Thursday, December 19, 2013

MWEKEZAJI WA SHAMBA LA KAPUNGA AACHIWA HURU NA MAHAKAMA

rubani wa ndege Andreas Daffee. akipongezana na wakili wake Lweikaza
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mbeya, imewaachia huru watuhumiwa watatu ambao ni Mwekezaji wa Shamba la Kapunga(Kapunga Rice Project) lililopo Wilayani Mbarali Mkoani Mbeya ambao walikuwa wakituhumiwa  kwa mashtaka matatu ambayo ni kula njama,  kumwaga sumu na kuharibu mashamba ekari 557 ya Wananchi.
 
Akisoma hukumu Mhakamani hapo, Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Michael Mteite alisema upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha mashtaka yaliyokuwa yakiwakabili watuhumiwa ambao ni Waldeman Veemark ambaye ni meneja wa shamba, Sergei Beacker ambaye ni Afisa Ugani wa kampuni pamoja na rubani wa ndege Andreas Daffee.
 
Mteite alidai kuwa mbali na upande wa mashtaka kuwa na mashahidi 155,ambapo kati yao mashahidi zaidi ya 20 hawakuweza kufika mahakamani huku wengine 9 wakitoa ushahidi wa uongo tofauti na mashtaka yaliyopelekwa.

MAGAZETI YA LEO ALHAMIS DESEMBA 19, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.


.

TAZAMA PICHA YA NDEGE ILIYOTUA KWA DHARURA KATIKA UWANJA MDOGO WA NDEGE WA ARUSHA BADALA KIA



http://jambotz8.blogspot.com/


Wednesday, December 18, 2013

MAGAZETI YA LEO JUMATANO DESEMBA 18, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
 

..

RASIMU YA PILI YA KATIBA MPYA YAKAMILIKA...!!!


wariobaMwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya katiba, Jaji Warioba. Picha na Maktaba
*********
Dar es Salaam.Hatimaye Tume ya Mabadiliko ya Katiba chini ya Mwenyekiti wake, Jaji Joseph Warioba imekamilisha kazi ya kuboresha rasimu ya kwanza na kupata rasimu ya pili ya Katiba Mpya tayari kwa hatua nyingine.

Taarifa zilizotufikia jana zilieleza kuwa Makamishna na Wajumbe wa Sekretarieti wa tume hiyo, walianza kurejea ofisini juzi na jana, wakitokea Hoteli ya White Sands walikojichimbia tangu Desemba Mosi mwaka huu kukamilisha rasimu hiyo. Awali, Rais Jakaya Kikwete aliiongezea tume hiyo siku 14 zaidi kukamilisha kazi zake. Siku hizo zitakamilika siku 11 kuanzia leo.
Jaji Warioba, Makamu wake Jaji Augustino Ramadhan na Katibu wa Tume hiyo, Assaa Rashid hawakupatikana kutokana na kilichoelezwa kuwa walikuwa kwenye kikao. Gazeti hili lililazimika kumtafuta Naibu Katibu, Casmil Kyuki ambaye naye alithibitisha taarifa hizo.
“Ni kweli sisi (Wajumbe wa Sekretarieti) tumerejea ofsini jana na wenzetu (Makamishna) walirejea tangu juzi. Kazi zetu tumezikamilisha kilichobaki tunafanya mawasiliano na Mkuu (Rais Jakaya Kikwete), tujue lini tutawasilisha kazi hii,” alieleza Kyuki

Tuesday, December 17, 2013

HILI NI SOMO MAALUM KWA WANAWAKE WANAOTAKA KUOLEWA...!!!

 Hata kama utapingana na mimi, lakini ukweli utabaki pale pale; Kila jinsia inahitaji sana kuungana na jinsia nyingine katika tendo muhimu na la kihistoria katika maisha liitwalo ndoa! 
Yes, huu ni ukweli ambao upo wazi na utaendelea kusimama kama ulivyo.
Jinsia zote zina umuhimu na jambo hili muhimu, lakini kuna tofauti kidogo, kwamba mwanamke anasubiri kufuatwa na mwanaume, wakati mwanaume anaamua kumfuata mwanamke anayemtaka na kwa wakati wake. 

Kuna kitu nataka kuweka sawa hapa, kwamba wanaume ndiyo huwa wa kwanza kupenda kabla ya mwanamke, ingawa mwanamke anaweza kuwa wa kwanza kupenda lakini akashindwa kufikisha hisia zake kwa mwanaume husika.  

Je unataka rafiki au mchumba? click neno 2-Chat

Wanawake wa ‘mjini’ huwa hawakubaliani na hili, kutokana na huu utandawazi unaohubiriwa siku hizi ikiwa ni pamoja na kampeni za usawa zinazotetewa na Wanaharakati Wanawake. 


Akina dada nao huchangamkia kueleza hisia zao kwa wanaume. Nadhani si jambo baya, ingawa linaweza kupokelewa kwa hisia tofauti na kila mwanaume.

Tuyaache hayo, hoja kubwa ya msingi hapa ni jinsi gani mwanamke anaweza kuolewa haraka na mpenzi wake. Ikumbukwe kwamba, hapa nazungumza na wanawake ambao tayari wapo katika uhusiano, lakini wenzi wao hawana habari kabisa na mambo ya ndoa.

KIJUE KISIWA CHA ROBBEN JELA AMBAYO MZEE MADIBA ALIISHI KWA MIAKA 27 ILIYOBEBA HISTORIA MZITO DUNIANI


NCHINI Afrika Kusini, hakuna eneo la kivutio cha kitalii linalotembelewa na wageni wengi kama Kisiwa cha Robben. Umaarufu wa eneo hili umekuwa ukiongezeka mwaka mpaka mwaka.
Lakini hakuna shaka kwamba, kiini cha kutembelewa sana kwa kisiwa hiki ni kutoka na kuwa kituo maalumu cha kuwafunga wapigania uhuru wa Afrika Kusini wakati huo, akiwamo Nelson Mandela.

Mandela, Rais wa kwanza Mwafrika nchini Afrika Kusini, ndiye mhimili wa kivutio cha utalii kwenye jela ya wafungwa wa kisiasa iliyojengwa ndani ya kisiwa hicho.

Kati ya wafungwa wengi wa kisiasa waliowahi kufungwa kwenye jela ya Robben, alikuwamo Govan Mbeki, baba mzazi wa Rais wa zamani wa Afrika Kusini aliyempokea madaraka Mandela, Thabo Mbeki. Ni Mandela pekee ndiye aliyekaa hapo muda mrefu.

RAIS ZUMA AZINDUA SANAMU YA NELSON MANDELA

zumapix_09bf0.jpg
Pretoria, Afrika Kusini. Rais Jacob Zuma amezindua sanamu ya shaba ya shujaa wa Afrika, Nelson Mandela kwenye jengo la Muungano lililopo mji wa Pretoria.
Sanamu hiyo yenye urefu wa mita tisa humuonyesha Mandela akitabasamu, huku akiwa ameonyesha ishara ya kukumbatia.


Wakati akizindua sanamu hiyo jana, Rais Zuma alisema kwamba sanamu nyingi za Mandela zinamuonyesha akinyoosha mkono wake mmoja juu kama ishara ya mapambano iliyokuwa ikitumiwa na Chama cha ANC.
Lakini, ishara ya kukumbatia iliyokuwa ikitumika katika sanamu hii ni tofauti, kwasababu inamuonyesha Madiba akikumbatia nchi nzima na watu wake wote bila kujali rangi, itikadi wala tabaka. Zuma aliizindua sanamu hiyo muda mfupi baada ya kumalizika kwa mazishi ya kiongozi huyo yaliyoshuhudiwa na umati mkubwa watu mbalimbali, wakiwamo viongozi wa nchi tofauti yaliyofanyika katika Kijiji cha Qunu.

LIYUMBA ADAI KUBAMBIKIWA KESI YA KUKUTWA NA SIMU GEREZANI...!!!

Liyumbapix_0473a.jpg
Dar es Salaam. Mkurugenzi wa zamani wa Utawala na Utumishi (DPA), Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Amatus Liyumba anayekabiliwa na kesi ya kukutwa na simu gerezani, ameiomba mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imfutie shtaka hilo na kumuachia huru kwa madai kuwa kesi hiyo ilipangwa kwa ajili ya kumkomoa.
Liyumba aliyaeleza hayo jana wakati akijitete mbele ya Hakimu Mkazi, Augustina Mmbando anayetarajia kutoa hukumu ya kesi hiyo, Januari 15, mwaka na kuzitaka pande zote mbili kuwasilisha majumuisho yao ya mwisho kama mshtakiwa ana hatia ama la, Desemba 30, mwaka huu.
"Kesi hii imepangwa kwa ajili ya kunikomoa, wakati natumikia kifungo sijawahi kuvunja sheria, kupewa adhabu wala kuonywa kwa kosa lolote, simu yenye namba 0653004662 siijui nimeiona hapa na kama imesajiliwa ni lazima mhusika atajulikana." alieleza Liyumba.
Alidai kuwa, Julai 2011 alikuwa mfungwa akitumikia kifungo cha miaka miwili na unapofikishwa huko ni lazima upekuliwe mara tatu kwa kuvuliwa nguo zote.

MBOWE AMNANGA ZITTO KABWE WAZI WAZI, AAPA KUTOVUMILIA USALITI...!!!

  MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amemvaa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe na kusema kamwe chama hicho hakiwezi kuvumilia usaliti wa aina yoyote.  
Akizungumza mjini Mwanza  jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika Viwanja vya Malimbe, alisema kwa namna yoyote ile hawatamfumbia macho mtu yeyote anayekwenda kinyume cha katiba na taratibu za chama hicho.
  Alisema Chadema ambayo imejengwa kwa damu za Watanzania haiwezi kukubali kuona mtu yeyote anatoboa ‘boti’ yake iendayo kasi katikati ya bahari wakati huu wa kuelekea katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 na Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika mwakani.
Mbali na kumshukia Zitto pia amekirushia kombora Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kusema kinatumia mbinu chafu kutaka kuiua Chadema kabla ya mwaka 2015. Alisema kamwe mbinu hizo hazitafanikiwa maana Chadema ipo kwa mpango wa Mungu.

JAMAA AISHI KWENYE HANDAKI MIAKA MINNE...!!!


 
Stori: Makongoro Oging’
DUNIA haiishi vituko! Chacha Makenge (36) mzaliwa wa Kijiji cha Kisangula, Mtukula, Serengeti mkoani Mara anaishi jijini Dar lakini ndani ya handaki aliloligeuza chumba kwa miaka minne sasa, ni ajabu lakini ni kweli.
Akizungumza na mwandishi wetu hivi karibuni nje ya handaki hilo lililopo mita chache kutoka majengo ya biashara ya Mlimani City, Makenge alisema alichukua uamuzi huo baada ya rafiki yake (jina linahifadhiwa) kumchomea nyumba na kuteketeza samani zote.

“Ilikuwa mwaka 2009 mwanzoni rafiki yangu huyo ndiye alinipa sehemu ya kiwanja chake nijenge nyumba. Nikawa naishi hapo huku nikiendelea na shughuli zangu za kila siku.

“Siku moja akabadili mawazo, akanitaka nihame katika eneo lake bila kunipa sababu, nilimwomba anipe muda nitafute pa kwenda.

“Julai 2009 akaja na polisi, akanikamata na kunipeleka Kituo cha Polisi cha Stakishari, nilipowauliza kosa langu, hawakunieleza.
“Baada ya siku mbili majirani walikuja kuniona na kuniambia kwamba nyumba yangu imechomwa moto na kila kitu kilichokuwa ndani kimeteketea, aliyefanya hivyo ni rafiki yangu. Nilijisikia vibaya sana.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE DESEMBA 17, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

Monday, December 16, 2013

"KATIBA MPYA 2014 HAIWEZEKANI" LIPUMBA


Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahimu Lipumba (pichani) amesema mchakato wa Katiba Mpya una vikwazo vingi na kwamba Katiba haiwezi kupatikana mwaka 2014 kama Rais Kikwete alivyoahidi hivyo, kuna haja ya kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa Bara.
              Hii ni mara ya pili kwa Lipumba kutoa kauli hiyo. Mei mwaka huu, alitoa tamko kama hilo alipoonyesha wasiwasi wake kuhusu upatikanaji wa Katiba Mpya akadai ni janja ya CCM kumwongezea muda Rais.
Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Lipumba alisema kuwa amekuwa akiutafakari kwa kina mchakato wa Katiba Mpya kama unaweza kukamilika mwaka 2014, lakini jibu linalomjia, hakuna.
Alitaja baadhi ya vikwazo ambavyo vinaweza kukwamisha kupatikana kwa Katiba Mpya kuwa ni Daftari la Kudumu la Wapigakura kama halijaboreshwa na kasi ndogo ya utoaji wa vitambulisho vya utaifa ambavyo vitatumika kupigia kura hiyo.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU DESEMBA 16, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.

ANGALIA MATUKIO YALIYOJILI JANA WAKATI WA MAZISHI YA MZEE MANDELA, QUNU AFRIKA KUSINI




Goodbye to an icon: Nelson Mandela's coffin is slowly lowered into the ground in the hills close to where he grew up at the small, private burial today in Qunu as military salute and mourners watch the poignant moment

Poignant: Nelson Mandela's coffin was carried to his grave and then the flag of the country he loved so ardently was removed and handed to his widow Graca Machel

United in grief: Mandela's widow Graca Michel and his ex-wife Winnie Mandela tearfully comforted one another as they sat next to president Jacob Zuma and Mandela's grandson Mandla as he was laid to rest

Special tribute: The South African air force fly over Mandela's grave in the hills of Qunu where he grew up, which was accompanied by a 21-gun salute


Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...