Wednesday, November 13, 2013

KAMPENI YA NANI MTANI JEMBE SASA YAHAMIA KANDA YA KASKAZINI. WATALII WAKATA MAUNO BALAA....!!!



Wakazi wa eneo la Maji ya Chai, Arusha wakiangalia burudani iliyokuwa inatolewa na timu ya kampeni ya ‘Nani Mtani Jembe’ inayohusisha mashabiki Simba na Yanga,  ili kuzipigia kura timu zao na kushinda kitita kingi kati ya Tsh.100 milioni zilizotelewa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager ambao ndio wadhamini wa timu hizo na timu ya Taifa. 
Timu hiyo ipo kanda ya Kaskazini na Mashariki inayojumuisha mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Singida na Tanga.






Watalii kutoka nchi mbalimbali wakicheza pamoja na washereheshaji wa kampeni ya ‘Nani Mtani Jembe’ inayohusisha mashabiki Simba na Yanga,  ili kuzipigia kura timu zao na kushinda kitita kingi kati ya Tsh.100 milioni zilizotelewa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager ambao ndio wadhamini wa timu hizo na timu ya Taifa. 
Timu hiyo ipo kanda ya Kaskazini na Mashariki inayojumuisha mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Singida na Tanga. Watalii hao walikuwa wakitembelea maeneo mbalimbali mkoani Arusha

Tuesday, November 12, 2013

BODI YA LIGI YAFUNGIA VIWANJA SABA


Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPL Board) imefungia viwanja saba vilivyokuwa vikitumiwa na timu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) na Ligi Daraja la Kwanza (FDL) hadi vitakapofanyiwa marekebisho ili kukidhi mahitaji ya mechi za mpira wa miguu.

Uamuzi huo umefikiwa na TPL Board katika kikao chake cha kwanza kilichofanyika juzi (Novemba 10 mwaka huu) jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine kilipitia ripoti za mechi za VPL na FDL katika mzunguko wa kwanza.

Viwanja vilivyofungiwa na marekebisho yanayotakiwa kufanyika kwanza ili viruhusiwe kutumika tena ni Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba (majukwaa yake yamechakaa, hivyo kuhatarisha usalama wa watazamaji), na Uwanja wa CCM Mkwakwani jijini Tanga (vyumba vya wachezaji kubadilishia nguo (dressing rooms) havina hadhi).
Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya (sehemu ya kuchezea- pitch ni mbovu), Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha (pitch ni mbovu), Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi (vyumba vya kubadilishia kutumika kwa ajili ya shule ya awali), Uwanja wa Majimaji mjini Songea (pitch ni mbovu) na Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro (pitch ni mbovu). 

BREAKING NEWZZZZZZ...!!! DR. SENGONDO MVUNGI AMEFARIKI DUNIA AFRIKA KUSINI

Sengondo Mvungi 1 
Ni jana tu ambapo Waziri wa mambo ya ndani Dr. Emmanuel Nchimbi alitangaza kushikiliwa kwa watu tisa wanaotuhumiwa kuhusika na ujambazi uliofanywa dhidi ya Dr. Sengondo Mvungi aliekua mjumbe wa Tume ya Marekebisho ya Katiba Mpya na kiongozi wa NCCR-Mageuzi.
Taarifa iliyotumwa inasema Dr Mvungi amefariki dunia akiwa mahututi hospitalini nchini Afrika Kusini muda mfupi uliopita na taarifa kutumwa nyumbani Tanzania ambapo wafanyakazi wenzake ofisi ya tume ya mabadiliko ya katiba wameambiwa wakae karibu na simu zao ili kikitokea chochote kingine wafahamishwe.
Tayari viongozi mbalimbali kama Mh. Warioba, Katibu wa tume, naibu na watumishi wengine wachache wamekwenda nyumbani kwa marehemu.
kifo cha Sengondo Mvungi Nov 12 2013 2

Pichani ni Wafanyakazi wenzake baada ya kupata taarifa za msiba ofisini.



kifo cha Sengondo Mvungi Nov 12 2013

Chanzo: millardayo.com

MSIMU WA SIKUKUU UMEWADIA TANGAZA BIASHARA YAKO NASI KWA BEI NAFUU



MAGAZETI YA LEO JUMANNE NOVEMBA 12, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.
.

ZAIDI YA WATU 10,000 WAHOFIWA KUFARIKI UFILIPINO


017217323_35400_2f32e.jpg
Wanajeshi na polisi wa Ufilipino wamepelekwa katika miji ilioathirika na kimbunga kikali kuwahi kuipiga nchi hiyo ili kudhibiti wizi wa mali unaohatarisha juhudi za kutoa misaada ya kibinaadamu kwa waathirika.
Zaidi ya watu 10,000 wanahofiwa kufariki kutokana na kimbunga hicho kwa jina Haiyan kilichopiga kwa mawimbi mazito na upepo mkali na kusababisha athari kubwa nchini Ufilipino siku ya Ijumaa, huku mji wa Tacloban ukiwa moja ya miji ilioathirika pakubwa.
Waokoaji kwa sasa wanajaribu kupeleka misaada ya chakula na malazi kwa waathirika wa kimbunga hicho katika mji huo ulio na idadi ya watu 220,000.
Hata hivyo hatua hiyo iliendeshwa kwa changamoto kubwa kutokana na wizi uliokuwa ukiendelea. Waporaji walivunja maduka pamoja na kuvamia gari la misaada la msalaba mwekundu na kuchukua vile vilivyokuwemo ndani.
Baadhi ya waathiriwa ambao ni wafanyabiashara wadogo pia wameripoti kuibiwa kwa televisheni, na mashini za kufulia nguo. 
Kulingana na msemaji wa wizara ya ulinzi wa raia nchini humo, Reynaldo Balido, kurejesha usalama na hai ya utulivu katika mji huo wa Tacloban, ni moja ya mambo wanayoyapa kipaumbele.

KIONGOZI WA MSAFARA WA RAIS AKUTWA NA ZAIDI YA KILO 297 ZA DAWA ZA KULEVYA

558644_610253689038629_153892185_n_a1d1b.jpg
KASHFA NZITO LIBERIA: Msafara wa Rais Ellen Johnson Sirleaf wakutwa na zaidi ya kilo 297 za bangi. Watu 4 akiwemo kiongozi wa msafara washikiliwa kwa mahojiano.
== Liberia's Drug Enforcement Agency has arrested the head of the presidential motorcade for allegedly using an official vehicle to smuggle 297 kilograms (654 pounds) of marijuana into Liberia from neighboring Sierra Leone, officials said Monday.
The motorcade commander, Perry Dolo, was arrested over the weekend along with three other men after crossing from Sierra Leone via the town of Bo Waterside, said DEA Director Anthony Souh. The other three men were a Liberian official, a Guinean and a Sierra Leonean believed to be a member of the armed forces, Souh said. He did not provide further details about the men.
The vehicle used in the operation is known as "Escort 1," the jeep that normally leads the president's convoy, Souh said.
"He took the car during his day off to go do this thing. He was not on duty, but he used the official car," Souh said of Dolo.
Journalists were denied access to the suspects because they were still being interrogated at the DEA after their arrest by a joint force that included members of the Emergency Response Unit.
"They are still with me going through the process," Souh said. "We want to speedily send them to court as soon as possible because the case is too high. Using a presidential car? It's too big."
Liberia's DEA has in recent years tried to combat marijuana farming in Liberia's interior counties, which is primarily done for local sale and consumption. However, weak drug laws have made the practice difficult to curtail.
According to the 2012 World Drug Report from the United Nations Office on Drugs and Crime, 9 percent of Liberian high school students use cannabis.
———
abc News

Monday, November 11, 2013

MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOVEMBER 11, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARDNEWS

.
.

,
,

VAN PERSIE AIZAMISHA ARSENAL, MAN UNITED WAFUFUA MATUMAINI YA UBINGWA

article-2497133-1954DA9800000578-907_634x446_f36bf.jpg
MHOLANZI Robin van Persie amezamisha klabu yake ya zamani, Arsenal akiifungia bao pekee la ushindi Manchester United na kuirejeshea matumaini ya kutetea ubingwa wa Ligi Kuu England.
Van Persie alifunga bao tamu kwa kichwa akiunganisha kona iliyochongwa kitaalamu na Wayne Rooney dakika ya 27 Uwanja wa Old Trafford.
Kikosi cha United kilikuwa; De Gea, Smalling, Vidic/Cleverley dk45, Evans, Evra, Valencia, Jones, Carrick, Kagawa/Giggs dk78, Rooney na Van Persie/Fellaini dk85.
Arsenal; Szczesny, Sagna, Koscielny, Vermaelen, Gibbs, Arteta/Gnabry dk82, Flamini/Wilshere dk61, Ramsey, Ozil, Cazorla/Bendtner dk78 na Giroud.

TAARIFA RASMI YA ZITTO KABWE KUHUSU KINACHOITWA “TAARIFA YA SIRI YA CHADEMA”

Zitto-Kabwe_c2a4f.jpg
Tamko rasmi la Ndugu Zitto Z. KABWE (MB) kuhusiana na kinachoitwa "Taarifa ya Siri ya CHADEMA"
Ndugu Wanahabari,
NILIPOKUWA katika ziara ya bara la Ulaya kati ya Oktoba 21 mpaka Novemba 2 mwaka huu (2013), nilipokea kwa njia ya barua pepe ripoti inayoitwa "Taarifa ya Siri ya Chadema" ambayo pia ilikuwa imesambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii.
"Taarifa ya Chadema inasema kwamba chama hicho (chama changu) kilikuwa kimechunguza mwenendo wangu tangu
mwaka 2008 hadi 2010 na kubaini kuwa mimi napokea fedha kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kuivuruga Chadema.
Ripoti hiyo ilinihusisha pia na mwananchi raia wa Ujerumani, Andrea Cordes ambaye, kwa mujibu wa ripoti hiyo, alinisaidia kupokea na kuhifadhi kiasi cha dola 250,000 za Marekani kupitia kwenye akaunti yake binafsi.
Taarifa hii ya kutunga na iliyojaa uongo wa kiwango cha kutisha, imenifadhaisha, kunisikitisha na kunikasirisha.

KENYA YAIUNGA MKONO TZ A.MASHARIKI

131110120158_amina_mohamed_304x171_bbc_nocredit_860b3.jpg
Amina Mohamed,waziri wa mambo ya nje wa Kenya
Kenya imekuwa nchi ya kwanza kutoka Jumuia ya Afrika Mashariki kuipongeza Tanzania kwa hatua yake ya kutangaza bayana kwamba haiko tayari kutoka katika jumuiya hiyo kama ilivyodhaniwa.
Wasiwasi kuwa Tanzania ingejitoa kutoka jumuia ya Afrika Mashariki ulitokana na hali iliyojitokeza kwa baadhi ya nchi za jumuia hiyo kuendesha mikutano yao bila kuishirikisha Tanzania na Burundi.
Baadhi ya wanasiasa na wananchi nchini Tanzania walitaka nchi yao iachane na jumuia hiyo wakizishutumu Kenya, Rwanda na Uganda kuitenga Tanzania hata katika mikutano ya masuala yaliyohitaji maamuzi ya jumuia.
Kufuatia mfarakano huo, ulionekana kutishia uhai wa Jumuia ya Afrika Mashariki, Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania, wiki hii alilihutubia bunge la Muungano wa Tanzania mjini Dodoma, katikati ya nchi na kutangaza bayana kuwa Tanzania haitatoka katika jumuiya ya Afrika Mashariki, kwani imefanya kazi kubwa kuifufua na kuiunda upya baada ya kusambaratika mwaka 1977.

Sunday, November 10, 2013

TUCTA YATAKA SH. 750, 000 KIMA CHA CHINI

kazi 857ac
Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta) Mkoani Mbeya, limetangaza kiwango kipya cha mishahara inayotakiwa kuwa kima cha chini ni Sh 750,000.
Mwenyekiti wa Tucta mkoani hapa, Alinanuswe Mwakapala alisema kwa maisha ya sasa kima cha chini lazima kiwe Sh750,000 na kwamba, pendekezo hilo la mkoa litawasilishwa kwenye ngazi za juu za Tucta ili kulibariki.
Mwakapala alisema hayo kwenye hafla ya Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kukabidhiwa jengo la ghorofa tano lililojengwa na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT).
"Wafanyakazi nchini sasa wamechoshwa na mishahara midogo, hivyo wakati umefika kwa wafanyakazi kutoogopa maandamano na migomo kudai haki," alisema huku akishangiliwa.
Hata hivyo, Rais wa CWT, Gratius Mukoba alisema madai ya wafanyakazi yaliyowasilishwa Serikalini ni kutaka nyongeza ya mishahara kwa asilimia 100.
Mkoba alisema CWT hivi sasa wanasubiru ndani ya miezi mwili hadi Desemba kupata majibu.
hayatapatikana basi Serikali ijue imejipalia mkaa.
''Hatuwezi kuendelea kuwaona watu wasiofanyakazi wanapata mishahara mikubwa wakati wafanyakazi wanasota. Mwisho wa matatizo hayo ni sasa'' alisema huku akiwataka wafanyakazi hususan walimu kuachana na njama za kutaka kuwatenganisha.
Alisema Serikali inatakiwa kuwalipa walimu Sh49 bilioni wanazodai zikiwamo Sh30 bilioni walizopunjwa katika mishahara na kwamba pia lazima ipunguze kodi kwa wafanyakazi na kuboresha mazingira ya kazi.
CHANZO MWANANCHI

NHIF YAWARUKA WANAOTUMIA DAWA ZA KUONGEZA MAUMBILE


article-2265277-17117548000005DC-778 306x423 a9381
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), umesema hautahusika na malipo ya matibabu kwa wanachama wao watakaoathirika na utumiaji wa dawa za kuongeza maumbile.


Akizungumza kwenye kongamano la wadau wa mfuko huo mkoani hapa hivi karibuni, Kaimu Mkurugenzi Tiba na Ushauri wa NHIF, Dk Mkwabi Fikirini alisema mfuko hautatoa huduma kwa mwanachama aliyeathirika na dawa za kuongeza maumbile ambazo zimepigwa marufuku na Serikali.
Dk Fikirini alisema mfuko huo unatoa huduma ya matibabu kwa wanachama wake, ila hauhusiki na waathirika wa dawa zilizopigwa marufuku na Serikali ikiwamo za kuongeza maumbile maarufu kama dawa za Kichina.

BUNGE LAITOSA TUME YA WARIOBA

jkbungeni_na_msimamo_13eee_a4a9e.jpg
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba wa mwaka 2013, huku kukiwa na ushindani wa maeneo mawili ambayo baadhi ya wabunge walionyesha hofu.
Muswada huo ulipelekwa bungeni kwa hati ya dharura kutokana na makubaliano yaliyofikiwa katika mazungumzo yaliyofanyika Oktoba 15, mwaka huu, baina ya Rais Jakaya Kikwete na viongozi wa vyama vya siasa vyenye uwakilishi bungeni, baada ya muswada wa awali kususwa na vyama vya upinzani bungeni.
Katika mjadala ulioanza juzi na kuhitimishwa jana, wabunge wengi kutoka pande zote; CCM na upinzani waliyaunga mkono mapendekezo ya Serikali, lakini kulikuwa na hofu kuhusu idadi ya wajumbe watakaoteuliwa na Rais kuingia kwenye Bunge Maalumu na suala la ukomo wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.


Marekebisho hayo yameiweka kando Tume ya Mabadiliko ya Katiba, ambayo haitakuwapo baada ya kukabidhi rasimu ya pili ya Katiba hiyo kwa Rais Jakaya Kikwete, Desemba 15, mwaka huu.
Uhai wa tume hiyo ni miongoni mwa mambo yaliyozua ubishi baina ya wabunge wa Kambi ya Upinzani waliokuwa wakitaka iendelee kuwapo na wale wa chama tawala na Serikali, ambao walitaka iondoke kwa maelezo kwamba haitakuwa na kazi baada ya kukabidhi rasimu kwa rais kama inavyoeleza sheria ya kuanzishwa kwake.

MLINZI WA KAGAME AFANYIWA UMAFIA

ALIYEKUWA Mlinzi mkuu (bodyguard) wa Rais wa Rwanda, Paul Kagame, Luteni Joel Mutabazi, ametekwa na kikosi cha Jeshi la Uganda na kukabidhiwa kwa Serikali ya Rwanda.

Taarifa za kiintelijensia zinasema kuwa Luteni Mutabazi, alikuwa akiishi nchini Uganda kwa hati maalumu ya ukimbizi ya Umoja wa Mataifa, baada ya kutoroka nchini Rwanda pamoja na aliyekuwa Mkuu wa Majeshi ya nchi hiyo, Faustin Kayumba Nyamwasa.

Luteni Mutabazi alitorokea nchini Uganda Oktoba 2011, baada ya kutoroka jela yenye ulinzi mkali wa kijeshi ya Kami nje kidogo mwa mji wa Kigali akituhumiwa kwa kuhusishwa na kutoroka kwa mkuu huyo wa majeshi na kukimbilia Afrika Kusini. Alikuwa mlinzi mkuu wa Rais Kagame mpaka mwaka 2010, alipotoroka na kukimbilia Uganda.

Mlinzi huyo pia anashutumiwa na Serikali ya Rwanda kwa kutoa siri kwa Kikosi Maalumu cha Umoja wa Mataifa chini ya Majeshi ya Umoja ya Kulinda Amani nchini Kongo, (MONUSCO) na kuwezesha kuchakazwa na kushindwa kwa kikosi cha waasi wa M23.

Kutokana na tukio hilo, hivi sasa Serikali ya Rais Yoweri Museveni, imelazimika kumsimamisha kazi Mkuu wa Intelijensia wa Jeshi la Polisi, Joel Aguma, ambaye alihusika kumteka na kumkabidhi Luteni Mutabazi kwa Serikali ya Rwanda.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI NOVEMBA 10, 2013

.
.

.
.

TANZANITE YAUA 5-1, KUTUA DAR MCHANA

tanzanite_189c1.jpg
Timu ya Taifa ya wanawake chini ya miaka 20 (Tanzanite) imefuzu kucheza raundi ya pili ya michuano ya Kombe la Dunia kwa ushindi wa jumla ya mabao 15-1 baada ya leo (Novemba 9 mwaka huu) kuibugiza Msumbiji mabao 5-1.
Mabao ya Tanzanite katika mechi hiyo iliyochezwa Uwanja wa Taifa wa Zimpeto jijini Maputo yalipatikana kupitia kwa Sherida Boniface alipiga matatu (hat trick) wakati mengine yalifungwa na Vumilia Maarifa na Donesia Minja.
Msafara wa Tanzanite ulioongozwa na mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Kidao Wilfred utawasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) leo Jumapili (Novemba 10 mwaka huu) saa 8.30 mchana kwa ndege ya LAM.
Tanzanite inayofundishwa na Rogasian Kaijage itacheza mechi ya raundi ya pili dhidi ya Afrika Kusini. Mechi ya kwanza itachezwa jijini Dar es Salaam kati ya Desemba 6 na 8 mwaka huu wakati ile ya marudiano itafanyika Afrika Kusini kati ya Desemba 20-22 mwaka huu.
Boniface Wambura Mgoyo
Kaimu Katibu Mkuu
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

UTAFITI VYUO VIKUU WAUZWA MITAANI

jengo_9a969.jpg
Wakati Serikali ikiwa katika hatua za utekelezaji wa Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) kwenye elimu, imebainika kuwa baadhi ya wanafunzi wa vyuo vikuu wanaohitimu, wanafanya udanganyifu kwenye utafiti kwa kufanyiwa na watu wengine au kununua uliokwisha andikwa.
Kila mwanafunzi anayesomea shahada ya kwanza, uzamili au uzamivu hutakiwa kufanya utafiti ikiwa ni sehemu ya vigezo vya kukamilisha masomo yake.
Hata hivyo, Mwananchi imebaini kuwapo kwa wanafunzi wengi wanaotumia mbinu mbalimbali za kuandika utafiti huo bila kwenda maeneo husika.
Uchunguzi wetu uliofanyika kwa muda mrefu kwenye vyuo mbalimbali jijini Dar es Salaam, umebaini kuwa baadhi ya wanafunzi huchukua tafiti za zamani na kuzinakili upya, huku wengine wakichukua kutoka kwenye mitandao na kuzifanyia marekebisho kidogo ili zifanane na eneo analotaka kufanyia utafiti huo.
Mtafiti Mwandamizi ESRF
Mtafiti Mwandamizi, Taasisi ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF), Dk Donatila Kaino anasema ni asilimia 20 tu ya wanafunzi wanaomaliza vyuo vikuu nchini, ndiyo wanaoweza kuandika utafiti kwa ufasaha.

Saturday, November 09, 2013

MWISHO WA UTEJA WA MIAKA 10 WA ARSENAL KWA MAN UNITED UMEWADIA?

article-2492557-1949D60F00000578-262_634x452_377d1.jpg
ILIKUWA Novemba 28, mwaka 2011, Arsenal ilipoondoka imetota vibaya Uwanja wa Old Trafford ikitandikwa mabao 8-2, siku ambayo Wayne Rooney alifunga Hat-trick na Ashley Young akafunga mawili. Danny Welbeck pia alifunga.
Kwa kiasi kikubwa Arsenal imekuwa ikinyanyaswa na Mashetani hao Wekundu, wakiwa wameweza kushinda mechi moja tu ndani ya misimu 10 na wao wakifungwa mechi 11.
Man United 2-1 Arsenal, Ligi Kuu Novemba 3, 2012
Van Persie alihitaji dakika tu kuwakumbusha mashabiki wa Arsenal kipi watakosa kwa kuuzwa kwake kwa Pauni Milioni 24 kwenda Old Trafford, akifunga bao la kwanza kwa guu la kulia. Patrice Evra akaifungia la pili United baada ya mapumziko na Santi Cazorla akaipatia bao la kufutia machozi Arsenal. Kipigo hicho kiliwaacha Arsenal na pointi 15 baada ya mechi 10, mwanzo mbaya zaidi katika historia yao kwenye Ligi Kuu ya England chini ya Wenger.
Man United 8-2 Arsenal, Ligi Kuu Novemba 28, 2011
article-2492557-0D9C44C500000578-470_634x401_176d4.jpg
.

SIMBA YAWEKA WAZI USAJILI MPYA

julio_31d1c.jpg
SIMBA imepanga kuongeza kiungo mkabaji, beki wa kati na mshambuliaji kwenye dirisha dogo la usajili ingawa pia imedai itaangalia kwa jicho la tatu nafasi ya kipa inayoonekana kusuasua.
Kocha Msaidizi wa Simba, Jamhuri Kihwelu 'Julio' alisema nafasi hizo ndizo zimeonekana zina mianya.
Julio, ambaye kikosi chake kina wachezaji 26 alisema wanahitaji kujipanga upya na watawasilisha mapendekezo yao kwa uongozi.
"Tumesuasua katika baadhi ya mechi na nafasi ambazo tunaweza kuongeza dirisha dogo ni mshambuliaji mmoja, beki wa kati na kiungo mkabaji ingawa pia tutaangalia nafasi ya kipa, nayo tunaweza kuongeza nguvu kwani pia inasuasua," alisema Julio, ambaye habari za ndani zinadai huenda naye akatolewa kwenye benchi la ufundi la timu hiyo.
Simba ilifanya vizuri katika mechi kadhaa za mzunguko wa kwanza ingawa ilikuja kupepesuka na kutoka kileleni ikagota nafasi ya nne.
Hata hivyo Julio alitetea uamuzi wao wa kuwapeleka wachezaji walioshuka viwango kwenda timu ya vijana baada ya baadhi ya mashabiki na wanachama kuponda mfumo huo.
"Hatuwezi kuacha jambo hilo, litaendelea hivyo hivyo hata kama hawataki, kwani ndiyo funzo la wachezaji wasiotaka kujituma.
Mchezaji ukishindwa kuonyesha kiwango unaenda timu B ili upandishe kiwango chako na ukipelekwa kule wale waliobaki timu kubwa lazima nao watajituma zaidi,"alisema Julio, ambaye ni mchezaji wa zamani wa Simba.

MAGAZETI LEO JUMAMOSI NOVEMBA 09, 2013

DSC 0283 8ca4a

DSC 0284 6d190

Friday, November 08, 2013

MAGAZETI YA LEO IJUMAA NOVEMBA 08, 2013

DSC 0008 4d1e7
DSC 0009 f4e40

HOTUBA YA MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE...!!!


Jakaya-Kikwete_4f6c2.jpg
HOTUBA YA MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, ALIYOITOA BUNGENI KUHUSU JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI, 7 NOVEMBA, 2013, DODOMA

Mheshimiwa Anne Makinda, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Dkt. Mohamed Gharib Bilal, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania;
Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi;
Mheshimiwa Mizengo Pinda, Waziri Mkuu;
Waheshimiwa Mawaziri na Naibu Mawaziri;
Mheshimiwa Freeman Mbowe, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni;
Waheshimiwa Wabunge;
Mabibi na Mabwana;

Nakushukuru sana Mheshimiwa Spika kwa kukubali ombi langu na kutenga muda wenu ili niweze kuzungumza na Wabunge wa Bunge lako Tukufu kuhusu masuala muhimu kwa uhai, ustawi na maendeleo ya nchi yetu na watu wake.

Mheshimiwa Spika;
Nimeambiwa kuwa taarifa ilipotolewa kuwa ninaomba kuja kuzungumza na Waheshimiwa Wabunge, kumekuwepo na dhana mbalimbali. Wapo waliodhani kuwa nakuja kuzungumzia mchakato wa kuunda Katiba mpya na hasa matukio ya wiki chache zilizopita. Wapo waliodhani nakuja kuzungumzia "Operesheni Tokomeza". 

Tena wapo waliokwenda mbali na kufikiria kuwa nakuja kuwakaripia Waheshimiwa Wabunge waliotoa maoni yao kuelezea kasoro zilizojitokeza katika utekelezaji wa Operesheni hii muhimu. Na wapo pia waliodhani ninakuja kuzungumzia ushiriki wa majeshi yetu ya Tanzania katika Jeshi la Kulinda Amani la Umoja wa Mataifa nchini Kongo.

Mheshimiwa Spika;
Hayo si makusudio yangu. Kinachonileta mbele ya Bunge lako Tukufu ni kuzungumzia Jumuiya ya Afrika Mashariki na mustakabali wa Tanzania katika Jumuiya hiyo. Lakini, kwa sababu ya umuhimu wa masuala hayo niliyoyataja na rai niliyopewa kuwa niyasemee japo kidogo. Nimeona ni vyema nifanye hivyo.

Mheshimiwa Spika;
Kuhusu mchakato wa Katiba mpya, napenda kusema kuwa tumefikia hatua nzuri katika utekelezaji wake. Kama mjuavyo Tume ya Mabadiliko ya Katiba imekamilisha, kwa mafanikio, hatua ya mwanzo ya kusikiliza maoni ya wananchi kuhusu Katiba wanayoitaka. Pia walishatoa Rasimu ya Kwanza ya Katiba na kukamilisha mchakato wa Mabaraza ya Katiba. Kinachosubiriwa kwa hamu na sisi wote, ni Rasimu ya Pili ya Katiba ambayo inatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 15 Desemba 2013 au kabla ya hapo.

AZAM FC NA KOCHA WAKUBALI KUACHANA, YASEMEKANA JUMA KASEJA AMEJIUNGA YANGA

aje_7811f.jpg
Taarifa za kipa nyota, Juma Kaseja kutua Yanga zimewachanganya watu wengi. Ingawa zimekuwa hazina uhakika, lakini Salehjembe imepata taarifa za uhakika kwamba mchana wa jana ndiyo amemalizana na Yanga. Lakini bado watu wamekuwa wakihaha kutaka kujua kuhusiana na suala hilo.
Mmoja wa viongozi wa Yanga alisema; "Sitaki kulizungumzia kwa sasa, kama kuna walioandika sawa, lakini kumalizana
kwetu na Juma ni leo (Alhamisi). Tulimpa mkataba, anao yeye, hivyo tutakutana na kumalizana na tumegawanya makundi mawili, moja litakuwa uwanjani katika mechi dhidi ya Oljoro na lingine katika ishu hiyo ya Kaseja."
stewart_hall_62acc.jpg
Na Mahmoud Zubeiry
KOCHA Muingereza, Stewart John Hall ameamua kujiuzulu kufundisha klabu ya Azam FC baada ya kukubaliana na wamiliki wa timu hiyo na jana amewaaga wachezaji wa timu hiyo.
Stewart aliwaaga wachezaji na benchi la Ufundi mara tu baada ya mchezo wa mwisho wa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baina ya timu hiyo na Mbeya City ulioisha kwa sare ya kufungana mabao 3-3 Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

KAMANDA WA M23 AJISALIMISHA UGANDA

131105144849_m23_304x171_getty_d4f56.jpg
Maafisa wa Serikali ya Uganda wanasema kuwa kamanda wa kijeshi wa wapiganaji walioshindwa katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, DRC, M23, amejisalimisha kwa utawala wa Uganda.
Ripoti kutoka Uganda zinasema kuwa mamia ya wapiganaji wamejisalimisha pamoja na kiongozi wao, Sultani Makenga.
Wapiganaji hao wamejisalimisha katika eneo la hifadhi ya Wanyama ya Pori ya Mgahinga, kwenye mpaka wa Uganda na DRC.
Mnamo Jumanne M23 walisema kuwa wamesitisha maasi yao ya miezi 20 Mashariki mwa Congo, baada ya kutimuliwa katika ngome zao Mashariki mwa Congo na wanajeshi wa Serikali wakishirikiana na askari wa kudumisha amani wa Umoja wa Mataifa.
Hata hivyo serikali za Uganda na DRC hazijaweza kuthibitsha madai haya.
Mapema wiki hii, M23 ilisema kuwa inamaliza uasi wake wa miezi kumi na tisa masaa chache baada ya majeshi ya serikali kudai ushindi dhidi ya waasi hao.
Ripoti zinasema kuwa Sultani Makenga na waasi wengine 1,700, wamesalimisha silaha zao na wanazuiliwa na jeshi la Uganda katika kambi ya jeshi ya Mgahinga, karibu na mpaka na DRC.
Mapema wiki hii, maafisa wa DRC walisema Makenga alitoroka na kuingia Uganda au Rwanda.
Uganda imekuwa mwenyeji wa mazungumzo ya amani kati ya waasi na serikali ya DRC , ingawa hakuna mkataba wa amani umefikiwa.

Thursday, November 07, 2013

POLISI WAFANYA JARIBIO KATIKA HOTELI YA GOLD CREST MWANZA KUONA JINSI WANANCHI WANAVYOWEZA KUJIAMI NA MATUKIO YA UVAMIZI

WAPINGA MAREKEBISHO SHERIA YA MAGAZETI


lissu_5a412.jpg
Wakati Serikali imewasilisha muswada wa marekebisho ya sheria mbalimbali ikiwemo Sheria ya Magazeti, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, imepinga marekebisho ya sheria hiyo kwa madai kuwa hayakufanyiwa tafakuri na utafiti.
Akiwasilisha maoni hayo bungeni jana, Msemaji wa Kambi hiyo kuhusu Sheria, Tundu Lissu, alisema mapendekezo hayo yamefikishwa bungeni bila kufanyia tafakuri au utafiti wowote.
"Mwanasheria Mkuu wa Serikali angefanya utafiti kidogo tu angegundua kwamba kifungu cha 55 hakina na hakijawahi kuwa na, sababu yoyote ya kuendelea kuwepo katika kanuni ya adhabu,"alisema .
Alisema hiyo inatokana na kifungu hicho hicho kutungwa upya, kwa maneno yale yale, kama kifungu cha 31 cha Sheria ya Magazeti kwamba kifungu hicho hakikupaswa kuwepo kwa sababu, makosa ambayo kifungu hicho kinafafanua hayako tena kwenye kanuni ya adhabu na badala yake, yako katika Sheria ya Magazeti.
"Inaelekea katika fasta fasta ya kupitisha muswada wa Sheria ya Magazeti, kifungu cha 55 kilisahauliwa katika kanuni ya adhabu wakati vifungu vyote vinavyohusu makosa ya uchochezi na kashfa ya kijinai vilipohamishiwa katika Sheria ya Magazeti,"alisema Lissu.

MBUNGE WA UKEREWE AFUTIWA DHAMANA NA KUAMRIWA AENDE SELO SIKU 14

560843761_fd884.jpg
Na mwanahabari Bundala William
DHAMANA ya mbunge wa jimbo la Ukerewe, Salvatory Machemli (CHADEMA) imefutwa na ameamuriwa na mahakama kwenda rumande siku 14 kwa kuwa wadhamini wake wamekosa sifa baada ya mshitakiwa na wadhamini wake watatu kushindwa kufika mahakamani ili kuwezesha kesi inayomkabili kusikilizwa kama ilivyopangwa.
Pia, Mbunge huyo ametakiwa kuwasilisha vitambulisho vyake katika kituo cha polisi na amezuiliwa kutoka nje ya wilaya bila kibali cha mahakama.
Hakimu mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya hiyo Faustine Kishenyi ametoa uamuzi huo leo baada ya upande wa mashitaka kuomba mshitakiwa afutiwe dhamana.


Wadhamini ambao ni Shellifu Ngelezya, Max Mhogo na Konsolata Machemli wamepoteza sifa hivyo udhamini wao umefutwa.
Mwendesha mashitaka wa jeshi la polisi, Inspekta Samweli Onyango amesema mshitakiwa kwa makusudi ameshindwa kufika mahakani zaidi ya mara tano bila kutoa taarifa wakati kesi yake ikitajwa.

MATOKEO YA LIGI YA MABINGWA ULAYA

ARSENAL YAIKALISHA BORUSSIA DORTMUND, ETO'O APIGA MBILI CHELSEA IKIUA WAJERUMANI...MESSI KAMA KAWA, AIPIGIA MBILI BARCA IKIINYANYASA AC MILAN ULAYA
article-2488571-193C99A200000578-202_634x431_c6de5.jpg
Zama za ushindi: Aaron Ramsey (kulia) na Mesut Ozil wakishangilia bao pekee la ushindi la Arsnal
BAO pekee la Aaron Ramsey dakika ya 62, limeipa Arsenal ushindi wa 1-0 ugenini dhidi ya wenyeji Borussia Dortmund nchini Ujerumani.
Hilo linakuwa bao la 13 kwa mchezaji huyo msimu huu na bao la tano katika michuano ya Ulaya msimu huu. Pamoja na kufungwa, wenyeji ndio waliocheza vyema usiku huu na kabla ya Arsenal kupata bao lake, hawakuweza kutengeneza nafasi hata moja ya kufunga.
Borussia ambayo inapewa sifa ya moja ya timu bora kabisa Ulaya kwa sasa, iliingia kwenye mechi hiyo ikiwa na kumbukumbu ya ushindi wa 6-1 dhidi ya Stuttgart katika ligi ya kwao, Bundesliga, lakini ilikalishwa na mtutu mmoja wa bunduki.

Wednesday, November 06, 2013

LULU AFUNGUKA KUHUSU YEYE KUCHUMBIWA...!!!

 
Muigizaji wa filamu nchini Elizabeth Michael aka Lulu amekanusha fununu zilizoandikwa kwenye gazeti la udaku liitwalo ‘Filamu’ kwamba amechumbiwa na muda mchache ataolewa.
 
Akizunguza jana  kwenye kipindi cha XXL cha Clouds FM, muigizaji huyo wa Foolish Age, alisema hajachumbiwa na mtu yeyote ila ni magazeti ya udaku tu ndio yamekuwa yakiandika kile yanachojisikia.
 
“Mimi sijachumbiwa na hakuna mtu yeyote aliyenichumbia na kama itatokea siku nikachumbiwa kila mtu atajua, na ni mimi mwenyewe ndiye nitakaesema,” alisema mrembo huyo.
  “Lakini sasa sijajua wao wamepata hiyo habari kutoka kwenye chanzo gani, by the way kwaajili kumekuwa na habari kila kukicha kila mtu anayejisikia kuandika anaandika ,anaamka anaandika, anaamka anandika. 

 "Kwa hiyo leo wameandika nimechumbiwa, kesho wataandika nimeolewa, kwa hiyo inategemea na mood ambayo wao waliamka nayo, kwamba ‘leo Lulu tumchumbie, tumuozeshe, tumuachishe’, I don’t know.
 
“Kuchumbiwa, kuolewa,kuwa mke ni vitu ambavyo tumeumbiwa binadamu, vipo kama ukiwa mpango wa mwenyezi Mungu nitachumbiwa na nitaolewa.” Lulu

ANGALIA PICHA ZA JUX KING OF PAMBA KWA WASANII WA BONGO

http://distilleryimage8.ak.instagram.com/d08bd338f3c411e289bf22000a1fa4a9_7.jpg

http://distilleryimage2.ak.instagram.com/ddfe26f6ef9611e2a63622000a9e28ec_7.jpg


http://distilleryimage11.ak.instagram.com/cbffd894453311e3984822000a1f9707_7.jpg 
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...