Friday, September 27, 2013

TAARIFA YA JKT KWA VIJANA WANAOTAKA KUAHIRISHA MAFUNZO

JKT1_4a456.jpg
Vijana waliochaguliwa kujiunga na JKT awamu ya tatu na pia wamechaguliwa kujiunga na vyuo vya elimu, wambao wanataka kuahirisha mkataba wa JKT, wanatakiwa kuandika barua Makao Makuu ya JKT kuomba kuahirisha mkataba wa JKT.
1. Barua binafsi kuomba kuahirisha mkataba iwe na picha yake.
2. Nakala ya barua ya kucahguilwa kujiunga na chuo (Joining instructions)
3. Barua hiyo ieleze kuwa utajiunga na JKT baada ya kuhitimu masomo.
4. Barua zao zifike Makao Makuu ya JKT kabla ya tarehe 02 Kotoba, 2013.
ANGALIZO
Kujiunga na JKT kwa mujibu wa sheria ni lazima. Hivyo ni wajibu wa kila mhitimu kuhudhuria mafunzo hayo.
Agizo hili limetolewa na Jeshi la Kujenga Tafia, Makao Makuu.
---
Imetolewa kwenye tovuti: http://jkt.go.tz/mkataba-jkt.html

Source: http://www.wavuti.com/#ixzz2g4C18z5v

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...