Thursday, March 14, 2013

DIAMOND ATANGAZA KUJENGA MSIKITI

Kwa mujibu wa staa huyo ambaye kwa sasa anaminya kimapenzi na mtangazaji wa DTV, Penniel Mungilwa ‘Penny’, msikiti huo utakuwa kumbukumbu yake kwa watakaoutumia kama sehemu ya kurudisha kwa…
 Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.
Na Sifael Paul Global Publishers
SIKU chache baada ya kuwachefua Waislamu wenzake kwa kutimba kwenye Maulid na kuomba dua akiwa amevaa hereni na mkufu, msanii wa Bongo Fleva mpenda totoz, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ametangaza kujenga msikiti jijini Dar es Salaam, kwani ni jambo alilolipanga kwa muda mrefu.

Kwa mujibu wa staa huyo ambaye kwa sasa anaminya kimapenzi na mtangazaji wa DTV, Penniel Mungilwa ‘Penny’, msikiti huo utakuwa kumbukumbu yake kwa watakaoutumia kama sehemu ya kurudisha kwa jamii inayompa sapoti kubwa.
Diamond ambaye amemjengea mama yake, Sanura Kassim ‘Sandra’ nyumba ambayo hadi sasa imegharimu Sh. milioni 260 alifunguka: “Ninajitahidi sana kununua viwanja au vinyumba vidogovidogo maeneo tofauti. Nipo kwenye plan (mpango) ya kujenga msikiti japo sijapanga sehemu hasa hadi nipate eneo la kutosha.
“Nataka iwe kumbukumbu ili hata kesho na keshokutwa nikifa, vizazi vijavyo wawe wanaswali kwenye msikiti uliojengwa na Diamond.
“Kwa kufanya hivyo itanipa baraka kubwa sana na soon tu nina imani mwenyezi Mungu atanisaidia nijenge huo msikiti.”

No comments:

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...