Saturday, April 13, 2013

SHAA AJILINGANISHA NA AKINA DIAMONDA & OMMY DIMPOZ

MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Sara Kaisi ‘Shaa’ amejinasibu kuwa kiwango alichonacho sasa hakina tofauti na wasanii wengine wakali kama Omary Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ na Nassib Abdul ‘Diamond’.
                                                     Shaa akifanya vitu vyake.
Shaa aliyabainisha hayo jijini Dar es Salaam jana wakati akifanya mahojiano na mwandishi wa habari hii aliyekuwa akitaka kufahamu kiwango cha fedha anachokipata katika shoo zake mbalimbali anazofanya.

“Hivi sasa kama mtu anaweza kumchukua Ommy ama Diamond kwa dau hilo analowapa, basi anaweza pia kunichukua mimi kwa shoo zake kwa kiwango cha nyota hao wawili, kwani uwezo ninao,” alisema.

Aliongeza kuwa ili kudumu katika fani ya muziki wa kizazi kipya, kunatakiwa kuongeza ubora wa kazi kwa kufanya kazi na wadau mbalimbali wa muziki wa ndani na nje ya nchi.
Shaa alisema kwa sasa wimbo wake wa ‘Lover Lover’ unaendelea kufanya vema katika vituo mbalimbali vya redio hapa nchini na Afrika Kusini, ambako video ya wimbo huo inachezwa zaidi.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...