Wednesday, February 19, 2014

MAGAZETI YA LEO FEBRUARI 19, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MATOKEO YA MANCHESTER CITY vs BARELONA

Screen Shot 2014-02-19 at 7.09.55 AM 
Kwenye zile game za UEFA ambazo zitaingia kwenye rekodi ya kutazamwa na mamilioni mwaka 2014 na hii imo ambapo Manchester City wamefungwa goli mbili zote kwenye kipindi cha pili.
Screen Shot 2014-02-19 at 7.11.49 AM 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

WACHEZAJI WATATU KUFUATA NYAYO ZA AKINA MBWANA SAMATTA

Wadau wengi wa michezo wanakua wakiwaangalia sana wachezaji waliotoka Bongo kwenda nje ya nchi kucheza soka la kulipwa na miongoni mwao ni Mbwana Samatta ambaye kwa mshahara wake peke yake umezua gumzo mtaani,
Sasa taarifa kutoka TFF ambayo ame-amplify Ofisa habari wa TFF Boniface Wambura unaambiwa Wachezaji watatu kutoka Tanzania ambao ni wachezaji wa mpira wa miguu tayari wameombewa hati ya uhamisho wa Kimataifa[ITC] ili wakacheze katika nchi za Thailand na Ujerumani.
Miongoni mwao ni mchezaji Khamis Mroki Jamal ambaye timu yake ilikua Daraja la Kwanza ya Polisi Dar es Salaam yeye ameombewa ITC na Chama cha Mpira wa Miguu Thailand (FAT) ili akajiunge na Kabinburi ya nchini humo.
Wengine ni Said Ali Nassor aliyekuwa akichezea FC Turkey ya Zanzibar na Samuel Chuonyo hao wote wameombewa na ITC na Chama cha Mpira wa Miguu Ujerumani (DFB) kwa ajili ya kujiunga na klabu ya VfB Eichstatt.
Kwa sasa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linafanyia kazi maombi hayo na mara taratibu zote zitakapokamilika ikiwemo ridhaa ya klabu zao za hapa Tanzania TFF itatoa ITC hizo na jamaa kwenda kujiunga na timu hizo.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

TCIB: WAGOMBEA UCHAGUZI WAPIMWE AFYA


kibamba_9c593.jpg
Mkurugenzi Mtendaji wa TCIB, Deus Kibamba.PICHA|MAKTABA
Dar es Salaam. Kituo cha Taarifa kwa Wananchi (TCIB), kimeitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kubadilisha mfumo wa uendeshaji Uchaguzi Mkuu ikiwamo kuweka kipengele kitakachowalazimisha wagombea wa nafasi za uongozi kupima afya zao ili kuepuka kuchaguliwa viongozi wenye maradhi yatakayowafanya washindwe kumudu majukumu yao ya kazi.
Pia kimeitaka NEC kuweka zuio la kufanyika kwa uchaguzi na kutoza faini kali kwa mgombea anapotangaza kujitoa katika hatua za mwisho kabla ya kufanyika uchaguzi wenyewe.
Hayo yalisemwa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa TCIB, Deus Kibamba wakati akitoa tathimini ya uchaguzi mdogo wa udiwani uliofanyika katika Kata 27 na funzo kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa na ule wa Ubunge katika Jimbo la Kalenga mwezi ujao.
Alisema, Novemba 2012 kulifanyika uchaguzi kujaza nafasi 29 za udiwani wakati Juni 2013 kulifanyika tena uchaguzi katika kata 22 na mwezi huu umefanyika uchaguzi katika kata 27, huku baadhi ya kata zikiwa tayari zimekwisharudia chaguzi zaidi ya mara moja ndani ya kipindi cha miaka mitatu.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 

Tuesday, February 18, 2014

TAARIFA YA CCM KUHUSU MAAMUZI YA VIKAO VYAKE, KIKUBWA NI KUHUSU ADHABU YA AKINA LOWASSA NA SUMAYE


IMG_2949
Nape Moses Nnauye Katibuwa Itikadi, Siasa na Uenezi akizungumza na waandishi wa habari leo mchana katika makao makuu ya CCM Lumumba  ofisi ndogo ya chama jijini Dar es salaam kuhusu maamuzi ya vikao vya chama vilivyomalizika mjinDaodoma hivi karibuni.
…………………………………………………………………………………..
Kati ya tarehe 13/02/2014  na tarehe 18/02/2014 kumekuwa na mfululizo wa vikao kadhaa vya Chama kitaifa vilivyoshughulikia suala la maadili ndani ya Chama.
Vikao hivyo ni pamoja na Kamati Ndogo ya Udhibiti tarehe 13-14/02/2014, Tume ya Udhibiti na Nidhamu 18/02/2014 na Kamati Kuu tarehe 18/02/2013.
Waliohojiwa katika mfululizo wa vikao hivi ni wafuatao:-
1.    Ndg. Frederick Sumaye
2.    Ndugu Edward Lowasa
3.    Ndugu Bernard Membe
4.    Ndugu Stephen Wassira
5.    Ndugu January Makamba
6.    Ndugu William Ngeleja
Baada ya kuwahoji ilithibitika kuwa baadhi ya tuhuma dhidi yao ni za kweli na hivyo kupendekeza adhabu.  Mapendekezo hayo yalipelekwa kwenye Tume ya Udhibiti na Nidhamu na hatimaye Kamati Kuu ya CCM ambayo ilitoa adhabu kwa wahusika.
Kwa ujumla waliohojiwa wamethibitika kuwa na makosa yafuatayo:-
1.    Walithibitika kuanza kampeni za kutafuta kuteuliwa kugombea Urais kabla ya wakati kinyume na Kanuni za Uongozi na Maadili za CCM Toleo la Februari 2010, Ibara 6(7)(i).
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 

UTAJIRI MKUBWA WA VICKY KAMATA WAANIKWA....!!!

WANAWAKE na maendeleo, tufanye kazi, tusonge mbele, yelele…yelele… Hii sehemu ya mashairi ya wimbo wa staa wa muziki wa kizazi kipya na Mbunge wa Viti Maalum (UVCCM), Geita, Vicky Kamata anayetajwa kuwa na utajiri balaa.
http://jambotz8.blogspot.com/Mbunge wa Viti Maalum (UVCCM), Geita, Vicky Kamata.

Vicky amepata mafanikio makubwa ambayo kila mwanamke Tanzania angependa kuyapata. Mwandishi wa habari hii alimchimba kwa kina na kupata utajiri wote alionao kwa sasa.
 
KABLA YA SIASA, KABLA YA BONGO FLEVA
Kabla ya siasa aliishi maisha ya dhiki ambayo hakutegemea kama angekuja kupata mafanikio makubwa. Ni miongoni mwa Watanzania waliozaliwa katika familia duni.
Katika kutafuta ‘kutoka’ kimaisha, Vicky amewahi kuwa mwanamuziki wa Bongo Fleva na kutunga nyimbo mbalimbali, wimbo wa Wanawake na Maendeleo ndiyo uliomtambulisha zaidi katika jamii.
“Nimezaliwa kwenye familia duni, nimeishi maisha ya dhiki sana, mbali na muziki, nimewahi kuwa mwalimu wa shule ya msingi kule Moshi (Kilimanjaro) katika harakati za kusaka maisha, baadaye nilikwenda Morogoro. “Kila kitu kinabadilika kama ukimwamini Mungu,” alisema Vicky mwenye watoto wawili, Revocatus na Glory (jina la baba halikutajwa).
 
MAFANIKIO YAANZA
Mwaka 2006, Vicky alifanikiwa kuajiriwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT) akiwa ni afisa uhusiano.
Mwaka 2010, Vicky alifanikiwa kuwa mbunge wa viti maalum akiuwakilisha Mkoa wa Geita.
 
MJENGO WA GHOROFA MBILI
Akiwa mbunge, Mheshimiwa Vicky ameingia kwenye orodha ya wanawake mabilionea nchini kwa kuangusha mjengo wa kifahari wa ghorofa mbili Sinza jijini Dar es Salaam wenye thamani ya shilingi bilioni moja na milioni mia nne.
Ndani ya ghorofa hilo kuna bwawa la kisasa la kuogelea ‘swimming pool’ ambalo linatumiwa na familia yake. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMANNE FEBRUARI 18, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.


.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Monday, February 17, 2014

MAMBO MATANO (5) YANAYODIDIMIZA MAHUSIANO NA NDOA...!!!

Makala hii ni tafakari huru kuhusu mambo ya msingi katika mahusiano.  Hapa utapata tafakari ya maana ya maneno na imani ambazo zinatutatiza wengi wetu.

Labda kipengele hiki tuanze kwa kueleza kuwa kunaweza kuwepo ndoa, lakini yasiwepo mahusiano wala mapenzi. Inaweza kuonekana kama inachanganya kidogo, lakini ndio ukweli wenyewe.  Ndoa ni namna tuu ambayo wawili walio kwenye mahusiano wanaamua kuwataarifu rasmi watu wengine kuwa wao wapo rasmi katika mahusiano. 
Ndoa ni kiapo mbele ya watu wengine , na ni namna ya kutaka kumuhakikishia mwenza wako kuwa endapo kiapo hicho kitatokea kuvunjika, basi unakubali rasmi kuwajibika kwa mujibu wa taratibu zilizopo za ndoa husika, ikiwemo kukubali kuitwa kwenye mabaraza ya usuluhishi, kugawana mali, n.k. 
Na kwa upande wa kiroho, inabeba maana zaidi kuwa unaweka kiapo kwa Mungu wako kuwa utalinda mahusiano yako na huyo unayemchagua.
 Hivyo basi, ndoa haijengi mahusiano wala mapenzi. Kiuhalisi inabidi kwanza yawepo mahusiano na mapenzi kisha ndio kiapo kifanyike, kwani kinyume cha hivyo ni kuwa unakula kiapo ‘feki’.
Ndio maana basi, ni muhimu kwa wapenzi kutambua kweli kama wanahitajiana, kuwa kwenye mahusiano na kutafakari kwa uhuru kama kweli wanataka kuweka kiapo rasmi cha kuwa pamoja.
Kutumia ndoa kama kinga ya kuhakikisha mahusiano yako yanadumu ni maamuzi magumu ambayo pengine yanaweza yasilete faida hapo baadae. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Sunday, February 16, 2014

KIKWETE AWATAKA WANA-CCM KUACHA UNYONGE...!!! ASEMA UNYONGE UNA KIKOMO...!!!


03_ecd2e.jpg
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Taifa, Rais Jakaya Kikwete amewataka wanachama wa chama hicho kuacha unyonge na kusema uvumilivu una kikomo chake.
Aliyasema hayo jana wakati anafungua kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) ya CCM, kilicholenga kuweka msimamo wa chama kuhusu Rasimu ya Katiba Mpya ambayo inaanza kujadiliwa Jumanne wiki ijayo.
"Tuna uchaguzi mdogo, Iringa, Kalenga, tumeshapata mgombea na tumefanya hiyo kazi kwa niaba yenu kwa sababu hatukupata muda wa kuitisha Kikao cha Halmashauri Kuu, lakini mmetupatia mamlaka ya kufanya hivyo na Katiba imetupa fursa ya kufanya uteuzi kwa niaba yenu,"alisema.
CCM imemteua Godfrey Mgimwa ambaye ni mtoto wa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, marehemu Dk William Mgimwa, kupeperusha bendera katika uchaguzi mdogo utakaofanyika baadaye mwaka huu. Dk Mgimwa hadi anafariki dunia alikuwa Waziri wa Fedha.
Uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Kalenga lililopo mkoani Iringa unatarajiwa kufanyika Machi 16, mwaka huu, huku tayari vyama vya CCM na Chadema vikiwa vimetaja wagombea wake, Chadema kikiwa kimetangaza, Grace Tendega Mvanda.
Rais Kikwete alisema chama hicho kinashindana na vyama vingine katika uchaguzi huo mdogo.
"Tunashindana na wenzetu wagomvi, maana wao ugomvi ndiyo sehemu ya mwongozo wa kufanya kazi ya siasa,"alisema Kikwete bila kutaja chama chochote cha siasa kwa jina.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 

UMECHOKA KUAJIRIWA UNATAKA KUJIAJIRI?! HAYA HAPA MAMBO 8 MUHIMU YA KUZINGATIA


Kuna sababu mbalimbali kwanini mtu atake kuajiri, badala ya kuajiriwa, mfano kipato kidogo anachopata katika kazi husika, hitaji la kutaka uhuru zaidi binafsi wa kufanya kazi, hitaji la kuweza kutoa ajira kwa wengine na zaidi sana kuweza kutumia vema kipaji na uwezo wa kuzalisha ambao katika kazi ya sasa mtu hapati nafasi ya kufanya hivyo.  
Kujiajiri ni jambo linalohitaji maandalizi ya muda mrefu na kuna mambo ya msingi kuyafahamu, haiwezekani tuu , ukaacha kazi na kusema ok, acha nijiajiri.
Makala hii inachambua mambo ya msingi ya kujiandaa na kuyafahamu kabla mtu hajaamua kuacha kuajiriwa.
 
Mkakati ni muhimu: Wazo au ndoto isiyo na mkakati wa kuitimiza ni upuuzi yaani ndoto hiyo au wazo hilo halina maana, hivyo basi ndoto yako ya kujiajiri siku moja, ni lazima iwekewe mkakati wa kuifanikisha ikiwa ni pamoja na muda hasa wa lini utaitimiza hiyo ndoto. 
Katika kuweka mkakati huu wa kutimiza ndoto yako, fanya utafiti wa kina kuhusu mipango yako binafsi ya maisha, mtazamo wako kuhusu maisha, mpenzi/mke wako, familia yako, na hali ya jamii kwa ujumla inavyoenda kama vile mabadiliko ya hali ya kisiasa, teknolojia, na uchumi. 
Tengeneza malengo ya aina ya shughuli unayotaka kuifanya ukiacha kuajiriwa, na pima uwezekano wa shughuli hiyo kufanyika kweli na kama itakulipa. Utambue pia aina ya watu na rasilimali nyingine utakazozihitaji, na jinsi utakavyozipata. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MECHI KALI ZA LEO NA KESHO ZA KOMBE LA FA


http://jambotz8.blogspot.com/ 
LIGI KUU ENGLAND Wikiendi hii itakuwa ‘mapumziko kidogo kupisha Mechi za Raundi ya Tano za FA CUP ambazo zitachezwa Jumapili na Jumatatu.
Jumapili Februari 16
16:30 Everton v Swansea
18:00 Sheff Utd v Nottm Forest
19:00 Arsenal v Liverpool
Jumatatu Februari 17
2245 Brighton v Hull
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 

KESI YA MOHAMMED MOSRI KUSIKILIZWA LEO

Mohammed Morsi akiwa mahakamani
Aliyekuwa rais wa Misri Mohammed Morsi atafika katika mahakama moja mjini Cairo ili kusikiza mashtaka ya upelelezi na njama ya kutaka kutenda ugaidi yanayomkabili.
Bwana Morsi aling'atuliwa mamlakani na jeshi mnamo mwezi Julai na sasa anakabiliwa na mashtaka mengine matatu.
katika kesi hiyo yeye na wanachama wengine 35 wa vunguvu la Muslim Brotherhood wanatuhumiwa kwa kushirikiana na makundi ya kigeni kama vile Hamas,Walinzi wa mapinduzi nchini Iran na Hezbollah kupanga mashambulizi nchini Misri.
Iwapo atapatikana na hatia bwana Morsi anakabiliwa na hukumu ya kifo.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

KIONGOZI WA DHEHEBU LA SHIA AJIUZULU


Moqtada al-Sadr akitoa taarifa kwa vyombo vya habari
Kiongozi wa Dhehebu la Shia nchini Iraq Moqtada al-Sadr ametoa taarifa akitangaza kujiuzulu kwake katika ulingo wa kisiasa.
katika tangazo ambalo halikutarajiwa na wengi na ambalo liliwekwa katika mtandao wake,Bwana Sadr amesema kuwa hatashikilia wadhfa wowote wa serikali wala kuwa na wawakilishi bungeni.
Taarifa hiyo pia imesema kuwa atazifunga afisi zake zote isipokuwa zile za kutoa misaada pekee.
Bwana Sadr na wanamgambo wake wa Mahdi walipata ushawishi nchini Iraq baada ya uvamizi wa marekani nchini humo mnamo mwaka 2003.
lakini katika miaka ya hivi karibuni amepoteza umaarufu wake kufuatia mzozo kati yake na waziri mkuu nchini humo Nouri al-Maliki.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

TANGAZO MUHIMU KWA WAJUMBE WA BUNGE MAALUM LA KATIBA



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA




BUNGE MAALUM

TAARIFA KWA WAJUMBE WA BUNGE MAALUM LA KATIBA _______________________________________________

 Kufuatia wito wa Serikali kuwa Wajumbe wote wanaombwa kufika Mjini Dodoma kuanzia tarehe 16 Februari, 2014 katika Viwanja vya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano na Katibu wa Baraza la Wawakilishi, Zanzibar wanapenda kuwaarifu Wajumbe wote maandalizi yafuatayo: -


1.0        USAFIRI WA KUFIKA DODOMA 

Wajumbe wote wanatakiwa kujigharamia wenyewe kufika Dodoma kwa vyombo vya usafiri wa umma.  Wajumbe watarejeshewa gharama za usafiri wa kufika Dodoma kutoka maeneo wanayotoka baada ya kuwasilisha stakabadhi za gharama walizotumia kwa usafiri.


2.0        MALAZI

Utaratibu wa malazi umeandaliwa.  Hoteli zilizoteuliwa kwa malazi kwa Wajumbe kuchagua kwa kadri itakavyowapendeza zimeainishwa.  Hoteli hizo ni hizi zifuatazo: 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz   

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI FEBRUARI 16, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz  

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...