Monday, November 18, 2013

'KACHAA' BALOTELLI AFURAHIA KUREJEA ENGLAND

balotel_94581.jpg
Siku za furaha: Mario Balotelli akiwa mwenye furaha wakati wa mazoezi ya Italia Uwanja wa Craven Cottage jana
'KACHAA' Mario Balotelli alikuwa mwenye furaha aliporejea England wakati mshambuliaji huyo wa AC Milan alipokuwa akifanya mazoezi na kikosi cha Italia Magharibi mwa London.
Balotelli aliichezea Manchester City kabla ya kutibuana na aliyekuwa kocha wa timu hiyo Roberto Mancini na wachezaji wenzake kadhaa hivyo kuondoka, lakini nyota huyo mwenye umri wa miaka 23, aliyeondoka Etihad miezi 10 iliyopita, alikuwa mtulivu jana.
Kikosi cha The Azurri kinaendelea na maandalizi ya Fainali za Kobe la Dunia mwakani nchini Brazil na leo usiku kitacheza mechi ya kirafiki na Nigeria, kwenye Uwanja wa Fulham, Craven Cottage.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...