Sunday, September 29, 2013

MATOKEO YA LIGI KUU YA UINGEREZA LEO JUMAPILI

Stoke-City-Vs-Norwich-City_81e66.png
Stoke City 0 - 1 Norwich City
Timu ya Norwich City imeweza kupata goli hilo katika dk ya 34 na mfungaji alikuwa ni Jonathan Howson. mchezo huo ukiluwa mzuri lakini mpaka mpira unamalizika matokeo yaliendelea  kuwa Stoke City 0 - 1 Norwich City.
Endelea kuifuatilia mjengwablog kwa matokeo ya mchezo baina ya Sunderland na Liverpool ambao mpaka sasa bado hawajafungana na ni kipindi cha kwanza.

KENYA: MAAFISA WALIKUWA NA TAARIFA

westgate 34bc1
Mawaziri wa serikali walipokea taarifa kuhusu tisho la mashambulizi ya kigaidi kabla ya kundi la Al Shabaab kushambulia jengo la Westgate mjini Nairobi.


Kwa mujibu wa taarifa za kijasusi zilizofichuliwa, zilionyesha maelezo ya mipango ya mashambulizi hayo kufanyika Nairobi au mjini Mombasa.
Taarifa zinazohusianaKenya
Mawaziri wanne na mkuu wa majeshi walikuwa wamefahamishwa kuhusu tisho la kufanyika shambulizi la kigaidi.
Watu 67 walifariki na mamia kujeruhiwa katika shambulizi la kigaidi ambalo Al Shabaab walikiri kulifanya Septemba 21 mjini Nairobi.
Kwa mujibu wa taarifa za gazeti la Daily Nation, mawaziri walipokezwa taarifa za kati ta yarehe 13 na 20 kuhusu uwezekano wa kufanyika mashambulizi kadhaa ya kigaidi mjini Mombasa na Nairobi.

TAMKO LA SERIKALI LA KUYAFUNGIA MAGAZETI YA MWANANCHI NA MTANZANIA

DSC_0068_b4d0a_d830f.png
DSC_0066_048af_a3496.png
Serikali imeyafungia kutochapishwa Magazeti ya MWANANCHI na MTANZANIA kuanzia 27 Septemba, 2013 kutokana na mwenendo wa magazeti hayo kuandika habari na makala za uchochezi na uhasama kwa nia ya kusababisha wananchi wakose imani kwa vyombo vya dola hivyo kuhatarisha amani na mshikamano ulipo nchini.
Gazeti la MWANANCHI limefungiwa kutochapishwa kwa siku kumi na nne (14) kuanzia 27 Septemba, 2013. Adhabu hii imetangazwa kwa Tangazo la Serikali (Government Notice) Namba 333 la tarehe 27 Septemba, 2013.


Gazeti la MWANANCHI limepewa adhabu hiyo kutokana na hivi karibuni kuchapisha habari zenye mwelekeo wa
uchochezi na uvunjifu wa amani, mfano tarehe 17 Julai, 2013 katika toleo Namba 4774 ilichapisha habari isemayo "MISHAHARA MIPYA SERIKALINI 2013" kwa kuchapisha waraka uliozuiliwa kwa matumizi ya vyombo vya habari waraka huo ulikuwa wa Siri haukupaswa kuchapishwa Magazetini.
Aidha, katika toleo la Jumamosi, tarehe 17 Agosti, 2013 lilichapisha habari yenye kichwa kisemacho "WAISLAM WASALI CHINI YA ULINZI MKALI" habari hiyo ilikolezwe na picha ya mbwa mkali mwenye hasira.

Saturday, September 28, 2013

ANGALIA MAJINA YA WALIOPATA MIKOPO VYUO VIKUU 2013/2014

NOTICE TO SUCCESSFUL LOAN APPLICANTS FOR 2013/2014 ACADEMIC YEAR
The Higher Education Students’ Loans Board is hereby announcing names of successful first time loan applicants for 2013/2014 Academic Year who applied and were eligible for student loans.

The list includes the Institution to which the student is admitted to and the amounts of loans allocated to a particular student in all or part of the loanable items as per Guidelines and Criteria for Issuance of Loans and Grants for 2013/2014 Academic Year.

Loan applicants can access their loan status by keying in their Form Four Index Numbers to view the results. Loan applicants are reminded that the loan money will be sent to their respective institutions where they will be required to sign to acknowledge receipt of the loans, after registration processes.


Issued by:
The Executive Director
Higher Education Students’ Loans Board
P. O. Box 76068

RATIBA YA LIGI KUU YA UINGEREZA LEO JUMAMOSI

Barclays-Premier-League-fixtures-May-_05dde.jpg
14:45 Tottenham Hotspur na Chelsea
17:00 Aston Villa na Manchester City
17:00 Fulham na Cardiff City
17:00 Hull City na West Ham United
17:00 Manchester United na West Bromwich Albion
17:00 Southampton na Crystal Palace
19:30 Swansea City na Arsenal
Endelea kuifuatilia Mjengwablog ili kupata matokeo ya mechi hizi.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI SEPTEMBA 28, 2013

DSC 0066 048af
DSC 0067 182bf

"SINA MIKOSI KAMA WATU WANAVYOENEZA MANENO MITAANI" AUNTY EZEKIEL

Stori: Mayasa Mariwata
STAA wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel amesema hana mkosi kama watu wasiomtakia mema wanavyoeneza maneno mitaani.
Akipiga stori na paparazi wa Ijumaa juzikati, Aunt alisema kuna baadhi ya watu wasioitakia mema ndoa yake wamekuwa wakieneza maneno kwamba ana mkosi ndiyo maana kila mwanaume anayekuwa naye hupatwa na balaa.
Staa huyo aliongeza kuwa haumizwi kichwa na maneno hayo kwa kuwa anaamini kila kinachotokea katika maisha yake ni mipango ya Mungu.
“Maneno yao ni imani potofu na siwezi kumfikiria mwanaume niliyewahi kuwa naye huko nyuma kabla ya kuolewa na mume wangu Demonte kwani hakuna baya lililomfika tangu tulipooana,” alisema Aunt.
-GPL

MMILIKI ARSENAL ASEMA WENGER ANABAKI ARSENAL

wenger 24bf5
CHIFU wa Arsenal, Stan Kroenke anataka kocha Arsene Wenger abaki katika klabu hiyo kwa muda mrefu na kuleta taji la Ligi Kuu ya Enland Emirates.
Mfaransa huyo amekuwa katika klabu hiyo kwa miaka 17 na The Gunners ikiwa inakabiliwa na ukame wa mataji kwa msimu wa tisa sasa, amekuwa akipigwa zengwe aondoke, hususan kutokana na Mkataba wake kumalizika mwishoni mwa msimu.
Lakini mtu mwenye hisa nyingi za klabu, Kroenke hana shaka anataka Wenger abaki.
Mmarekani huyo amesema kwamba hafikiri kama kuna mwingine bora kuliko yeye na anaamini Wenger anafanya kazi nzuri.
Alipoulizwa kama mwalimu huyo mwenye umri wa miaka 63 yumo kwenye mipango ya muda mrefu ya klabu hiyo, Kroenke alisema: "Hiyo ni sahihi kabisa. Arsene anafahamu ambavyo tunahisi, falsafa zetu ni nini, nini tunataka kufanya na ninahisi tuko pamoja sana,".
Kufuatia klabu kuvuna rekodi yake ya usajili kwa kumsaini Mesut Ozil kutoka Real Madrid.
Kroenke alisema: "Kwa kweli namfurahia Arsene - safi sana, mweledi. Ana upeo mkubwa wa uongoza timu na klabu. Yuko sahihi katika hilio.
Kroenke pia amesema Wenger hastahili lawama kwa klabu hiyo la Kaskazin mwa London kumkosa mshambuliaji Luis Suarez, kwani ni Liverpool ndio hawakuwa tayari kumuuza nyota huyo kutoka Uruguay. Chanzo: binzubeiry

WAKUU WA USALAMA KUHOJIWA KENYA

wakuu_wa_usalama_ce362.jpg
Maafisa wakuu wa ujasusi wametakiwa kufika mbele ya kamati ya ulinzi ya bunge ili kuhojiwa kuhusu mashambulizi ya kigaidi dhidi ya jumba la Westgate mjini Nairobi.
Taarifa kwenye vyombo vya habari nchini humo zinaonyesha kuwa hali ya kulaumiana imeanza kuibuka huku mashirika ya usalama yakinyosheana kidole.
Watu 67 waliuawa kwenye shambulizi hilo huku zaidi ya miamoja sabini na tano wakipata majeraha mabaya. Shirika la Red Cross nalo linasema kuwa watu 61 wangali hawajulikani waliko.
Wataalamu wa uchunguzi wa mauaji wangali wanafanya uchunguzi wao wakitafuta miili na dalili za kilichosababisha shambulizi hilo.
Kamati ya bunge inataka maafisa wanaohusika na maswala ya usalama waweze kuwajibishwa.
Kundi la kigaidi la nchini Somalia, al-Shabab limedai kufanya mashambulizi hayo yaliyodumu siku nne kama hatua ya kulipiza kisasi kwa Kenya kujihusisha nchini Somalia kijeshi.
Hii leo ni siku ya tatu ya maombolezi kwa wathiriwa wa shambulizi hilo wakiwemo raia na wanajeshi.
Rais Uhuru Kenyatta amehudhuria mazishi ya mpwa wake na mchumba wake mjini Nairobi ambapo aliwahutubia waumini.
Walipuuza onyo?
Hatua ya kuwataka maafisa hao wa usalama kufika mbele ya tume ya bunge siku ya Jumatatu, inakuja kutokana na wasiwasi miongoni mwa wakenya kuhusu kiwango cha maafisa hao kujiandaa kwa tukio lolote la kigaidi sawa na lililotokea Westgate.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari mmoja wa maafisa waliotakiwa kufika mbele ya kamati hiyo ni mkuu wa shirika la ujasusi Michael Gichangi, anayesema alitoa taarifa za ujasusi kuhusu shambulizi hilo kwa polisi.
Lakini, afisaa mmoja mkuu katika idara ya polisi alikana kuwa taarifa hiyo ilitolewa kwa polisi.

BAADAYA KUTOSWA NA DIAMOND, MDOGO WAKE AIMBA NYIMBO YA KUMPONDA

HUU wimbo hatari tupu. Inaelezea maisha ya Diamond kabla hajatoka kimuziki. Dogo aloimba anadai Diamond ni ndugu yake wa damu na hakumbuki alipotoka. Duuh kaongea mambo mengi sana. Sina mbavu kwa kweli. Isikilize hapa Chini. Ni balaa tupu. Ni bonge moja la Ngoma.

ANGALIA VIDEO YA NDOA YA WATOTO WADOGO HUKO MJINI DODOMA



Vitendo vya ukatili wa kijinsia bado vipo katika jamii yetu, huko mkoani Dodoma ilishuhudiwa ndoa ya watoto wadogo kabisa, kiukweli ni ya kushangaza na hata huwezi kuamini, ila ndio mambo ya walimwengu hawa.


  ANGALIA VIDEO HAPO CHINI...

Friday, September 27, 2013

MJUE GAIDI SAMANTHA ALYEONGOZA AL-SHABAAB KUUA KENYA


Samantha20Lewthwaite-9559681 1f85a 
Adaiwa kuuawa Westgate
*Alifika Tanzania kwa Pasipoti ya Afrika Kusini
Ssamantha Lewthwaite, mwanamke wa Uingereza anayetajwa kuwa kiongozi wa ugaidi uliofanyika Nairobi, Kenya

WAKATI umwagaji wa damu katika kituo cha biashara cha Westgate ukiingia siku ya nne jana, Mwanamke ambaye ni raia wa Uingereza, Samantha Lewthwaite (29), anayetajwa kuwa ndiye aliyeongoza kundi la Al-Shabab kufanya shambulizi hilo, anahofiwa kuuawa.

Gazeti la Daily Mail la Uingereza, lilikariri vyanzo vyake vilivyoko ndani ya Jeshi na mfumo wa usalama nchini Kenya, ambavyo vimethibitisha kuwa mwanamke huyo ni miongoni mwa magaidi waliouawa na Serikali ya Kenya.
Hata hivyo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Amina Mohamed, katika mahojiano yake na kituo cha habari cha PBS, hakusema kama mwanamke huyo ameuawa lakini alithibitisha kuwa miongoni mwa magaidi waliovamia Westgate ni mwanamke wa Uingereza ambaye hata hivyo hakumtaja jina.
Hatua hiyo iliibua tetesi kwenye vyombo vya habari vya Kenya ambavyo vilimtaja mwanamke huyo kuwa ni Samantha.
Hata hivyo kauli hiyo ya Waziri huyo inaonekana kupingana na ile iliyotolewa awali na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Kenya, ambaye alisema kuwa magaidi wote waliovamia kituo hicho walikuwa wanaume na kwamba huenda baadhi yao walivalia mavazi ya kike.

TAARIFA YA JKT KWA VIJANA WANAOTAKA KUAHIRISHA MAFUNZO

JKT1_4a456.jpg
Vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT awamu ya tatu na pia wamechaguliwa kujiunga na vyuo vya elimu, wambao wanataka kuahirisha mkataba wa JKT, wanatakiwa kuandika barua Makao Makuu ya JKT kuomba kuahirisha mkataba wa JKT.
1. Barua binafsi kuomba kuahirisha mkataba iwe na picha yake.
2. Nakala ya barua ya kucahguilwa kujiunga na chuo (Joining instructions)
3. Barua hiyo ieleze kuwa utajiunga na JKT baada ya kuhitimu masomo.
4. Barua zao zifike Makao Makuu ya JKT kabla ya tarehe 02 Kotoba, 2013.
ANGALIZO
Kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria ni lazima. Hivyo ni wajibu wa kila mhitimu kuhudhuria mafunzo hayo.
Agizo hili limetolewa na Jeshi la Kujenga Tafia, Makao Makuu.
---
Imetolewa kwenye tovuti: http://jkt.go.tz/mkataba-jkt.html

Source: http://www.wavuti.com/#ixzz2g4C18z5v

KENYA YAMSAKA SAMANTHA LEWTHWAITE

nairobi c0494
Polisi wa kimataifa Interpol, wamemuweka mwanamke aliyeshukiwa kuongoza mashabulizi ya kigaidi nchini Kenya raia Muingereza Samantha Lewthwaite, kwenye orodha ya watu wanaosakwa sana duniani.
Hatua hii ni kutokana na ombi la serikali ya Kenya kwa Interpol.
Bi Lewthwaite, mwenye umri wa miaka 29, ni mjane wa mlipuaji aliyefanya shambulizi la kujitoa mhanga mjini London Uingereza mwezi Julai mwaka 2005
Anajulikana kama "white widow", na amehusishwa na kundi la kigaidi la Al Shabaab nchini Somalia.
Polisi wa Interpol hata hivyo hawakuhusisha hatua ya kumsaka Samantha na shambulizi la kigaidi dhidi ya jumba la maduka la Westgate mjini Nairobi lililowaua watu 67.
Hata hivyo, hatua hii ya kumsaka Bi Lewthwaite inakuja punde baada ya shambulizi hili la kigaidi nchini Kenya.
Al-Shabab ilikiri kufanya mashambulizi hayo yaliyotokana na kutekwa kwa jengo la Westgate na kisha kutekwa kwa raia wa kawaida waliokuwa ndani ya jengo hilo kwa siku nne.
Kwa mujibu wa polisi wa Interpol, mwanamke huyo anasakwa na serikali ya Kenya kwa kumiliki mabomu na kupanga njama ya kufanya mashambulizi kuanzia Disemba mwaka 2011.
Ikiwa mwanamke huyo atakamatwa katika nchi mwanachama wa Interpol, atazuiliwa na kusibiri kupelekwa katika nchi anayotakikana kwa kesi kufunguliwa dhidi yake.
Bi Lewthwaite anajulikana kwa jina bandia la, "Natalie Webb" –na alikuwa anasakwa kwa madai ya kumiliki hati bandia ya usafiri nchini Afrika Kusini.
Ni mjane wa Germaine Lindsay, mmoja wa washambuliaji wanne waliohusika na shambulizi la kigaidi mjini London ambapo watu 52 waliuawa na mamia ya wengine kujeruhiwa. 
Chanzo: bbcswahili

MAGAZETI YA LEO IJUMAA SEPTEMBA 27, 2013

DSC 0064 dad11
DSC 0065 8682d

Thursday, September 26, 2013

BAADA YA KENYA SASA AL-SHABAAB YAIGEUKIA TANZANIA....WATISHIA KUIVAMIA MUDA WOWOTE


*Yajigamba kufanya mashambulio muda wowote
*Watanzania wapewa mafunzo ya ugaidi nje ya nchi
*Polisi nchini wasema vyombo vya ulinzi viko macho
*Mtanzania akamatwa Kenya akihofiwa gaidi
 
WAKATI wananchi wa Afrika Mashariki wakijawa na hofu ya mashambulio yanayopangwa kufanywa na vikundi vya ugaidi vya Al Qaeda na Al Shabab, imebainika kuna Watanzania waliopewa mafunzo ya ugaidi wanaojiandaa kufanya maovu.

Hayo yamebainika siku chache baada ya wanamgambo wa kundi la Al Shabab kufanya mashambulio katika Jengo la Biashara la Westgate mjini Nairobi na kuua watu zaidi ya 70 na kuacha mamia wengine wakiwa wamejeruhiwa.

Mkuu wa Interpol Tawi la Tanzania, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP), Gustav Babile aliyasema hayo jana katika mahojiano maalumu na MTANZANIA.

YAFAHAMU MAJINA YA ASILI YA BAADHI YA MASTAR WA BONGO MOVIES

 KWA kawaida binadamu yeyote huzaliwa na kubatizwa jina ambalo hulitumia katika masomo na hata kazi yake.

Tofauti na ilivyo katika fani nyingine, wasanii wamekuwa wakijibatiza majina ya ziada (a.k.a). Mbaya zaidi, majina hayo huwa yanaanza kama utani lakini inafika wakati msanii husika

analizoea jina hilo jipya na kulifanya kuwa kama rasmi. Leo Amani linakuletea orodha ya baadhi ya mastaa ambao majina waliyopewa na wazazi wao ‘yamekufa’, hawayatumii kabisa: LULU

Jina lake halisi ni Elizabeth Michael, Lulu lilizoeleka kupitia tasnia ya uigizaji. Alianza kulitumia wakati alipojiunga na Kundi la Sanaa la Kaole.

Hadi leo hii, siyo rahisi kabisa mtu kutokea na kumuita jina la Elizabeth, wengi wanamfahamu kwa jina la Lulu.
RAY
Ray ndiyo jina ambalo limezoeleka na wengi. Vincent Kigosi alilopewa na wazazi wake ni kama limekufa. Kwa zaidi ya miaka kumi sasa tangu alipokuwa kwenye Kundi la Sanaa la Kaole hadi sasa.
Jina la Ray ndiyo watu wanalolifahamu zaidi ingawa hivi karibuni baadhi ya wasanii wenzake wamekuwa wakijaribu kumuita Vincent ili kurudisha uhai wa jina hilo.

JOHARI
Jina lake halisi ni Blandina Chagula. Johari lilizaliwa kwenye Tamthiliya iliyobeba taito ya jina hilo. Akiwa katika Kundi la Kaole, alianza kujiita Blandy, baadaye alibadilisha jina hilo na kuwa Johari walipoingiza tamthiliya hiyo ambayo pia ilizaa filamu.

MWANAFUNZI AMCHINJA MWALIMU WAKE DARASANI...!!!

KUSHOTO: Mwalimu Sun Wakang. KULIA: Damu ikiwa imetapakaa darasani muda mfupi baada ya tukio hilo.
Mwanafunzi wa China amemchinja mwalimu wake katika kulipiza kisasi baada ya simu yake ya mkononi kutaifishwa.
Mwanafunzi huyo, aliyetajwa kwa jila la Lei katika taarifa za habari za mjini humo, alibambwa na mwalimu wake, Sun Wakang akiwa anachezea simu wakati wa somo la Kemia katika shule moja mjini Fuzhou, mashariki mwa jimbo la Jiangxi nchini China.
Siku iliyofuata Lei alikwenda kwenye darasa analofundisha Sun ambako mwalimu huyo alikuwa ameketi akisahihisha mitihani, na kumchinja kutokea kwa nyuma.
Mwalimu huyo mwenye miaka 32 ambaye ni baba wa watoto watatu alifariki papo hapo huku mwanafunzi huyo akitokomea kusikojulikana.
Jana Lei alipiga namba ya simu ya dharura na kukiri kuhusika na uhalifu huo kabla ya kujisalimisha mwenyewe polisi mjini Shanghai.
Sun alifanya kazi kama mwalimu wa Kemia katika Shule ya Kati ya Linchuan No. 2 kwa miaka mitano kabla ya mauaji yake ya kutisha, ofisa wa shule Xiong Hainshuo alieleza.

NI AL-QAEDA, SI AL SHABAAB

westgate 870d9
  • Magaidi wa Marekani, Uingereza, Syria wahusika
SHAMBULIO la kigaidi lililofanywa nchini Kenya Jumamosi iliyopita na watu waliodhaniwa kuwa wafuasi wa Al- Shabab, sasa limeelezwa kutekelezwa na mtandao mpana zaidi wa kigaidi wa kundi la Al-Qaeda.


Baadhi ya wachambuzi na wachunguzi wa masuala ya kiusalama na kimataifa, wameyataja mambo matatu ambayo yanathibitisha pasipo shaka kwamba waliotekeleza tukio hilo la kuvamia, kuteka nyara na kuua watu wapatao 68 katika Kituo cha Biashara cha Westgate, ni wa aina ya kundi ambalo kinadharia na kimatendo linafanana na lile la kigaidi duniani la Al-Qaeda. Mambo yanayotajwa na wachambuzi na wachunguzi hao ni pamoja na mbinu, teknolojia na aina ya watu waliotumika kutekeleza shambulio hilo.
Katika uchambuzi wao, wameeleza kuwa mbinu iliyotumiwa na magaidi hayo kuvamia pasipo kujulikana mara moja na vyombo vya ulinzi na usalama vya nchini Kenya, lakini pia aina ya silaha walizokuwa nazo, inaonyesha kuwa kundi hilo limeamua kutumia kivuli cha Al-Shabab kufikisha ujumbe kwa dunia kwamba lipo licha ya uongozi wake kubadilika.
Kwamba mbali na mbinu pamoja na teknolojia, pia aina ya watu waliohusika kutekeleza shambulio hilo ambao wamebainika kutoka katika mataifa mbalimbali duniani, ndio ambao wamewafanya wachambuzi na wachunguzi hao waanze kupata shaka kwamba huenda kuna kundi kubwa zaidi lililotekeleza shambulio hilo, ambalo limejivika taswira ya Al-Shabab.

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI SEPTEMBA 26, 2013

DSC 0054 223dc
DSC 0055 3bc8f

MANJI AWATULIZA WACHEZAJI YANGA


MWENYEKITI wa Yanga SC, Alhaj Yussuf Mehboob Manji amewaambia wachezaji wa timu hiyo kwamba hana matatizo nao kwa matokeo ya awali ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara na amewataka waelekeze nguvu zao katika mechi zijazo.
Yanga imeambulia pointi sita katika mechi tano za awali za Ligi Kuu ya Vodacom, kutokana na sare tatu, kushinda moja na kufungwa moja, hivyo kuachwa kwa pointi tano kileleni na wapinzani wao wa jadi, Simba SC.
Jana Manji alikutana kwa chakula cha jioni na wachezaji wa timu hiyo katika hoteli ya Serena, Dar es Salaam akiwa ameambatana na Makamu wake Mwenyekiti, Clement Sanga, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Isaac Chanji na Mjumbe wa Sekretarieti, Patrick Naggi.
Katika kikao hicho, Manji aliwaambia wachezaji wa Yanga hamlaumu yeyote kwa matokeo hayo, kwani ligi bado mbichi, ila akawataka waunganishe nguvu zao kuelekea mechi zijazo, ili kurejesha ushindi na furaha klabuni.
Pamoja na hilo, Manji alizungumzia suala la madai ya baadhi ya
wachezaji ya fedha za usajili na akaliweka sawa kwa wale ambao walikuwa wanadai kuwawekea utaratibu wa malipo haraka, jambo ambalo Naggi ametakiwa kuhakikisha analishughulikia mara moja.

M23 WAHOFIWA KUJIFICHA MAKANISANI DAR

m23 pic 40eb7
WASIWASI umeibuka miongoni mwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, kuhusu uwepo wa makamanda wa wapiganaji wa kikundi cha waasi wa M23, ambao wamejipenyeza nchini kwa kivuli cha kuendesha shughuli za kihoro katika baadhi ya makanisa.
Duru za uchunguzi zimeonyesha kuwa baadhi ya watu walioingia nchini kwa mwamvuli wa uchungaji wakitokea nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, majina yao yamo kwenye orodha ya wapiganaji wa kikundi hicho cha waasi.
Taarifa mbalimbali zilizokusanywa na gazeti hili zimeonyesha kuwa, raia hao wa Kongo mbali na kufanya kazi za kiroho, pia wanajihusisha na shughuli mbalimbali za kijamii pamoja na kufanya biashara ndogo ndogo.
Baadhi ya wachungaji waliozungumza Jumatano kuhusu suala hilo, walishindwa kukubali au kukanusha kuhusu taarifa hizo.
Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la Mikocheni B, Assemblies of God, Getrude Lwakatare, ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Morogoro (CCM), alipoulizwa kupitia simu yake ya kiganjani iwapo anazo fununu za uwepo watu wa aina hiyo ambao kwa kiasi kikubwa wameanza kujenga taswira mbaya katika baadhi ya makanisa, alikaa kimya kwa muda kisha akakata simu.

PAPA BENEDICT AKANUSHA KUTOKUWAJIBIKA KWA KASHFA ZA KANISA.

papa_g_2_1b32e.jpg
Papa wa zamani Benedict ameibuka kutoka kwenye ukimya binafsi ndani ya Vatican na kukanusha hadharani kwamba alificha vitendo vya manyanyaso ya kingono kwa watoto na mapadri wa kanisa katoliki.
Katika barua ndefu kwa mtunzi wa vitabu wa Italia asiye na dini na mwanamahesabu (Piergiorgio Odifredi) na kuchapishwa jana Jumanne na gazeti la La Republica , Benedict alikana kutokuwajibika kwa kashfa ya ngono kwa watoto.Lakini amesema kanisa lazima lifanye kila iwezalo kuzuia vitendo kama hivyo kutokea tena.
Makundi ya waathirika wamemshutumu Papa huyo kwa kutokufanya vya kutosha kuzuia manyanyaso hayo, kabla ya kuwa Papa na baada , wakati alipoongoza ofisi ya kanuni ya Kanisa, ambayo ilihusika na kesi za manyanyayaso.

ALL HAIL FOR THE KING "HE'S BACK" - HUU NDIO UJIO MPYA WA CPWAA

CherekoCherekoArtwork_1_7a659.jpgCross-Borders_Therapy_Artwork_bd180.jpg
Mashabiki wake hupendelea kumuita "King of BongoCrunk"....jina halisi ni Ilunga Khalifa a.k.a CPwaa! Msanii wa muziki wa kizazi kipya Tanzania ambaye baada ya ukimya mrefu sasa kuachia kazi zake mpya.

C.P a.k.a CPwaa mwenye tuzo 3 za Tanzania Kilimanjaro Music Awards na Multiple Channel O Africa Music Video Awards nominations anakuja kivingine kabisa mwaka huu. Tarehe 1 mwezi wa October 2013, CPwaa ataachia single yake mpya na ya kwanza kabisa kwa mwaka huu.Single hiyo iitwayo "Chereko Chereko" yenye mahadhi ya AfroDance imefanywa chini ya studio za 'De Fatality Music" na producer "Mesen Selekta" ambaye mwaka huu alichukua tuzo ya mtayarishaji bora Tanzania anayechipukia.Nyimbo hii itapatikana kwenye mitandao yote na media zote kuanzia tarehe moja October.

TANZANIA NA BURUNDI WAICHARUKIA EAC....WATAKA MAELEZO YA KINA KUTOKA RWANDA UGANDA NA KENYA



HALI ya mambo imezidi kuwa tete katika Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), baada ya Tanzania na Burundi kutaka maelezo ya kina kutoka kwa nchi nyingine tatu wanachama za Kenya, Uganda na Rwanda zilizoanzisha ushirikiano mpya kinyemela kati yao, kwa kuzitenga nchi hizo mbili.
Katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita kumekuwa na mfululizo wa matukio yanayoashiria kuwa Tanzania na Burundi zimetengwa na nchi hizo tatu ambazo zimeanzisha ushirikiano mpya kati yao kinyemela, kinyume cha mkataba ulioanzisha Jumuiya hiyo mwaka  1999.
Jumuiya ya sasa ilizaliwa tena upya Novemba 30, mwaka 1999 ikishirikisha nchi za Tanzania, Uganda na Kenya, wakati Rwanda na Burundi zilikaribishwa baadaye mwaka 2008.
Jumuiya hiyo mpya ilizaliwa baada ya ile ya awali iliyoanzishwa mwaka 1968 kuvunjika mwaka 1977 kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kushindwa kuelewana kwa wakuu wa nchi wanachama kwa wakati huo, Mwalimu Julius Nyerere (Tanzania), Jommo Kenyatta (Kenya) na Idd Amin (Uganda).
Habari za hivi karibuni zilizopatikana kutoka ndani ya EAC zinabainisha kwamba Tanzania na Burundi zimekerwa na hatua ya nchi wanachama wenzao za Kenya, Uganda na Rwanda kuanza mchakato wa kuanzisha shirikisho la kisiasa bila ya kuzishirikisha nchi hizo.

BABU WA LOLIONDO AINENEA MAZITO TANZANIA.....AMWELEZA PINDA MAMBO ALIYOOTESHWA NA MUNGU

 
MCHUNGAJI Ambilikile Mwaisapila wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) amesema Mungu ameendelea kujifunua kwake na kumuonyesha kuwa Tanzania itakuwa kioo cha Afrika na baadaye kioo cha dunia.

Ametoa kauli hiyo Jumanne, Septemba 24, 2013 mbele ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakati akizungumza na wakazi wa kijiji cha Samunge, wilayani Ngorongoro mkoani Arusha wakati msafara wa Waziri Mkuu uliposimama nyumbani kwake ili kumsalimia akiwa njiani kurejea mjini Arusha. 
Mchungaji Mstaafu Mwaisapila maarufu kama Babu wa Samunge alisema kuna mambo mengi ambayo yameandikwa kwenye Biblia lakini hayakutokea Israeli na sasa yatafanyika hapa Samunge. “Mungu ametupenda sana, yanakuja mambo makubwa na wala hayako mbali. Kama mimi ni mzee na nitayaona, kwa hiyo mtarajie kuwa hayako mbali kutokea,” alisema huku akishangiliwa. 

Wednesday, September 25, 2013

WATU WAWILI WAKAMATWA NA MAITI YENYE MADAWA YA KULEVYA TUMBONI HUKO TABATA



POLISI Kanda Maalumu ya Dar es Salaam inawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kukutwa na maiti, iliyokuwa na pipi 33 za dawa za kulevya aina ya heroin tumboni.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Kanda hiyo, Kamishna wa Polisi, Suleiman Kova alitaja waliokamatwa kuwa ni Nasri Omari (36), maarufu kama Rajabu Robot na Mwanaisha Salim( 36), mkazi wa Kigogo Luhanga.
Kila pipi ina urefu wa sentimita sita...tulipata taarifa kutoka kwa raia wema kuwa huko Tabata kuna mtu mmoja alifariki ghafla muda mfupi baada ya kutoka bafuni kuoga na tukaamua kulifuatilia tukio hilo” alisema.
Alisema makachero walifika eneo la tukio, nyumbani kwa Omari na kuhoji hatimaye kugundua uwepo wa maiti sebuleni ikiwa imelazwa chali katika godoro sakafuni huku akiwa hana nguo na amefunikwa na shuka.
Omari ambaye ndiye mmiliki wa chumba kilichokutwa maiti, alisema marehemu anajulikana kwa jila la Rajabu Kandunda (43), maarufu kama Mashaka Mabruki” alisema.
Kamishna Kova alisema uchunguzi wa awali, ulionesha kuwa Kandunda alifika kutoka Mtwara Septemba 21 kwa maelezo kwamba alikuwa mgonjwa na alikwenda kuchukuliwa na watuhumiwa hao wawili.

ANGALIA VIDEO IKIONYESHA JINSI FAMILIA HII ILIVYO OKOLEWA KUTOKA NDANI YA JENGO LA WESTGATE-SAD



We’ve all seen this iconic photo of this mother and her two young children laying down calmly as the attack went on on Nairobi’s Westgate mall. Here is a short video showing them being evacuated to safety. Notice the little girl did not let go of her freshly bought Bata paper bag containing her new pair of shoes.

it is so sad that the children actually knew they had to lie still, even the little boy must have known that something is terribly wrong, so he didnt move even a bit... it just makes me so sad.. children never should have experience such bad things

 Video: Exclusive Footage of The Rescue Of Mother & Her Children #WestgateMall

MAGAZETI YA LEO JUMATANO SEPTEMBA 25, 2013

DSC 0027 aa995
DSC 0028 f54fc

KENYA YAOMBOLEZA KWA SIKU 3

zzzzzkenyatta_maombi_640x360_bbc_nocredit_06884.jpg
Kenya inaanza siku tatu za maombolezi ya kitaifa kwa waathiriwa wa mashambulizi ya kigaidi yaliyofanyika katika jengo la kibiashara la Westgate mjini Nairobi.
Watu 67 wameuawa ikiwemo wanajeshi kadhaa wa usalama, ingawa kuna hofu kuwa idadi ya waliofariki huenda ikaongezeka.
Maafisa wa uchunguzi wa kimataifa wanaungana na wale wa Kenya kujaribu kuondoa mili ambayo imenaswa kwenye vifusi vya jengo hilo ambalo sehemu yake iliporomoka jana. Nia ni kujaribu pia kutambua uraia wa washambulizi hao.
Baraza la usalama wa kitaifa linatarajiwa kukutana leo kudadisi yaliyotokea na kujiandaa kwa mkakati mpya wa kigaidi.
Magaidi watato waliuawa katika shambulizi hilo lililodumu siku nne na kuwa washukiwa wengine 11 walikamatwa wakijaribu kuondoka nchini.
Katika hotuba yake kwa taifa siku ya Jumatano , Rais Uhuru Kenyatta alisema kuwa alihisi uchungu mkubwa na kuwa Kenya imejeruhiwa vibaya,lakini alielezea matumaini kwa kuwa shambulizi limeisha na kusema kwamba waliohusika watakiona cha mtemakuni.

AL SHABAAB NI NANI...???

00 a9dd3
ULIMWENGU umepatwa na mshtuko mkubwa kwa kuona picha za tukio kubwa la kigaidi kwenye moja ya maduka makubwa jijini Nairobi. Hili ni shambulio kubwa la kigaidi kupata kutokea Afrika Mashariki tangu lile la mwaka 1998. Na ajabu ya kihitoria ni kuwa matukio mengi ya kigaidi yametokea katika mwezi wa Septemba.
La Nairobi ni shambulizi la kigaidi la kulaaniwa vikali na wapenda amani wote ulimwenguni. Hata hivyo, moja ya tafsiri ya vitendo vya kigaidi tunavyovishuhudia Nairobi ni kuwepo kwa hali ya vita vya kigaidi vyenye kuendeshwa kwenye maeneo ya mijini (Urban terrorism).
Ni shambulizi lenye athari mbaya kiuchumi si tu kwa nchi ya Kenya, bali hata majirani zake ikiwemo Tanzania. Ni shambulizi lililowaogopesha wageni wengi wakiwamo wawekezaji pia. Kwamba Al Shabaab inalenga pia nchi za Magharibi. Hivyo basi,
hata raia wake. Kunahitajika jitihada za pamoja kuwaondoa hofu watu wa mataifa ya nje, kuwa kilichotokea Nairobi kitadhibitiwa kwa njia zote, kisitokee tena.
Na hakika, aina hii ya ugaidi ni ngumu sana kudhibitika hatakama nchi ina jeshi kubwa na lenye vifaa vya kisasa. Inahitaji ushiriki wa raia wema katika kutoa taarifa za wahalifu hata kabla hawajafanya matendo yao maovu. Inahitaji pia maandalizi makini, ya kuwa na vikosi vilivyo tayari wakati wote kukabiliana na matukio kama haya.
Ni dhahiri, kuwa mbinu inazotumika kikundi cha kigaidi cha Al Shaabab ambacho maana hasa ya jina hilo ni ' Vijana', ni moja ya changamoto kubwa katika mapambano dhidi ya ugaidi.

MANJI: YANGA SHWARI, HAKUNA MGAWANYIKO

Manji 21 55726
MWENYEKITI wa Yanga SC, Alhaj Yussuf Mehboob Manji amesema hakuna mgawanyiko ndani ya klabu hiyo na habari kwamba Seif Ahmed 'Magari' ametengwa ni uzushi, lakini habari za ndani kutoka kwenye klabu hiyo zinasema uongozi unaamini unahujumiwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).



Kumekuwa na habari kwamba Seif Magari ameondolewa katika sehemu ya uongozi wa klabu na kwa sababu hiyo, hata swahiba wake, Abdallah Ahmed Bin Kleb ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano Yanga, naye amejitoa pia.

"Hakuna mgawanyiko, hayo ni maneno tu, Seif yupo na Majjid (Suleiman) wote tupo nao. Na hatuna wasiwasi na ligi, Simba SC inaongoza inatuzidi pointi tano tu.
Tumefungwa na Azam FC kwa bahati mbaya, sisi ndio tulicheza mpira mzuri na kila mtu ameona,"alisema Manji.

Tuesday, September 24, 2013

BREAKING NEWZZZZZZZZZ....!!! MKUU WA WILAYA YA URAMBO BI. ANNA MAGOHA AFARIKI DUNIA

Aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Urambo Marehemu Bi.Anna Magoha enzi za uhai wake akiwajibika kazini 
****
Serikali ya rais Jakaya Kikwete imepata pigo kubwa baada ya aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Urambo Bi. Anna Magoha kufariki dunia  akiwa Chang'ombe jijini Dar kufuatia maradhi yaliyokuwa yakimsibu.
Mkuu huyo wa wilaya Bi. Anna Magoha amefariki jioni ya leo akiwa njiani kukimbiza Hospitali ya taifa ya Muhimbili.

Marehemu Anna Magoha ambaye alishawahi kuwa Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa aliteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya na Rais Jakaya Kikwete mnamo mwaka 2006.

Marehemu alikuwa ni mkazi wa wilaya ya Kilolo mkoa wa Iringa.

VIKOSI VYA KENYA 'VIMEDHIBITI' WESTAGE

westgate 5472a
Hatimaye vikosi vya usalama nchini Kenya vinasema vimelidhibiti jengo zima la Westgate mjini Nairobi, ikiwa ni zaidi ya siku tatu baada ya jengo hilo kuvamiwa na wanamgambo. (HM)


Milipuko ikifuatiwa na milio ya risasi imesikika kutoka ndani ya jengo hilo asubuhi ya leo huku duru zikisema kuwa vikosi vya usalama vinaelekea kukamilisha operesheni hiyo.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari, magaidi sita waliokuwa wamesalia wameuawa huku wengine watatu wakiuawa hapo jana.
Serikali imesema zaidi ya watu 60 wameuawa na wengine zaidi ya 170 kujeruhiwa katika shambulio hilo ambalo Al shabaab imekiri kulitekeleza.
Wizara ya mambo ya ndani imesema wanajeshi wanaendelea kulisaka jengo zima la Westgate kutoka orofa moja hadi nyengine kuhakikisha kwamba hakuna mateka aliyesalia
Wakati huohuo, waziri wa mambo ya nje amesema kuwa wawili kati ya wanamgambo watatu waliofanya shambulii hilo ni raia wa Marekani pamoja na mwanamke muingereza.

OBAMA AIPONGEZA TANZANIA...!!!


Rais wa Marekani Barack Obama ametoa pongezi na sifa kwa Tanzania kwa kuwa miongoni mwa nchi chache duniani ambazo zimetia saini mkataba wa Ushirikiano wa Serikali Zinazoendeshwa kwa Uwazi ambao unalenga kujenga na kuendeleza nafasi ya taasisi zisizokuwa za Kiserikali katika utawala bora, uwazi na uwajibikaji katika uendeshaji wa Serikali.
Rais Obama ametoa pongezi hizo kwa Tanzania leo, Jumatatu, Septemba 23, 2013, wakati akizungumza katika mkutano maalum aliouandaa mwenyewe Rais Obama kuzungumzia nafasi za Serikali katika kuunga mkono na kuendeleza asasi na taasisi zisizokuwa za Kiserikali na kuzishirikisha zaidi katika kuboresha shughuli za utawala bora uliofanyika kwenye Hoteli ya Hilton, mjini New York, Marekani.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete alikuwa miongoni mwa viongozi wachache duniani walioalikwa kushiriki mkutano huo maalum ambao pia ulishirikisha wawakilishi wa asasi zisizokuwa za Kiserikali 300.
Baadhi ya nchi nyingine za Afrika zilizoalikwa na kushiriki katika mkutano huo ni pamoja na Liberia, Ghana, Benin, Libya, Tunisia, Senegal, Afrika Kusini na Botswana.
Shabaha kuu ya mkutano huo wa saa moja ilikuwa ni kutafuta namna ya kuongeza kiwango cha kuungwa mkono kwa taasisi na asasi hizo na jinsi gani ya kuzilinda ili kuziwezesha kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.
Aidha, mkutano huo ulilenga kuzitaka Serikali ambazo zinaweka vikwazo kwenye utendaji wa asasi hizo kuondoa vikwazo hivyo haraka ambavyo vinahujumu utendaji kazi na mchango wa asasi hizo katika uendeshaji wa utawala bora.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE SEPTEMBA 24, 2013

DSC 0016 5b08d
DSC 0017 4b107

WANAFUNZI 300 ELIMU YA JUU KUKOSA MIKOPO

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa
Zaidi ya wanafunzi 300 wa elimu ya juu wa vyuo mbalimbali watakosa mikopo kutoka Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), kutokana na kushindwa kujaza fomu za kuomba mikopo katika kipindi kilichowekwa.
Watakaokosa mikopo hiyo kwa mwaka wa masomo wa 2013/2014 ni kuanzia mwaka wa pili na kuendelea, ambao hawakujaza fomu za kuonyesha taarifa zao mpya kwa bodi.
Wanafunzi hao walitakiwa kuwasilisha maombi ya kupewa mikopo kati ya Mei hadi Julai 30, mwaka huu.
Mkugenzi Msaidizi wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa HELSB, Cosmas Mwaisobwa, aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam alipozungumza na waandishi kuhusu utendaji wa kazi wa bodi hiyo.
Mwaisobwa alisema kwa kuwa wanafunzi hao hawakujaza fomu za kuomba mikopo, mwaka huu hawatapata fursa hiyo na kwamba kwa mujibu wa utaratibu wao, kila mwaka lazima mwanafunzi aombe.

SIMU ZA WATU MILIONI NANE KUFUNGIWA MWISHO WA MWEZI HUU


WATUMIAJI wa simu wapatao milioni nane wapo hatarini kufungiwa simu zao ifikapo mwishoni mwa mwezi huu, Tanzania Daima limebaini.
Tayari Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeziandikia kampuni za simu waraka wa kuzitaka zianze kukata kodi mpya ya laini (simu card) mara moja kuanzia Julai 30, 2013.
Hatua hiyo inatokana na serikali kushindwa kufuta kodi hiyo ya sh 1,000 iliyopitishwa na Bunge kama alivyoagiza Rais Jakaya Kikwete baada ya kukutana na wadau wa sekta ya mawasiliano.
Kwa maana hiyo kila anayemiliki laini moja ya simu atakatwa sh 3,000; anayemiliki laini mbili sh 6,000 na anayemiliki laini tatu sh 12,000, lengo ni kuhakikisha serikali inakusanya sh bilioni 178 zitakazopelekwa kwenye bajeti kuu ya serikali.
Watumiaji wa simu sasa watalazimika kulipia kodi hiyo ya miezi mitatu ya Julai, Agosti na Septemba kwa wakati mmoja.
Bunge kupitia Kamati ya Bajeti inayoongozwa na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge (CCM) lilitaka kuwapo kwa kodi hiyo ili kusaidia shughuli za bajeti ya Serikali Kuu.

MTANZANIA MMOJA AJERUHIWA KWENYE SHAMBULIO LA AL-SHABAAB JIJINI NAIROBI

 
UBALOZI wa Tanzania, nchini Kenya umesema raia wake moja alijeruhiwa juzi wakati wapiganaji wa Kikundi cha Al Shababu walipoteka jengo la Westgate mjini Nairobi. Taarifa iliyotumwa na Ubalozi wa Tanzania jana, ilimtaja raia huyo kuwa ni Vedastus Nsanzugwanko ambaye ni Meneja katika Taasisi ya Kimataifa ya Child Protection, inayofadhiliwa na Shirika la Kuhudumia Watoto Ulimwenguni, (UNICEF).

Taarifa hiyo,ilisema Nsanzugwanko amejeruhiwa kwa risasi na magruneit katika miguu yake yote miwili na amelazwa hospitali ya Aga Khan.

“Anaendelea kupatiwa matibabu, huku hali yake inaendelea vizuri, hata hivyo ubalozi unaendelea kufuatilia kwa lengo la kupata taarifa zaidi endapo kutakuwapo na Watanzania wengine katika tukio hilo,

Majeruhi huyu bado yuko hospitali na hatujaweza kumpiga picha,” ilisema taarifa hiyo,”ilisema taarifa hiyo.

Katika hatua nyingine, Ubalozi wa Tanzania nchini Kenya kwa kushirikiana na Uongozi wa Chama cha Watanzania wanaoishi Kenya (TWA), umeandaa utaratibu maalumu utakaowezesha Watanzania waishio Kenya kujitokeza kwa ajili ya kutoa damu.

Wakati huo huo, Umoja wa Mabalozi wa Nchi za Afrika ulikutana na uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje kwa lengo la kuwasilisha salamu za rambirambi kutoka kwa wakuu wa nchi zao. Taarifa zinasema wajumbe hao walikutana na Rais Uhuru Kenyatta na kutoa

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...