Friday, May 01, 2015

BAN KI-MOON ASIKITISHWA NA MAPIGANO YEMEN

 Ban Ki-moon
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ameelezea tahadhari yake kuhusiana na hatari ya raia kuendelea kupigana, Nchini Yemen. Anasema kuwa zaidi ya watu elfu moja mia tano wameuwawa na wengine laki tatu wametoroka makazi yao, katika kipindi cha majuma sita yaliyopita.

Mashambulizi katika majumba ya raia zikiwemo hosptali na maghala ya vifaa vya misaa ya kibinadamu yamekuwa yakiendelea.
Mapigano Yemen
Kumekuwa na taarifa watu wenye silaha wamekuwa wakiwateka raia katika mitaa ya Aden.
Shirika la Umoja wa mataifa la misaada ya chakula limesema halina jinsi zaidi ya kusitisha mipango yake ya kusambaza misaada kutoka na tatizo la mafuta.

Kwa sasa mapigano makali yanaendelea katika mipaka ya eneo la Yemen na Saudia Arabia. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MAANDAMANO MAPYA BALTIMORE MAREKANI


Kumetokea maandamano mapya nchini Marekani katika mji wa Baltimore kufuatia kifo cha kijana mweusi Freddie Gray aliyekufa kutokana na majeraha akiwa mikononi mwa polisi. Mamia ya watu wameandamana katika mitaa, wakionyesha ujasiri licha ya hali mbaya ya hewa iliyokuwepo.

Matokeo ya mwanzo ya uchunguzi wa polisi wa jinsi kijana wa miaka ishirini na mitano mwenye asili ya weusi alivyouawa bado hayajawekwa hadharani.

Maandamano Baltimore
 
Mtetezi wa haki za binadamu, Mchungaji Al Sharpton, ameitisha mkutano mjini Baltimore ili kuimarisha uhusiano baina ya polisi na wanajamii. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

YANGA INA MATUMAINI YA USHINDI

 
Kocha mkuu wa Yanga Hans Pluijm.
 
Kocha mkuu wa Yanga, Hans Pluijm amesema wana ari ya kushinda mechi yao ya mwishoni mwa wiki hii dhidi ya Etoile du Sahel licha ya kuwaacha wachezaji wake tegemezi katika msafara wao wa Tunisia.

Yanga imeondoka Dar es Salaam Jumatano usiku huku wachezaji wake tegemezi, wakiwemo Hassan Dilunga, Salum Telela na Danny Mrwanda, aliyekuwa akicheza soka la kulipwa nchini Vietnam wakiachwa kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za kifamilia. “Yanga imesajili zaidi ya wachezaji 20, wote ni muhimu katika timu”.

“Ni kweli niliwahitaji katika mechi yetu ngumu dhidi ya Etoile, lakini sababu mbalimbali zimepelekea kuachwa kwao”, amesema Pluijm. Yanga itacheza na wenyeji wao, Etoile du Sahel katika mechi ya marudiano ya raundi ya 16 bora ya michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika.

Katika mechi iliyochezwa wiki mbili zilizopita jijini Dar es Salaam, Yanga ililazimishwa sare ya 1-1 hivyo kuwa na kibarua kigumu cha kushinda ugenini huku wenyeji wao wakililia sare ili kucheza hatua inayofuata. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

TAZAMA PICHA ZA YANGA WAKIWA KATIKA MAZOEZI NCHINI TUNIS

IMG-20150501-WA0002
Katika mazoezi ya jana usiku kocha mkuu wa Yanga, Hans van der Pluijm amewaambia vijana wake kujiamini na kucheza soka la kushambulia ili kufunga magoli ya mapema  na kuwachanganya Etoile du Sahel katika mechi ya leo usiku kuanzia majira ya saa 3:00 usiku kwa saa za Tanzania.
Mkuu wa Idara ya habari na Mawasiliano wa Yanga, Jerry Muro naye kama kawaida yupo Tunisia kufuatilia mambo yanavyokwenda. Yanga wanahitaji ushindi au sare ya angalau magoli 2-2 ili kusonga mbele moja kwa moja kwasababu mechi ya kwanza jijini Dar es salaam timu hizi zilitoka sare ya 1-1.
Maelekezo ya hapa na pale kabla ya kuanza mazoezi.
Mrisho Ngassa (kushoto) na Simon Msuva (kulia) wanatarajia kuongoza safu ya ushambuliaji leo
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

BEN DAVIES APASULIWA BEGA

 
timu ya Wales 
 
Beki wa kulia wa Tottenham Ben Davies ameenguliwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Wales baada ya kufanyiwa upasuji wa bega. Mlinzi huyu aliumia wakati wa mchezo wa ligi kati ya timu yake na Southampton uliofanyika wiki iliyopita.

Davies hatojumuika na wenzake katika mchezo wa kuwania kuzufu kwa michuno ya ulaya ya mwaka2016. Ambapo Wales watakua na mchezo dhidi ya Ubelgiji , tayari kocha wa timu hiyo Chriss Coleman amemuita kikosini beki wa Swansea City's Neil Taylor kuziba pengo hilo.

Hii inasababisha mchezaji huyu kukosa michezo iliyobaki ya ligi ya England. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...