Thursday, January 22, 2015

MWIGULU ATII AGIZO LA KINANA, ASITISHA ZIARA ZAKE MIKOANI

Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba 

Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amesitisha ziara zake za mikoani ili kutii agizo alilopewa na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana.
Nchemba ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, alisema jana kuwa anawajibika kutekeleza amri hiyo kutoka ndani ya chama.
Alisema agizo hilo halina lengo baya zaidi ya kukijenga chama ili kufikia malengo ikiwa ni pamoja na kuimarisha nidhamu miongoni mwa wanachama.
“Huwa ananituma, anaweza akaniambia nifanye au nisifanye jambo ambalo halina masilahi ya chama,” alisema Nchemba.
Utekelezaji huo umekuja baada ya Nchemba kuandikiwa barua na Kinana ambayo pia imezagaa katika mitandao ya kijamii ikimtaka kusitisha ziara anazozifanya maeneo mbalimbali kwa kuwa hazina baraka za chama hicho.
Katika barua hiyo iliyoandikwa Januari 18, ilieleza Nchemba amekuwa akifanya ziara nyingi katika mikoa na wilaya bila ya ushirikishwaji wa makao makuu, mikoa na wilaya na hasa kamati za siasa.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...