Wednesday, February 10, 2016
WEST HAM YAITUPA NJE LIVERPOOL
Wagonga nyundo wa
London West Ham United imewatupa nje majogoo wa Anfield Liverpool katika
mchezo wa raundi ya nne ya kombe la FA.
West Ham walianza
kuandika bao lao la kwanza kupitia kwa Michail Antonio katika dakika ya
45 ya kipindi cha kwanza baada ya kunganisha krosi nzuri Enner
Valencia's
Liverpool wakachomoa bao hilo kupitia kwa kiungo Philippe Coutinho aliyepiga mpira wa adhabu na kujaa nyavuni moja kwa moja.
Dakika tisini zikamalizika kwa sare ya bao 1-1, katika dakika 30, za nyongeza West Ham wakapata bao kupita kwa Angelo Ogbonna,
West Ham watawavaa Blackburn ugenini katika mchezo wa raundi ya tano ya michuano hiyo hapo Februari 21. Like page yetu ya facebook Jambo Tz
Tuesday, February 09, 2016
MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA POLE KWA MKE WA PINDA
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amemtumia
salamu za pole Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu Mama Tunu Pinda aliyepatwa na
ajali ya gari, iliyotokea jana tarehe 08 Februari, 2016 akiwa safarini
kutoka Dodoma kwenda Dar es salaam.
Ajali
hiyo imetokea katika eneo la Mkundi lililopo katika Manispaa ya
Morogoro ambapo gari aliyokuwa akisafiria Mama Tunu Pinda, ilipinduka
baada ya kumgonga mwendesha pikipiki aliyeingia ghafla barabarani.
Katika
salamu hizo alizozituma kupitia kwa Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa
Mizengo Kayanza Peter Pinda, Rais Magufuli amesema amepokea kwa mshtuko
taarifa za kutokea kwa ajali hiyo na amemuombea Mama Pinda na Majeruhi
wengine kupona haraka.
"Kupitia
kwako Mheshimiwa Waziri Mkuu Pinda, naomba unifikishie pole nyingi kwa
mkeo Mama Pinda kwa kuumia katika ajali hii, na namuomba Mwenyezi Mungu
awaponye majeruhi wote ili waweze kuendelea na shughuli zao za kila
siku" alisema Rais Magufuli.
Mama Tunu Pinda anaendelea kupata matibabu Jijini Dar es salaam, na hali yake inaendelea vizuri.
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dodoma
09 Februari, 2016
Subscribe to:
Posts (Atom)