Friday, April 05, 2013

DAWA MPYA ZA KIENYEJI ZA KUKUZA MAKALIO ZAWATEKA WAREMBO WENGI

BAADA ya zile dawa za Kichina za kuongeza makalio, ‘hips’ na matiti zilizotikisa Bongo na kubainika kubeba madhara makubwa kama vile ‘kalio’ moja kuwa kubwa kuliko lingine, kujazia zaidi chini kuliko juu na mwili kufa ganzi, zilikosa soko, lakini sasa zimeibuka nyingine za kienyeji


Uchunguzi uliofanywa na audifacejackson blog kupitia kwa wataalam mbalimbali wa tiba za asili TANZANIA , ulibaini kuwa dawa hizo zimejaa tele kwa waganga wa kienyeji. 

Ilifahamika pia kuwa hivi sasa dawa hizo zinachangamkiwa na wanawake ile mbaya wakiamini kwamba hazina madhara kama zile za Kichina. 

NI MCHANGANYIKO WA MITI 60 
Mmoja wa wataalam hao aliyezungumza na audifacejackson blogalisema kuwa, dawa hiyo ni mjumuisho au mchanganyiko wa miti zaidi ya 60 inayopatikana kwenye misitu mikubwa hasa mikoani.

JINA LAKE 
audifacejackson blog jina la dawa hiyo, mtaalam huyo alisisitiza:“Nimeshakuambia ni mchanganyiko wa miti zaidi ya 60, haina jina isipokuwa mteja akifika anatakiwa aseme kama anataka mzigo wa saizi gani.”


UNACHAGUA KALIO UNALOTAKA 
Mtaalam huyo alikwenda mbele zaidi na kuweka kweupe kuwa dawa hiyo ni kiboko ya Mchina kwani dozi na bei yake hutegemea aina ya kalio analolitaka mteja husika.

“Ukitaka dogo, la kati au kubwa, kila moja lina dozi na bei yake hivyo  inategemea mteja amechagua la aina gani,” alisema mtaalam huyo. WATAALAM WA TIBA ASILIA WANASEMAJE?
waandishi wa audifacejackson blog waliendelea kufanya mahojiano na wataalam mbalimbali wa tiba za asili ambapo walikuwa na haya ya kusema:

MJUKUU WA BABU 
Mganga maarufu kwa jina la Mjukuu wa Babu anayepatikana Mwananyamala jijini Dar es Salaam alifunguka:
“Nakwambia hii dawa ni kiboko ya zile za Kichina. Ni dawa nzuri na kusema kweli watumiaji ni wengi. Ni mchanganyiko wa miti zaidi ya sitini ambao huwa unatoa aina moja ya dawa.

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...