Tuesday, July 16, 2013

WALIOSAJILIWA NA WALIOTEMWA KWENYE LIGI KUU


 
Mabeki wa Toto African, Evarist Maganga (kushoto) na Peter Mutabuzi wakimkaba mshambuliaji wa Azam Brian Umony. Beki Mutabuzi amejiunga na Kagera Sugar kwa ajili ya msimu ujao wa ligi. Picha na Michael Matemanga.
 
*********
 
Mosses Oloya wa Uganda anayecheza soka la kulipwa nchini Vietnam anaweza akawa ndiye mchezaji anayetikisa zaidi kwenye usajili wa soka la Bongo kwa timu 14 zinazojiandaa kushiriki Ligi Kuu Bara msimu ujao.
Oloya anamudu vyema kucheza nafasi ya winga wa kushoto pamoja na kulia kama ilivyokuwa kwa mfungaji hatari wa Simba, Emmanuel Okwi aliyetua klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia Januari mwaka huu, baada ya kupata mafanikio makubwa akiwa na Simba.
Nyota Oloya yupo sokoni, anawindwa na klabu zote kubwa, Simba na Yanga. Oloya amekuwa akibeba vichwa tofauti kwenye magazeti mbalimbali nchini.


Ufuatao ni baadhi ya wachezaji wapya waliosajiliwa katika klabu za Ligi Kuu nchini na wachezaji waliotemwa na klabu hizo:
Prisons Mbeya
Wapya: Wilbert Mweta (Simba), Ibrahim Mamba (Oljoro).
Walioondoka: David Abdallah (Mbeya City), Sino Agustino (Simba), Elias Maguri (Ruvu Shooting), Misango Magai, Emmanuel Gabriel na Henri Mwalugala (wameachwa).
Mbeya City
Wapya: David Abdallah (Prisons), Paul Nonga (Oljoro).
Walioachwa: kipa Amani Simba. Pia kocha wa Mbeya City, Juma Mwambusi anasema,”nafikiri nitafute baada ya wiki moja nitakuwa na jibu zuri la kukujibu zaidi.”
Coastal Union
Wapya: Haruna Moshi, Juma Nyosso (Simba), Said Rubawa, Marcus Ndahel (Oljoro), Crispin Odulla (Bandari, Kenya), Keneth Masumbuko (Polisi Moro) na Abdullah Othman (Jamhuri ya Pemba).
MWANANCHI

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...