Tuesday, July 30, 2013

WAFUNGWA MBEYA WAMUOMBA NCHIMBI KUCHUNGUZA MAUAJI GEREZANI...!!!



WAFUNGWA wa Gereza  la Ruanda lililopo mjini Mbeya wameiomba ofisi ya Waziri wa Mambo  ya ndani ya nchini kuunda tume huru kuchunguza mauaji ya kikatili ya mahabusu wawili katika Gereza hilo.



Kupitia barua ya Septemba 22,2012 ya wafungwa hao kwenda ofisi hiyo, imesema kuwa kama si lengo la kupunguza ufanisi wa kazi za waziri wa Wizara hiyo basi ni mikakati iliyoundwa kwa ajili ya kuchafua wizara nzima.



‘’Mhe. Waziri, Uongozi wa Gereza hili la Ruanda umekabidhi Mamlaka ya utendaji wa shughuli za gereza mikononi mwa kundi dogo la wafungwa wanne, kundi hilo ujulikana kwa jina la Maumau’’ imesema barua hiyo yenye kurasa tatu.



Barua hiyo imesema kuwa endapo mfungwa au mahabusu atahoji uhalali wa kundi hilo na kwa bahati mbaya kundi hilo likitambua, uhai wa mtu huyo unakuwa mikononi mwa kundi hilo la Maumau.



Imesema mnamo July 11 mwaka 2012, kuna mahabusu aliuawa kwa kipigo baada ya kuhoji  uhalali wa kundi hilo ambapo aliuawa kwa kupigwa na mfungwa Biroka au Edo ambaye ni miongoni mwa kundi linalounda kundi la Mau mau.



‘’Alipigwa mbele ya Afisa usalama na uhai wake ulitoweka akiwa ndani ya Dispensary, mnamo tarehe 30.08.2012 mwingine alipigwa na kuzimia na kutibiwa kwa siku saba katika Dispensary’’imesema barua hiyo.



Imeeleza kuwa Septemba 19 mwaka huu kundi la Maumau lilipata taarifa zisizosahihi kuwa wafungwa na Mahabusu walitaka kugomea chakula ili kupinga vitendo vya kundi hilo ndipo uongozi ukaamuru wafungwa wote na mahabusu kulala chini na kupigwa.



Wamewataja wanaodaiwa kuuawa kuwa ni Jafari Mwaipopo aliyepigwa Septemba 19,2012 na kufa Septemba 21,2012, Fadhili Ruvanda aliyepigwa July 1, 2012 na kufa July 14, 2012 na Robert Kigodi alivunjwa mkono na Nyapala mkuu msaidizi.



Nakala ya barua hiyo imepelekwa kwa Kamishina mkuu wa Magereza Dar es Salaam, Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Mkuu wa Magereza Mbeya na Mkuu wa gereza Ruanda ambapo wameomba ofisi ya Waziri wa mambo ya ndani kuunda tume itakayofika gerezani hapo na kukutana na wafungwa na mahabusu ili kuthibitisha tuhuma hizo.



Baadhi ya mamlaka za Serikali zimekiri kupata nakala ya barua hiyo ambapo zimesema kuwa hali hiyo ipo kila Gereza nchini kutokana na mfumo ulivyo.



Hata hivyo baadhi ya wadau wa haki za binadamu wamependekeza kuwa endapo tume hiyo itaundwa iundwe tume ya vyombo vya dola vinavyohusika na uchunguzi wakiwemo wajumbe kutoka usalama wa taifa, Polisi na Takukuru na si vingenevyo. 
Na Kalulunga

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...