amesema Serikali imenuia kumaliza kabisa ujangili nchini, ikiwa ni hatua ya kunusuru wanyama walio hatarini kutoweka katika hifadhi za taifa.
Hakusita kusisitiza kwamba, nia ya dhati ya Serikali ni kuhakikisha mkakati huo unakamilika, japokuwa kumekuwa na changamoto zinazotokana na ukubwa wa hifadhi hizo na uhaba wa vitendea kazi pamoja na askari wa wanyamapori.
Akizungumza wakati wa kupokea magari 11 ya kisasa kwa ajili ya kusaidia operesheni ya kupambana na ujangili kutoka kwa Shirika la Frankfurt Zoological Society (FZS) la Ujerumani, Kikwete alisema tatizo hilo limekuwa la muda mrefu, lakini juhudi za kulikomesha zinafanyika.
Alisema, pamoja na ukubwa wa tatizo hilo, bado kuna tatizo la uhaba mkubwa wa wafanyakazi wanaotakiwa kudhibiti majangili, ambapo kwa sasa kuna wafanyakazi 1,155 sawa na asilimia 24 tu ya mahitaji halisi ya wafanyakazi 4,000 wanaohitajika.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

HII NDIO VIDEO YA AJALI YA NDEGE KUMGONGA MTU, MAAJABU...!!!

Screen Shot 2014-03-11 at 4.58.21 PM
Screen Shot 2014-03-11 at 4.57.11 PM
Hii imetokea Florida Marekani ambapo mtu mmoja alikua anaruka akiwa na Parachuti lakini akakutana na ndege hii ndogo ambayo baada ya kumgonga walianguka chini wote huku ndege ikiangukia pua.
Pamoja na ajali hii, hakuna mtu aliepoteza maisha ila wote walipata majeraha madogomadogo baada ya kuanguka kwenye umbali wa futi 75 na wakapelekwa hospitali ambapo mwenye Parachuti John Frost (49) aliruhusiwa kuondoka.
Hili tukio limenaswa jinsi lilivyotokea kwa sababu kulikua na mpiga picha aliekua na camera karibu na alikua anashuhudia kila kitu.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO MARCHI 12, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

KURA BADO KITENDAWILI BUNGE LA KATIBA

Wakati wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba wakipitisha Rasimu ya Kanuni za kuendesha Bunge hilo, suala la aina ya kura kwa ajili ya kuamua masuala mbalimbali, limekwama na litaamuliwa na wabunge baada ya kuanza kwa vikao rasmi vya Bunge hilo.
Hatua hiyo imekuja baada ya kuwapo kwa mvutano wa takriban wiki nne kuhusu rasimu, hasa kifungu cha 37 na 38 kinachoeleza aina ya kura kati ya wazi na ya siri.
Hata hivyo, wajumbe wawili wa Bunge hilo, Mchungaji Christopher Mtikila wa DP na Felix Mkosamali wa NCCR- Mageuzi walisusia kupitisha azimio la kukubali Kanuni za Bunge hilo, wakidai kusalitiwa katika uamuzi huo na wenzao walioko kwenye Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).
Wajumbe na viongozi mbalimbali wa vyama vyenye ushawishi bungeni, kwa pamoja waliridhia na kulegeza misimamo yao ili upatikane mwafaka wa kutengeneza Katiba Mpya ndani ya wakati. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

RIDHIWANI, "SIKUSHINIKIZWA KUGOMBEA"

RidhiwaniKikwete_11ac5.jpg
MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Chalinze kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ridhiwani Kikwete ameahidi kuwa atajitahidi kutatua kero za maji, umeme na ajira kwa vijana. Alisema hayo jana baada ya kuchukua fomu katika ofisi za Msimamizi wa Uchaguzi wa Wilaya ya Bagamoyo, Shija Andrew.
Leo anatarajia kurudisha fomu hiyo. Ridhiwani alipokuwa akienda kuchukua fomu hiyo, alisindikizwa na mamia ya wanachama wa CCM wa majimbo ya Chalinze na Bagamoyo, wakiwa wanaimba na kucheza kumshangilia mgombea huyo.
Baada ya kuchukua fomu kutoka kwa Ridhiwani alimhakikishia ofisa huyo kuwa atazingatia taratibu zote za uchaguzi na kutoendesha kampeni za matusi na vurugu.
Baada ya kuchukua fomu hiyo na nakala nyingine muhimu za uchaguzi, aliongozana tena na mamia ya wafuasi wake, kuelekea kwenye ofisi za CCM Wilaya ya Bagamoyo, ambapo alizungumza na waandishi wa habari.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...