Uamuzi na msimamo wa Japan umetangazwa
jana jijini Dar es Salaam na Waziri wa Uchumi, Biashara na Viwanda wa
nchi hiyo, Toshimistu Motegi alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais
Jakaya Kikwete, Ikulu.
Taarifa ya Ikulu iliyosambazwa na
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, ilimnukuu Motegi akisema: "Kwa kuanzia
kampuni mbili za Honda na Panasonic zimekubali kujenga viwanda nchini,
kimoja kwa ajili ya kutengeneza pikipiki za Honda na kingine kwa ajili
ya kutengeneza vifaa vya umeme."
Akaweka msisitizo: "Huu ni mwanzo tu
Mheshimiwa Rais (Kikwete) kwa sababu kama nilivyosema kuwa tunataka
Tanzania kuwa nchi ya mfano ya uwekezaji wa Japan katika eneo hili la
dunia, na namna hiyo kwa pamoja tutakuwa tumeshirikiana katika kuongeza
ajira kwa wananchi wa Tanzania."
Monday, August 12, 2013
SHEIKH PONDA NA UAMSHO WAHUSISHWA NA SHAMBULIO LA TINDIKALI, ZANZIBAR

Gazeti la kila siku la Telegraph la hapa Uingereza linaripoti kuwa baadhi ya viongozi wa dini ya Kiislam visiwani Zanzibar wanaamini kuwa shambulio la tindikali dhidi ya mabinti wawili wa Kiingereza, Kirstie Trup na Katie Gee lilifanywa na wafuasi wa kikundi cha UAMSHO, ambacho kinataka Zanzibar ijitenge na Tanzania Bara na kisha kuanzisha sheria kali za Kiislam.
Huko nyuma kumeshatokea mashambulizi dhidi ya viongozi wa dini ya
Kiislam na Kikristo, ikiwa ni pamoja na mashambulio ya tindikali na
mauaji.
"Ofkoz, itakuwa kazi ya Uamsho," alinukuliwa Sheikh Fadhil Soraga,
aliyeshambuliwa kwa tindikali Novemba mwaka jana, na anaamini wahusika
katika tukio hilo dhidi yake walikuwa UAMSHO.
Wiki mbili zilizopita, vipeperushi vya vyenye wito mkali wa uchochezi
dhidi ya Wakristo vilisambazwa sehemu mbalimbali huo Zanzibar, tukio
linalohusishwa na harakati za UAMSHO.
"Siku 10 tu zilizopita, walikuwa wanasema wanaandaa kitu kikubwa. Tukio
hili, ambalo Waislamu wote twapaswa kulilaani, ni kazi ya kundi hilo
(UAMSHO)," alisisitiza Sheikh Soraga.
MWANAUME AFIA GESTI AKIFANYA MAPENZI NA MPENZI WAKE JIJINI DAR....!!!
MFANYABIASHARA wa sokoni Kariakoo jijini Dar ambaye pia ni mkazi wa Kigogo Flesh, Hamad Kiponda (46), amefia nyumba ya kulala wageni akiwa na mpenzi wake Latifa Saidi (25).
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Marietha Minangi alisema tukio hilo lilitokea juzi saa saba mchana katika nyumba hiyo iitwayo Sansiro iliyoko Kiwalani kwa Gude.
Alisema kuwa kutokana na tukio hilo, Latifa alitoa taarifa polisi kwamba mpenzi wake aliishiwa na nguvu ghafla na kuanza kutokwa povu mdomoni wakati wakifanya mapenzi. Minangi alieleza kuwa mtoa taarifa huyo aliomba msaada kwa wahudumu wa gesti hiyo, lakini Kiponda alifariki papo hapo kabla ya kupelekwa hospitali.
Chanzo cha kifo chake bado hakijafahamika, wakati mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa uchunguzi zaidi huku Latifa akishikiliwa kwa kuhojiwa.
Wakati huo huo, moto umezuka ghafla katika nyumba ya Matiku Nestori (43) mkazi wa Tuamoyo Kigamboni, yenye vyumba sita na kuteketeza vyumba vinne pamoja na mali zote zilizokuwemo ndani ambazo bado thamani yake haijajulikana. Kwa mujibu wa Kamanda Minangi tukio hilo lilitokea juzi saa nane mchana na chanzo cha moto huo inasadikiwa ni hitilafu ya umeme iliyosababisha moto kuanzia kwenye nguzo.
Alisema kuwa kutokana na tukio hilo, Latifa alitoa taarifa polisi kwamba mpenzi wake aliishiwa na nguvu ghafla na kuanza kutokwa povu mdomoni wakati wakifanya mapenzi. Minangi alieleza kuwa mtoa taarifa huyo aliomba msaada kwa wahudumu wa gesti hiyo, lakini Kiponda alifariki papo hapo kabla ya kupelekwa hospitali.
Chanzo cha kifo chake bado hakijafahamika, wakati mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa uchunguzi zaidi huku Latifa akishikiliwa kwa kuhojiwa.
Wakati huo huo, moto umezuka ghafla katika nyumba ya Matiku Nestori (43) mkazi wa Tuamoyo Kigamboni, yenye vyumba sita na kuteketeza vyumba vinne pamoja na mali zote zilizokuwemo ndani ambazo bado thamani yake haijajulikana. Kwa mujibu wa Kamanda Minangi tukio hilo lilitokea juzi saa nane mchana na chanzo cha moto huo inasadikiwa ni hitilafu ya umeme iliyosababisha moto kuanzia kwenye nguzo.
MAN UNITED WAIBUKA VINARA WA NGAO YA HISANI BAADA YA KUITUNGUA WIGAN KWA MAGOLI 2 KWA O KATIKA DIMBA LA WEMBLEY

Meneja
Mpya Wa Man U David Moyes akiwa ameshika ngao ya Hisani pamoja na
Mchezaji wa Man U mara baada ya kukabidhiwa leo katika uwanja wa Wembley
baada ya kuitungua Wigan Kwa Magoli 2 kwa 0. Hili ni Kombe la Kwanza
kwa Kocha Mpya huyo wa Man United david Moyes



Wachezaji
wa Man U wakishangilia Mara baada ya Kuibuka Kinara kwa kuitungua Wigan
2 kwa 0 katika Mchezo wa Kuwania Ngao ya Hisani uliofanyika Katika
Dimba la Wembley Uingereza
Sunday, August 11, 2013
SERIKALI YA RWANDA IMEAPA KUTOWAFUKUZA WATANZANIA...!!!

Akizungumzia sakata la wahamiaji haramu wa Kinyarwanda kufukuzwa na serikali ya Tanzania amesema, kila nchi inayo mamlaka ya kufanya vile inafaa lakini ingekuwa vizuri Tanzania ingewasiliana na Rwanda ili kujua wataondokaje na kupokelewa vipi.
Amesisitiza, "Kwa kuwa wenzetu wameamua kufanya hivyo, tupo tayari kuwapokea wananchi wetu" Lakini pia, Waziri huyo amesema waasi wa FDRL ni kikundi cha wauaji wanaojipanga kuangamiza watu fulani nchini Rwanda hivyo wanatakiwa kupingwa kwa nguvu zote badala ya kuwatambua na kuzungumza nao kama kundi halali na lenye nia njema.
Naye Mtanzania Mohammed, amependekeza Rais Kagame na Kikwete wakutane na kufikia suluhu.Pia baadhi ya Wanyarwanda wamelalamikia kutokutendewa haki kwa kutenganishwa na wake,waume, n.k
TAARIFA RASMI YA JESHI LA POLISI KUHUSU KUPIGWA RISASI SHEKHE PONDA

Advera Senso- SSP-Msemaji wa Jeshi la Polisi.
--
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NDANI

JESHI LA POLISI TANZANIA
DAR ES SALAAM AGOSTI 10, 2013.
1. MNAMO
TAREHE 10, AGOSTI ,2013 MAJIRA YA SAA 8 MCHANA, MAENEO YA SHULE YA
MSINGI KIWANJA CHA NDEGE MANISPAA YA MOROGORO, KULIFANYIKA KONGAMANO LA
BARAZA LA EID LILILOANDALIWA NA UMOJA WA WAHADHILI MKOANI MOROGORO.
DAKIKA KUMI KABLA YA KONGAMANO HILO KUMALIZIKA ALIFIKA SHEKHE PONDA
ISSA PONDA AMBAYE ALIZUNGUMZA KWA MUDA MFUPI.
2.
KONGAMANO HILO LILIFUNGWA MAJIRA YA SAA 12:05 JIONI AMBAPO WATU
WALIANZA KUTAWANYIKA, BAADHI YAO WAKIWA WAMEZINGIRA GARI DOGO ALILOKUWA
AMEPANDA SHEKHE PONDA. BAADA YA KUTOKA KATIKA ENEO HILO, ASKARI WA
JESHI LA POLISI WALIZUIA GARI HILO KWA MBELE KWA NIA YA KUTAKA KUMKAMATA
SHEKHE PONDA AMBAYE MPAKA SASA ANATUHUMIWA KWA KOSA LA KUTOA MANENO YA
UCHOCHEZI SEHEMU MBALIMBALI HAPA NCHINI YENYE MLENGO WA KUSABABISHA
UVUNJIVU WA AMANI.
3.
BAAADA YA ASKARI KUTAKA KUMKAMATA, WAFUASI WAKE WALIZUIA UKAMATAJI HUO
KWA KUWARUSHIA MAWE ASKARI. KUFUATIA PURUKUSHANI HIYO, ASKARI WALIPIGA
RISASI HEWANI KAMA ONYO LA KUWATAWANYA.
4.
KATIKA VURUGU HIZO, WAFUASI HAO WALIFANIKIWA KUMTOROSHA MTUHUMIWA. HIVI
SASA IMETHIBITIKA KUWA SHEKHE PONDA YUKO KATIKA HOSPITALI YA TAIFA YA
MUHIMBILI AKITIBIWA JERAHA KATIKA BEGA LA MKONO WA KULIA LINALODAIWA
ALILIPATA KATIKA PURUKUSHANI HIZO.
5.
KUFUATIA TUKIO HILO, TIMU INAYOSHIRIKISHA WAJUMBE KUTOKA JUKWAA LA HAKI
JINAI IKIONGOZWA NA KAMISHINA WA JESHI LA POLISI CP ISSAYA MNGULU
IMEANZA KUFANYA UCHUNGUZI WA TUKIO HILO.
6. AIDHA, JESHI LA POLISI LINATOA WITO KWA WANANCHI KUWA WATULIVU WAKATI SUALA HILI LINASHUGHULIKIWA KISHERIA.
Imetolewa na:-
Advera Senso- SSP
Msemaji wa Jeshi la Polisi.
SERIKALI YADAIWA KUMGEUKA DR ULIMBOKA YADAI AMEFICHA USHAHIDI WA KUTEKWA KWAKE

SIKU chache baada ya Mahakama ya Kisutu kumwachia mtu aliyedaiwa kumteka na kumtesa kiongozi wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk. Steven Ulimboka, serikali imemshukia daktari huyo na kudai ndiye chanzo cha kukwama kwa dola kukamata watu waliomteka.
Jana Mwendesha Mashitaka Mkuu wa Serikali (DPP), Eliazer Feleshi, alidai kuwa vyombo vya dola vimeshindwa hadi sasa kuwakamata waliohusika katika shambulio hilo kutokana na Dk. Ulimboka kukwepa kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi.
Feleshi ambaye jana aliambatana na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Said Mwema, katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, alidai lawama zinazosukumwa kwa Jeshi la Polisi kwa madai ya kushindwa kuwakamata waliomtendea unyama daktari huyo hazina msingi, kwa kuwa mhusika mwenyewe hajafika polisi, licha ya kuitwa mara nyingi kutoa maelezo.
Alisema kama Dk. Ulimboka angetoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi kungekuwa na mafanikio makubwa katika kuwasaka na hata kuwatia mbaroni waliohusika katika unyama huo.
“Kila mara mmekuwa mkilaumu polisi wanashindwa kukamata wahalifu lakini tutakamataje kama wenye ushahidi hawataki kutoa ushirikiano?
Kwa mfano mdogo tu ni ‘ishu’ (suala) ya Dk. Ulimboka, hadi leo hajatoa taarifa lakini polisi wanaendelea kusakamwa na kutukanwa tu,” alisema.
Hata hivyo, wakati Feleshi akitoa kauli hiyo, Dk. Ulimboka katika andiko lake alilolitoa mara tu baada ya kurejea nchini kutoka Afrika Kusini alikopelekwa kwa ajili ya matibabu, alimtaja mtu anayeaminika kuwa mfanyakazi wa Idara ya Usalama wa Taifa, Ramadhani Ighondu, kuwa ndiye aliyemteka na kumtesa.
Ulimboka akimtumia Wakili Nyaronyo Kicheere alisema Ighondu na wenzake ni mhusika mkuu katika unyama aliofanyiwa, kauli ambayo imekanushwa mara kadhaa na serikali.
Mapema wiki hii, raia wa Kenya, Joshua Mulundi, aliyekuwa akikabiliwa na tuhuma za kumteka na kumtesa Dk. Ulimboka aliachiwa na Mahakama ya Kisutu baada ya DPP Feleshi kumfutia shitaka. Hata hivyo Mulundi alikamatwa tena na sasa amefunguliwa mashitaka ya kutoa maelezo ya uongo kwa polisi.
KUTOKA KWENYE MTANDAO WA DAILYMAIL UINGEREZA:SHEIK PONDA AHUSISHWA NA KESI YA MABINTI WA UINGEREZA WALIOMWAGIWA TINDIKALI
Sheikh Ponda Issa who is suspected of inciting the attack on Kirstie Trup and Katie Gee was shot by police in Tanzania's capital last night
A radical Muslim preacher wanted in
connection with an acid attack on two British teenagers in Zanzibar has
been shot by police, it was reported.
Sheikh
Issa Ponda Issa was hit in the shoulder with a tear gas canister as he
tried to escape from officers after being cornered near Tanzania's
capital Dar es Salaam, The Sunday Mirror said.
JAPAN KUJENGA KIWANDA CHA PIKIPIKI TANZANIA
WAINGEREZA WALIOMWAGIWA TINDIKALI WAITESA SERIKALI

Siku tano baada ya raia wawili wa Uingereza kumwagiwa tindikali visiwani Zanzibar, Serikali kupitia vyombo vyake vya uchunguzi imeibuka na kueleza kuwa bila wananchi kutoa taarifa za ushahidi wa uhalifu wa aina mbalimbali, ni vigumu kuwabaini wahusika. (HM)
Kauli hiyo ilitolewa kwa pamoja jana
na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Said Mwema, Mkemia Mkuu wa
Serikali, Profesa Samwel Manyele na Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali
(DPP) Eliezer Feleshi, katika mkutano wao na waandishi wa habari,
uliolenga kueleza mikakati ya kupambana na matumizi yasiyo sahihi ya
tindikali nchini.
Katika ufafanuzi wao walisema, "Kutoa taarifa ya uhalifu wa jambo lolote siyo hiari, ni jukumu la kisheria na kikatiba," huku Feleshi akitolea mfano jinsi Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk Steven Ulimboka alivyoshindwa kutoa ushahidi wa tukio lililomkuta la kutekwa, kupigwa na kisha kutupwa katika Msitu wa Mabwepande, hivyo kufanya uchunguzi kuwa mgumu.
Katika ufafanuzi wao walisema, "Kutoa taarifa ya uhalifu wa jambo lolote siyo hiari, ni jukumu la kisheria na kikatiba," huku Feleshi akitolea mfano jinsi Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari nchini, Dk Steven Ulimboka alivyoshindwa kutoa ushahidi wa tukio lililomkuta la kutekwa, kupigwa na kisha kutupwa katika Msitu wa Mabwepande, hivyo kufanya uchunguzi kuwa mgumu.
Saturday, August 10, 2013
NDEGE YA KIJESHI YALIPUKA NA KUTEKETEA KWA MOTO WAKATI IKITUA KWA DHARURA.
Ndege hiyo ilikuwa ya jeshi la Ethiopia.MOJA YA NDEGE ZA NCHI YA SOMALIA.
PICHA YA NDEGE ZA JESHI YA MAKTABA SIO YA SOMALIA.
NDEGE ya kijeshi imelipuka na kuteketea nchini
Somalia baada ya kutua kwa dharura katika uwanja wa kimataifa wa ndege
mjini Mogadishu.
Inasemekana kuwa ndege hiyo ilikuwa ya jeshi la Ethiopia.
Kuna ripoti kuwa ndege ilikuwa imebeba zana za kivita.
Wafanyakazi katika uwanja huo wa ndege waliel
ezea kusikia milipuko kadhaa huku moto ukienea kwa ndege hiyo.
JESHI LA POLISI LATANGAZA DAU LA MILIONI 10 KWA MTU ATAKAYEWATAJA WATU WALIOWAMWAGIA TINDIKALI WAZUNGU

Zanzibar, Tanzania — Kamanda wa Polisi, Kamishna Musa
Ali Musa amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeahidi kutoa Shilingi
milioni 10/= kwa mtu yeyote atakayetoa taarifa zitakazofanikisha kukamatwa kwa
watu waliowashambulia mabinti wawili kutoka Londona, Uingereza, Kirstie Trup na
Katie Gee.
Mabinti hao walishambuliwa kwa tindikali usoni, kifuani na mikononi siku ya Jumatano walipokuwa njiani kuelekea kwenye chakula cha jioni.
Mabinti hao walishambuliwa kwa tindikali usoni, kifuani na mikononi siku ya Jumatano walipokuwa njiani kuelekea kwenye chakula cha jioni.
Friday, August 09, 2013
JAJI MUTUNGI AANZA KUTUMA SALAMU ZA UTENDAJI KAZI WAKE ....!!!
Jaji Mkuu, Mohamed Chande Othman akimpongeza Francis Mutungi baada ya
kuapishwa na Rais Jakaya Kikwete kuwa Jaji wa Mahakama Kuu katika hafla
iliyofanyika Ikulu, Juni 19,2012. Jaji Mutungi jana aliteuliwa kuwa
Msajili wa Vyama vya Siasa. Picha na Maktaba.
********
Dodoma. Msajili mteule wa Vyama vya Siasa
nchini, Jaji Francis Mutungi amewataka Watanzania kutulia na kusubiri
utendaji wake atakapokabidhiwa rasmi jukumu hilo jipya alilopewa na Rais
Jakaya Kikwete.
Mutungi aliteuliwa kushika wadhifa wa msajili wa
vyama vya siasa kuchukua nafasi ya John Tendwa ambaye amestaafu. Tendwa
aliiongoza taasisi hiyo kwa miaka 13.
Mutungi alisema: “Ninafahamu nina majukumu mazito
mbele yangu, lakini siwezi kusema chochote kwa kuwa sijakabidhiwa rasmi
ofisi. Ninachotaka kusema ni kwamba nitakuwa mtumishi wa kila mmoja.”
MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ASHIRIKI SWALA YA SIKUKUU YA IDDI KITAIFA MKOANI TABORA


Subscribe to:
Comments (Atom)






