Thursday, March 12, 2015

BAYERN MUNICH, PSG ROBO FAINALI UEFA

Bayern Munich siku walipopambana na AC Roma
Timu ya Bayern Munich ya Ujerumani na Paris St. Germain ya Ufaransa zimesonga mbele katika hatua ya robo fainali ya Michuano ya Klabu Bingwa barani Ulaya kufuatia matokeo waliyayapata usiku wa kuamkia leo.
Wakicheza kwa kujiamini Bayern Munich ilidhihirisha kuwa ni moto wa kuotea mbali katika mashandano hayo baada ya baada ya kuwapa kichapo cha mbwa mwizi wapinzani wao Shakhtar Donetsk ya Ukrine cha magoli 7- kwa mtungi.
Magoli ya Bayern Munich yalitiwa kimiani na Thomas Muller, Jerome Boateng ,Franck Ribery,Holger Bastuber, Robert Lewandowski na Mario Gotze.
Nayo Paris St. Germain ya Ufaransa imesonga mbele hatua ya robo fainali baada ya kuwaondoa Chelsea katika mashindano hayo japo timu hizo zilitoka sare ya magoli mawili kwa miwili lakini magoli ya ugenini iliyoyafunga hapo jana ndio yaliyowanufaisha Paris St. Germain.
Hivyo mshindi katika mechi hiyo ilibidi kupatikana katika dakika thelathini za nyongeza baada ya dakika tisini za kawaida kumalizika huku timu zote zikiwa zimefungana goli moja kwa moja.
Wakiwa na matumaini ya kuingia robo fainali Chelsea ndio waliokuwa wa kwanza kupata goli kupitia Gary Cahill katika 81 lakini Mlinzi wa zamani wa Chelsea David Luiz akafutilia ndoto hizo mbali baada ya kusawazisha goli hilo katika dakika ya 86.
Na hivyo hadi dakika 90 za kwanza zinamalizika Chelsea 1 na Paris St. Germain 1 na hivyo kulazimika kucheza dakika 30 nyingine ili kumpata mshindi. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

CHELSEA WAONDOLEWA UEFA WAKIWAA KWAO...!!!

zlatan 1
Vinara wa ligi kuu ya England, Chelsea leo usiku wamejikuta wakiambulia majonzi baada ya kutolewa katika michuano ya klabu Bingwa barani Ulaya na Wapinzani PSG huku wakiwa mbele ya mashabiki wao kunano Uwanja wa Stamford Bridge  baada ya kulazimishwa sare ya 2-2.
Licha ya PSG kucheza wakiwa pungufu kwa kipindi kirefu kufatia Nyota wake Zlatan Ibrahimovic kupewa kandi nyekundi ya moja kwa moja baada ya kumfanyia madhambi Oscar katika dakika ya 32 kipindi cha kwanza, hawakuweza kuvunjika Moyo zaidi waliongeza nguvu na kusaka ushindi hatimaye sasa Wametinga hatua ya Robo fainali ya michuano hiyo mikubwa barani Ulaya kwa ngazi ya Vilabu.hazard  2
Chelsea ndio walianza kupata bao kupitia kwa Gary Cahill kunako dakika ya 80 kipindi cha pili kufatia kona iliyopigwa na mabeki wa PSG wakashindwa kuosha mbele ndipo mchezaji huyo akafumua shuti ambalo lilitinga kambani, Bila kukata tamaa Wafaransa hao (PSG) walikomaa na kujipatia bao la kusawazisha katika dakika ya 85 kupitia kwa David Luiz, ambapo hadi dakika 90 zinamalizika Chelsea ilikuwa imebanwa mbavu na PSG kwa kukubali sare ya 1-1.
Kama kawaida ziliongezwa dakika 30 ili kupatikana mbabe wa mchezo, Thiago Silva beki wa PSG  akanawa mpira katika eneo la 18 na muamuzi akawazawadia Chelsea Penati ambayo ilipigwa na Eden Hazard na kuipatia timu yake bao la 2 ikiwa ni dakia ya 95. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Wednesday, March 11, 2015

TAZAMA PICHA ZAIDI ZA AJALI YA BASI LA MAJINJAH LILILOANGUKIWA NA KONTENA ENEO LA CHANGALAWE MAFINGA MKOANI IRINGA...!!!




 Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

HII NDIO ORODHA YA ABIRIA WALIOANZIA SAFARI STENDI KUU MBEYA, NANE NANE, UYOLE NA CHIMALA NA BASI LA MAJINJAH SPECIAL


Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.


Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...