Wednesday, October 16, 2013

RAIS WA ZANZIBAR DKT. SHEIN ASISITIZA AMANI BARAZA LA IDD ZANZIBAR

DSC_0112
Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Shein wapili kushoto akiomba Dua pamoja na viongozi wengine wa Kitaifa katika Swala ya Idi –El-Hjji ilioswaliwa Kitaifa huko katika kitongoji cha Marumbi Mkoa wa Kusini Wilaya ya Kati Unguja.kulia kwake ni Kadhi Mkuu wa Zanzibar Khamis Haji Khamis na kushoto yake ni Katibu mtendaji wa Wakfu na Mali ya Amana Sheikh Abdalla Twalib,Makamo wa Kwanza wa Rais wa Zanizbar Maalim Seif Sharif Hamadi na wamwisho ni Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Mahmod Mussa Wadi. DSC_0230
Rais wa Zanzibar Dk Ali Mohd Shein akitoa hotuba katika baraza la Idi -El-Hajji lililofanyika huko Tunguu Mkoa wa Kusini Wilaya ya Kati Unguja DSC_0206
Baadhi ya Viongozi na Wananchi waliohudhuria katika Baraza la Idi-El-Hajji lililofanyika huko Tunguu Mkoa wa Kusini Wilaya ya Kati Unguja
PICHA ZOTE NA YUSSUF SIMAI ALI-HABARI MAELEZO ZANZIBAR

MUME AMKATA MKEWE MGUU HUKO TARIME MKOANI MARA

Na Waitara Meng’anyi, Tarime


 Ghati Chacha (21) mkazi wa kijiji cha Nyanitira kata ya Nyansincha Wilayani Tarime amesababishiwa kilema cha maisha kwa kukatwa mguu wake wa kulia na Mume wake baada ya kuchelewa kumfungua mlangao nyakati za usiku.

Akisimulua mkasa huo hivi karibuni akiwa wodi namba sita alikolazwa akiuuguza vidonda na majeraha,Ghati alisema, mume wake  aliye mtaja kwa majina ya Chacha Mwita(23) alifika nyumbani saa mbili usiku akiwa amelewa.

ANGALIA VIDEO YA RAIS KIKWETE ALIPOKUTANA NA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA


JAMBO TZ INAWATAKIA EID MUBARAK NYOTE!


KUMBE SHOW ZA MAJUU SIO KAMA ZA BONGO! - OMMY DIMPOZ


Ommy alikuwa akiongea na kipindi cha Ampilifaya jana baada ya kurejea kutoka nchini Marekani alikokuwa kwenye ziara ya wiki tatu.

“Naweza kusema hapa nyumbani tunalipwa hela nyingi kuliko tunavyopata nje kwa msanii yeyote kwa asilimia kubwa. Inategemea pia unaenda kufanya tamasha sehemu gani. Kwahiyo asilimia kubwa hela unatengeneza zaidi nyumbani,”alisema Ommy.

Alisema hiyo ni kwasababu show za Tanzania huhudhuriwa na watu wengi zaidi kuliko inavyokuwa nchi za nje ambako ni watu wachache sana huingia japo kiingilio ni kikubwa na wengi wanaohudhuria ni watu waliotoka Afrika Mashariki zaidi.
Katika hatua nyingine, leo Ommy Dimpoz kupitia Instagram, ameandika maneno ya shukrani kwa wote walioifanikisha show yake.

“AssaLaam ALeykum Ndugu zangu, Eid MubaraQ Ndugu, jamaa, Marafiki, and all my Fans all over the world…Namshukuru Mungu Alhamdulilah nimerudi nyumbani Salama Kuendelea na Majukumu mengine baada ya Tour ya Takriban Mwezi Mmoja…Ningependa kuchukua Nafasi hii kuwashukuru @Dmkglobal promotion na J&P kwa kufanikisha tour yangu ambayo imeweza kuwa na Mafanikio makubwa Na kufanikisha baadhi ya malengo ambayo mengine sikuyatarajia.Pia ningependa kuwashukuru watu wote ambao walionyesha support kipindi chote cha tour yangu hususan Watanzania wenzangu na Watu wa Africa Mashariki na Kati ambao walionyesha Ushirikiano na support ya kutosha tangia mwanzo mpaka mwisho wa tour yangu…Nachoweza kuwaahidi ni kuwa mengi mazuri Yanakuja na Naimani sitawaangusha.Nawatakia mapumziko na sherehe njema za sikukuu ya Idd…. Mimi na team nzima ya pozkwapoz tutakuwa DARLIVE tukitoa Huduma Karibuni sana.LOVE U ALL.” na Vijimambo Blog

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ASHIRIKI SWALA YA EID EL HAJ MSIKITI WA ANWAAR MSASANI, DAR ES SALAAM

 Makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na waumini wa dini ya Kiislamu baada ya kushiriki nao katika Swala ya Sikukuu ya Idd El Haj, iliyofanyika katika Msikiti wa Anwaar uliopo Msasani, jijini Dar es Salaam leo. Picha zote na Ofisi ya Makamu wa Rais
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akijumuika na waumini kushiriki Swala ya Sikukuu ya Idd El Haj na Waumini wa dini ya Kiislam katika Msikiti wa Anwaar, uliopo Msasani jijini Dar es Salaam, leo asubuhi.

MAGAZETI YA LEO JUMATANO OKTOBA 16, 2013

DSC 0137 46fbc
DSC 0138 47cac

Tuesday, October 15, 2013

WAPINZANI KUTINGA IKULU LEO ... MKUTANO MUHIMU WA JK, MBOWE, MBATIA NA PROFESA LIPUMBA LEO UTOE MAJIBU HAYA

Viongozi wa vyama vikuu vya upinzani nchni kutoka kushoto: James Mbatia (NCCR Mageuzi), Freeman Mbowe (Chadema) na Profesa Ibrahimu Lipumba (CUF).
Viongozi wa vyama vikuu vya upinzani vyenye wabunge bungeni wanatarajia kukutana leo na Rais Jakaya Kikwete Ikulu, jijini Dar es Salaam kuzungumzia utata wa baadhi ya masuala yaliyojitokeza katika mchakato unaoendelea wa kupata Katiba Mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kama wengi tunavyotegemea, mazungumzo hayo kwa vyovyote ni ya masuala nyeti ambayo yamesababisha mvutano na kuibua hisia kali miongoni mwa makundi ya kijamii, pengine kwa kutambua fika kwamba kupuuza madai ya wapinzani ingekuwa sawa na kumwaga petroli katika nyumba inayoungua, busara za rais wetu zimemfanya awaite viongozi wa kisiasa kuteta nao Ikulu.
Wakati viongozi hao, Freeman Mbowe wa Chadema, James Mbatia wa NCCR Mageuzi na Profesa Ibrahimu Lipumba wanakutana na kiongozi wa nchi leo, pengine akiwa hajasaini Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ambao ulipelekwa mezani kwake baada ya kupitishwa bungeni na wabunge wa CCM wiki chache zilizopita, watampa mwanga kilichowafanya waugomee bungeni, maana katika hotuba yake alisema ameambiwa hiki na kile sasa atasikia laivu kutoka kwao.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE, OKTOBA 15, 2013

DSC 0064 8df93
DSC 0065 72acc

KESI YA BABU SEYA NA PAPII KOCHA KUUNGURUMA OKTOBA 30

sEYA11_4aa61.jpg
MAHAKAMA ya Rufaa Oktoba 30 mwaka huu inatarajiwa kusikiliza marejeo ya hukumu iliyotolewa na mahakama hiyo katika kesi iliyokuwa ikimkabili mwanamuziki Nguza Viki maarufu kama Babu seya na wanawe.
Baada ya hukumu hiyo, Babu Seya na mwanawe pamoja na wakili wao Mabere Marando waliomba marejeo ya hukumu hiyo.
Marejeo hayo yanatarajiwa kusikilizwa na Jopo la Majaji watatu wa mahakama hiyo ambao ni Nathalia Kimaro, Mbarouk Mbarouk na Salum Massati. 

Katika hukumu hiyo iliyotolewa Februari 2010, mahakama hiyo iliridhia hukumu ya kifungo cha maisha kwa Babu Seya na mwanawe, Papii Nguza huku ikimuwaachia huru watoto wawili wa Babu Seya, Nguza Mbangu, na Francis Nguza.

KIKWETE: TUMESHINDA MAADUI ZETU

Picha_na_8_7b2d0.jpg
Rais Jakaya Kikwete amesema maadui wote ambao walitaka kupandikiza chuki miongoni mwa Watanzania kwa lengo la kuvuruga amani ya nchi wamedhibitiwa .
Rais Kikwete alisema kuwa Serikali yake itaendelea kulinda amani ya nchi na maadui wote wanaohusika na kutaka kuvuruga nchi watachukuliwa hatua kali za kisheria. "Kulikuwapo na upepo mbaya, lakini kwa sasa Tanzania ni shwari na tumemshinda adui," alisema Rais Kikwete jana kwenye Maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere yaliyoandamana na sherehe za kuzima Mwenge wa Uhuru, mkoani Iringa.
Alisema katika siku za hivi karibuni, maadui wasioitakia mema Tanzania walikuwa na mkakati wa kuvuruga amani ya nchi, lakini Serikali kwa kushirikiana na vyombo vya dola vimewadhibiti na nchi iko salama.
Rais Kikwete alisema kuwa Serikali haiwezi kuvumilia vitendo vya uvunjifu wa amani kwa sababu inajua wazi kwamba nchi ikiingia kwenye mgawanyiko, mshikamano utavurugika na shughuli za maendeleo zitasimama.

RAILA ODINGA AELEZA NYERERE ALIVYOMSAIDIA KUSOMA NJE

odinga_79ebe.jpg
Waziri Mkuu wa zamani wa Kenya, Raila Odinga ameeleza kuwa bila ya Pasipoti ya Tanzania aliyopewa kwa msaada na Mwalimu Julius Nyerere asingeweza kwenda Ujerumani kusoma baada ya Idara ya Uhamiaji ya Kenya kumnyima hati hiyo ya kusafiria.
Odinga ambaye hivi sasa ni kiongozi mkuu wa Muungano wa Cord ameeleza hayo katika kitabu chake kiitwacho The Flame of Freedom, ambamo ameelezea historia yake na familia yake katika mambo mbalimbali.
Idara ya Uhamiaji ya Kenya ilimnyima Odinga hati hiyo kutokana na Serikali ya kikoloni kuzuia hati ya baba yake, mzee Jaramogi Odinga kwa sababu alitembelea nchi za Urusi na China zilizokuwa maasimu wakubwa wa nchi za Magharibi.

Hata hivyo, Mzee Jaramongi aliamua kusafiria hati ya kimataifa alizopewa na Kwame Nkurumah wa Ghana, pamoja na Gamel Abdel Nasser wa Misri.
Odinga alihitaji hati hiyo kwa kuwa baba yake alitaka amalizie masomo yake nchini Ujerumani baada ya kukatishwa masomo akiwa kidato cha pili mwaka 1962 katika Shule ya Maranda.
Katika kitabu hicho, Odinga alisema hakushangaa kunyimwa hati hiyo.

KLABU 7 ZATAWALA UBINGWA WA SOKA TANZANIA BARA

vodacom_premier_league_1497c.jpg
Na DANIEL MBEGA
LIGI Kuu Tanzania Bara inaendelea kutimua vumbi katika harakati za kutafuta bingwa katika mwaka wake wa 49 tangu harakati za kutafuta klabu bingwa zilipoanza mwaka 1965.
Mikiki mikiki yote hii isingekuwepo leo kama lisingekuwa wazo la kocha

wa Taifa Stars wa wakati huo, Milan Celebic wa Yugoslavia, alilolitoa mwaka 1964 kama njia ya kusaidia kuchagua wachezaji wa timu ya taifa badala ya kutegemea michuano ya Sunlight Cup (sasa Taifa Cup).
Badala ya michuano ya Sunlight iliyohusisha klabu na timu za Majimbo, Celebic aliona kulikuwa na umuhimu wa kuwepo mashindano ya klabu pekee katika ngazi ya taifa na siyo yale ya mkoa, hasa wa Pwani (Dar es Salaam ya sasa), hivyo 'akaliuza' wazo lake kwa Chama cha Ligi ya Soka cha Dar es Salaam (DFLA) ambao walianzisha mashindano hayo mwaka 1965 yakijulikana kama Ligi ya Taifa.
Mkutano Mkuu wa Mwaka wa TFA (TFF) uliofanyika kati ya Desemba 19-20, 1964 (Jumamosi na Jumapili) katika Ukumbi wa Arnautoglou mjini Dar es Salaam ndio uliojadili pamoja na mambo mengine, uanzishwaji wa Ligi ya Taifa. Tembelea jambotz8.blogspot.com na kenypino.blogspot.com kila siku.

Monday, October 14, 2013

HAYA NI MAMBO 11 YALIYOPINGWA NA BABA WA TAIFA, MWALIMU NYERERE

 Ni miaka kumi na nne sasa imepita tangu mzee wetu mpendwa baba wa taifa hayati Mwl Julius Kambarage Nyerere aiage dunia.
Mwalimu Nyerere ni Rais wa kwanza na ni muasisi aliyeliletea taifa hili uhuru wa kweli toka katika makucha ya mkoloni 9 December, 1961. Mwalimu Nyerere alizaliwa April 22, 1922 katika kijiji kidogo cha mwitongo huko Butihama, kasikazini mwa Tanzania karibu kabisa na ziwa Victoria . 
Alikuwa ni mototo wa chifu Burito Nyerere wa kabila dogo la wazanaki
Nyerere alifariki dunia kwa ugonjwa wa kansa ya damu, siku ya Alhamisi Oktoba 14, 1999 saa 4:30 asubuhi [kwa saa za Afrika Mashariki], katika hospitali ya Mtakatifu Thomas London, Uingereza akiwa amezungukwa na timu ya madaktari bingwa.
Ndipo wananchi wote tulipigwa na butwaa kwa kumpoteza kiongozi mwenye msimamo thabiti na busara duniani. 
Mwalimu bado ni taa inayong’aa gizani, umuhimu wake nazidi kuonekana kadiri miaka inavyokwenda licha ya kwanza amekwisha tuacha.
Wakati wa uhai wake Mwalimu Nyerere alichukia na kukemea vikali mambo yasiyofaa kwa mustakabali wa maendeleo ya Tanzania , Afrika na Dunia kwa ujumla. Baadhi ya mambo hayo ni:

1. UJINGA 

Mwalimu Nyerere alikuwa ni miongoni mwa wasomi wachache na ni mtanzania wa kwanza kupata nafasi yamasomo ya juu katika Chuo Kikuu cha Edinburg , Uingereza na kuhitimu mwaka 1952 akiwa ni gwiji wa uchumi na historia.
Mwalimu hakupenda ujinga na hivyo alipigana vita kali dhidi ya ujinga, na alifanikiwa kwa nafasi yake kuwaondoa ujinga watanzania wengi, wakiwemo viongozi wetu wa sasa ambao walisomeshwa ‘bure’ katika mazingira mazuri yakuridhisha kwa manufaa ya nchi yetu. Ndiyo maana Rais Kikwete Februari 3, 2007 alisema “….sisi tuliwekezwa na ni lazima tuwekeze kwenu ili miaka 30 ijayo Rais atoke miongoni mwenu….”

HIVI NDIVYO MKASA WA MWANDISHI WA ITV UFOO SARO ULIVYOKUWA

Mwandishi wa habari wa ITV, aliyejeruhiwa kwa risasi jana asubuhi, alilazimika kuvumilia majeraha ili kujiokoa yeye mwenyewe na wadogo zake watatu waliokuwa wakipigwa risasi, baada ya mama yake mzazi, Anastazia Saro (58), kuuawa.



Mauaji hayo ya kusikitisha, yalifanyika katika eneo la Mbezi Kibwerere, nyumbani kwa mama yake Ufoo ambako alikuwa akiishi na wadogo zake Ufoo ambao ni Goodluck, Innocent na Jonas.

Mtuhumiwa wa unyama huo ametajwa kuwa ni Anthery Mushi, ambaye ni baba mtoto wa Ufoo, na siku ya tukio wawili hao walitokea Mbezi Magari Saba nyumbani kwa Ufoo, kwenda kuzungumza kifamilia na mama mzazi wa mwandishi huyo.
Mushi (40) ni Mhandisi wa kitengo cha Mawasiliano katika Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) nchini Sudan na aliwasili nchini juzi na kwenda moja kwa moja nyumbani kwa Ufoo Mbezi Mgari Saba.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura, Ufoo amejeruhiwa katika paja na tumboni, mama yake mzazi alikufa papo hapo baada ya kupigwa risasi ya kifuani na mtuhumiwa Mushi ambaye naye alijiua baada ya kujipiga risasi kichwani katika eneo la kidevuni.

 Walivyowasili nyumbani
Akizungumza na wavuti hii jana mdogo wake Ufoo, Goodluck alisema; "Walikuja wakiwa pamoja (Ufoo na Mushi) mapema alfajiri wakiwa ndani ya gari saa 12 kabla ya kuingia ndani walitusalimia kisha wakaingia sebuleni na kuanza mazungumzo na mama."

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...