Sunday, August 04, 2013
AUA MKE WAKIBISHANA KIPI KITANGULIE KUPIKWA KATI YA MAINI NA NYAMA ....!!!

Mkazi wa kijiji cha Minyughe, wilayani Ikungi, Bonphace Misanga (70) anashikiliwa na polisi mkoani Singida, kwa tuhuma za kumpiga mkewe Amina Kunyonga (67) hadi kufariki dunia baada ya kuzuka mabishano ya nini kianze kupikwa kati ya nyama na maini.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida, Geofrey Kamwela, aliwaeleza waandishi wa habari kuwa tukio hilo lilitokea Jumanne wiki hii.
Alisema siku hiyo wanandoa hao walikwenda kwenye mnada kijijini hapo na baada ya kunywa kiasi kingi cha pombe ya kienyeji walikubaliana wanunue nusu kilo ya maini na nusu ingine ya nyama mchanganyiko ya ng'ombe, huku wakiwa tayari wamekwisha lewa.
TANESCO WAANZA KUTUMIA TRANSFORMA ZISIZOTUMIA MAFUTA KUDHIBITI WIZI

Dar es Salaam. Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limelazimika kufunga transfoma zisizotumia mafuta kutokana na tatizo kubwa la wizi wa mafuta ya transfoma kwa maeneo mengi nchini.
Meneja mawasiliano wa Tanesco, Badra Masoud amesema, shirika hilo limelazimika kufunga transfoma zijulikanazo kama ‘Dry type Transfoma’ambazo hazitumii mafuta ili kupambana na changamoto za wizi wa mafuta unasababisha baadhi ya maeneo kukosa umeme.
“Tatizo la wizi wa mafuta ya Transfoma ni kubwa, limesababisha shirika kununua transfoma zisizotumia mafuta ambazo zinapatikana kwa gharama kubwa ukilinganisha na transfoma zitumiazo mafuta ili kuepusha kutokukatika kwa umeme kwa maeneo husika,” alisema Badra
Aliyataja baadhi ya maeneo ambayo yamefungwa transfoma zisizotumia mafuta kutokana na kukithiri kwa tatizo la wizi huo kuwa ni pamoja na Mbezi Beach na maeneo mengi katika Wilaya ya Temeke.
Saturday, August 03, 2013
MAKAMU WA RAIS JANA AKABIDHI ZAWADI ZA WASHINDI WA SHINDANO LA TATU LA KUHIFADHI QUR'AN TUKUFU JIJINI DAR
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akizungumza za waumini wa dini ya Kiislamu, wakati wa hafla ya
kukabidhi zawadi kwa washindi wa shindano la tatu la kuhifadhi Qur'an
Tukufu, iliyofanyika jana usiku Agosti 2, 2013 katika Msikiti wa
Istiqaama, jijini Dar es Salaam.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akimkabidhi zawadi ya Sh. milioni 2, mshindi wa kwanza wa kuhifadhi
Juzuu 30, Abdulkarim Khamis, wakati wa hafla ya kuwakirimu na kukabidhi
zawadi kwa washindi hao iliyofanyika kwenye Msikiti wa Istiqaama, Ilala
jijini Dar es Salaam, jana usiku.
NAPE NNAUYE AWACHEFUA WAZEE WA CCM ...!!!
Wazee kwenye mkutano wa CCM, Uwanjwa wa Community Cetre Mwanga hivi karibuni mkoani Kigoma.
Katibu
wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye (katikati) akibadilishana jambo na mmoja wa
wanachama wakongwe wa kata ya Elerai hivi karibuni.SIMBA YAMSAINI RASMI BEKI WA KATI NAHODHA WA TIMU YA TAIFA YA BURUNDI GILBERT KAZE
Chanzo: Shaffih Dauda Blog
KESI YA JENGO LA GHOROFA JIRANI NA IKULU LAZIDI KUWANASA WATU WENGI
UPANDE
wa Jamhuri katika kesi ya jengo refu la ghorofa 18 lililojengwa jirani
na Ikulu bila kufuata utaratibu unatarajia kuita mashahidi 13 na
vielelezo 20 kuthibitisha mashtaka dhidi ya vigogo walioruhusu ujenzi
huo.
Hayo yalielezwa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na Wakili wa Serikali kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Leonard Swai.
Hayo yalielezwa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na Wakili wa Serikali kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Leonard Swai.
Alikuwa akisoma maelezo ya awali ya kesi hiyo mbele ya Hakimu Mkazi Sundi fimbo.
Swai alisema kesi hiyo itaanza kusikilizwa Agosti 7 mwaka kwa ajili ya mashahidi wa upande wa mashtaka kutoa ushahidi wao.
Washitakiwa katika kesi hiyo ni Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Makumba Kimweri na Msanifu Mkuu wake Richard Maliyaga.
RAIS KIKWETE AMVAA KAGAME, MSHANGAA KWA LUGHA ZA MATUSI NA KEJELI.
RAIS KIKWETE.
RAIS KAGAME.DAR ES SALAAM. KWA mara ya kwanza Rais Jakaya Kikwete amemtolea uvivu Rais wa Rwanda, Paul Kagame kutokana na kitendo chake cha kumtolea lugha za matusi baada ya kumshauri kukaa meza moja na vikundi vya waasi wa nchi yake (FDLR), huku akimtaka kuacha kukuza mgogoro usiokuwepo.
Rais Kikwete alitoa ushauri huo kwa Rwanda
takribani miezi miwili iliyopita wakati akizungumza katika kikao cha
Mkutano wa Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika mapema mwaka huu, mjini
Addis Ababa, Ethiopia, ambao ulikuwa ukij
adili suala la amani ya Jamhuri
ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) pamoja na Ukanda wa Maziwa Makuu.
Ushauri huo pia uliwagusa Rais Yoweri Museveni wa
Uganda na Joseph Kabila (DRC), ambao aliwataka kufanya mazungumzo na
waasi wanaopingana na Serikali zao.
MZEE MAJUTO AFUNGA NDOA YA SIRI NA MSICHANA "MBICHI"....!!!

Mzee Majuto aliambatana na wasanii wenzake Suleiman Barafu aliyekuwa mpambe wake na mwingine aliyefahamika kwa jina la utani kama mama Sharon.
Baada ya waandishi wetu kupata taarifa kuhusu tukio hilo, waliwahi kutia timu Mbagala, nyumbani kwa binti huyo.
Baada ya kufika, waandishi wetu walibaini kuwa ni kweli kulikuwa na shamrashamra za ndoa ambayo ilikuwa ikifanyika kwa siri huku watu wakizuiliwa kupiga picha.
Muda mfupi baadaye, gari aina ya Toyota Noah (namba za usajili tunazo) lililowabeba mzee Majuto na wapambe wake liliwasili.
Subscribe to:
Comments (Atom)





