Israel imekanusha madai hayo na Waziri
Mkuu wake Benjamin Netanyahu leo hii anatarajiwa kuendeleza kampeni
yake dhidi ya kufikia makubaliano ya nyuklia na Iran wakati
atakapokutana na Rais Vladimir Putin wa Urusi mjini Moscow.
Thursday, November 21, 2013
HOFU YATANDA KAMATI KUU YA CHADEMA, KIKAO CHAFANYIKA CHINI YA ULINZI MKALI WA BLUE GUARD
********
Hali ya wasiwasi iligubika eneo kinapofanyika kikao cha Kamati
Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kilichoanza Dar es
Salaam jana.
Ulinzi mkali wa walinzi wa Chadema (Blue Guard),
uliimarishwa katika ukumbi wa Ubungo Plaza kinapofanyika kikao hicho
ambacho kinatarajiwa kumalizika leo, huku kukiwa na maagizo
yaliyoashiria kuwapo kwa mambo mazito.
Maazimio ya kikao hicho yanasubiriwa kwa hamu na
wafuatiliaji wa mambo ya siasa nchini kwani kinafanyika katika kipindi
ambacho chama hicho kikuu cha upinzani nchini kinapita katika misukosuko
na hasa ya malumbano baina ya makamanda wake wa juu.
MAZUNGUMZO YA NYUKLIA YA IRAN YAANZA
Catherine Ashton Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja (kushoto) na Waziri wa mambo ya nje wa Iran Mohammad Javad Zarif wakiwa katika mkutano na waandishi wa habari mjini Geneva baada ya kushindwa kufikiwa kwa makubaliano. (10.11.2013).
Mazungumzo magumu yanaanza leo kati ya Iran na mataifa makubwa kutafuta makubaliano kwa mpango wa nyuklia wa Iran ambayo pia yatawaridhisha wanasiasa wa msimamo mkali huko Marekani, Israel na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Mazungumzo hayo yanafanyika Geneva wakati kukiwa na hali ya mvutano inayoongezeka Mashariki ya Kati ambapo waziri wa mambo ya nje wa Iran akiishutumu Israel kwa kujaribu kuvuruga mchakato huo kufuatia mirupuko miwili ya mabomu iliouwa takriban watu 23 nje ya ubalozi wa Iran mjini Beirut hapo jana.Wizara ya mambo ya nje ya Iran imeilaumu Israel na mamluki wake kwa kuhusika na miripuko hiyo.
WAZIRI NCHIMBI, MWAKYEMBE WAFANYA KIKAO NA WATENDAJI WAKUU WA WIZARA ZAO JIJINI DAR
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk
Emmanuel Nchimbi (kushoto-meza kuu) akizungumza na Watendaji Wakuu wa
wizara yake pamoja na wa Wizara ya Uchukuzi katika Kikao cha utendaji
kazi cha kuimarisha uhusiano kati ya wizara hizo kilichofanyika katika
Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi jijini Dar es
Salaam. Kulia (meza kuu) ni Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe.
Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison
Mwakyembe (kulia-meza kuu) akizungumza na Watendaji Wakuu wa wizara yake
pamoja na wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi katika Kikao cha utendaji
kazi cha kuimarisha uhusiano kati ya wizara hizo kilichofanyika katika
Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi jijini Dar es
Salaam. Kushoto (meza kuu) ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk
Emmanuel Nchimbi. Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya
Nchi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk
Emmanuel Nchimbi akizungumza na Watendaji Wakuu wa wizara yake pamoja na
wa Wizara ya Uchukuzi (hawapo pichani) katika Kikao cha utendaji kazi
cha kuimarisha uhusiano kati ya wizara hizo kilichofanyika katika Ukumbi
wa Mikutano wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi jijini Dar es Salaam.
Kulia ni Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe. Picha zote na Felix
Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
KITENGO CHA MAWASILIANO YA SERIKALI
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
Wednesday, November 20, 2013
EMMANUEL ADEBAYOR AONESHA UTAJIRI WAKE, JUMBA LA KIFAHARI, MAGARI NA NDEGE
Mchezaji wa Tottenham Hotspur Emmanuel Adebayor ni mmoja kati ya wachezaji matajiri sana Africa na anamiliki nyumba kwao Togo,Ghana,UK na Marekani.
Adebayor mwenye miaka 29 ametoa picha zake zikionyesha magari yake ya kifahari, private jet na vitu vingine vingine.
Enjoy picha 15 kutoka kwa Adebayor ambaye siku chache zilizopita alikuwa kwenye harusi ya Peter wa P Square pamoja na Diamond Platnums.
WATU ZAIDI YA 50 WAFUKIWA BAADA YA JENGO KUPOROMOKA AFRIKA KUSINI
Watu
wawili wamefariki na wengine takriban watu 50 kukwama kwenye vifusi
baada ya paa ya jumba la maduka lililokuwa linajengwa kuporomoka nchini
Afrika Kusini.
Inaarifiwa watu 29 wameweza kuokolewa.
Taarifa zinazohusianaAfrika Kusini
Madaktari kutoka kampuni ya kibinafsi ya Netcare 911 walifika kutoa huduma ya kwanza katika eneo hilo la Tongaat Kaskazini mwa mji wa Durban.
Madaktari kutoka kampuni ya kibinafsi ya Netcare 911 walifika kutoa huduma ya kwanza katika eneo hilo la Tongaat Kaskazini mwa mji wa Durban.
"Shughuli hii itachukua mda mrefu. Itatuchukua muda kuwafikia wale waliokwama," alisema msemaji wa kampuni hiyo.
Hata hivyo ni mapema mno kujua sababu ya kuporomoka kwa jengo hilo.
Inaarifiwa watu wengine 26 wamepelekwa hospitalini wakiwa na majereha mabaya.
CHANZO BBC SWAHILI
LIST YA WASANII WALIOLIPWA PESA NYINGI DUNIANI 2012 - 2013
List mpya kutoka Forbes inahusisha wasanii waliolipwa pesa nyingi
duniani kwa kipindi cha June 2012 hadi June 2013 ambapo pesa hizo
zinatokana na mauzo ya album, show(tour) na vitu vingine.
Wakongwe bado wapo kwenye list na Justin Bieber pamoja na umri wake mdogo lakini bado ameendelea kubaki kwenye top 10 ya list hii. List kamili hii hapa.....
1. Madonna – $125 million
2. Lady Gaga - $80 million
3. Bon Jovi – $79 million
4. Toby Keith – $65 million
5. Coldplay – $64 million.
6. Justin Bieber – $58 million
7. Taylor Swift – $55 million
8. Elton John – $54 million
9. Kenny Chesney – $53 million
9. Beyonce – $53 million (tie)
11. Sean “Diddy” Combs – $50 million
12. Sir Paul McCartney – $47 million
13. Calvin Harris – $46 million
14. Jennifer Lopez – $45 million
15. Roger Waters – $44 million
16. Muse – $43 million (tie)
16. Rihanna – $43 million (tie)
18. Jay Z – $42 million
18. One Direction – $42 million (tie)
20. Dr. Dre – $40 million
20. Red Hot Chili Peppers ($40 million, tie)
22. Rolling Stones – $39 million (tie)
22. Katy Perry – $39 million (tie)
24. Tim McGraw – $33 million (tie)
25. Pink – $32 million (tie)
25. Tiësto – $32 million (tie)
MSIMU WA SIKUKUU UMEWADIA TANGAZA BIASHARA YAKO NASI KWA BEI NAFUU
Kuza biashara yako msimu huu wa sikuu, kwa kutangaza na http://jambotz8.blogspot.com/
Piga simu no:- 0687 221198/ 0715 221198/ 0766 221198
Piga simu no:- 0687 221198/ 0715 221198/ 0766 221198
UFARANSA YAIPIGA UKRAINE 3-0 NA KUFUZU KOMBE LA DUNIA.
Ufaransa imefanikiwa kufuzu kucheza
Kombe la Dunia baada ya kuigeuzia kibao Ukraine na kuichapa mabao
3-0. Awali Ukraine ilishinda kwa mabao 2-0 ikiwa nyumbani na kuweka
matumaini ya juu kusonga mbele katika mechi hiyo ya marudiano
ugenini.
Lakini leo kwa mabao ya Mamadou Sakho aliyefunga mawili na
Karim Benzema, Ufaransa imetinga fainali ya Kombe la Dunia. Ilionekana
ni vigumu kwa Wafaransa kusonga mbele baada ya kufungwa mabao 2-0 katika
mechi ya kwanza
Tuesday, November 19, 2013
KIWANDA CHA KUTENGENEZA VIYWAJI VIKALI CHAFUNGWA SHINYANGA
Kiwanda cha kutengeneza vinywaji cha Trully African kilichopo Mtanda Manispaa ya Shinyanga kimefungwa na Halmashauri ya mji huo kwa kutokidhi
viwango vya ubora.... mengi kuhusu sakata hili endelea kusikiliza radio Faraja Fm na kutembelea mtanda huu wa jambotz8.blogspot.com.
Story na Steve Kanyeph na Isaac Edward Kisesa
Story na Steve Kanyeph na Isaac Edward Kisesa
MWANAFUNZI ANAYEDAI KUBAKWA NA KAPUYA HUYU HAPA AWEKEWA MTEGO NA KUBAINI MAMBO MAZITO
MNYONGE mnyongeni haki yake mpeni, skandali ya kumbaka na kumwambukiza
Ukimwi mwanafunzi, inamtafuna na kumuumiza Mbunge wa Urambo Magharibi
(CCM), Juma Athuman Kapuya.
Kuhusu ukweli wa skendo hiyo, vyombo vya sheria vitazungumza lakini
gazeti hili limejiridhisha pasipo shaka yoyote kuwa denti husika ni
tapeli na anacheza rafu ili kumharibia Kapuya kwa maslahi yake.
Mbunge wa Urambo Magharibi (CCM), Profesa Juma Athuman Kapuya.
Gazeti hili, liliamua kumchunguza denti husika ili kumjua kiundani
katika kutimiza ahadi ambayo Global Publishers Ltd, ilishaitoa kwenye
Gazeti la Risasi, nakala ya Jumamosi iliyopita kuwa waandishi wake
watafuatilia kinagaubaga na kuanika kila kitu kupitia magazeti yake,
utekelezaji unaendelea.JAMAA AUWA WAWILI NA KISHA KUJIUA YEYE MWENYEWE ILALA DAR LEO ASUBUHI
Inadaiwa kuna gari ilikua inatoka ndani ya geti kutoka ikiwa na dereva mwanaume, abiria mwanamke mbele, na abiria wengine wawili wakiwa seat ya nyuma.
Pembeni hapo kulikua na jamaa kasimama. Inadaiwa alishushwa hapo dakika chache toka katika tax, walipotokeza abiria hao kupitia gari yao alitoa silaha yake na kupiga risasi gari akilenga zaidi abiria wa mbele pande zote kisha na nyuma. Baada ya kumaliza hapo muuaji huyo naye alijipiga risasi na kufariki hapo hapo.
Dereva na abiria wake wa mbele wamefariki dunia, huku abiria wa nyuma mmoja mama mtu mzima kajeruhiwa na risasi mgongoni na dada mwingine kujeruhiwa kwa kupigwa risasi mguuni.
Source: global publishers & Jamii Forums
WACHUNGAJI WAMKALIA KOONI MZEE WA UPAKO KUHUSU RAMBI RAMBI YA MAREHEMU MOSES KULOLA
WACHUNGAJI wa makanisa mbalimbali nchini
wamemkalia kooni Mchungaji wa Kanisa la Maombezi, Antony Lusekelo
maarufu kama Mzee wa Upako, kwa kumtaka atoe rambirambi aliyoahidi mbele
ya umati wa watu siku ya kuaga mwili wa marehemu Askofu Moses Kulola
Temeke, jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa mtu wa kamati iliyoratibu mazishi ya kiongozi huyo wa kanisa, viongozi wote wa dini walioahidi kutoa rambirambi hizo wametoa isipokuwa Lusekelo aliyeahidi kwa mbwembwe kutoa shilingi milioni 15.
Katibu Mkuu wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania, Mchungaji David Mwasota alisema anamheshimu Lusekelo kwani ni mtumishi wa Mungu, lakini ni bora angetimiza ahadi yake kama walivyofanya wenzake.
“Mzee wa Upako ni mtu mwenye jina kubwa kwenye jamii na kwa Mungu, hivyo anapaswa kuangalia kwa undani kile anachoahidi kwa muda unaotakiwa na amuache mke wa marehemu apumzike kwa kuwa ametokwa na mpendwa wake na bado hana nguvu,” alisema na kuongeza;
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa mtu wa kamati iliyoratibu mazishi ya kiongozi huyo wa kanisa, viongozi wote wa dini walioahidi kutoa rambirambi hizo wametoa isipokuwa Lusekelo aliyeahidi kwa mbwembwe kutoa shilingi milioni 15.
Katibu Mkuu wa Makanisa ya Kipentekoste Tanzania, Mchungaji David Mwasota alisema anamheshimu Lusekelo kwani ni mtumishi wa Mungu, lakini ni bora angetimiza ahadi yake kama walivyofanya wenzake.
“Mzee wa Upako ni mtu mwenye jina kubwa kwenye jamii na kwa Mungu, hivyo anapaswa kuangalia kwa undani kile anachoahidi kwa muda unaotakiwa na amuache mke wa marehemu apumzike kwa kuwa ametokwa na mpendwa wake na bado hana nguvu,” alisema na kuongeza;
KAGAME, MUSEVENI NA KENYATTA WASHTAKIWA KORTI YA JUMUIYA
Serikali za Rwanda, Uganda, Kenya na
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki, zimefunguliwa kesi katika
Mahakama ya Afrika ya Mashariki, zikidaiwa kukiuka mkataba wa
kuanzishwa kwa jumuiya hiyo.
Hatua hiyo inatokana na Serikali hizo kufanya vikao vitatu mfululizo na kuzitenga nchi za Tanzania na Burundi.
Walalamikaji katika kesi hiyo, ni Ally
Msangi, David Makata na , John Adam, ambao ni Watanzania, wanaotetewa
na wakili Mwandamizi, Jimm Obedi wa jijini Dar es Salaam.
Pamoja na mambo mengine, walalamikaji
wamewaomba majaji katika mahakama hiyo, kutoa tamko la kusitisha
utekelezaji wa maazimio yote ya vikao vya wakuu wa nchi hizo tatu.
Pia wameomba majaji watoe tamko la kukomesha kurejewa kwa vikao kama hivyo kinyume cha mkataba wa jumuiya hiyo.
Kesi hiyo ya aina yake, ilifunguliwa
jana katika Mahakama ya Afrika ya Mashariki na kupokewa na Ofisa
Masijala i katika mahakama hiyo, Boniface Ogoti.
Kufunguliwa kwa kesi hiyo, kunakuja
siku kadhaa baada ya Rais Jakaya Kikwete kuzilalamikia nchi hizo, kuhusu
kuitenga Tanzania kwa kufanya mikutano mbalimbali ya maendeleo ya nchi
zao. Nchi nyingine iliyotengwa ni Burundi.
Kikao cha kwanza cha pamoja
kilifanyika Aprili mjini Arusha kabla viongozi hao kukutana Juni 25 na
26 jijini Entebbe nchini Uganda, walidai kuwa na nia moja ya kurahisha
mawasiliano katika nchi hizo.
Mkutano mwilingine ulifanyika mjini
Kigali Rwanda Oktoba 28 ukiwajumuisha Rais Yoweri Museven wa Uganda,
Uhuru Kenyatta (Kenya), Salva Kiir (Sudan Kusini) na Paul Kagame.
Wakili wa walalamikaji Obedi, alisema
katika kesi ya msingi, wanawashtaki Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya
Rwanda, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Uganda,Mwanasheria Mkuu wa
Serikali ya Kenya na Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo.
Monday, November 18, 2013
UFOO SARO: NI MIUJIZA YA MWENYEZI MUNGU TU NDIYO ILIYONIWEZESHA KUEPUKA KIFO.
Mwandishi wa habari wa Kituo cha Televisheni cha ITV, Ufoo Saro akisoma
somo kwenye biblia wakati wa ibada maalumu ya shukrani kwenye Kanisa la
(KKKT ) Usharika wa Kibamba nje kidogo ya Jiji la Dare Salaam jana.
Picha na Sanjito Msafiri.
******
DAR ES SALAAM.
MTANGAZAJI wa Kituo cha Televisheni cha ITV, Ufoo Saro ambaye alijeruhiwa kwa kupigwa risasi na mzazi mwenzake, Anthery Mushi, amefanya ibada na kusema: “Namshukuru Mungu kwa kumponya.”
******
DAR ES SALAAM.
MTANGAZAJI wa Kituo cha Televisheni cha ITV, Ufoo Saro ambaye alijeruhiwa kwa kupigwa risasi na mzazi mwenzake, Anthery Mushi, amefanya ibada na kusema: “Namshukuru Mungu kwa kumponya.”
Ni mara ya kwanza Saro kuzungumza tukio hilo tangu
aliporuhusiwa kutoka Taasisi ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu, MOI ya
Hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa amelazwa.
Katika ibada hiyo iliyofanyika katika Kanisa la
Kilutheli Tanzania (KKKT) Usharika wa Kibamba, Jimbo la Magharibi, Ufoo
huku akitokwa na machozi na wakati mwingine kushindwa kuzungumza
alisema: “Ni miujiza tu ya Mungu yeye kunifanya mimi kuwa hai leo.”
Mtangazaji huyo ambaye alilazwa kwa zaidi ya wiki
mbili, aliwashukuru watu wote waliomtia moyo, kumsaidia kipindi chote
alichokuwa mgonjwa.
'KACHAA' BALOTELLI AFURAHIA KUREJEA ENGLAND
Siku za furaha: Mario Balotelli akiwa mwenye furaha wakati wa mazoezi ya Italia Uwanja wa Craven Cottage jana
'KACHAA' Mario Balotelli alikuwa
mwenye furaha aliporejea England wakati mshambuliaji huyo wa AC Milan
alipokuwa akifanya mazoezi na kikosi cha Italia Magharibi mwa London.
Balotelli aliichezea Manchester City
kabla ya kutibuana na aliyekuwa kocha wa timu hiyo Roberto Mancini na
wachezaji wenzake kadhaa hivyo kuondoka, lakini nyota huyo mwenye umri
wa miaka 23, aliyeondoka Etihad miezi 10 iliyopita, alikuwa mtulivu
jana.
Kikosi cha The Azurri kinaendelea na
maandalizi ya Fainali za Kobe la Dunia mwakani nchini Brazil na leo
usiku kitacheza mechi ya kirafiki na Nigeria, kwenye Uwanja wa Fulham,
Craven Cottage.
Sunday, November 17, 2013
TAIFA STARS SASA KUIKABILI ZIMBABWE J4
Taifa
Stars sasa inacheza na Zimbabwe mechi ya Kalenda ya Shirikisho la
Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA)- FIFA Date itakayofanyika keshokutwa
Jumanne (Novemba 19 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Awali
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ilikuwa icheze
na Kenya (Harambee Stars), lakini Shirikisho la Mpira wa Miguu Kenya
(FKF) lilituma taarifa jana jioni (Novemba 16 mwaka huu) likieleza kuwa
timu yake haitacheza tena mechi hiyo.
Kikosi
cha Zimbabwe chenye msafara wa watu 30 kinatarajia kuwasili Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) kesho (saa 3 asubuhi) tayari
kwa mechi hiyo itakayochezwa kuanzia saa 11 kamili jioni.
NIGERIA YA KWANZA KUKATA TIKETI YA BRAZIL 2014 BAADA YA KUIFUMUA ETHIOPIA 2-0
Timu ya taifa ya Nigeria imekua nchi
ya kwanza ya Afrika kukata tiketi ya kecheza. Fainali za Kombe la Dunia
mwakani baada ya ushindi wa mabao 2-0 nyumbani dhidi ya Ethiopia
leo. Victor Moses alifunga kwa penalti dakika ya 20 na Victor Obinna
akaongeza la pili dakika ya 82 kwa mpira wa adhabu, hivyo Super Eagles
kufuzu kwa ushindi wa jumla wa 4-1, baada ya awali kushinda 2- mjini
Addis Ababa mwezi uliopita katika mchezo wa kwanza
IVORY COAST NAYO YAFUZU KOMBE LA DUNIA BAADA YA SARE YA1-1 NA SENEGAL
TIMU ya taifa ya Ivory Coast imefuzu
Fainali zijazo za Kombe la Dunia baada ya sare ya 1-1 usiku huu ugenini
na Senegal kwenye Uwanja wa Mohamed V in Casablanca, Morocco.
Matokeo hayo yanaifanya Didier Drogba
na wenzake wafuzu kwa ushindi wa jumla wa 4-2 na kuungana na Nigeria
iliyoitoa kwa jumla ya mabao 4-1 Ethiopia.
Ikiwa inajivunia ushindi wa 3-1 katika mchezo wa kwanza, Tembo walilazimika kusota kusawazisha bao baada ya Moussa Sow kutangulia kuwafungia Simba wa Teranga kwa penalti, kabla ya Salomon Kalou kusawazisha dakika za majeruhi.
Kikosi cha Senegal: Coundoul, S. Sane, L. Sane, Mane, Badji/Saivet dk82, P. Cisse, Mbodji, Gueye, Souare, Djilobodji na Ndoye/Sow 66.
Ivory Coast: Barry, K. Toure, Bamba, Gosso, Zokora, Romaric, Aurier, Y. Toure, Kalou, Gervinho/Sio dk80 na Drogba
Ikiwa inajivunia ushindi wa 3-1 katika mchezo wa kwanza, Tembo walilazimika kusota kusawazisha bao baada ya Moussa Sow kutangulia kuwafungia Simba wa Teranga kwa penalti, kabla ya Salomon Kalou kusawazisha dakika za majeruhi.
Kikosi cha Senegal: Coundoul, S. Sane, L. Sane, Mane, Badji/Saivet dk82, P. Cisse, Mbodji, Gueye, Souare, Djilobodji na Ndoye/Sow 66.
Ivory Coast: Barry, K. Toure, Bamba, Gosso, Zokora, Romaric, Aurier, Y. Toure, Kalou, Gervinho/Sio dk80 na Drogba
HASSAN DILUNGA ATUA YANGA
SAA
chache baada ya kufunguliwa kwa Dirisha Dogo la Usajili kwa msimu wa
2013/14, vinara wa Ligi Kuu ya Vodacom, Yanga jana walifanikiwa
kumsajili kwa mkataba wa miaka mitatu kiungo Hassan Dilunga kutoka Ruvu
Shooting ya Pwani.
Kwa
mujibu wa kanuni, klabu za Ligi Kuu na Daraja la Kwanza zenye fursa ya
kusajili wachezaji katika dirisha dogo ni zile ambazo hazijatumia nafasi
zote 30 za wachezaji, usajili uliofunguliwa jana Novemba 15 na
kutarajiwa kufungwa Desemba 15.
Mwenyekiti
wa Kamati ya Usajili wa klabu ya Yanga, Abdallah Bin Kleb, alisema jana
kwamba usajili wa kiungo huyo ni utekelezaji wa maagizo ya Kocha Mkuu,
Ernie Brandts, aliyoyaacha na benchi lake la ufundi kwa ajili ya
kuboresha kikosi.
"Kocha
aliacha mapendekezo ya usajili tuyafanyie kazi, la kwanza lilikuwa ni
kuhakikisha tunampata Kaseja ili kuongeza nguvu miongoni mwa makipa,
ambao tuliukamilisha mwishoni mwa wiki na sasa tumelimaliza la kiungo
Hassan Dilunga," alisema Bin Kleb na kuongeza.
Kikubwa
kuhakikisha kuwa, tunatekeleza maagizo yote yaliyo katika ripoti ya
benchi la ufundi na kuyafanyia kazi ili kujiweka katika mazingira mazuri
ya kuboresha kikosi chetu kwa ajili ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu na
michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Usajili wa Dilunga kiungo aliyeteuliwa
kikosi cha timu ya taifa, 'Taifa Stars', inayojiandaa kucheza mechi ya
kirafiki dhidi ya Harambee Stars, ametua Jangwani siku chache baada ya
mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu walipomsajili mlinda mlango wa zamani
wa Simba na Stars, Juma Kaseja, aliyekuwa hana timu tangu kumaliza
mkataba wake na Wekundu wa Msimbazi.
MAREKANI YAIWEKA PABAYA TANZANIA, YAIITA KITOVU CHA ‘BIASHARA’ YA BINADAMU
Marekani imetoa ripoti inayozungumzia usafirishaji wa binadamu ya mwaka 2013, huku ikiitaja Tanzania kuwa kinara wa kunyanyasa wasichana, kuwatumikisha katika ngono na usafirishaji wa binadamu.
Ripoti hiyo iliyotolewa na idara ya nchi hiyo inayohusika na diplomasia (US Department of State, Diplomacy in Action), pia inaitaja Tanzania kuwa ni kitovu cha njia ya kusafirisha wanawake, watoto na wanaume ambao hutumikishwa kwenye kazi za mashambani na biashara ya ngono.
Ripoti
hiyo iliyozinduliwa Julai mwaka huu na Waziri wa Mambo ya Nje wa
Marekani, Seneta John Kerry inaweka bayana kwamba biashara ya
usafirishaji wa binadamu hufanywa na baadhi ya ndugu na marafiki ambao
hutoa ahadi kwa wahusika kwamba wanakwenda kuwasomesha au kuwatafutia
ajira nzuri mijini.
"Unyonyaji
wa wasichana wadogo na utumikishaji majumbani ndilo tatizo
linaloongoza, ingawa kesi za watoto kusafirishwa kwa ajili ya biashara
ya ngono katika mpaka wa Tanzania na Kenya zinaongezeka. Pia, wasichana
wananyonywa kwenye maeneo ya utalii," inasema sehemu ya ripoti hiyo.
Saturday, November 16, 2013
KILI STARS YAPANGWA NA ZAMBIA, BURUNDI CHALLENGE 2013
Kikosi cha Taifa Stars amacho kinaundwa na wachezaji wengi wa Bara
Na Prince Akbar, Dar es SalaamTANZANIA Bara maarufu kama Kilimanjaro Stars imepangwa katika Kundi B kwenye michuano ya CECAFA Challenge pamoja na Zambia, Burundi na Somalia.
Katika michuano hiyo inayotarajiwa kuanza Novemba 27 mjini Nairobi, Kenya, wenyeji Harambee Stars wamepangwa na Ethiopia, Zanzibar na Sudan Kusini katika Kundi A.
Mabingwa watetezi, Uganda wamepangwa Kundi C pamoja na Rwanda, Sudan na Eritrea. Ratiba ya michuano hiyo inatarajiwa kutolewa wiki ijayo.
MAKUNDI CHALLENGE 2013:
KUNDI A- Kenya, Ethiopia, Zanzibar, South Sudan
KUNDI B- Tanzania, Zambia, Burundi and Somalia
KUNDI C- Uganda, Rwanda, Sudan and Eritrea.
MGAO WA UMEME KUANZA LEO NCHI NZIMA
Meneja Uhusiano wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Badra Masoud akieleza kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu kuwepo kwa upungufu wa umeme kwenye gridi ya Taifa kuanzia tarehe 16 hadi 26 November, 2013 kutokana na upungufu wa gesi kutoka katika Kisiwa cha Songosongo kilichopo Wilaya ya Kilwa, Mkoa wa Lindi Unaosababishwa na Matengenezo ya Kiufundi kwenye visima vya gesi unaofanywa na Kampuni ya Pan Afrika ili kuboresha upatikanaji wa gesi ya kutosha kwenye visima hivyo.
SHIRIKA LA UMEME TANZANIA
MPR/PR/12
Shirika la Umeme Tanzania(TANESCO)
linasikitika kuwajulisha wateja wake wote kwamba kutawepo na upungufu wa
umeme kwenye gridi ya Taifa kuanzia tarehe 16 hadi 26 November, 2013
kutokana na upungufu wa gesi kutoka katika Kisiwa cha Songosongo
kilichopo Wilaya ya Kilwa, Mkoa wa Lindi Unaosababishwa na Matengenezo
ya Kiufundi kwenye visima vya gesi unaofanywa na Kampuni ya Pan Afrika.
Lengo la matengenezo hayo ni kuboresha upatikanaji wa gesi ya kutosha kwenye visima hivyo.
Kutokana na Matengozo hayo Mikoa
iliyounganishwa katika gridi ya Taifaa itaathirika kwa kukosa umeme kwa
baadhi ya maeneo kwa nyakati tofauti.
Uongozi unaomba radhi kwa usumbufu utakaojitokeza kwa baadhi ya maeneo yatakayokuwa yakikosa umeme.
Imetolewa na: BADRA MASOUD
MENEJA UHUSIANO
RATIBA YA SHUGHULI YA KUAGA MWILI WA DKT. SENGONDO MVUNGI LEO - JUMAMOSI NOVEMBA 16 2013
Saa 12:50 jioni
Kuwasili kwa mwili wa Marehemu – Uwanja wa Ndege wa Mwalimu JKN
KESHO, NOVEMBA 16, 2013 – VIWANJA VYA KARIMJEE
Saa 2:00 – 3:30 asubuhi
Kuwasili kwa Wageni, Wananchi na Waombolezaji
Saa 3:30 asubuhi
Kuwasili Mwili wa Marehemu
Saa 4:00 – 5:45 asubuhi
Ibada ya Misa Takatifu, Viwanja vya Karimjee
Saa 5:45 – 6:55 mchana
Salaam za Rambirambi na Neno la Shukurani
Saa 6:55 – 8:40 Mchana
Kuaga Mwili wa Marehemu
Saa 9:00 Alasiri
Msafara kupeleka mwili wa marehemu Kibamba Msakuzi
KESHO KUTWA, NOVEMBA 17, 2013 – NYUMBANI KWA MAREHEMU - KIBAMBA, MSAKUZI
Saa 2:30 – 4:30 asubuhi
Ibada ya Misa nyumbani kwa marehemu
Saa 5:00 asubuhi
Kuanza safari ya kwenda Chanjale, Kisangara Juu, Mwanga, Kilimanjaro
TATOO NA MUONEKANO MPYA WA RAY..... VYAWACHEFUA WASHABIKI WAKE
Huu ni muonekano mpya wa Vicent Kigosi ambao ni moja ya maandalizi ya movie yake mpya ...
Ni muonekano ambao kwa kiasi flani umewachefua mashabiki wake ambao dakika chache baada ya picha hizo kuwekwa walijimwaga kwa comment ambazo hazikumuunga mkono kwa asilimia zote.
Ni muonekano ambao kwa kiasi flani umewachefua mashabiki wake ambao dakika chache baada ya picha hizo kuwekwa walijimwaga kwa comment ambazo hazikumuunga mkono kwa asilimia zote.
“Je nageukia bongoflava au kuna nini kinakuja?”. Aliadika Ray kwenye moja ya picha zake.
Subscribe to:
Posts (Atom)