Sunday, January 12, 2014

RAIS KIKWETE ATANGAZA JUMATATU JANUARI 13, 2014 KUWA NI SIKU YA MAPUMZIKO

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail:  ikulumawasiliano@yahoo.com press@ikulu.go.tz              

Fax: 255-22-2113425

PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
       P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
                                         
TAARIFA KWA  UMMA.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametangaza kuwa kesho, Jumatatu, Januari 13, 2014, itakuwa ni Siku ya Mapumziko (Public Holiday) kwa Watanzania wote kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Rais Kikwete ameutangaza uamuzi huo mjini Zanzibar ambako leo ameungana na Watanzania na Wazanzibari wote kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Januari 12, mwaka 1964.

Mapinduzi hayo yaliyoongozwa na mwasisi wa Zanzibar na Taifa la Tanzania, Hayati Abeid Amaan Karume yalifanikiwa kuung’oa madarakani utawala dhalimu wa Sultan na kuwawezesha kwa mara ya kwanza katika historia Waafrika walio wengine kujitawala ndani ya nchi yao wenyewe.

Yalikuwa ni Mapinduzi ya Zanzibar yaliyofungua njia ya kuzaliwa kwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar – miezi mitatu baada ya Mapinduzi hayo – Aprili 26, 1964.               
Naye Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Ali Mohamed Shein ametangaza kuwa kesho itakuwa Siku ya Mapumziko Tanzania Visiwani kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Rais Shein alitangaza mapumziko hayo wakati alipohutubia wananchi kwenye Uwanja wa Michezo wa Amaan mjini Zanzibar katika kusherehekea miaka 50 ya Mapinduzi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametangaza kuwa kesho, Jumatatu, Januari 13, 2014, itakuwa ni Siku ya Mapumziko (Public Holiday) kwa Watanzania wote kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Rais Kikwete ameutangaza uamuzi huo mjini Zanzibar ambako leo ameungana na Watanzania na Wazanzibari wote kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Januari 12, mwaka 1964.

Mapinduzi hayo yaliyoongozwa na mwasisi wa Zanzibar na Taifa la Tanzania, Hayati Abeid Amaan Karume yalifanikiwa kuung’oa madarakani utawala dhalimu wa Sultan na kuwawezesha kwa mara ya kwanza katika historia Waafrika walio wengine kujitawala ndani ya nchi yao wenyewe.

Yalikuwa ni Mapinduzi ya Zanzibar yaliyofungua njia ya kuzaliwa kwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar – miezi mitatu baada ya Mapinduzi hayo – Aprili 26, 1964.               
Naye Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Ali Mohamed Shein ametangaza kuwa kesho itakuwa Siku ya Mapumziko Tanzania Visiwani kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Rais Shein alitangaza mapumziko hayo wakati alipohutubia wananchi kwenye Uwanja wa Michezo wa Amaan mjini Zanzibar katika kusherehekea miaka 50 ya Mapinduzi.

Mwisho.

Imetolewa na;
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS
Ikulu,
es Salaam.
12 January, 2014

ANGALIA PICHA ZA MAADHIMISHO YA MIAKA 50 YA MAPINDUZI YALIVYOFANA ZANZIBAR LEO.

 Rais wa Zanzibar Dk.Ali Mohamed Shein akiwapungia wananchi wa Zanzibar wakati akiingia kwenye uwanja wa Amani  na gari la wazi kwenye maadhimisho ya miaka 50 ya Mapinduzi.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akiwapungia mamia ya wakazi wa Zanzibar wakati akiwasili kwenye Uwanja wa Amani kwenye kilele cha sikukuu ya miaka ya 50 ya Mapinduzi.
 Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni akisalimiana na baadhi ya viongozi waandamizi wa Jeshi kwenye uwanja wa Amani wakati wa maadhimisho ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

CHAMA KIPYA CHA SIASA CHAJA, WALIOFUKUZWA WATAJWA KUKIANZISHA


MSA 775c5
*Chadaiwa kuundwa na waliofukuzwa upinzani
WAKATI fukuto la kufukuzwa uanachama kwenye Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) likiwa bado bichi, chama kipya cha siasa kimeanzishwa na watu wanaodaiwa kuwa ni muungano wa wanachama waliofukuzwa kutoka vyama vya upinzani nchini.

Taarifa zilizotufikia na kuthibitishwa na Ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa nchini, zinakitaja chama hicho kuwa ni African Alliance for Change and Transparence (AACT) na kwamba mipango ya usajili wa muda wa chama hicho inadaiwa kuanza kuratibiwa kwa takribani mwezi mmoja sasa.
Chama hicho kimekamilisha baadhi ya taratibu na kinatarajiwa kupewa usajili wa muda na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa siku ya Jumanne, wiki ijayo.
Upo uwezekano wa wanachama waliofukuzwa uanachama kutoka Chadema hivi karibuni kujiunga na chama hicho. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

WAZIRI AUAWA KWA KUPIWA RISASI ALIPOKUWA ZIARANI...!!!

014915548-57daaf1f-2e9a-4da7-8305-4392c1149482_dcc90.jpg
Naibu Waziri wa viwanda nchini Libya ameuawa kwa kupigwa risasi wakati alipokuwa ziarani mjini Sirte Mashariki mwa Tripoli ambako alizaliwa.
Vyombo vya habari nchini humo vinasema kuwa watu wasiojulikana walimfyatulia risasi kadhaa Hassan al-Droui karibu na soko rasmi mjini humo. Ni mauaji ya kwanza ya afisa wa serikali ya mpito ya Libya.
Libya imekuwa ikikumbwa na vurugu tangu kuondolewa mamlakani kwa hayati Muammar Gaddafi mwezi Oktoba mwaka 2011. Sirte ilikuwa ngome ya mwisho ambako mapigano yalitokea wakati wa harakati za mapinduzi ya Muamar Gaddafi ambaye alikamatwa na kupigwa risasi akijaribu kujificha kutoka kwa waasi.
Bwana al-Droui alikuwa mwanachama wa zamani wa baraza la mpito lililosimamia kipindi cha mpito baada ya Gadaffi kuuawa. Aliteuliwa kama naibu waziri na waziri mkuu wa kwanza wa mpito na kuendelea kushikilia wadhifa huo hata baada ya Ali Zeidan kuchukua mamlaka.
 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MAKONDA AMVAA TENA MH. LOWASSA ...!!!


Paul Makonda, Mkuu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi Taifa, UVCCM
*******
KWA kipindi kirefu sasa vijana ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) tumeshuhudia na kusikia kauli na vitendo vya baadhi ya wanachama wa CCM vinavyoashilia ukiukwaji wa makusudi wa maadili, miiko na kanuni za Chama. CCM katika uhai wake wa miaka 37 baada ya kuunganisha TANU na ASP, imeendelea kukua na kushamiri kutokana na misingi imara ya kikatiba tuliyojiwekea tangu mwaka 1977, ambayo wana CCM wote kwa utashi na hiari tumeienzi na kuifuata. Asiyetaka, ni ruksa kuondoka na kutuachia chama chetu.

Ni kwa njia hii tumeweza kuimarisha mshikamano ndani ya Chama Cha Mapinduzi na kutuwezesha kushinda katika chaguzi mbali mbali, hivyo kuendelea kutoa uongozi katika ngazi zote za utawala nchini. Hivyo basi, kitendo chochote kile chenye mwelekeo wa kubomoa mshikamano ndani ya Chama, ni kitendo cha kutudhoofisha, hivyo kutuengua katika uongozi wa nchi. HILI KWA VIJANA WA CCM, HALIKUBALIKI!
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

VIJUE VYAKULA 10 AMBAVYO MWANAUME ANATAKIWA KULA ILI KUONGEZA UWEZO WAKATI WA TENDO LA NDOA...!!!

Aina hizi za samaki zinazovuliwa baharini huwa na madini ya zink na chumvi ambayo yanatajwa kusaidia uzalisha wa vichocheo vinavyohamasisha msisimko wa mwili wakati wa tendo la ndoa.
 
2. POMEGRANATE
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Saturday, January 11, 2014

MTOTO WA AJABU... ANAKULA SUFULIA ZIMA LA WALI, ANAKUNYWA MAJI NDOO MOJA NA KUMALIZA MIKATE SABA KWA MKUPUO LAKINI HASHIBI...!!!

AMA kweli ukistaajabu ya Musa utayaona ya Farao, Andrea Marcus (13), mkazi wa Mbezi-Kibanda cha Mkaa, Dar anadaiwa kuwa wa ajabu kutokana na vitendo vyake.
Mtoto huyu amedaiwa kuwa ni wa kichawi kutokana na maajabu yafuatayo:

 
Mkazi wa Mbezi-Kibanda, Andrea Marcus.
Ana uwezo wa kula ubwabwa sufuria moja la familia, anamudu kunywa maji ndoo moja, ana uwezo wa kuingiza tumboni mikate mikubwa saba kwa mlo mmoja,  amewahi kula mchele (si ubwabwa) ndoo nzima. Mbaya zaidi baada ya kula milo hiyo huwa haoneshi ameshiba.
Maajabu mengine ambayo yanawashangaza watu wanaoishi naye ni jinsi anavyokula chakula kwa kumwaga chini kisha kukomba mpaka udongo.
“Sina amani ya moyo, naomba Watanzania wanisaidie, mwanangu ananiuma sana, hata kujisaidia ni hapohapo, chakula anakula kupita kiasi, kama nilivyosema hashibi na bado hali kama mwanadamu wa kawaida,” alisema mama wa mtoto huyo.

BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI LAIVA....!!!

 
Rais Jakaya Kikwete, anaweza kutangaza mabadiliko katika baraza lake la mawaziri wakati wowote kuanzia sasa.
Hatua hiyo inafuatia uteuzi wa mawaziri watatu kutenguliwa, mmoja kujiuzulu na mwingine kufariki dunia.

Desemba 20, mwaka jana, Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira iliwasilisha bungeni taarifa ya uchunguzi kuhusiana na athari zilizojitokeza katika Operesheni Tomokeza Ujangili iliyositishwa na serikali wakati wa Mkutano wa 13 wa Bunge kufuatilia malalamiko ya wananchi, wabunge na wadau.

Akiwasilisha ripoti hiyo, Mwenyekiti wa kamati hiyo, James Lembeli, alisema uchunguzi wao ulibaini kuwa operesheni hiyo iliendeshwa bila kufuata taratibu na matokeo yake kusababisha mateso kwa raia, vifo na upotevu wa mali hususani mifugo.

Baada ya ripoti hiyo kuwasilishwa, wabunge walichachamaa na kushinikiza mawaziri ambao wizara zao zilihusika katika utekelezaji wa operesheni hiyo wawajibike kisiasa au wawajibishwe.

Aliyekuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, aliamua kujiuzulu wakati mjadala ukiendelea na siku hiyo baadaye Rais Kikwete, alikubaliana na mapendekezo ya wabunge kwa kutengua uteuzi wa mawaziri watatu, Dk. Emmanuel Nchimbi (Mambo ya Ndani ya Nchi); Mathayo David Mathayo (Mifugo na Maendeleo ya Uvuvi) na Shamsi Vuai Nahodha (Ulinzi na JKT).

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JANUARI 11, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

RAIS AJIUZULU BAADA YA SHINIKIZO KALI

 Rais wa mpito wa Jamuhuri ya Afrika ya Kati, Michel Djotodia, amejiuzulu kufuatia shinikizo kali na kukosolewa kwa mwendo wake wa kujikokota katika kusuluhisha mgogoro wa kidini unaotokota nchini humo.
Hatma ya Djotodia ilikuwa swala kuu katika ajenda ya mkutano wa viongozi wa kikanda kuhusu mzozo unaoendelea nchini humo. Taarifa zinazohusiana Afrika, Siasa
Mkutano huo ulifanyika nchini Chad huku maelfu wakiendelea kutoroka nchini humo kutokana na ghasia.
Maelfu ya watu waliandamana leo katika barabara za mji mkuu Bangui kumtaka Rais Djotodia, ajiuzulu.
Rais Djotodia amekosolewa vikali kwa kukosa kumaliza mapigano ya kidini kati ya wakristo na waliokuwa waasi waisilamu ambao walimsaidia kuingia mamlakani kwa njia ya mapinduzi mwaka jana.
Baraza lote la mpito katika Jamuhuri ya Afrika ya kati limekwenda nchini Chad ambako viongozi wa Afrika wanakutana kujadili mzozo unaoendelea nchini humo.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Friday, January 10, 2014

CHADEMA HAPAKALIKI TIMUA TIMUA YAENDELEA... KATIBU WA WILAYA ASIMAMISHWA KAZI

  Kamati ya utendaji ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi, imemsimamisha Katibu wake, Jordan Membe, kwa madai ya kwenda kinyume na katiba ya Chama.

Habari kutoka wilayani humo zilizothibitishwa na uongozi wa chama hicho, ngazi ya wilaya na ile ya mkoa, zinaeleza Membe amesimamishwa kutokana na
kukiuka maadili ya uongozi, ikiwa ni pamoja na kujihusisha na masuala ya kuleta na
kusababisha vurugu ndani ya chama.

Baadhi ya wajumbe waliohudhuria kikao hicho, kilichofanyika makao makuu ya ofisi ya chama hicho, wilayani Nachingwea, ambao hawakupenda majina yao kuandikwa kwenye vyombo vya habari kwa madai sio wasemaji wa Chama, wameeleza kuwa Membe anadaiwa kusambaza waraka unaopinga kuondolewa kwa aliyekuwa Naibu Katibu mkuu, Zitto Zuberi Kabwe na wenzake.


Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

IGP ATANGAZA MABADILIKO MAKUBWA JESHI LA POLISI


Mkuu Mpya wa Jeshi la Polisi, Inspekta Jenerali, Ernest Mangu ameanza kazi kwa kutangaza mabadiliko ya mfumo wa jeshi hilo huku akiunda vitengo vipya kwa lengo kuongeza ufanisi katika kukabiliana na uhalifu.
Katika mabadiliko hayo, IGP Mangu amesema polisi wameanzisha kamisheni mpya tano ambazo ni Intelijensia, Utawala, Fedha na Ugavi, Upelelezi, Uchunguzi wa Kisayansi wa Kesi za Jinai na Polisi Jamii.
Mfumo huo mpya wa polisi ndiyo uliowezesha kuundwa kwa nafasi mpya ya Naibu IGP, ambayo mteule wake wa kwanza ni Abdulrahman Kaniki ambaye kabla ya hapo alikuwa Kamishna wa Uchunguzi wa Sayansi wa Makosa ya Jinai. Nafasi hiyo sasa inakaimiwa na watu waliokuwa chini yake.
Viongozi wengine katika safu hiyo ni Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI), Kamishna Issaya Mngulu, Kamishna wa Operesheni na Mafunzo, Paul Chagonja, Kamishna wa Fedha na Ugavi, Clodwig Mtweve, Kamishna wa Utawala, Thobiasi Andengenye na Kamishna wa Polisi Jamii, Mussa Ali Mussa. Naibu Kamishna wa Polisi, Diwani Athuman yeye anakaimu nafasi ya Kamisheni ya Intelijensia.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA JANUARI 10, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MAJIBU YA UBALOZI WA TANZANIA CHINA JUU YA JACKIE CLIFF KUNASWA NA MADAWA YA KULEVYA HUKO MACAU/CHINA


J Cliff 1

Mwezi December 2013 taarifa zilitoka kwamba kuna binti wa Kitanzania mwenye umri wa miaka 28 aliekamatwa na dawa za kulevya huko Macao China ambapo baadhi ya taarifa zilizoripotiwa na Waandishi wa Tanzania zilisema aliekamatwa ni mrembo ambae amekua akionekana kwenye video kadhaa za wasanii wa bongofleva (Jackie Cliff).
Macao

Macao.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

WAFANYABIASHARA WA DAR WAGOMEA MASHINE ZA TRA TENA ... WAAMUA KUFUNGA MADUKA YAO




Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...