Monday, March 25, 2013

KAJALA AHUKUMIWA MIAKA 5, MUMEWE MIAKA 7

HUKUMU ya kesi iliyokuwa inamkabili staa wa filamu za Kibongo, Kajala Masanja na mumewe imetolewa leo na Hakimu Sundi Fimbo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar. Katika hukumu hiyo Kajala amehukumiwa kwenda jela miaka mitano au kulipa faini ya shilingi milioni 13 na mumewe kwenda jela miaka saba au kulipa faini ya shilingi milioni 200.
Kajala alikuwa anakabiliwa na kesi ya kuuza nyumba iliyowekwa kizuizini na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) baada ya mumewe, Faraji Agustino kukumbwa na msala wa kutakatisha fedha haramu.
Wasanii wa Bongo movie wanazichanga hapahapa kuzilipa ila zimepngua kidogo,Wema na Zamaradi wanakimbia ATM KUZICHUKUA ZINGINE.leo leo Kajala anafika nyumbani kwao

1 comment:

Kunjira Rugereza said...

Majaribu ni Mengi sana,pole sana kwa kukumbwa na masharibu,lakini Mungu Yuko ,na Wanao muogopa Mungu wakazane na maombi maana tumo nyakati za mwisho.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...