Friday, August 11, 2017

SERIKALIYAZIMBAMBWEYAKATAAWAFUNGWA KUPIGA KURA


Serikali ya Zimbabwe imekataa ombi la chama cha MDC-T la kuwaruhusu wafungwa kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo ambao utafanyika mwakani 2018.

Taarifa ambayo imetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Sheria ya Zimbabwe, Virginia Mabiza imeeleza kuwa hawawezi kuwaruhusu wafungwa kupiga kura kwani sheria za nchi hiyo haziruhusu.

Aisha Mabiza amekishauri chama hicho cha MDC-T kuwa kama inataka wafungwa waruhusiwe kupige kura basi watume maombi katika Bunge la nchi hiyo ili lifanye marekebisho ya kisheria ambayo yatawapa ruhusa wafungwa kupiga kura.

“Ninashauriwa na washauri watu na uamuzi ambao ninauchukua ni ambao unaruhusiwa na sheria ya nchi, na kama ni jambo ambalo linakiuka katiba jambo pekee ambalo linahitajika ni kwenda Bungeni kuomba kubadilisha sheria,” alisema Mabiza.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...