Thursday, January 22, 2015

UJUMBE WA UTURUKI SOMALIA WASHAMBULIWA

Hoteli ilioshambuliwa 
 
Kumekuwa na shambulizi la mlipuaji wa kujitolea muhanga katika hoteli moja mjini Mogadishu nchini Somali ambapo maafisa wa Uturuki walikuwa wakijiandaa kumlaki rais Recep Teyyip Erdogan.
Takriban raia watatu wa Somali waliuawa wawili kati yao wakiwa maafisa wa usalama wakati gari lililojaa vilipuzi lilipogonga lango la hoteli.
Uturuki hatahivyo imesema kuwa hakuna mjumbe wake aliyejeruhiwa na kwamba ziara ya rais Erdogan itaendelea kama ilivyopangwa siku ya ijumaa.
Kundi la wapiganaji wa Alshabaa limesema kuwa lilitekeleza shambulizi hilo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...