Tuesday, August 20, 2013

VIGOGO WAJUMUISHWA KESI YA LEMA....!!!

Mkuu wa Chuo cha Uhasibu cha Arusha, John Nanyaro na Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Arusha, Gillis Mroto, leo wanaanza kutoa ushahidi katika kesi ya tuhuma za uchochezi inayomkabili Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema. 
Mashahidi wengine katika kesi hiyo ni, Mkaguzi wa Polisi Bernard Nyambanyana na mwenzake aliyetajwa kwa jina moja la Jane.

Hali kadhalika PC Godfrey na Joachim Mahanyu . Wakili wa Serikali, Elinenya Njiro, alitaja mashahidi wengine watakaotoa ushahidi wao mahakamani kuwa Faraji Mnepe, Benjamin Simkanga na Naibu Hamidu, wote kutoka Chuo cha Uhasibu.

SHOMARY KAPOMBE KUJIUNGA NA AS CANNES YA UFARANSA

Hatimaye beki wa kimataifa wa klabu ya Simba na timu ya taifa ya Tanzania Shomary Kapombe amefuzu majaribio aliyokuwa akifanya barani ulaya kwa kufanikiwa kujiunga na klabu ya AS Cannes ya Ufaransa.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka mwandishi wa BBC - Abdul Mohamed ni kwamba Shomary Kapombe amefuzu majaribio hayo na sasa zimebakia taratibu tu za uhamisho ili ajiunge rasmi na timu hiyo ya AS Cannes inayoshiriki kwenye ligi daraja la nne nchini Ufaransa.

Kapombe aliondoka nchini takribani mwezi mmoja uliopita na kwenda barani ulaya kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa.

Mtandao huu upo katika kujaribu kufanya mawasiliano na uongozi wa Simba ili kupata taarifa rasmi juu ya usajili huu wa Shomary Kapombe.Credits: Shaffih Dauda Blog  

KESI YA MWANARIADHA OSCAR PISTORIUS ALIYEMUUA MPENZI WAKE KWA KUMPIGA RISASI ITAANZA MACHI MWAKANI....!!!


Mwanariadha mlemavu wa Afrika Kusini Oscar Pistorius amefika mahakamani ambapo ameshtakiwa kwa mauaji ya mpenzi wake.
Mahakama imemsomea makosa ya kumuua,Reeva Steenkamp. Kesi dhidi ya mwanariadha huyo itaanza Mwezi Machi mwaka ujao.

Oscar Pistorius alizingirwa na umati mkubwa wa waandishi wa habari alipofika mahakamani mji wa Pretoria. Akiandamana na jamaa wake mwanariadha huyo alifanya maombi maalum. Punde baada ya kusomewa makosa ya kumuua Mwanamitindo Reeva Steenkamp, Oscar alionekana kupatwa na huzuni kubwa.

Monday, August 19, 2013

CHADEMA WAVAANA NA POLISI KWENYE MAANDAMANO YAO...!!!


Maandamano ya chama cha CHADEMA yaliyokua yanafanyika huko Mwanza yamegeuka vurugu baada ya wandamanaji kuanza kupambana na polisi.

CHADEMA walikua wakiandamana katika kushinikiza Meya wa Ilemela Henry Matata aachie ngazi kwani hana sifa zakua meya, baada ya kuvuliwa uanachama na chama hicho.

Katika picha zilizokirushwa kupitia televisheni ya Barmedas Tv ya Mwanza,  barabara zimeonekana zikiwa zimefungwa kwa mawe na miti, huku  katika maeneo mengine uchafu ukiwa umejazwa barabarani na matairi kuchomwa.

katika mtaa wa Mission waandamanaji wamefunga barabara kwa uchafu uliokua katika dampo moja kando ya barabara hiyo.

Maandamoano hayo yalikua yamalizikie viwanja vya furahisha ambapo viongozi wa chadema walikua wahutubie.

Chanzo cha vurugu hizo hakijafahamika, ikizingatiwa CHADEMA walikua na kibali cha kufanya maandamano hayo.

Hivi sasa polisi wametanda mitaani katika kudhibiti vurugu hizo na hali inaonekana kutengamaa.

PONDA AFIKISHWA MAHAKAMANI MOROGORO HII LEO ASOMEWA MASHITAKA 3.


Sheikh Issa Ponda Akiwa mahakamani mkoani Morogoro asubuhi ya leo Sheikh Ponda Amesomewa Mashtaka Matatu katika Mahakama ya mkoa wa Morogoro Likiwemo la uchochezi alilolitoa Kwenye  Mkutano wa Hadhara Tarehe 10 mwezi huu Ambapo Inadaiwa alisema kwamba ''Ndugu waislamu Msikubali uundwaji wa kamati za ulinzi na usalama za Misikiti kwani kamati hizo zimeundwa na Bakwata ambao ni vibaraka wa Serikali ''katika viwanja vya shule ya kiwanja cha ndege Mkoani Morogoro.

VIONGOZI DECI JELA MIAKA 3 AU FAINI MILIONI 21 KILA MMOJA

SHERIA imewatia hatiani viongozi 4 kati ya 5 wa kampuni ya Development Entrepreneurship for Community Initiative (DECI) iliyokuwa ikijihusisha na shughuli za kuvuna na kupanda fedha nchini kinyume cha sheria.

Hayo yalibainika hii leo wakati wa hukumu ya kesi hiyo iliyodumu kwa miaka kadhaa huku mtuhumiwa mmoja katika kesi hiyo akiachiw huru baada ya upande wa mashitaka kushindwa kuthibitisha makosa yake.

Akisoma hukumu hiyo iliyo andikwa na Hakimu Mwenzake, Stuart Sanga, Hakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, Aloyce Katemana alitafsiri sheria kadhaa zilizowatia hatiani watuhumiwa hao.


Vigogo hao waliotiwa hatiani ni pamoja na Jackson Sifael Mtares, Dominick Kigendi, Timotheo Saigaran ole Loitginye, Samwel Sifael Mtares,Samwel Mtalis huku sheria ikimwachia huru Arbogast Francis Kipilimba baada ya kushindwa kumtia hatiani.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU AUGUST 19, 2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.

SIRI ZA TRAFIKI FEKI ZAFICHUKA, YADAIWA ALIANZA KAZI MKOANI SINGIDA,AKAJIPA UHAMISHO WA KIKAZI HADI DAR...!!!


SIKU chache baada ya kukamatwa kwa askari 'feki' wa Usalama Barabarani mwenye cheo cha Sajini, akifanya kazi ya kuongoza magari eneo ya Tabata Kinyerezi, Dar es Salaam, mambo mapya yamezidi kubainika juu ya sababu za mtu huyo kujiingiza katika kazi hiyo bila kutambuliwa na Jeshi la Polisi.


Habari zilizolifikia gazeti hili kutoka vyanzo vya kuaminika, zinasema trafiki huyo 'feki', ambaye inadaiwa jina lake halisi ni James Juma Hussein (45), mkazi wa Kimara Matangini, alianzia kazi hiyo mkoani Singida kabla ya kujipa uhamisho wa kikazi kwenda Dar es Salaam.


Chanzo chetu kilieleza kuwa, trafiki huyo alikuwa na shemeji yake aliyeitwa Shaban ambaye aliajiriwa na Jeshi la Polisi Kitengo cha Usalama Barabarani aliyekuwa akifanyia kazi mkoani Tabora.Vyanzo vyetu viliongeza kuwa, baada ya shemeji yake kufariki mkoani Tabora, trafiki huyo alipata mwanya wa kuchukua nguo za kazini alizokuwa akizitumia shemeji yake.

MECHI YA NGAO YA JAMII YA YANGA NA AZAM YAINGIZA MIL 208

 
Mechi hiyo ya Ngao ya Jamii (Community Shield) kuashiria ufunguzi wa msimu mpya wa 2013/2014 iliyochezwa jana (Agosti 17 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 208,107,000. Washabiki 26,084 walikata tiketi kushuhudia mechi hiyo ambayo ilimalizika kwa Yanga kushinda Azam bao 1-0.


Mgawanyo wa mapato ya mechi hiyo uliokuwa kama ifuatavyo; asilimia 18 ya Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) sh. 31,745,135.59, asilimia 10 ya mchango wa kusaidia jamii sh. 20,810,700, gharama ya tiketi sh. 7,309,866.


Uwanja sh. 22,236,194.76, gharama za mchezo sh. 13,341,716.86, Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 5,188,445.44, TFF sh. 13,341,716.86 na Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 6,670,858.43. Kila klabu imepata mgawo wa sh. 43,731,183.03.

MAJINA YA WALIOKOSEA KUJAZA FOMU ZA MIKOPO KWENDA CHUO KIKUU

Tizama majina kwa kubofya hapa chini 

1.NOTICE TO LOAN APPLICANTS TO CORRECT NECESSARY INFORMATION IN THEIR LOAN APPLICATIONS 
2.LOAN APPLICANTS TO CORRECT NECESSARY INFORMATION LIST 13: S - Z
3.LOAN APPLICANTS TO CORRECT NECESSARY INFORMATION LIST 12: S - S
4.LOAN APPLICANTS TO CORRECT NECESSARY INFORMATION LIST 11: N - S
5.LOAN APPLICANTS TO CORRECT NECESSARY INFORMATION LIST 10: M - N
6.LOAN APPLICANTS TO CORRECT NECESSARY INFORMATION LIST 9: M - M
7.LOAN APPLICANTS TO CORRECT NECESSARY INFORMATION LIST 8: M - M
8.LOAN APPLICANTS TO CORRECT NECESSARY INFORMATION LIST 7: M -M
9.LOAN APPLICANTS TO CORRECT NECESSARY INFORMATION LIST 6: L - M
10.LOAN APPLICANTS TO CORRECT NECESSARY INFORMATION LIST 5: K - L
11.LOAN APPLICANTS TO CORRECT NECESSARY INFORMATION LIST 4: J - K
12.LOAN APPLICANTS TO CORRECT NECESSARY INFORMATION LIST 3: F - J
13.LOAN APPLICANTS TO CORRECT NECESSARY INFORMATION LIST 2: B - F
14.NOTICE TO LOAN APPLICANTS TO CORRECT NECESSARY INFORMATION IN THEIR LOAN APPLICATIONS

DEREVA DALADALA AFUMANIWA GESTI AKIWA NA BINTIYE.....!!!


  Za mwizi 40:Temba baada ya kufumaniwa na mkewe akiwa na   bintiye.
 
 AMA kweli za mwizi arobaini! Mwanaume aliyetajwa kwa jina moja la Temba, mkazi wa Kimara-Rombo, Dar ambaye ni dereva wa daladala amefumaniwa laivu na mkewe akiwa gesti na binti yao wanayemlea.



NI MTEGO
Tukio hilo la aina yake lilijiri wiki iliyopita kwenye gesti hiyo iliyopo maeneo hayohayo ya Kimara-Rombo, majira ya saa 10:00 jioni ambapo Temba ambaye ni dereva wa daladala inayofanya safari kati ya Kimara na Kariakoo alinaswa kiulaini baada ya kuwekewa mtego.
OFM YATAARIFIWA
Baada ya mke wa Temba kuweka mambo vizuri aliitaarifu Oparesheni Fichua Maovu ya Global Publishers ambapo alihojiwa maswali muhimu kisha kutakiwa kuwajulisha polisi ili kuhakikisha kuna usalama wa kutosha.

                      Jamaa akipelekwa polisi na taulo lake
MWANZO WA YOTE HADI FUMANIZI
Kwa mujibu wa mke wa Temba, siku kadhaa nyuma aligundua kuwepo kwa mawasiliano ya kimapenzi kati ya mumewe na binti yao hivyo akalazimika kufanya uchunguzi wa kina.

BARCELONA YAFANYA KUFURU, YAIGONGA LEVANTE 7-0


Wachezaji wa Barcelona wakishangilia bao lao la kwanza lililofungwa na Alexis Sanchez dakika ya tatu.



Lionel Messi kama kawaida yake katupia mbili katika mechi ya leo.

Sunday, August 18, 2013

HII NDIO SABABU ILIYOFANYA AGNESS MASOGANGE KUSHTUKIWA NA POLISI NA HATIMAE KUKAMATWA NA UNGA AFRIKA KUSINI

Imebainika kwamba, Baada ya mpango madhubuti uliosukwa na wauza madawa ya kulevya hapa nchini wakishirikiana na baadhi ya watumishi wasio waaminifu wa uwanja wa ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es salaam wa kuwasafirisha watuhumiwa hao Agnes Gerald maarufu kwa jina la Masogange na mwenzake Melisa Edward, mtandao huo ulikuwa pia umejipanga vyema nchini Afrika Kusini kuwapitisha watuhumiwa hao bila kukamatwa.

Kilichomponza Masogange kukamwatwa ni pale alipochelewa kutoka uwanjani hapo kutokana na kujiremba, kitu ambacho kilisababisha kufanyiwa upekuzi wa dharura na askari ambaye hakujua kuhusu mpango huo. Tembelea http://jambotz8.blogspot.com/ kila siku.

Taarifa zinabainisha kwamba, baada ya Masogange na wenzake kufanikiwa kupita katika maeneo ya ukaguzi ya uwanja wa ndege wa Oliver Tambo nchini Afrika Kusini, mwenzake waliyesafiri pamoja aliyetajwa kwa jina la Mangunga alifanikiwa kuondoka uwanjani hapo na mabegi matatu yenye jumla ya kilo 60 za madawa hayo ya kulevya bila kujulikana.

"Kilichomponza Masogange ni pale alivyokuwa anajiremba baada ya kuruhusiwa kupita katika vizuizi vyote. Kiuhakika hakukamatwa katika mashine, bali ulikuwa ni ukaguzi usio rasmi uliofanywa na Polisi. Nadhani huyu Askari aliyewashika hakujua kuhusu mpango huo." kilisema chanzo kimoja ndani ya jeshi la Polisi kama ilivyonukuliwa katika gazeti la Tanzania Daima la Tarehe 17/8/2013

NEWS OF RWANDA WAANDIKA KUWA RAIS JAKAYA KIKWETE ANAWEZA KUWA NA ASILI YA GITEGA BURUNDI....!!!

Jakaya Kikwete, president of Tanzania, answers questions at a press conference at the United Nations (UN) building in Addis Ababa, Ethiopia, during the 12th African Union (AU) Summit.
Mtandao wa News of Rwanda juzi umeandika makala yenye kichwa cha habari, ‘If President Kikwete is Tanzanian, then most Rwandans being expelled are Tanzanians too’ na kuandika kile linachodai kuwa Rais Kikwete anaweza kuwa na asili ya Burundi.    Kwa mujibu wa wazee wa Burundi waliohojiwa na mtandao huo, umedai Rais Kikwete anaweza kuwa na asili ya Giteka, Burundi.

“They are of Rwandan origin, but speak Kirundi and solely prefer to be viewed as Burundians. By virtual of that country’s laws, they are indeed Burundians,” limeandika. So where did President Jakaya Mrisho Kikwete come from? There are no original residents of Bagamoyo in Tanzania where Kikwete’s parents are traced. Most people from that area are remnants of slaves who were seem as unfit for the market during the slave trade era.

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI AUGUST 18, 2013

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...