Wednesday, February 05, 2014

MTIBWA SUGAR KUWAKARIBISHA SIMBA UWANJA WA JAMHURI LEO MOROGORO

Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaingia raundi ya 16 leo (Februari 5 mwaka huu) kwa mechi tano huku Mtibwa Sugar ikiikaribisha Simba kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Kiingilio katika mechi hiyo ambayo itakuwa ya kwanza kuchezwa kwenye uwanja huo wenye uwezo wa kuchukua watazamaji 10,000 tangu uanze mzunguko wa pili wa VPL kitakuwa sh. 5,000. Jonisia Rukyaa kutoka Bukoba ndiye atakayechezesha mechi hiyo.
Mechi nyingine za ligi hiyo ni Tanzania Prisons vs Coastal Union (Sokoine, Mbeya), Mgambo Shooting vs Ruvu Shooting (Mkwakwani, Tanga), Rhino Rangers vs Oljoro JKT (Ali Hassan Mwinyi, Tabora) na JKT Ruvu vs Ashanti United (Chamazi, Dar es Salaam).
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

TANZANIA YAKAMATA DAWA ZA KULEVYA ZAIDI YA KILO 200

http://jambotz8.blogspot.com/
Polisi nchini Tanzania wamekamata shehena ya dawa za kulevya aina ya Heroin zenye uzito wa kilo 201 katika eneo la bahari kati ya Dar es Salaam na Zanzibar nchini humo.
Kamanda wa kikosi maalum cha kuzuia dawa za kulevya Godfrey Nzowa ameiambia BBC kuwa Watu 12 wanashikiliwa kuhusiana na shehena hiyo.
Kamanda Nzowa amesema dawa hizo za kulevya zimekamatwa na Polisi wa doria baharini muda wa saa sita usiku wa kuamkia Jumanne zikisafirishwa katika Jahazi.
Kwa mujibu wa Kamanda Nzowa Shehena hiyo ilikuwa ikitoka nchini Iran kuelekea nchi au eneo ambalo mpaka sasa bado halijafahamika.
Hivi karibuni kumekuwa na matukio ya kukamata dawa za kulevya aina mbalimbali kupitia viwanja vya ndege,nchi kavu na baharini, ambapo mwaka jana kiasi kikubwa cha dawa za kulevya zilizokamatwa ziliteketezwa.
CHANZO:BBC
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz 


MAGAZETI YA LEO JUMATANO FEBRUARI 05, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

NEC KUTANGAZA TAREHE YA UCHAGUZI JIMBO LA KALENGA

malaba1 38164
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema wiki hii itatangaza tarehe ya uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Kalenga, lililopo wazi baada ya aliyekuwa Mbunge wake, Dk William Mgimwa (CCM) kufariki dunia Januari Mosi mwaka huu nchini Afrika Kusini.
Licha ya Kalenga, tume hiyo imesema uchaguzi mdogo pia utafanyika Jimbo la Chalinze baada ya Mbunge wake, Said Bwanamdogo (CCM) kufariki dunia Januari 22 mwaka huu.
Akizungumza ofisini kwake jana, Mkurugenzi wa Uchaguzi, Julius Malaba alisema uchaguzi mdogo hauwezi kufanyika kama jimbo litakuwa wazi miezi 12 kabla ya Uchaguzi Mkuu.
"Wabunge hawa wamefariki dunia ikiwa imebaki miezi zaidi ya 12 kabla ya Uchaguzi Mkuu na kuvunjwa kwa Bunge, hilo
linamaanisha chaguzi zitafanyika na wiki hii NEC itatangaza tarehe ya uchaguzi jwa Kalenga," alisema Malaba.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

LIBYA YAHARIBU SILAHA ZA SUMU

libya1_43539.jpg
Libya imekamilisha uharibifu wa silaha za kemikali katika mpango ulioanza miaka tisa iliyopita chini ya uongozi wa aliyekuwa rais, Muammar Ghaddafi.
Tangazo hilo lilipitishwa katika mkutano wa wanahabari uliofanyika Jijini Tripoli na kuhudhuriwa na wajumbe wa kimataifa .
Ikisaidiwa na Marekani, Ujerumani, na Canada, Libya imeharibu shehena ya sumu ya mvuke pamoja na silaha nyengine zenye sumu.
Katika mkutano huo Katibu Mkuu wa Shirika la Silaha za kemikali zilizopigwa marufuku amepongeza Libya kwa kuchukua hatua hiyo muhimu.
Amesema kwamba hatua hiyo ni mfano mwema wa ushirikiano wa kimataifa ambao unaigwa na taifa la Syria kwa kiwango kikubwa.
Kwenye mkutano huo waziri wa maswala ya kigeni nchini Libya ameeleza kwamba hatua hiyo ni ya kihistoria na ni mafanikio kutokana na ushirkiano na washirika wa kimataifa.
Mnamo mwaka wa 2004,Libya ilikuwa na takriban tani 13 za sumu ya mvuke.
Mrundiko huo wa kemikali hatari kwa sasa umeharibiwa.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Saturday, February 01, 2014

MWILI WA MTOTO ALBINO WAZIKWA NDANI YA NYUMBA SUMBAWANGA

Kamanda Jacob  Mwaruanda.
Mwili  wa mtoto wa kike  mwenye umri wa miaka minne mwenye ulemavu wa  ngozi (albinism)  umezikwa  ndani ya nyumba ya babu yake  mjini Sumbawanga katika mkoa wa Rukwa  badala  ya kuzikwa katika  shamba la wafu  la  Wakatoliki.Tukio  hilo la  maziko  ya  mtoto  huyo  licha  ya  kuwa  gumzo mjini hapa, pia  lilihudhuriwa  na  umati mkubwa  wa waombolezaji.  
Uamuzi  huo  unasadikiwa  na  wengi   kuwa ni  hofu  kuwa  endapo  mwili wake  ungezikwa  katika  shamba la wafu  upo uwezekano mabaki yake kufukuliwa na kunyofolewa  viungo  vyake na watu  wenye  imani za kishirikina.
Mwaka jana watu wawili wenye ulemavu  wa ngozi walishambuliwa na kunyofolewa mikono yao na  watu  wenye imani  za kishirikiana  ambao  wanadaiwa kuamini kuwa  viungo vya binadamu hao    vina  uwezo  mkubwa  wa kumtajirisha  mtu  kwa muda mfupi.
Kwa mujibu wa Kamanda  wa Polisi mkoani hapa, Jacob  Mwaruanda watuhumiwa  katika  visa  vyote viwili  walikamatwa na  mashauri yao yako  katika  hatua  mbalimbali  za kusikilizwa   mahakamani.
Baadhi  ya waombolezaji  walioshuhudia  maziko ya mtoto  huyo yaliyofanyika juzi saa kumi na moja jioni  walisikika  wakisema; "Tumefarijika  mwili  wa marehemu kusitiriwa  ndani ya  nyumba ya  babu yake  tulikuwa na hofu sana maana  kama  angezikwa  makaburini   baada ya  waombolezaji  kuupa  kisogo  shamba hilo la wafu  hakika ungefukuliwa."
Akizungumza na  mwandishi  wa habari hizi  hapo  msibani, mjomba  wa marehemu  aitwaye  God  Mwangamila ' Kizibo'  ambaye alikuwa akiishi na mtoto  huyo  kuwa  aliaga dunia  Januari 29,  nyumbani kwake mjini hapa kutokana na ugonjwa wa malaria.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI FEBRUARI 01, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

UWANJA WA AZAM COMPLEX WARUHUSIWA KUCHEZEWA MECHI ZA KIMATAIFA

chamazi_2
Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika CAF leo tarehe 31 Januari 2014 limeupa kibali cha kuchezea mashindanoya kimataifa yanayoandaliwa na CAF uwanja wa Azam Complex Chamazi na kuufanya uwanja wa kwanzaunaomilikiwa na klabu Afrika Mashariki  kuruhusiwa kuandaa (ku-host) mashindano makubwa ya vilabu
Kwa mujibu wa barua pepe iliyotumwa leo na CAF kupitia kwa naibu mkurugenzi wa mashindano Bwana Khaled Nassar, Uwanja wa Azam Compex Chamazi umepita vigezo vyote vinavyohitajika na CAF kuchezewa mashindano ya kimataifa hivyo kuanzia tarehe ya leo, uwanja huu unaruhusiwa “kuchezewa mechi za CAF
Bwana Khaled ameandika katika taarifa yake ya barua pepe kwenda TFF na Azam FC kuwa CAF ilimtuma mkaguziwake toka nchini Zimbabwe Bwana Wilfried Mukuna kuja kukagua uwanja huu. Bwana Mukuna aliwasilisha ripoti CAF iliyopelekea shirikisho hilo kutoa kibali kwa Azam FC na TFF kuruhusiwa kuutumia uwanja huu kwa mechi zinazoandaliwa na CAF
Uongozi wa Azam FC umetoa shukrani kwa mkaguzi wa CAF Bwana Mukuna, Uongozi wa TFF chini ya Rais Jamal Malinzi, na uongozi wa CAF Cairo Misri hasa Bwana Khaled Nasser kwa kuwezesha zoezi hili kufanyika kwa uwazi na uweledi wa hali ya juu uliopelekea uwanja wetu kupata kibali cha kutumika kwenye michezo ya kimataifa.
Azam FC sasa imewatangazi wapenzi wake kuwa kuanzia msimu huu mechi zake za  CAF zitachezwa Azam Complex Chamazi.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Thursday, January 30, 2014

MKUU WA WILAYA AFUNGA KIWANDA CHA SUKARI

miwa e4424
Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Antony Mtaka amekifungia kwa muda usiojulika shughuli za uzalishaji, Kiwanada cha Sukari cha Mtibwa mpaka kiwanda hicho kitakapolipa madeni ya wafanyakazi na wakulima wa miwa.
Akitoa msimamo wa Serikali ya wilaya hiyo juu ya kukifungia kiwanda hicho mbele ya wafanyakzi na wakulima hao katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika ofisi za mtendaji wa kata ya Mtibwa wilayani hapa, Mtaka alisema, wamechukua uamuzi huo baada ya mabishano ya muda mrefu baina ya pande mbili kutofikia muafaka.
Mkuu huyo wa wilaya katika mabishano hayo ya muda mrefu juu ya madai ya wakulima na wafanyakazi alisema wanakidai Kiwanda cha Mtibwa zaidi ya Sh1.9 bilioni ambazo ni za mauzo ya miwa na mishahara ya wafanyakazi.
Mtaka alisema shughuli nyingine kiwandani hapo zitaendelea kama huduma ya afya, ulinzi na idara ya fedha ili kuwezesha makundi hayo kupata mafao yao mwishoni mwa wiki hii kama ilivyoahidiwa na uongozi wa kiwanda hicho.
Meneja mkuu Hamad Juma alisema, kiwanda hicho kilikwama kulipa madeni hayo kutokana na uingizwaji mwingi wa sukari nchini uliosababisha wao kukosa soko ingawa waliahidi kuanza kulipa mwezi huu. Chanzo: mwananchi

MAN UNITED YAKATAA MABILIONI KWA JANUZAJ

JANU eb4eb
HATUTAKI, na tena hatutaki hata kusikia. Na ikiwezekana msirudi tena. Ndivyo ambavyo mapovu yamewatoka mdomoni watu wa Manchester United baada ya PSG kurudi mezani juzi Jumapili na ofa ya kumtaka kinda wao mahiri, Adnan Januzaj.
PSG wamekuwa wakitokwa udenda kwa kinda huyo mwenye asili ya Albania aliyezaliwa Ubelgiji miaka 18 iliyopita na hawajali kama aliingia mkataba mpya wa kuichezea Man United mwishoni mwa msimu uliopita.
Hata hivyo, kocha David Moyes amekataa ofa hiyo ya PSG inayodhaniwa kuanzia Pauni 25 milioni na kuendelea huku wakisisitiza kwamba hawana mpango hata wa kukaa chini na kuzungumza na matajiri hao wa mafuta kutoka Paris.
Man United imempatia mkataba mrefu wa miaka mitano Januzaj Oktoba mwaka jana baada ya kugundulika kuwa huenda mchezaji huyo angekuwa huru na kuondoka Mei mwaka huu mara baada ya msimu kumalizika.

RAIS KIKWETE AMPIGA KIJEMBE RAGE

rage1 1d2f4
RAIS Jakaya Kikwete amemshangaa Mwenyekiti wa Simba SC ya jijini Dar es Salaam, Ismail Aden Rage kwa kuitisha mkutano wenye ajenda moja kwa ajili ya wanachama wa klabu hiyo. Wiki iliyopita, Mwenyekiti wa Simba Rage, alitangaza kuwepo kwa mkutano wa klabu hiyo Machi 23 na kueleza wazi kuwa kutakuwa na ajenda moja ya kujadili mapungufu ya Katiba.
Akizungumza mbele ya umati wa watu waliohudhuria mazishi ya Mbunge wa Chalinze, Saidi Bwanamdogo mwishoni mwa wiki iliyopita, Rais Kikwete ambaye alifika katika eneo la makaburi, alimuuliza Mwenyekiti huyo wa Simba kuhusiana na maandalizi ya mkutano huo.
"Ndugu yangu Rage mimi Mwenyekiti mwenzio, lakini sijawahi kuona mkutano wenye ajenda moja ndio kwanza huo wa kwako, yaani wewe kiboko, pamoja na makelele yote lakini umeweza kutuliza hali ya mambo mpaka leo umedumu kuwa mwenyekiti," alisikika Rais Kikwete akisema huku mamia ya waombolezaji wakicheka.
Akizungumzia kauli hiyo ya Rais Kikwete, Rage alisema ili kuwa kiongozi imara ndani ya klabu za Simba na Yanga, inakupasa kuwa na roho ngumu, kwani bila ya kufanya hivyo wanachama watakuwa wakikuchezea kila kukicha.
"Mheshimiwa Rais kuwa kiongozi ndani ya klabu hizi mbili kunahitaji umakini sana, kwani bila ya kufanya hivyo wewe utakuwa ni kiongozi wa kupelekwa kila siku na hatimaye unamaliza muda hakuna ulichokifanya ndani ya uongozi wako," alisema Rage. Chanzo: mtanzania

IKULU YAVUNJA UKIMYA KUHUSU "MAWAZIRI MIZIGO" ...!!!


kawambwa_2846f.jpg
SHUKURU KAWAMBWA
Dar es Salaam. Ikulu imetaka kufungwa kwa mjadala wa kuhusu kurudishwa kwa mawaziri wanaodaiwa kuwa ni mizigo kwenye Baraza la Mawaziri na badala imetaka waachwe wafanye kazi.
Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu alisema kuendeleza mjadala huo ni kupoteza muda, kwani Rais Jakaya Kikwete alishamaliza kazi yake.

Rweyemamu alisema Rais ndiye mwenye mamlaka ya kuteua mawaziri ambao wana wajibu wa kumsaidia katika utekelezaji wa majukumu yake, hivyo si sahihi wateule hao kuitwa 'mizigo' kwani yeye (Rais) ameona wanafaa.
"Rais anapoteua watu anaangalia wanaofaa kumsaidia na si vinginevyo. Kwani lengo lake ni kuona nchi ina 'move forward' (inasonga mbele) kimaendeleo," alisema Rweyemamu. Alisema watu wanapaswa kukumbuka kuwa mtu anapoteuliwa kwenye uwaziri kuna suala la uwajibikaji: "Anatakiwa kutekeleza uwajibikaji wa pamoja. Sasa kumshambulia mtu binafsi na kumwita mzigo siyo sahihi."

Rweyemamu alisema mjadala huo kwa sasa umepitwa na wakati na kuwataka wananchi na wachambuzi kuwaacha mawaziri hao kuchapa kazi.
"Ni vizuri wananchi wakawapa nafasi mawaziri hawa ya kufanya kazi na baadaye kuwapima na kuwachambua kutokana na utendaji wao," alisema.
Chimbuko la majadala
Mjadala kuhusu suala hilo unatokana na Rais Kikwete kuwarejesha katika Baraza la Mawaziri baadhi ya mawaziri ambao walidaiwa kuwa ni mizigo kutokana na udhaifu katika utendaji wao.

NEC "DAFTARI LA WAPIGA KURA LITABORESHWA"

 
Mwenyekiti wa Nec, Jaji Damian Lubuva.PICHA|MAKTABA 
**********
Pamoja na kushindwa kutaja tarehe rasmi ya kuanza kuboresha daftari la kudumu la wapigakura, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) imesema daftari hilo litaboreshwa kabla ya kuanza kwa upigaji wa kura ya maoni kwa ajili ya kupata Katiba Mpya. Upigaji wa kura hiyo utafanyika ndani ya siku 70 baada ya kumalizika kwa Bunge Maalumu la Katiba linalotarajiwa kuanza katikati ya mwezi ujao mjini Dodoma. Litafanyika kwa kati ya siku 70 na 90.

Nec imetoa ufafanuzi huo baada ya kuwepo kwa malalamiko kutoka kwa vyama vya siasa na wananchi kwamba tangu uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, daftari hilo halijawahi kuboreshwa, jambo ambalo litasababisha upigaji wa kura kwa ajili ya kupata Katiba Mpya kutawaliwa na vurugu. Malalamiko hayo yanatokana na kuwepo kwa idadi kubwa ya watu waliotimiza umri wa kupiga kura lakini hawamo katika daftari hilo.
Pia waliopoteza vitambulisho vya kupigia kura na wenye kasoro mbalimbali zinazowafanya wapoteze sifa.

HAYA HAPA MATOKEO YA MECHI ZA LIGI KUU YA UINGEREZA, USIKU WA JUMATANO

MAGAZETI YA LEO JANUARI 30, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...