Saturday, August 03, 2013

SIMBA YAMSAINI RASMI BEKI WA KATI NAHODHA WA TIMU YA TAIFA YA BURUNDI GILBERT KAZE

Klabu ya Simba imekamilisha rasmi usajili wa beki wa kati Gilbert Kaze kutoka Vital O ya Burundi. Gilbert aka Demunga ni mmoja wa mabeki bora walionyesha kiwango kizuri hasa kwenye michuano ya Cecafa iliyopita. Amesaini mkataba wa miaka miwili wa kuitumikia Simba. Gilbert Kaze pia ni nahodha wa timu ya taifa ya Burundi - na alikuwa mmoja wa wachezaji muhimu wa timu hiyo walioiwezesha Burundi kufuzu kucheza CHAN mwakani nchini South Africa.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...