Saturday, March 02, 2013

DStv REWARDS YAENDELEA KUIBUA MAMILIONEA: AHMED SALIM SALEH ASHINDA Tshs.5,000,000



Ahmed Salim Saleh, mshindi wa Tshs, 5,000,000 za DStv Rewards akiwa na uso wa furaha huku ameshikilia mfano wa hundi aliyokabidhiwa.
Katika muendelezo wa kampeni ya DStv Rewards kampuni ya MultiChoice Tanzania inayo furaha kumtangaza rasmi mshindi wake wa tatu. Mshindi huyo ni Ahmed Salim Saleh, mfanyakazi wa Access Bank ya jijini Dar-es-Salaam.   Kupitia droo ya DStv Rewards, MultiChoice Tanzania inaibua baadhi ya wateja wao kuwa “mamilionea” ambapo katika kila wiki mteja mmoja huibuka mshindi wa kitita cha Shilingi Milioni 5. (Tshs 5,000,000)
Meneja Masoko wa MultiChoice Tanzania, Furaha Samalu, akiwa na mshindi wa DStv Rewards kwa wiki ya tatu, Ahmed Salim Saleh, baada ya kumkabidhi mfano wa hundi ya kitita cha Tshs. 5,000,000 alichojishindia.
DStv Rewards ni sehemu ya kampeni maalum ya kampuni ya MultiChoice Tanzania kuwashukuru wateja wao kutokana na ushirikiano mkubwa inaoupata kutoka kwao.   Kampeni hiyo maalumu ilianza tarehe 5 February, 2013 na inaendelea mpaka tarehe 10 April, 2013. Wateja ambao wanakuwa na nafasi ya kuibuka “mamilionea” ni wale ambao hulipia akaunti zao za DStv kabla hazitajakatwa kwa kulipia kifurushi chochote kati ya DStv Access, DStv Family, DStv Compact, DStv Compact Plus na DStv Premium.
Mshindi wa DStv Rewards, Ahmed Salim Saleh, akisaidiwa na baadhi ya wafanyakazi wenzake kushangilia kwa kuibuka mshindi wa Tshs, 5,000,000 alizoshinda.

WANAO DAI KUWA LULU MICHAEL KAFANYIWA SHEREHE YA KUTOKA GEREZANI NI WAONGO NA WANAMPANGO WA KUMKWAMISHA KISHERIA..:...FAMILIA YA LULU YANENA



Kulipuka kwa habari kuwa staa wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amefanyiwa sherehe na kigogo baada ya kutoka Segerea, Dar kwa dhamana, familia yake imecharuka na kudai kuwa hakukuwa na jambo kama hilo wala haifikirii kufanya hivyo

Habari za uhakika zilidai kuwa Lulu ambaye anakabiliwa na kesi ya kumuua bila kukusudia msanii mwenzake, Steven Kanumba, mara baada ya kuachiwa kwa dhamana Januari 26, mwaka huu, kuliibuka minong’ono kutoka kwa marafiki zake mbalimbali walioelezwa kuwa walitaka kumfanyia pati lakini ndugu walikataa.

Ilielezwa kuwa licha ya ndugu hao kukataa kumfanyia sherehe ndugu yao (Lulu), bado kuna kikundi cha watu kiliendelea kueneza taarifa za kizushi kwamba lazima kuwe na sherehe ya kumpongeza baada ya kutoka gerezani.


Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana ndani ya familia ya Lulu zilieleza kuwa taarifa zilizosambaa mwishoni mwa wiki iliyopita kwamba alifanyiwa bonge la pati na kikundi hicho kama madai ya awali yalivyokuwa, hazikuwa na ukweli wowote na mbaya zaidi zililenga kumjengea Lulu mazingira magumu ya kisheria.


Akizungumza na mwandishi wetu kwa sharti la kutochorwa jina , dada wa Lulu alisema kuwa familia ilikerwa kupita maelezo na kuwepo kwa taarifa hizo huku akisisitiza kwamba hazina ukweli wowote.

“Sisi kama familia hatujamfanyia wala hatufikirii kumfanyia sherehe ya aina yoyote kwa ajili ya kumpongeza. Tunaomba ieleweke hivyo na hao wanaoeneza habari za uongo waache haraka, hatuzipendi,” alisema dada huyo.

HATIMAYE SERIKALI YAANZA KUJENGA KIWANDA CHA GESI MTWARA


Rais Jakaya Kikwete akiangalia shughuli za uzalishaji umeme hivi karibuni, baada ya vutanikuvute ya muda mrewfu Serikali imeamua kujenga kiwanda cha gesi mkoani Mtwara
                                                      ***********
 
HATIMAYE ujenzi wa kiwanda cha kusafisha gesi kabla ya kusafirishwa kwenda Dar es Salaam umeanza mkoani Mtwara.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi alisema jana kuwa ujenzi huo unaofanywa na Kampuni ya China Petroleum and Technology Development Co-operation (CPTDC), ambao awali, ulipaswa kuanza wiki iliyopita, umeanza juzi baada ya Serikali kufikia mwafaka na wananchi wa Kijiji cha Msimbati kinapojengwa.
“Mkuu wa Wilaya ya Mtwara (Wilman Ndile) na vijana wake walilazimika kufika Kijiji cha Msimbati, ambako wananchi walikuwa na mgogoro na watu wa Marine Park,” alisema Maswi.

KILIMANJARO MARATHON YAZINDULIWA

Maandalizi ya Mbio za Nyika za Kilimanjaro Maarufu kama Kilimanjaro Marathon 2013 yanafikia kiele hii leo na kesho ndio kivuvumbi na jasho wakati maelfu ya wanariadha na watu wa kawaida wakitimua vumbi katika mbio hizo zinazofanyika katiua mji wa Moshi mkoani Kilimanjaro.

Pichani ni baadhi ya wakimbiaji wakijiandikisha kwaajili ya kushiriki mbio hizo zitakazo fanyika Machi 3,2013 mjini Moshi na zitakuwa za makundi mbalimbali 42KM, 21KM na 5km Fun Run.
Makundi mbalimbali katika Jamiui nayo yanashiriki ikiwa ni pamoja na walemavu ambao pichani wakiwa katika banda la kujiandikishia.
Maofisa watakao simamia Mbio hizo Machi 3, 2013 wakiwa Uwanja wa Ushirika Mjini Moshi kuchukua vifaa.
Mbio za kujifurahisha kwa watoto na watu wazima zipo na hapa wakijiandikisha.
Baadhi ya wadhamini wakiwa tayari wamesha pamba mabanda yao ndani ya Uwanja wa Ushirika Mjini Moshi.
Mitaani napo Mabango ya Mbio hizo yamewekwa

Rais Obama awa miongoni mwa viongozi walioalikwa katika sherehe za kumuapisha rais mpya wa Kenya.


Rais Barrack Obama wa Marekani amekuwa miongoni mwa viongozi wakubwa wa dunia walioalikwa katika hafla ya kuapishwa kwa rais wa nne wa Kenya.
Mkuu wa Huduma za Jamii Francis Kimemia serikali imewaalika viongozi kama vile Waziri Mkuu wa Uingereza Bw. David Cameroon na Mkuu wa Mataifa ya umoja wa Ulaya.
Pia wamealikwa marais wa Jumuiya ya Nchi za Afrika Mashariki (EAC) ikiwa ni pamoja na rais Yoweri Museveni wa Uganda, Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania, rais Paul Kagame wa Rwanda na rais Pierre Nkurunziza wa Burundi.
Rais mpya wa Kenya  anatarajiwa kuapishwa kuchukua madaraka hapo Machi 3 mwaka huu, ikiwa ni wiki tatu baada ya wakenya kufanya uchaguzi.
 

Wafanyakazi Ikulu Waadhimisha Siku ya Mazingira Afrika kwa Kufanya Usafi wa Mazingira.


Naibu Katibu Mkuu Ikulu Mama Suzana Mlawi (mwenye blauzi ya kijani) na Mkurugenzi wa Huduma Ikulu Bw. Julius Mogore(mbele)   wakiongoza shughuli za usafi kuzunguka maeneo ya Ikulu jijini Dar es salaam leo Machi 1, 2013 katika kuadhimisha Siku ya Mazingira Afrika. Siku hiyo itaadhimishwa kitaifa siku ya Jumapili.


Picha zingine zinaonesha  Wafanyakazi wa kila kada Ikulu bila kujali nyadhifa zao  wanafanya kazi bega kwa bega kuhitimisha Siku ya Mazingira Afrika kwa kufanya usafi.(PICHA NA IKULU).

Rais Kikwete aongoza kikao cha baraza la Mawaziri leo jijini Dar.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongoza kikao  cha baraza la Mawaziri kilichofanyika Ikulu, Dar es salaam, leo Machi 1, 2013.(PICHA NA IKULU).
 

HUYU NDIYE MSANII MAARUFU ALIYEFARIKI NIGERIA,REST IN PEACE JUSTUS ESIRI



 

Last Wednesday turned out to be another sad day in the annals of the Nigerian entertainment industry. It was a day the industry recorded the death of yet another of its legendary actors, Mr. Justus Esiri. FLORENCE UDOH reports
The news about the death of veteran actor, Justus Esiri, threw the Nigerian entertainment industry into mourning last week, while still trying to recover from the shock of Lugard Onoyemu, Goldie Harvey and Collins Ifeanyi Chukwu's deaths.
The legendary actor and father of musician, Dr. Sid died on Tuesday night at the graceful age of 71.
Late Esiri, was born on November 20, 1942, in Oria-Abraka, Delta State. He attended Urhobo College and later went to Germany to study Engineering before he developed interest for the theatre.
Famous for his role in the popular television series "The Village Headmaster" in the 80's, Esiri rose to prominence playing the role of a teacher in that long-running drama on national television. He started his acting career in Germany and also worked for the Voice of Nigeria (VON) and German Service as a translator. He was a recipient of the honorary award, MON from the Federal government of Nigeria.

Polisi wanane mbaroni Afrika Kusini kwa kuhusishwa na kifo cha dereva taxi aliyeburuzwa kwenye gari ya polisi.


 

Maafisa wanane wa Polisi nchini Afrika Kusini wamekamatwa kuhusiana na kifo cha dereva taxi, ambaye anadaiwa kuburuzwa nyuma ya gari la polisi.
Uchunguzi ulianzishwa kufuatia kutolewa kwa picha ya video, iliyomuonyesha mwanaume mmoja akiwa amefungiwa pingu kwenye gari na kisha kuanza kubururwa katika barabara ya Daveyton, mashariki mwa mji wa Johannesburg.
Mtu huyo ametajwa kuwa ni Mido Macia, raia wa Msumbiji mwenye umri wa miaka 27, ambaye alifariki baadae akiwa katika kizuizini mwa polisi.
Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini ameliita tukio hilo kuwa la kutisha kabisa na lisilokubalika huku taafifa zikisema takriban maafisa wanane watafikishwa mahakamani Machi 4, 2013 kuhusiana na tukio hilo.

MWENDESHA MASHTAKA WA ICC YUPO TANZANIA

Rais Dk.Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama ya Kimataifa(ICC) Bibi Fatou Bensouda(Wapili kushoto) mara baada ya kufanya mazungumzo ikulu jijini Dar es Salaam leo.Wengine katika picha kushoto ni Mwanasheria Mkuu Jaji Frederick Werema,Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Bibi Angellah Kairuki(Wanne kushoto) na kulia Mwendesha Mashtaka mkuu wa Serikali Bwana Feleshi. (picha na Freddy Maro wa Ikulu)

PINDA AZINDUA TUME NA KUSEMA: TUSAIDIENI KUTAFUTA KIINI CHA KUSHUKA KWA ELIMU


Waziri Mkuu akihutubia leo asubuhi



Azindua tume ya watu 15, aipa wiki sita kukamilisha kazi


WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amezindua Tume maalum aliyoiunda ili ifanye uchunguzi wa
matokeo ya mtihani wa kidato cha nne yaliyotangazwa Februari 18, mwaka huu na
kuwataka wajumbe wa Tume hiyo watafute kiini cha mserereko wa kushuka kwa
ufaulu kuanzia mwaka 2010 hadi 2012.

Ametoa kauli hiyo leo asubuhi (Jumamosi, Machi 2, 2013) wakati akizungumza na wajumbe
wa Tume hiyo kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Magogoni, jijini Dar es
Salaam. Mkutano huo ulihudhuriwa pia na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,
Dk. Shukuru Kawambwa.

“Nimetafuta takwimu za tangu mwaka 2005, Serikali ya Awamu ya Nne ilipoingia madarakani na
kubaini kuwa tangu wakati huo hadi mwaka 2009 tulikuwa tukifanya vizuri, lakini
kuanzia mwaka 2010 hadi 2012 matokeo yamekuwa yakishuka sana,” aliwaambia
wajumbe wa Tume hiyo na waandishi wa habari waliohudhuria uzinduzi huo.

Alisema hali hiyo haikuwa kwenye shule za sekondari za umma (kata) peke yake bali hata
kwa shule za Serikali, za watu binafsi na kwenye seminari ambazo kwa miaka
mingi zimekuwa na sifa ya kufanya vizuri kuliko shule za kawaida.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI 2/3/2013





UNIVERSITY OF DAR ES SALAAM
Academic Staff Assembly


Utangulizi

Wapendwa waandishi wa habari. Tunaomba kupitia ninyi tuweze kuongea na watanzania wenzetu kuhusu hali ya amani ilivyo nchini mwetu kufuatia kila aina ya dalili ya watanzania kukosa uvumilivu wa kidini. Tunatambua kuwa serikali yetu imefanya mambo mazuri mengi tu nchini, hilo hatuna mashaka nalo; hata hivyo kama watanzania tunadhani kuna baadhi ya mambo hayaendi sawa. Hivyo basi, tunaomba kuchukua nafasi hii kuelezea wasiwasi wetu kuhusu migogoro hii ya kidini inayozidi kukua nchini.

Migogoro hii ilianza kuvuka kama moshi lakini sasa inaanza kulipuka na kusambaa zaidi. Tumeshuhudia uchomaji moto wa kanisa kule Mbagala, kumwagiwa tindikali shekhe mmoja kule Zanzibar na Shekhe mwingine kuuawawa, kuchomwa makanisa Zanzibar, kupigwa risasi viongozi wa kikristo kule Zanzibar na pia mgogoro wa kuchinja huko Geita ambako tumeshuhudia mchungaji mmoja akiuawa.

Mbali na hayo, kuna matukio kadhaa kwenye shule zetu za sekondari yakihusisha migogoro ya kidini kati ya wakristo na waislamu. Haya tumeshahudia yakitokea sekondari za Bagamoyo, Ndanda, Kibiti, Ilboru na kwingineko. Pia yapo malalamiko yasiyo rasmi kuhusu udini kwenye sehemu za kazi na kwenye taasisi mbalimbali za serikali. Wapo wanaodai kuwa baadhi ya taasisi binafsi, za kidini na hata za serikali zinazohudumia watanzania wengi zimekuwa zikiajiri wafanyakazi kwa misingi ya kupendelea dini fulani fulani. Jambo hili hata kama ni la kuzungumzwa tu, ni vema likafanyiwa kazi maana hisia hizi zikipanuka hujenga chuki na kusababisha watanzania wasielewane.
Read more

Friday, March 01, 2013

SOGGY DOGGY "HUNTER" AACHA KAZI UHURU FM,ATIMKIA KWA WANYARU-IRINGA

 


Msanii/Mtangazaji Soggy Doggy ameacha mzigo pande za redio Uhuru na leo rasmi ameondoka Dar es salaam nakwenda Iringa ambapo atakuwa akifanya kazi katika kituo kingine cha Redio kinachoenda kwa jina la Ebony Fm.Soggy Doggy ashawahi kufanya kazi katika vituo vya redio mbalimbali hapa nchini kama Arusha na Mwanza.

Mtendaji mkuu TAZARA Bw. Akashambatwa Mbikusita-Lewanika aachia ngazi.



Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) Bw. Akashambatwa Mbikusita-Lewanika,(Pichani) hatimaye ameachia ngazi baada ya kuendesha kampeni kali ya miezi kadhaa kutaka aendelee kuongoza Mamlaka hiyo kwa miaka mingine mitatu.
Hatua hiyo ya kuachia ngazi imekuja baada ya Bodi ya Wakurugenzi na Baraza la Mawaziri la Mamlaka hiyo kuonyesha dhahiri kutotaka Mzambia huyo aendelee na uongozi wa TAZARA kutokana na utendaji wake mbovu na uongozi mbaya uliowabagua wafanyakazi wa Mamlaka hiyo kwa misingi ya utaifa wao.
Habari za ndani za Mamlaka hiyo zimesema Bw. Akashambatwa ambaye kipindi chake cha uongozi kiliisha tarehe 22 Januari, 2013 kiliongezwa kwa maombi maalum ya Serikali ya Zambia kwamba Serikali hiyo ilihitaji muda mrefu kidogo kumpata mbadala wake, licha ya Serikali ya  Tanzania kutoridhishwa na utendaji wake.
Katika kikao chake cha tarehe 20 Februari, 2013 jijini Lusaka, Zambia, Baraza la Mawaziri lilijadili kwa siri na kwa kirefu suala la mtendaji Mkuu huyo ambaye inasemekana aliombewa tena na Serikali ya Zambia kipindi cha nyongeza, ombi ambalo inadaiwa lilipingwa vikali na ujumbe wa Serikali ya Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe.
Taarifa za uhakika ndani ya Wizara ya Uchukuzi zinasema Serikali ya Tanzania haikumtaka Mtendaji Mkuu huyo kwa sababu kadhaa zikiwemo :uwezo mdogo, ubadhirifu, kuchochea ubaguzi kati ya Watanzania na Wazambia, ukaidi na uchochezi. Inadaiwa kuwa Mtendaji Mkuu huyo alizuia kuanzishwa kwa mradi wa usafiri jijini Dar es Salaam bila sababu yoyote ya msngi na kuishia kusambaza taarifa za uongo na uchochezi Zambia na magazeti mbalimbali nchini.
Tarehe 25 Februari, 2013 Gazeti la kila siku la Zambia, Zambia Daily Mail, liliripoti tukio hilo la kuachia ngazi kwa kiongozi huyo ambaye anajulikana sana nchini Zambia kama mfanyabiashara na kiongozi wa kimila (chief),                                              
Gazeti hilo lilinukuu barua ya Bw. Akashambatwa ya tarehe  22 Februari, 2013 kwenda kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Ujenzi, Ugavi na Mawasiliano ya Zambia, akielezea kuwa hakuna faida ya kuomba kurefushwa kwa mkataba wake wakati vyombo vikuu vya uongozi vya TAZARA, Bodi ya Wakurugenzi na Baraza la Mawaziri, havionyeshi kumkubali.
Kuondoka kwa Bw. Akashambatwa kwenye uongozi wa TAZARA kunatarajiwa kupokewa na wafanyakazi wa TAZARA kwa nderemo na vifijo.

Google Waja na Miwani Inayopiga na Kurekodi Picha kwa Maelekezo.

Glass ya google
TEKNOLOJIA waliyotumia Google kutengeneza miwani ambayo ina uwezo wa kumpiga picha mtu au kurekodi bila muhusika kujua (google glass) sio mpya ila Kampuni ya Google ndio wakwanza kuja na teknoloji hiyo, ili kila mtu aweze kutumia na inakadiriwa huwenda bidhaa hii ikafanya vizuri sana katika mauzo.
Google glass ni rahisi sana kutumia, kama unataka kupiga picha unachotakiwa kusema ni “OK Glass, take a picture.” upo kwenye foleni unaona fujo unataka kuchukua video, mwambie Google Glass naye atakusaidia kuchukua video. Hii ndio kali, unataka kuwaonyesha ndugu na marafiki kitu unachokiona wakati huo huo? Google glass inafanya yote hayo, inakuja na kitu kama “Skype-style video chat”.
Umesafiri kwenda kuchukua mzigo China? Google glass itakusaidia kuchukua kutafsiri lugha. Umeenda Zanzibar kutembelea majengo ya kitalii na unabaki kushangaa shangaa, uliza Google glass na itakupa tour guide.
Google glass ni kifaa ambacho unaweza kutumia kurekodi video, kupiga picha, kutafuta habari katika Google, kutafsiri lugha, na unaweza fanya yote haya bila kutumia mikono yako (hands free). Tatizo ni kwamba, ukishavaa hiki kifaa kama miwani, watu hawajui kama unawarekodi kwenye video au vipi, na kwa wabongo walivyo wanavyojua kujihami kupigwa picha au kurekodiwa kwenye video, ukivaa Google glass unaweza tolewa baa.

 Kwa nchini Tanzania kifaa hiki ambacho kitakuwa na wastani wa bei ya sh. mil 2. 2 ($1500). Hata hivyo kifaa hicho kinachovaliwa kama miwani, sijui kama utaweza kutembea nacho hata hatua kumi kabla ya vibaka kukuvaa baada ya kujua thamani yake. Tusubiri Google wakiwezeshe kifaa hiki kiweze elewa kiswahili ndio na sisi tutakifaidi zaidi kwani hapa hamna kubonyeza bonyesha ni kuongea tu. Je ukipata Google glass utatumia kifaa hiki cha kisasa kufanyia nini? Acha maoni yako.
*Imeandaliwa na www.thehabari.com

MWANAMZIKI AMUITA SHABIKI JUKWAANI NA KUANDA "KUDENDEKA" NAYE



 Baada ya Mziki kukolea Msanii Akimuita shabiki stajini ili wacheze naye lakini mambo yalikolea zaidi pale walipojikuta wana kisiana stejini kitu kilichosababisha minongono kwa mashabiki



Udaku spesho.

Rais Kagame wa Rwanda akanusha kuwa na nia ya kugombea tena urais kwa awamu ya tatu.


 

Rais Paul Kagame wa Rwanda amesema hana mpango wa kugombea tena muhula wa tatu madarakani baada ya muhula wake wa sasa kumalizika mwaka 2017.
Akizungumza mjini Kigali, rais Kagame amevishutumu vyombo vya habari kuanzisha mjadala juu ya iwapo ataibadili katiba ili aweze kuwania muhula mwingine.
Mjadala huo ulifuatia hatua ya rais huyo mapema mwezi huu kuunda kamati katika chama chake, kutafakari mwelekeo wa nchi baada ya muda wake madarakani kumalizika.
Chama cha upinzani cha FDU-Inkingi, kimetoa tangazo kikilaani njama zozote za kuifanyia marekebisho katiba ili kuruhusu muhula wa tatu kwa rais.-DW

Balozi mpya wa Uingereza nchini Tanzania Mhe.Dianna Melrose awasilisha hati zake za utambulisho ikulu



Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akipokea hati za utambulisho kutoka kwa balozi mpya wa Uingereza nchini Tanzania Mhe.Dianna Melrose ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi (Picha na Freddy Maro)

Hivi ndivyo Chadema walivyotikisa Mbeya jana


Mapokezi makubwa ya Mh. Freeman Mbowe katika viwanja vya Rwanda Nzovwe jijini Mbeya.



 Burudani mbalimbali pia zilikuwepo





 




Mh. Mbowe pia alimtaka waziri wa Elimu na mafunzo  ya ufundi kujiudhuru pamoja na naibu waziri wa wizara hiyo kutokana na matokeo mabaya ya kidato cha nne  na kusema kuwa katika siku 14 alizozitoa zimebaki siku tatu za wao kuendelea kuwepo madarakani na kuongeza kuwa wasipofanya hivyo wataitisha maandamano ya nchi nzima kushinikiza waondolewe katika nafasi hizo. Mara baada ya kauli hiyo Mbowe aliwataka wananchi kuchangia fedha kwaajili ya wahanga siku ya maandamano ambapo zilichangishwa fedha kiasi cha sh. 3, 267, 550/=



 

Wakichangisha fedha kwaajili ya wahanga wa maandamano yatakayofanyika pindi mawaziri wataposhindwa kujiudhuru picha ya kwanza ni Mh. Sirinde, inayofuata ni Mh. Msingwa na ya mwisho ni Mh. Mbowe.

 

Picha na Keny Pino

JOKETI KUPAMBA UZINDUZI KAMPENI YA UNYANYASAJI




Na Mwandishi wetu

MWANAMITINDO nyota nchini, Joketi Mwegelo, anatarajiwa kunogesha uzinduzi wa kampeni ya kupinga unyanyasaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto kike, unaotarajiwa kufanyika keshokutwa, ambapo shughuli mbalimbali na mada zitatolewa.


Joketi, ambaye anawika katika tasnia mbalimbali nchini  ikiwemo urembo, mitindo, muziki na filamu, atashiriki kwenye uzinduzi wa kampeni hiyo ijulikanayo kama Okoa Mtoto wa Kike Tanzania utakaofanyika katika Kata ya Nyamongo wilayani Tarime, Mara.


Taarifa ya Mkurugenzi wa Kampuni ya Nyumbani Kwanza Media Group iliyoandaa kampeni hiyo, Mossy Magere, imesema kuwa maandalizi yote muhimu yamekamilika na Joketi atawasili wilayani Tarime kesho tayari kwa kushiriki na atatoa mada ya masuala ya ujasiriamali kwa washiriki wa tamasha hilo linalosubiriwa kwa hamu kubwa.


Mossy alisema kuwa mbali na Joketi, wasanii mbalimbali watashiriki kutoa burudani wakiwemo wasanii nyota wa bongo fleva na wale wa asili wanaotamba mkoani Mara.


'Maandalizi yote ya msingi yamekamilika na kinachosubiriwa ni muda wa uzinduzi ufike, Joketi anatarajiwa kuwasili hapa kesho tayari kwa kushiriki nasi. Atapata fursa ya kutoa mafunzo na mbinu

za kimaisha kwa washiriki ambao wengi ni wanafunzi wa shule mbalimbali wilayani hapa,' alisema Mossy.


Kampeni hiyo ambayo itadumu kwa kipindi cha miezi sita, itazinduliwa rasmi keshokutwa na Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudentia Kabaka, ambaye ameshirikishwa kwa karibu na Kampuni ya Nyumbani Kwanza.
Alisema mchakato wa uundwaji wa klabu za wapinga unyanyasaji  katika shule mbalimbali za sekondari wilayani Tarime ambapo kampeni hiyo inaanzia umekamilika na wanafunzi wamevutiwa na kujiunga kwa wingi kwenye klabu hizo ambazo zitakuwa kichocheo cha kuendeleza kampeni hiyo.


Mossy aliongeza kuwa, uundwaji wa klabu hizo unalenga kukiwezesha kizazi cha sasa na kijacho kuwa mstari wa mbele kukataa vitendo vya unyanyasaji.


“Kila jambo jema huanzia ngazi za chini, kwa sasa tunaendelea kuunda klabu za wapinga unyanyasaji ambazo zitakuwa zikipewa mafunzo na mbinu mbalimbali ili kuwajenga kufahamu madhara wakiwa wangali  wadogo shuleni.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...