Monday, January 06, 2014

RAIS WA ZIMBABWE ROBERT MUGABE AZIRAI GHAFLA...!!!

mu 77055

Mtu kutoka ndani ya chama tawala cha serikali ya Zimbabwe amesema kuwa kiongozi wa muda mrefu na rais wa taifa hilo la Afrika, Robert Mugabe amezirai ghafla.

Happyton Bonyongwe, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kijasusi la Zimbabwe alilipotiwa akisema kwamba ulinzi umeimarishwa katika ikulu ya Zimbabwe, siku moja baada ya hofu ya kuzirai kwa Mugabe na hali yake yake ya kiafya kuenea nchi nzima.

Baba Jukwa, ambaye ni mtoa taarifa ndania ya chama tawala cha Zanu-PF ambaye anatumia mtandao wa facebook ameanika rushwa na ufisadi katika serikali ya Mugabe vimekithiri huku taarifa ya kuanguka na kuzirai kwa Mugabe zikiwa zimezagaa nchi nzima.
Hata hivyo, aliongeza kuwa Rais Mugabe hali yake ya kiafya si nzuri lakini katibu wa Rais huyo ndugu George Charamba, alikanusha taarifa hizo kwamba Mugabe ni mgonjwa.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

ANGALIA MAZISHI YA WAZIRI MGIMWA KATIKA PICHA

IMG 0035 1811f

IMG 0086 0993a

IMG 0095 4d12c
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

ASKARI WAWILI MBARONI KWA KUTEKA MAGARI MBEYA...!!!


 
Askari mwenye cheo cha sajini katika  Gereza la Ruanda na polisi mwenye cheo cha konstebo  katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini Mbeya, wamekamatwa kwa tuhuma za kushirikiana na watu wengine watatu, kwa kuteka gari  na kupora  fedha na mali  katika eneo la Mlima wa Kawetere, Barabara ya Mbeya-Chunya, juzi jioni.
Inadaiwa kuwa katika tukio hilo, watuhumiwa walipora Sh3.5 milioni  na mabegi yaliyokuwa na  vitu mbalimbali.
Watuhumiwa hao wanadaiwa kushiriki katika kupora mali ya mfanyabiashara Sheedhar Paupeleti (38) baada ya kuteka gari alilokuwa akisafiria akiwa na watu wengine wawili.
Habari zilisema katika tukio hilo, dereva wa gari hilo Ezekiah Matatira, alifungwa pingu.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Ahmed Msangi, alisema majambazi hayo yalikamatwa baada ya polisi kwenda katika  eneo la tukio, kutokana na taarifa zilizotolewa na wananchi kwa njia ya simu.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JANUARI 06, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC 0020 ed8be
DSC 0021 61136
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Saturday, January 04, 2014

HAWA HAPA NDIO WALIOPENDEKEZWA NA CHADEMA ILI WATEULIWE NA RAIS BUNGE LA KATIBA


Kamati Kuu CHADEMA leo kimewapendekeza Prof. Abdallah Safari, Mabere Marando, Nasra Juma Baruan na Method Kimomogolo ili wateuliwe na Rais Bunge la Katiba.
Professor Abdallah Safari ni mwanasheria nguli wa chama hicho na pia ni Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Pwani. Huku Method Kimomogolo ni mwanasheria maarufu wa Chama hicho ambaye ameongoza kesi nyingi zilizokwishafunguliwa dhidi ya Chadema na viongozi wake.

Wasifu wa Mabere Marando kila mtu anaujua kwani ni nguli aliyeongoza Mageuzi Tanzania tokea kabla ya mfumo wa vyama vingi. Kwa sasa ni mjumbe wa Kamati Kuu Chadema na ni mmoja wa wanasheria wake huku akiwa pia Makamu Mkiti wa Chadema Kanda ya Pwani.

Rais anatarajiwa kuteua majina mawili tu kutoka Chadema na kwa mujibu wa sheria ni sharti katika wateuliwa hao mmoja atoke Zanzibar na pia lazima mmoja awe mwanamke.

TAZAMA JINSI MWILI WA ALIYEKUWA WAZIRI WA FEDHA NA UCHUMI, DK. WILLIAM MGIMWA ULIVYOWASILI NCHINI UKITOKEA AFRIKA KUSINI



Mwili wa aliyekuwa Waziri wa Fedha, Dk.William Mgimwa umewasili nchini kwa ndege ya shirika la Kenya (KQ) na kupokelewa na viongozi mbalimbali wa chama na Serikali wakiongozwa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue pamoja na Mawaziri mbalimbali na Wabunge.

Ndege iliyobeba mwili wa marehemu William Mgimwa ikiwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar majira ya saa 7.45 mchana.

Gari maalum lililoandaliwa kwa ajili ya kubeba mwili wa marehemu.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JANUARI 04, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MOTO MKUBWA WAZUKA JANCO MOTEL JIJINI MBEYA JANA USIKU

Moto mkubwa umezuka katika hotel ya Janco forest mpya jijini Mbeya chanzo cha moto hakijajulikana mpaka tunaondoka katika tukio hilo

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Friday, January 03, 2014

"SARAFU YA TSH. 50,000 HAITATUMIKA KATIKA MANUNUZI" PROF. NDULU

Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT) imetoa sarafu maalumu ya kumbukumbu ya miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar yenye thamani ya sh 50,000.

Gavana wa BoT, Profesa Benno Ndulu, alisema jana kuwa sarafu hiyo iliyotengenezwa kwa madini ya fedha kwa asilimia 92.50, imetolewa kwa ajili ya kumbukumbu tu na haitaingizwa katika mzunguko wala kutumika kwa kulipia malipo ya aina yoyote.


Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

WACHINA WENGINE WAKAMATWA NA MENO YA TEMBO 81 BANDARINI DAR ES SALAAM

 
TAARIFA KWA UMMA

Mamlaka ya Bandari Tanzania kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii pamoja na vyombo vingine vya Dola, tarehe 2 Januari 2014 majira ya saa tatu asubuhi kwenye Bandari ya Dar es Salaam, imekamata meno 81 ya tembo yenye uzito wa kilo 303 sawa na tembo 41. Aidha, magamba 120 ya kakakuona na mazao ya bahari nayo yamekamtwa. 

Hii ni baada ya Askari wa Bandari kutilia shaka mizigo iliyokuwa kwenye gari ikiingizwa bandarini. Meno ya tembo yaliyokamatwa bado ni mapya ikiwa na maana tembo hao wameuawa katika kipindi kizichozidi mwezi mmoja uliopita.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

DK.SHEIN AFUNGUA MAONESHO YA MIAKA 50 YA MAPINDUZI

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein, akipata maelezo kutoka Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Hassan Khatib, (kulia) alipotembelea banda la Ofisi ya faragha Ikulu, wakati wa Maonesho ya Miaka 50 ya Mapinduzi Zanzibar, yaliyofanyika jana viwanja vya Beit el Ras, katika shamra shamra za sherehe za Mapinduzi
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

WARIOBA: SERIKALI TATU SI MZIGO

MWENYEKITI wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba nchini, Jaji Mstaafu Joseph Sinde Warioba, ametetea muundo wa serikali tatu kuwa hauna gharama, tofauti na inavyotafsiriwa na wengi. Mbali na kutetea gharama za uendeshaji wa serikali tatu, Jaji Warioba pia amewashukia wanaodhani mapendekezo ya muundo wa serikali tatu ni yake binafsi, kutokana na msimamo wa siku nyingi wa kiongozi huyo.
 
 Akizungumza na Jukwaa la Wahariri nchini (TEF), Jaji Warioba alisema muundo wa serikali tatu umepunguza gharama za uendeshaji. Kwa mujibu wa Jaji Warioba, chini ya muundo huo hata Bunge linatarajiwa kuwa na wabunge 75 tu, hatua ambayo itapunguza gharama. Mwenyekiti huyo alisema kuwa gharama za uendeshaji wa Serikali ya Muungano zitakuwa katika Wizara ya Ulinzi na Usalama pamoja na Mambo ya Nje huku katika maeneo yaliyobaki gharama zake zitakuwa zimepungua zaidi. 
“Hivi kwa nini hili la muundo wa muungano tunajadili gharama wakati kila mwaka tunapoongeza mikoa, wilaya, tarafa, majimbo na vijiji gharama zinaongezeka wala hakuna anayezungumzia wala kuhoji? Hivyo hivyo kwa kuwa na serikali tatu, hakuna gharama, tena kimsingi tumepunguza gharama za migogoro ya mara kwa mara ya kushughulikia kero za Muungano,” alisema Jaji Warioba.

MAGAZETI YA LEO IJUMAA JANUARI 03, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS



.
.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Thursday, January 02, 2014

MWANAJESHI AUA VIJANA WAWILI KWA BASTOLA

Mwanajeshi wa Jeshi la Wananchi Tanzania(JWTZ), ambaye jina lake limehifadhiwa anashikiliwa na Jeshi la Polisi baada ya kuwaua kwa kuwapiga risasi vijana wawili na kisha kuwajeruhi vibaya wengine wawili walipokuwa katika shamrashamra za kuukaribisha mwaka mpya. Tukio hilo lilitokea majira ya saa sita na robo usiku wa kuamkia jana, katika eneo la Pugu Kinyamwezi, Ilala jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Mwandishi wa habari jana Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Ilala, Marietha Minangi (pichani) alisema tukio hilo lilitokea baada kundi la vijana waliokuwa wakisherehekea mwaka mpya kuzingira gari la mwanajeshi huyo aliyekuwa akielekea nyumbani kwake Pugu Kinyamwezi, akitokea katikati ya Jiji kwa shughuli zake.
Alisema mwanajeshi huyo alikuwa na gari aina ya Toyota Rava 4 na baada ya kufika katika eneo hilo alizingirwa na kundi la vijana hao waliokuwa wakisherehekea mwaka mpya na ndipo aliamua kutoa bastola yake na kufyatua risasi ambapo iliwapata vijana hao na kufa papo hapo na kujeruhi wengine.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

RAY C AFUNGUKA KUHUSU JACK CLIF... ASEMA WACHA AFE TU TENA ANYONGWE KABISA...!!!


Kutokana na maswahibu makubwa yaliyompata Ray C juu ya madawa ya kulevya, ameshindwa kujizuia kutokusema ya moyoni mwake juu ya mwanadada Jack Cliff aliyekamatwa na madawa ya kulevya nchini China. Kafunguka maneno mengi sana na alionyesha ni jinsi gani alivyokuwa hamuonei huruma mwanadada Jack mpaka kuamua kutamka bora anyongwe tu. 

Soma alichokisema hapa
 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...