Tuesday, May 21, 2013

GODBLESS LEMA AUMBUKA....VODACOM WADAI KWAMBA ULE UJUMBE WA VITISHO HAUKUTOKA KWA MKUU WA MKOA


BARUA  TOKA  VODACOM

KAMANDA wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas, amedai kuwa uchunguzi wa awali kuhusu ujumbe unaodaiwa kutumwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, umetumwa na mtandao wa simu wa nje ya nchi.
Kamanda alisema katika ujumbe huo ambao Lema anadai uliandikwa na Mkuu wa Mkoa Mulongo na kutumwa kwenye simu yake Aprili mwaka huu, uchunguzi wa polisi umeonyesha kwamba haukutumwa kupitia kampuni moja wapo ya simu za mikononi ya hapa nchini.

BABA YAKE DULLY SYKES ANASWA AKIVUTA BANGI....!!

   Baba mzazi wa mwanamuziki wa bongo flava nchini Dully Sykes, Mzee Sykes pichani kama inavyoonekana akiwa na madawa haram ya kulevya aina ya bangi mkononi huku mbegu mbegu zikiwa zimedondoka chini.-----  

Baba mzazi wa mwanamuziki nyota wa bongo flava nchini Dully Sykes , Mzee Sykes hivi karibuni alinaswa  akichambua bangi mikononi mwake kwa ajili ya kuivuta.

Tukio hilo la aina yake lilitokea  nyumbani kwa msanii aliyefahamika kwa jina la Shebo, na kushuhudiwa na mwandishii wetu ambae alifanikiwa kumpiga picha mzee huyo akiwa na bangi mkononi mwake.

Mzee huyo akiwa hana shaka yoyote alionekana  akichambua bangi hiyo huku mbegu zake zikidondoka chini kama mchele ( picha ya juu)

Hata hivyo mzee huyo alishindwa kuendelea na zoezi la kuitayarisha bangi hiyo kutokana na kumtilia wasi wasi mwandishi akidhani ni afande.

Prof. Jay ajiunga CHADEMA Angalia PICHA


 


Msanii mkongwe wa muziki wa kizazi kipya maarufu kama Bongo Fleva, Joseph Haule (Prof. Jay) amejiunga rasmi leo na chama cha CHADEMA.

KUTOKA JAMII FORUM, SIRI YA KIFO CHA KAMANDA BARLOW ZAVUJA. KAMANDA MUNA ATAJWA.....!!!

Sasa ni wazi kwamba aliyekuwa kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza ameuawa na genge ndani ya Polisi akiwemo Kamanda Polisi anayejulikana kwa jina la Muna, gazeti la Jamhuri limeripoti katika ukurasa wa Mbele kabisa (Nimesoma kwenye website yao Deo Balile akilalamika gazeti kununuliwa kwa jumla na watu wasiojulikana)

Kuvuja kwa siri hiyo kumetokana na mmoja wa jambazi sugu ajulikanaye kwa jina la
Edward Malele kujisalimisha ktk vyombo vya ulinzi na kutoa siri zote.

Jambazi huyu aliombwa wa genge ndani ya polisi kushiriki katika mpango wa kumwua kamanda Barlow. Akakataa kwa kuwa aliwahi kumfahamu kwa karibu kamanda Barlow.

Baada ya kukataa kutekeleza agizo hilo baada ya siku chache alishtakiwa kwa kosa la ujambazi na kuswekwa Rumande.

" MATOKEO YA KIDATO CHA SITA".....SIFURI KIBAO ZAFUTWA KIMYA KIMYA


MPANGILIO wa alama mpya za kufaulu kwa wahitimu wa kidato cha sita waliohitimu mwaka jana, ambao matokeo ya mitihani yao yanaweza kutangazwa wakati wowote kuanzia sasa, unadaiwa kuzua aibu na kama si uamuzi uliotajwa bungeni wa matumizi ya alama za ufaulu za zamani, matokeo hayo yangeibua aibu kama ilivyojitokeza kwa kidato cha nne, 2012.

Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari kutoka Baraza la Taifa la Mitihani (NECTA) ambalo linaendelea kupanga matokeo hayo ya kidato cha sita kwa kuzingatia alama za zamani kama ambavyo taarifa ya awali ya Tume iliyoundwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, ilivyosomwa bungeni hivi karibuni, hali ingekuwa mbaya zaidi katika ufaulu kwa wanafunzi wa kidato cha sita kiasi cha kuweza kutishia uhai wa vyuo vikuu nchini kukosa wanafunzi wa kutosha.


“Hali ilikuwa mbaya sana kama alama za kufaulu zingeachwa zitumike zile mpya na si za zamani. Vyuo vikuu nchini visingeweza kupata wanafunzi wa kutosha.


 "Tatizo hapa si uwezo wa wanafunzi moja kwa moja katika kumudu mitihani bali ni kufanywa kwa mabadiliko ya alama bila kuwaandaa.

HII NDIO PRIVATE JET ATAKAYOKUWA AKIITUMIA MAKAMU WA RAISI WA KENYA RUTO


Full size bed ndani ya ndege hiyo
Huu ni mlango wakuingilia kwenye ndege hiyo
Breakfast and diner on board 

BIASHARA YA NGONO YASHAMIRI DODOMA..... MACHANGU WA DAR WAKIMBILIA HUKO



BIASHARA ya ngono katika mji wa Dodoma imeshika kasi kubwa ambapo imebainika kuwa wateja wakubwa ni watumishi wa serikali, wanasiasa na madereva.

Uchunguzi wetu  umebaini kuwa katika biashara hiyo kuna makundi mbalimbali yanayotofautiana kwa malipo ya biashara hiyo.
Wapo wanafunzi wa vyuo vikuu na wanawake ambao wamedai kuwa wanalazimika kufanya biashara hiyo kutokana na kubanwa na maisha, hususani katika marejesho ya mikopo wanaichukua kutoka katika taasisi mbalimbali ya kifedha.

Mmoja wa wafanyabiashara ya ngono (jina tunalo) bila kujua anaongea na nani, alieleza kuwa kwa sasa katika mji wa Dodoma kuna ushindani mkubwa wa biashara ya ngono kwani wanafunzi wa vyuo vikuu vya mjini hapa vimeteka soko hilo.

Alisema kutokana na ushindani huo kwa sasa kima cha chini ni sh 7,000 kwa mchepuo mmoja na sh 30,000 hadi 40,000 kwa kulala.

Mfanyabiashara huyo alieleza kuwa wateja wakubwa wa ngono ni wafanyakazi wa serikali, wanasiasa (wabunge), madereva pamoja na wafanyakazi wa benki.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE TAREHE 21.03.2013

DSC 0043 f478a

DSC 0047 b993f

DSC 0045 6ff67

Monday, May 20, 2013

BREAKING NEWZZZZZZZZZZZZZ : MSIGWA APEWA DHAMANA


MBUNGE WA CHADEMA IRINGA MCHUNGAJI MSIGWA HATIMAYE AMEPEWA DHAMANA SASA HIVI NA WENGINE 60 WALIOLETA VURUGU KUBWA SANA JANA MJINI IRINGA NA KUHARIBU MALI NYINGI SANA ZA WANANCHI

LOVENESS DIVA AMKEJELI TENA MH. ZITTO KABWE.....!!!



Baada  ya  kutangaza  kumpiga  chini  Mh.Zitto Kabwe, Loveness  Diva  ameamua  kumchokonoa  tena  kwa  kumkejeli  kuhusu  uamuzi  wake  wa kugombea Urais.....

Huu  ni ujumbe wake aliouweka instagram: 

 ".Ivi  kwa akili yako unadhani  unastahili  kweli  kuwa Rais mteule wa taifa  hili....??

"Usiponijibu nikaridhika, basi  ntakuchukulia  kama  mtu mwenye upeo finyu asiyejua alitendalo.."

MWENYEKITI WA CHADEMA AACHIA NGAZI......!!!

Lushoto. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wilayani Lushoto, mkoani Tanga, kimepata pigo baada ya Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Kwekitui, Miraji Kassim kujiuzulu, kufuatia kile alichokielezea kuwa ni kukosa ushirikiano kutoka kwa viongozi wenzie ngazi ya kijiji ambao wote ni wa CCM.
Mwenyekiti huyo ambaye alichaguliwa Aprili 27 mwaka huu katika uchaguzi mdogo, aliwashangaza wafuasi wake baada ya Kaimu Mtendaji wa kijiji hicho Athumani Kibiriti, kusoma baraua ya kujiuzulu kwake katika mkutano wa hadhara.
Mkutano huo uliitishwa na Mbunge wa Bumbuli ambaye pia ni Naibu Waziri wa Sayansi na Teklonojia, January Makamba.

YANGA: MRISHO NGASSA ATAMBULISHWA RASMI KUREJEA YANGA HII LEO



Katibu Mkuu wa Mabingwa wa Soka Tanzania Bara, Yanga ya jijini Dar es Salaam, Lawrence Mwalusako amemtambulisha rasmi Mshambuliaji Mrisho Khalfan Ngassa kuwa mchezaji mpya kujiunga na timu hiyo msimu ujao wa Ligi na michuano ya kimataifa.


Mrisho Ngassa ambaye anarudi Yanga baada ya kuihama timu hiyo kwa kutimkia kwa Matajiri wa Bongo, Azam FC na baade mwaka jana kuzwa Simba kwa Mkopo baada ya kutokea sintofahamu za kimaadili ndani ya Klabu yake hiyo.

Ngassa alienda kuichezea Simba msimu uliopita baada ya Klabu yake ya Azam kuchukizwa na kitendo chake cha kuibusu jezi ya Yanga wakati timu hizo zikicheza.

Ngassa anakuwa ni mchezaji wa kwanza kuatangazwa na klabu hiyo kumsajili muda mfupi tu baada ya kumalizika kwa Ligi Kuu na tayari ameshaanguka saini ya kuichezea klabu yake hiyo ambayo anamapenzi nayo makubwa hapa nchini kwa miaka 2.

MBUNGE MSIGWA AFIKISHWA MAHAKAMANI IRINGA MCHANA

 Mbunge  Msigwa akishuka katika gari ya  polisi baada ya kufikishwa mahakamani mchana  huu
 Mbunge  Msigwa akishuka katika gari hilo la polisi tayari kwa kuelekea  chumba cha mahakama
 Mbunge Msigwa akiwa na gazeti mkononi baada ya  kufikishwa mahakamani  leo
 Watuhumiwa  wengine wa vurugu  za machinga  na polisi  wakishuka katika karandinga la polisi

BUNGE LAAHIRISHWA BAADA YA KAULI NZITO TOKA UPINZANI


Bunge limeahirishwa baada ya kambi upinzani kudai kwamba serikali inatoa kucha, macho, meno na kuwaua waandishi wa habari. Hayo yalikuwepo ktk hotuba ya kambi ya upinzani iliyosomwa na msemaji wa wizara hiyo mheshimiwa Sugu. Kwa mujibu wa asasi ya kimataifa (jina limenitoka) inafuatilia haki na usalama wa waandishi wa habari, Tanzania iko ktk nchi kumi hatari kwa maisha ya waandishi wa habari ktk ripoti yake ya 2012.

Kama serikali haihusiki, kwa nini serikali isiunde tume ya kimahakama kama ilivyoombwa na chadema ili tujue ukweli? Ama waunde tume ya mahakama au wakubali tu kwamba wao ndo wanaohusika.

JK: MNAOTAKA URAIS 2015 ANZENI KUPITAPITA.


MWENYEKITI WA CCM DK JAKAYA KIKWETE.
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete amefungua milango kwa kuwataka baadhi ya watu ndani ya chama hicho wanaowania urais mwaka 2015 kuendelea na mchakato huo.
Rais Kikwete amewatahadharisha watu hao kuendesha kampeni zao kwa ustaarabu pasipo kuibua chuki wala kujenga makundi ambayo alisema ni hatari kwa kuwa yanaweza kukipasua chama.
Rais Kikwete aliyasema hayo katika mkutano ndani wa wabunge wa chama hicho uliofanyika jana katika ukumbi wa CCM (white house) mkoani hapa.
Mkutano huo ambao ulianza saa 3.00 asubuhi ulilenga kujadili masuala mbalimbali ya taifa ikiwamo utekelezaki wa ilani ya uchaguzi ya chama hicho katika majimbo na ahadi mbalimbali za viongozi wa taifa.
Chanzo chetu cha habari kutoka ndani ya ukumbi huo kilieleza kuwa Rais Kikwete aliwataka wanachama wenye nia ya kugombea urais kuwa na tahadhari na watu aliowaita vishoka wa siasa.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, Rais Kikwete alisema watu wa aina hiyo wana tabia ya kula huku na huku kwa kujiingiza katika kambi zaidi ya moja.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...