Friday, May 17, 2013

HUU NDIO WARAKA WA 'ANTIVIRUS' KWENDA KWA RUGE NA KUSAGA!! USOME HAPA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg5XHEZ5q85-oyxw_UcRunmglJKxUKAuUy-5b4mEa-6uNsPv06vU8iPGScZjMT2LvGytaQjZa33m5EEesulepmqHh2kcbWXXTtQc9hLq1KCfyiG4wBvq7hmj9A4A9AyS_vrJbtnwvM8u2k2/s1600/Anti+virus.jpgANTiVIRUS DAWA YA Virus WA Hiphop in Tanzania

WARAKA NAMBA 1(ZIPO 88) KILA WIKI UTAPATA WARAKA MMOJA

Ni wazi na dhahiri kabisa kesi iliofunguliwa mahakamani dhidi ya Lady JayDee haina maana yoyote isipokuwa ni hofu ya mafisadi wa muziki nchini (Kusaga na Ruge) kwa kuwa waraka wa pili ulikuwa utoke tar 15 may na mwingine tar 17 may mwaka huu wa 2013.

Hapa la kujiuliza ni juu ya interview ya Rugen a kinachoendelea sasa,eti suala limefika mahakamani,kweli Kusaga na Ruge mmeweza kuthibitisha nyie ni mafisadi na mnamuaibisha Rais Kikwete ambaye nina uhakika anajua kuwa nyie ndio kikwazo kikubwa na hata Bungeni alishawahi kuzungumza kuwa alitoa studio na pango kumbe tatizo sio hilo,tujiulize wote kuna nini wanachoficha hadi kumtafutia kesi raia mwema asie na hatia?

Tena anaejitafutia rizki ambayo wao wanapigana nayo kwa kumkandamiza?
Huku wakitumia mabavu wakilindwa na baadhi ya viongozi wa serikali na waandishi ambao majina yao mtayapata kupitia nyaraka zinazokuja (zipo 88) na huu ndio wa kwanza.
Nimesikitika sana na njia pekee ya kuufahamisha umma juu ya ufisadi huu wa Ruge Mutahaba na Joseph Kusaga ni kuyaanika yote ambayo jamii na Viongozi wa Serikali kama mlikuwa hamjui sasa ndio wakati muafaka wa kuwajua watu hawa ambao kila kukicha ni kuimarisha ufisadi wao na kujipendekeza kwa Viongozi sambamba na watoto wao (mtajua mpaka majina yao)

Tukio la bomu latua UN


Tukio la kutupwa bomu katika Kanisa Katoliki la Joseph Mfanyakazi, Arusha limetua katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UN) baada ya kuwasilishwa na Balozi wa Vatican UN, Askofu Mkuu Frances Chullikatt.
Askofu Chullikatt anakuwa kiongozi wa kwanza wa Vatican kutoa tamko kuhusiana na shambulizi hilo ambalo mmoja wa viongozi wake alikuwapo.
Bomu hilo lilirushwa katika kanisa hilo wakati likizinduliwa na Balozi wa Vatican nchini, Askofu Mkuu Francisco Padilla Mei 5, mwaka huu na kusababisha vifo vya watu watatu na
kujeruhi zaidi ya 50.

Wakati wa shambulizi hilo, Askofu Padilla na Askofu Mkuu wa Jimbo la Arusha, Josephat Lebulu walionusurika.

LINAH, BARNABA KUTUPIWA VILAGO THT?

Msanii Linah 
Barnaba
Na  Andrew Chale
KUELEKEA shoo maalumu ya Miaka 13, ya mwanamuziki nguli wa bongo fleva nchini na kiongozi wa bendi yenye msisimko mkubwa ya ‘Machozi Band’, Judith Wambura ‘Lady Jay Dee’ au Jide’  huenda kwa upande wa wasanii wa Nyumba ya Vipaji ya THT, Linah Sanga na Barnaba  mwaka huu ukawa mchungu kwao kufuatia kuwepo taarifa za kutimuliwa na uongozi wa juu. 
Kwa mujibu wa vyanzo kutoka kwa mtu wa karibu wa Linah kilieleza kuwa mpaka sasa msanii huyo hana raha na wala hajui ataanza vipi katika harakati zake za kimuziki hasa kufuatia hivi karibuni kukacha shoo ya nguli Lady Jay Dee kwa shinikizo kutoka kwa wakubwa zake. 
Hata hivyo, Linah inadaiwa uongozi wa juu umekaa kikao na hatua iliyofuatia kwenye kikao hicho ni kuwaondoa kabisa kwani huenda wakatia doa wasanii wenzao ndani ya kundi hilo.
“Juzi Lina,haikuwa kawaida yake maana hata alipopigiwa simu na ** kwa ajili ya hatua zingine alionekana kuw na hofu, na wala hakutaka kusikia ushauri wangu ambao nilikuwa nikimhusia kuwa aachane na mawazo hayo kwani jambo analoliwaza huenda likaisha na hata maamuzi yatakayotoka yatakuwa ni kawaida” kilieleza chanzo kutoka kwa mtu wakaribu wa Lina, amabaye hata hivyo alisema kuwa huenda ukweli wa jambo ukawa hadharani.

T.I.D NAE AJITOA KATIKA SHOW YA LADY JAYDEE, HIKI NDO ALICHOKISEMA.


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgoEWu1lllJh5WkHOymJ8BTvguRy_0NBr6aFmlmkY-F3UY9hJJWH3rLa9WK6OmqIBG3xsGAvlak8T4GhVKY_V-g83fwaedgdypfPbtJtmuhGikj0cm2wa5YA2f4nR3-UO5OdmZelF4GKa1p/s400/DSC05754.JPGShow ya miaka 13 katika muziki ya Lady Jaydee inazidi kupata pigo baada ya TID kuwa msanii mwingine latest kujitoa kwenye show hiyo.

401187_10150536949328749_793704636_n
Moja ya sababu anayosema TID ni kuwa ana mkataba mwingine wa show unaolipa zaidi.. Sababu ya pili ni kuwa hataki kuwa katikati ya ugomvi wowote.
Hivi ndivyo alivyoandika TID kwenye ukurasa wake wa Facebook.
“Three reason why i can’t do lady JIDE SHOW ………….No.1 I have better contract pays me better than.No.2 I really don’t want to be between anybody’s conflict ya kwangu yananishinda naona nieupushe shari…No.3 nataka kuoa muda wangu ndo huu ……………kama nimekukosea captein na madame kazeni but I have been thru same shit.”
Tayari Linah, Barnaba na Matonya wamejitoa kutumbuiza kwenye show hiyo.

MWANAMAMA HUYU AMEKUWA GUMZO KATIKA MJI WA MTWARA MTIZAME HAPA CHINI



 Pikipiki ilirukiwa fasta na Mwana mama huyu, wasio mfahamu wengi walimshangaa, alivaa Kofia ngumu kisha akapachika pochi yake anapotaka na kisha akaiwasha. Huu ni usafiri wake anaoumiliki na huutumia mara zote katika mishe mishe zake.

Safari ikaanza na gia ziilingizwa mama huyu ni maarufu sana Mjini Mtwara
  
Nilikuwa naona vumbi tu linatimka na masihara niliyodhani anafanya kumbe ndio alikuwa akiondoka na huo ndio usafiri wake.Picha na Father Kidevu

VUNJA MBAVU ZA WAZIRI MAGUFULI BUNGENI DODOMA


Waziri wa Ujenzi, Dk. John Pombe Magufuli.
Na Mohammed Kuyunga
WAZIRI wa Ujenzi, Dk. John Pombe Magufuli ndiye waziri namba moja hadi sasa kwa kulivunja mbavu Bunge la Bajeti linaloendelea mjini Dodoma kutokana na vichekesho vyake wakati alipokuwa akijibu hoja za wabunge mbalimbali hivi karibuni.

Magufuli ambaye wengi humuita ‘Jembe’ kutokana na uchapa kazi wake, alikuwa akiwasilisha bajeti ya wizara yake na kuomba kuidhinishiwa Shilingi Trilioni 1.22 kwa mwaka wa fedha 2013/14.

Mheshimiwa huyo alimudu kuwafanya waheshimiwa wacheke sana huku ujumbe ukifika tofauti na mawaziri wengine waliopita ambao hotuba zao zinadaiwa kuwa zilijaa ushawishi wa usingizi.

KIONGOZI WA CHADEMA ATUHUMIWA KUMLAZIMISHA KUTOA MIMBA

"Fridah Kerubo mwanafunzi wa chuo cha MDU Rohtaki India anayesoma masters ya Sheria yupo tayari kutoa ushuhuda jinsi Mtanzania Ben Saanane alivyompa Mimba na kisha baadae kumshawishi kuitoa la sivyo angemuonyesha kila rangi na kisha baadae kwenda uinereza.
Pia yupo Sally Mukhanji ambaye yupo Tanzania sasa hivi amemaliza kutupa ushuhuda jinsi Ben maarufu kama HR yaani Hit and Runalivyokua akifanya biashara ya Dola Fake,na Euro akiwa New Delh India. Picha hiyo ya wadada wa pili ambaye alipiga na Ben ambaye mkono ndiyo unaonekana ameitoa pamoja na nyingine nitazileta soon. Huyu anajua mengi yaliyofichwa . Sasa kama chadema imejaza watu kama akina Lema aliyebaka, Mnyika aliyekutwa na mwanafunzi quality plaza na mbowe aliyempa mimba mbunge wa viti maalumu kama alivyoripoti kamaradi Mtela Mwampamba unategemea nini. Hawa Wakenya wanalalamika na nitashangaa kama kuna mwanaume wa kitanzania atafurahi kuchafuliwa image yake kama ben alivyoharibu sifa ya wanaume wa kitanzania.Turekebishe tabia za wanasiasa wetu. Matusi ya vijana wa Chadema hayanisumbui maana kama mnapanga kuteka watu hakuna msiloshindwa
KWA HISANI YA Eddah Kishimba

MAGAZETI YA LEO IJUMAA TAREHE 17.05.2013

DSC 0230 cd07d

DSC 0236 d1506

MBUNGE MSIGWA AMTAKA KINANA KWENDA MAHAKAMANI KESHO



Mbunge  wa  jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa amewataka  wafanyabiashara  ndogo ndogo (machinga ) mjini Iringa  kuendelea  kufanya kazi katika  eneo la Mashine  tatu  bila  kufanya  vurugu  zozote kwa  wale wanaozuia kufanya  hivyo. 
Akizungumzia  suala la Machinga  kuendelea  kunyanyasika  mbunge Msigwa amesema  kuwa tayari suala  hilo ameanza  kulipigania bungeni  kwa waziri  mwenye dhamana  hivyo kamwe  machinga  Iringa  wasikubali  kunyanyasika . 
Aidha mbunge  huyo amemtaka  katibu mkuu  wa chama  cha mapinduzi (CCM) Bw  Kinana  kutosubiri muda  wa  siku  21 alizozitoa  kumfikisha mahakamani kuwa  yupo tayari  kwenda mahakamani hata kesho. 
Mbunge Msigwa amesema kuwa katika  ukweli kama  hata  kuwa tayari kumwogopa mtu na kuwa siku  zote atasimama katika  ukweli katika  kupigania maslahi ya Taifa  hiliMbunge  Msigwa amesema  kuwa hatua ya katibu mkuu  wa CCM kukimbilia katika  vyombo  vya habari  kutishia  kumfikisha mahakamani bila yeye mhusika  kupelekewa taarifa  ni  sawa na kumwogopa na  hivyo suala la Kinana kwenda Mahakamani  si  sawa ni  kumtishia nyau mtu mzima. 
Kwani  alisema  kuwa  Chadema  ina  mawakili  waliojitosheleza na  kuwa hawatanyamaza kusema  ukweli kwa  kuogopa vitisho vyovyote .
Mbunge  wa  jimbo la Iringa mjini akiwahutubia umati mkubwa wa wananchi  wa  jimbo hilo jioni hii katika eneo la stendi kuu ya mabasi ya mikoani.

MSANII WA CAMP MULLA ALIYEWAHI PIGA CHAFU ATIMULIWA NDANI YA KUNDI HILO


 

Habari zilizosambaa katika mitaa ya area code +254 zinadai kuwa kundi la hip hop lenye mafanikio makubwa nchini Kenya, Camp Mulla limempiga chini first lady na lead singer wa kundi hilo, Miss Karun  kutokana  na  skendo  zinazomkabili
Kwa mujibu wa maneno ya mtaani  inasemekana nafasi ya Miss Karun itachukuliwa na mrembo mwingine aitwaye Tiri, ambaye ni mpenzi wa member na producer wa kundi hilo K’cous
Miss Karun
Siku chache zilizopita kulizuka uvumi wa uwezekano wa members wa kundi hilo kuendelea na solo projects kwa kila mmoja wao ifikapo mwezi June 2013, kitu ambacho kinafanya tetesi za Miss Karun kuondolewa kundini kuchukuliwa kama dalili za kuvunjika kwa kundi hilo.
Camp Mulla wanategemea kupanda kwenye jukwaa moja na Snoop Lion katika concert ya MTV all stars Kwa Zulu-Natal hivi karibuni nchini Africa Kusini, show ambayo watampandisha mrithi wa Miss Karun kwa mara ya kwanza.

Thursday, May 16, 2013

BAADA YA FERGIE NA SCHOLES - DAVID BECKHAM NAE ATANGAZA KUSTAAFU SOKA MWISHONI MWA MSIMU HUU


Kustaafu ndio habari iliyoshika hatamu nchini Uingereza hiv sasa - wiki moja baada ya kustaafu kwa Sir Alex Ferguson, Paul Scholes, leo hiimchezaji wa zamani wa Man United na nahodha wa zamani wa EnglandDAVID BECKHAM ametangaza kutundika daluga. Beckham, 38, ameisadia Paris Saint-Germain kubeba kombe la  Ligue 1 kwa mara ya kwanza ndani miaka 19 mwishoni mwa wiki hii.
Pamoja na kupewa ofa ya mkataba mpya na timu hiyo ya Ufaransa, mkongwe huyo atastaafu baada ya mchezo wa mwisho tarehe 26 mwezi huuA.
Alisema: “Shukrani sana kwa PSG kwa kunipa nafasi ya kuendelea kuwa hapa lakini sasa nadhani ni muda sahihi wa kustaafu, kucheza kwenye soka la kiwango cha juu”
Becks alianza kucheza akiwa na Manchester United, akifunga mabao 85 katika mechi 394, kabla ya kuhamia Real Madrid.
Aliondoka Spain kwa uhamisho mnono kujiunga na LA Galaxy mwaka 2007 pia aliwahi kucheza kwa mkopo mara kadhaa kwenye klabu ya AC Milan wakati akiwa kwenye Major League Soccer. 

CCM YAWAPONGEZA VIONGOZI WA DINI


   Kamati Kuu ya Chama Cha Mapinduzi iliyokutana jana Mjini Dodoma imeipongeza serikali kwa hatua inayoendelea kuchukua katika kuchunguza chanzo cha tukio la mlipuko wa Bomu uliotokea Kanisani Jijini Arusha.
Bomu hilo lilirushwa Mei Tano mwaka huu wakati wa uzinduzi wa Kanisa la Romani Katoliki la Mtakatifu Joseph Mfanyakazi Parokia ya Olisiti na kusababisha vifo vya watu watatu na majeruhi kadhaa.
Akizungumza leo Jijini Dar es salaam Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi NAPE NNAUYE ameeleza kuwa taarifa hiyo ya serikali iliwasilishwa jana katika kikao hicho na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Dokta EMMANUEL NCHIMBI .
Kufuatia tukio hilo, Kamati Kuu imelaani na imeitaka serikali kuharakisha uchunguzi pamoja na kuongeza kasi ya uchunguzi wa suala hilo sanjari na kutafuta mzizi wa matukio hayo pamoja na kutoa taarifa mara kwa mara kuhusu maendeleo ya uchunguzi wa tukio hilo.

AUNT LULU AAMUA KUACHANA NA MASHOGA....!!


MWIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Lulu Semagongo ‘Aunty Lulu’ amepigwa ‘stop’ kutembea na marafiki wanaodaiwa kuwa ni wanaume wenye vitendo vya kike ‘Kuku Watamu’.

Akizungumza na mwandishi  wetu, Aunty Lulu alisema baada ya kuandamwa na maneno juu ukaribu wake na wanaume hao, mama yake mzazi na mpenzi wake wa sasa ambaye hakutaka kumtaja, wamemzuia ‘kumpiga stop’ kumuona na watu hao.
  
“Sasa hivi ndugu zangu ndiyo wamekuwa marafiki zangu, sitembei kabisa na kuku watamu. Siwezi kumuudhi mume wangu mtarajiwa, mama na hata ndugu wengine, nimeamua kuachana nao,” alisema Aunty Lulu ambaye pia ni mtangazaji ‘deiwaka’.

KOCHA WA TAIFA STAR KIM ATAJA TIMU YAKUIKABILI MORROCO

kocha Mkuu wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Kim Poulsen ameongezewa mkataba wa miaka miwili, leo ametaja kikosi cha timu hiyo kitakachoingia kambini kujiandaa na mchezo dhidi ya Morocco mwezi ujao kuwania tiketi ya kucheza Kombe la Dunia mwakani.


Katika kikosi hicho, kocha huyo Mdenmark amemuorodhesha kipa wa Yanga, Ally Mustafa ‘Barthez’ pamoja na makipa wengine watatu, Juma Kaseja wa Simba SC, Mwadini Ally na Aishi Manula wa Azam.

Upande wa mabeki amewaita Erasto Nyoni, Aggrey Morris wa Azam, Kevin Yondan, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ wa Yanga SC, Shomary Kapombe wa Simba SC na Yahya Mudathir wa Azam.

Kwa viungo, Poulsen amewaita Haroun Chanongo, Mrisho Ngassa wa Simba SC, Simon Msuva, Frank Domayo, Athumani Iddi ‘Chuji’ wa Yanga SC, Salum Abubakar, Khamis Mcha ‘Vialli’ wa Azam FC na washambuliaji ni Mbwana Samatta, Thomas Ulimwengu wa TP Mazembe ya DRC, John Bocco wa Azam FC, Juma Luizio wa Mtibwa Sugar na Zahor Pazi wa JKT Ruvu.

UKAHABA WALIGUSA BUNGE


Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Kundi la Vijana Mkoa wa Arusha, Catherine Magige aliyeanzisha mjadala.
Spika wa Bunge, Anne Makinda.

BIASHARA ya ukahaba imeligusa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwani Jumanne iliyopita takribani dakika nane zilitumika kuijadili inavyoshamiri na namna ya kuitokomeza.
Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Kundi la Vijana Mkoa wa Arusha, Catherine Magige, ndiye aliyeanzisha mjadala asubuhi katika kipindi cha maswali na majibu, baada ya kumuuliza Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto kuhusu mpango wa serikali kudhibiti ukahaba.

Magige aliuliza kuhusu fikra za serikali juu ya mpango wa kupeleka muswada bungeni, kuhusu uundwaji wa sheria ya kudhibiti ukahaba nchini.
Swali hilo la Magige, lilikwenda sambamba na maelezo kuwa biashara ya ukahaba inavyoshamiri, inazidi kusababisha mmomonyoko mkubwa wa maadili.
Alisema, biashara hiyo vilevile ni kichocheo cha kushamiri kwa maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi, kuongezeka kwa watoto wa mitaani na kukua kwa uhalifu kwa sababu kuna uporaji hufanyika kwa kuwatumia hao wanaojiuza.
Akijibu swali hilo kwa niaba ya Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, Sophia Simba, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Angela Kairuki alisema serikali inajitahidi kuimaliza biashara ya ukahaba nchini.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...