
Wakati akizindua sanamu hiyo jana,
Rais Zuma alisema kwamba sanamu nyingi za Mandela zinamuonyesha
akinyoosha mkono wake mmoja juu kama ishara ya mapambano iliyokuwa
ikitumiwa na Chama cha ANC.
Lakini, ishara ya kukumbatia iliyokuwa
ikitumika katika sanamu hii ni tofauti, kwasababu inamuonyesha Madiba
akikumbatia nchi nzima na watu wake wote bila kujali rangi, itikadi wala
tabaka. Zuma aliizindua sanamu hiyo muda mfupi baada ya kumalizika kwa
mazishi ya kiongozi huyo yaliyoshuhudiwa na umati mkubwa watu
mbalimbali, wakiwamo viongozi wa nchi tofauti yaliyofanyika katika
Kijiji cha Qunu.







NCHINI
Afrika Kusini, hakuna eneo la kivutio cha kitalii linalotembelewa na
wageni wengi kama Kisiwa cha Robben. Umaarufu wa eneo hili umekuwa
ukiongezeka mwaka mpaka mwaka.

















